Nikiwa mtaani nitamjuaje mtu kuwa huyu ni member wa JF. Naombeni dalili!

Kubadili jina nafanyaje? Kila nikijaribu nashindwa
 
Nawajua marafiki zangu waliopo humu na huwa tunapiga story za jf ila bado wanaisaka ID yangu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]..
Kuna kipindi nilihisi kama kuna mtu kaishtukia, ikabidi niwaombe mods waibadili jina na nikafanyiwa faster . Ila ndo hivyo ilinipa shida mwanzoni maana watu ambao tulikwishaanza kujuana ni full kupishana kama hatujuani humu yaani kama vile mtu aliyefanyiwa surgery ya uso anavyopishana ndugu zake.
 
We jamaa nakuchoraga sana Tabata The Great,
 
Kabla ya kuwa na ID hii ya Sigara Kali,nilikua na ID fulani ambayo mwisho iligundulika na college mate wangu wa chuo baada ya siku moja kuniita a.k.a yangu ya chuo ,nikaona huyu jamaa anataka kuniletea mazoea,nikabadili ID
Unabadili vp mkuu
 
Kuna dogo ni graduate one day nilikutana nae Ubungo nikampa JF ID yangu japo yeye alikataa katakata kuniambia anatumia I'd gani...humu kama unahororojoka mitusi mizitomizito utakuwa na guts saa ngapi za kutoa I'd yako si utahisi tcra na polisi wamekuja kukuunganisha na korokoroni
 
Uzuri natumia jina tangu chuo hadi leo linalogo mahali kabisa sina shaka na hunikuti jukwaa la siasa kirahisi
 
Like zimefika tu 3 na miji umetaja minne na umetumia wingi ktk maandshi ilihli kuna mafungu ya kutosha ya watu huko!!
Kwa upendeleo, ni wastani wa mtu mmoja kwa kila mji! Hali c nzuri bado.
 
Ni ngumu sana kumjua mtumiaji wa JF na ukimjua tuu sa hiyo hiyo atabadili ID!

Haka ka rule ka kutumia fake names kametuathiri sana!
 
Sijawahi na sitaki hata kujua nani anatumia jf hapa mtaani kwetu
 
Mimi nimewagundua watu wa karibu kama wa 3 hivi ID zao humu ila sijawaambia,ni rahisi sana kugundulika ni nani na mtu wa karibu akikuhisi akaanza kukufuatilia,maana kuna uzi utataja kabila,kuna mwingine utataja shuke yako ya msingi,Sekondari au Chuo na kuna siku uta share story ambayo inawezekana na yeye umeshawai kumhadithia

Inabidi uwe smart sana humu ila kuto blow cover
 
Ni ngumu sana kumjua mtumiaji wa JF na ukimjua tuu sa hiyo hiyo atabadili ID!

Haka ka rule ka kutumia fake names kametuathiri sana!
Kwa hiyo watu mnaogopa kabisa kuwa revealed? Sijawahi kuogopa na sidhani itatokea. Kuna mtu alisema japo tunatumia ID fake, tunayoandika hayapo mbali na uhalisia wetu.
 
✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️✍️
 
Kuficha ID kunafanyika tangu binadamu ameumbwa. Mambo yote yale unayoyasema ukiwa umejificha si kwamba ni uongo bali ni mazingira yanamtengenezea mwanadamu.

Kuna watu wanadhani JF itashindwa kesi halafu ije ifutwe. Thubutu. Hakuna kitu kama hicho. JF inachokifanya ndiyo maisha. Tusipoyazungumza hapa tutayazungumza huko bar na hata wapelelezi ambako siku hizi sidhani kama wanahangaika nako sana.

Hivyo, kama unajifanya eti kila kitu kwako ni open, hakunaga binadamu aliyezaliwa akawa hivyo. Hata Yesyu kuna mambo aliwaambia mitume kadhaa tu.


Kwa hiyo watu mnaogopa kabisa kuwa revealed? Sijawahi kuogopa na sidhani itatokea. Kuna mtu alisema japo tunatumia ID fake, tunayoandika hayapo mbali na uhalisia wetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…