Nigeria: Mahakama yaridhia uamuzi wa Polisi aliyepata ujauzito nje ya ndoa kufutwa kazi

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374

Mahakama Kuu Nchini Nigeria imedumisha uamuzi wa kikosi cha Polisi kumfuta kazi afisa wa polisi wa kike ambaye alipata ujauzito nje ya ndoa mwaka jana.

Jaji Inyang Ekwo amesema hakuona sababu ya kutosha kuvuruga nidhamu ya jeshi.

Kesi hiyo iliwasilishwa Mahakamanina Chama cha Wanasheria wa Nigeria kufuatia kufutwa kazi kwa afisa ambaye hajaolewa ambaye alipata ujauzito Januari 2021.

"Maafisa wa Polisi wa kiume na maafisa wa Polisi waliooa katika Jeshi la Polisi la Nigeria hawabaguliwi, kuwekewa vikwazo, kuonewa na kudhalilishwa hivyo," ilisema.

Source: BBC Swahili
 
Unaweza kushusha link tujisomee, haya mambo mengine isije ikawa lost in translation
 
Aiseee bado wana mambo ya kizamani
 
Maamuzi sahihi kwa lengo la kuwalinda wanawake na wototo, hii itapunguza uwepo wa single mothers, na watoto wa mitaani, itajenga jamii iliyostaarabika ktk mahusiano ya kimapenzi

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…