Niifate Simu yangu ama Niipotezee? Maana binti kaolewa na mwanaume mwingine

Niifate Simu yangu ama Niipotezee? Maana binti kaolewa na mwanaume mwingine

holoholo

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2023
Posts
1,859
Reaction score
2,986
Wakuu,
Kuna binti kijiji jirani toka nilipo mimi,nilimpenda sana nae akanipenda sana,

Ilifikia hatua nikamnunulia simu, tukawa tunawasiliana, mapenzi yakakolea wakuu,binti kila anaekuja kuchumbia anamkataa,mpaka wazazi wake wakakaa nae kitako, wakamuuliza kama unakataa kuolewa je unataka uolewe na nani?

Akajibu nataka kuolewa na holoholo ikabidi nitafutwe na wazazi wa binti, ishu nikaikubali,wakaniambia nikajitambulishe, nikagoma

Katika matumizi ya simu binti alikuwa anatumia kwa siri sana,ila badae akaja akagundulika kuwa anatumia simu,akabanwa akasema kuwa nimempa mimi, akanyang'anywa, nikapigiwa simu niifuate nikagoma

Binti akaondoshwa pale nyumbani akapelekwa wilaya tofauti na ninayoishi mimi ila akawa ananipigia simu kwa siri, baadae akapatikana mchumba,binti akakataa katakata kuolewa lakini akalazimishwa kuolewa, binti akaolewa

Nipo katika dilema je niifuate simu yangu kwa wazazi wa binti au niipotezee.

Ushauri wenu wakuu

NB: stori hizi ninazoleta jukwaani si za kutunga.
 
Watu tunafuata mpaka memory we unaacha simu
1739803597153.jpg
 
Uliitwa ukajitambulishe, ukakataa
Ukaitwa ukachukue simu yako, ukakataa pia
Sasa unataka nikushauri nini hapo?
Inaonekana ulikuwa unamtumia tu kwa haja zako, wala hukuwa na nia ya kumuoa
Ukweli usemwe tu
Imekuuma alipoolewa, lakini kumbuka alikupenda wewe lakini vijana mnapenda kuwapotezea mda wasichana
Ila huyo naona kajitambua maana kuna wengine huwa wanasema tuko pamoja huu mwaka wa 10 na hawajaoana na hawana watoto
Ila kiukweli wameisha ua watoto kibao
 
Uliitwa ukajitambulishe, ukakataa
Ukaitwa ukachukue simu yako, ukakataa pia
Sasa unataka nikushauri nini hapo?
Inaonekana ulikuwa unamtumia tu kwa haja zako, wala hukuwa na nia ya kumuoa
Ukweli usemwe tu
Imekuuma alipoolewa, lakini kumbuka alikupenda wewe lakini vijana mnapenda kuwapotezea mda wasichana
Ila huyo naona kajitambua maana kuna wengine huwa wanasema tuko pamoja huu mwaka wa 10 na hawajaoana na hawana watoto
Ila kiukweli wameisha ua watoto kibao
dah!Moyo unadunda kupoteza tecno camon19
 
Umenikumbusha clip ya:
"Maria Maria nataka sweta langu, yani sweta langu umempa babaako anavaa anapendeza, yani bora hata asingependeza.
Nataka sweta langu Maria"
 
Wakuu,
Kuna binti kijiji jirani toka nilipo mimi,nilimpenda sana nae akanipenda sana,

Ilifikia hatua nikamnunulia simu, tukawa tunawasiliana, mapenzi yakakolea wakuu,binti kila anaekuja kuchumbia anamkataa,mpaka wazazi wake wakakaa nae kitako, wakamuuliza kama unakataa kuolewa je unataka uolewe na nani?

Akajibu nataka kuolewa na holoholo ikabidi nitafutwe na wazazi wa binti, ishu nikaikubali,wakaniambia nikajitambulishe, nikagoma

Katika matumizi ya simu binti alikuwa anatumia kwa siri sana,ila badae akaja akagundulika kuwa anatumia simu,akabanwa akasema kuwa nimempa mimi, akanyang'anywa, nikapigiwa simu niifuate nikagoma

Binti akaondoshwa pale nyumbani akapelekwa wilaya tofauti na ninayoishi mimi ila akawa ananipigia simu kwa siri, baadae akapatikana mchumba,binti akakataa katakata kuolewa lakini akalazimishwa kuolewa, binti akaolewa

Nipo katika dilema je niifuate simu yangu kwa wazazi wa binti au niipotezee.

Ushauri wenu wakuu

NB: stori hizi ninazoleta jukwaani si za kutunga.
Kufuata simu ukakataa, kwenda kujitambulisha ukakataa pia.

Makataa yako hayo yote yanaongozwa kwa kibri au busara?

Kama ulishafanya uamzi wa kukataa kuifuata, kwa nini uje tena kwetu 'kutula kisogo' kwa kutuomba ushauri wa jambo ulilokwisha kuamua, unatuchukuliaje sisi kijana?
 
Kufuata simu ukakataa, kwenda kujitambulisha ukakataa pia.

Makataa yako hayo yote yanaongozwa kwa kibri au busara?

Kama ulishafanya uamzi wa kukataa kuifuata, kwa nini uje tena kwetu 'kutula kisogo' kwa kutuomba ushauri wa jambo ulilokwisha kuamua, unatuchukuliaje sisi kijana?
shida mkuu,nimeona si sawa kupotezea simu yangu,hivyo nimeona kabla sijafanya maamuzi yeyote basi nipite mitaa ya jf nipewe nondo.
 
Back
Top Bottom