Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
- Mwanafunzi huyo alikuwa anajisomea ndani ya kanisa la Redeemed Christian Church of God (RCCG) wakati wa tukio hilo
- Familia yake ilipokea simu kutoka mama mmoja wa kanisa hilo
- Uwavera alikimbizwa hospitalini baada ya mlinzi kumpata sketi yake ikiwa imechanika na blauzi yake ikiwa imelowa damu
- Alikata roho hospitalini siku ya Jumamosi, Mei 30, kutokana na majeraha aliyopata
Wanigeria wamezua hamaki mitandaoni kufuatia mauaji ya kinyama ya mwanafunzi mwenye miaka 22, Uwavera Omozuwa aliyeuawa kanisani.
Kampeni ya kutaka atendewe haki imeenea kwenye mitandao ya kijamii nchini Nigeria, huku familia yake ikiomba msaada wa kumtafuta muuaji.
Uwavera alikuwa anajisomea ndani ya kanisa la Redeemed Christian Church of God(RCCG) wakati wa tukio hilo. Picha: Yabaleft.
Kulingana na dada yake marehemu,Judith Omozuwa, Uwavera alikuwa anajisomea vitabu vyake ndani ya kanisa la Redeemed Christian Church of God(RCCG), karibu na nyumbani kwao Benin City wakati wa tukio hilo.
Familia yake ilipokea simu kutoka mama mmoja wa kanisa hilo mnamo Jumatano, Mei 27.
Judith alifichua kwamba dada yake mpendwa alibakwa kabla ya kuawa na wahalifu hao.
Uwavera alikua amejiunga na Chuo Kikuu cha Benin kusomea microbiolojia.Picha:Yabaleft.
Dada huyo alisimulia kwamba Uwavera alikimbizwa hospitalini baada ya mlinzi kumpata sketi yake ikiwa imechanika na blauzi yake ikiwa imelowa damu.
Mwanafunzi huyo ambaye alikuwa na ndoto ya kuwa muuguzi, alikata roho hospitalini siku ya Jumamosi, Mei 30, kutokana na majeraha aliyopata baada ya kushambuliwa.
Mwanzilishi wa kanisa la RCCG E.A.Adeboye ameshtumu tukio hilo. Picha: UGC.
Uwavera alikua amejiunga na Chuo Kikuu cha Benin kusomea microbiolojia kabla ya kukumbana na mauti yake.
Dada yake alifichua kwamba marehemu alikuwa na mazoea ya kwenda kujisomea katika kanisa hilo ambalo liko karibu na nyumbani kwao kwa sababu ya utulivu.
Mwanzilishi wa kanisa hilo Pasta E.A. Adeboye alizungumzia kisa hicho cha kinyama na kumtaka kila mmoja kuombea familia ya marehemu ili wapate haki.
- Familia yake ilipokea simu kutoka mama mmoja wa kanisa hilo
- Uwavera alikimbizwa hospitalini baada ya mlinzi kumpata sketi yake ikiwa imechanika na blauzi yake ikiwa imelowa damu
- Alikata roho hospitalini siku ya Jumamosi, Mei 30, kutokana na majeraha aliyopata
Wanigeria wamezua hamaki mitandaoni kufuatia mauaji ya kinyama ya mwanafunzi mwenye miaka 22, Uwavera Omozuwa aliyeuawa kanisani.
Kampeni ya kutaka atendewe haki imeenea kwenye mitandao ya kijamii nchini Nigeria, huku familia yake ikiomba msaada wa kumtafuta muuaji.
Kulingana na dada yake marehemu,Judith Omozuwa, Uwavera alikuwa anajisomea vitabu vyake ndani ya kanisa la Redeemed Christian Church of God(RCCG), karibu na nyumbani kwao Benin City wakati wa tukio hilo.
Familia yake ilipokea simu kutoka mama mmoja wa kanisa hilo mnamo Jumatano, Mei 27.
Judith alifichua kwamba dada yake mpendwa alibakwa kabla ya kuawa na wahalifu hao.
Dada huyo alisimulia kwamba Uwavera alikimbizwa hospitalini baada ya mlinzi kumpata sketi yake ikiwa imechanika na blauzi yake ikiwa imelowa damu.
Mwanafunzi huyo ambaye alikuwa na ndoto ya kuwa muuguzi, alikata roho hospitalini siku ya Jumamosi, Mei 30, kutokana na majeraha aliyopata baada ya kushambuliwa.
Uwavera alikua amejiunga na Chuo Kikuu cha Benin kusomea microbiolojia kabla ya kukumbana na mauti yake.
Dada yake alifichua kwamba marehemu alikuwa na mazoea ya kwenda kujisomea katika kanisa hilo ambalo liko karibu na nyumbani kwao kwa sababu ya utulivu.
Mwanzilishi wa kanisa hilo Pasta E.A. Adeboye alizungumzia kisa hicho cha kinyama na kumtaka kila mmoja kuombea familia ya marehemu ili wapate haki.