Nikiwa mtaani nitamjuaje mtu kuwa huyu ni member wa JF. Naombeni dalili!

Nikiwa mtaani nitamjuaje mtu kuwa huyu ni member wa JF. Naombeni dalili!

This is my secreto to you amigos dont tell anybody 'bout my name... My name is Gonzalo De La cruz caballero Miguel
 
Wewe kama mimi yani. Sina cha kuficha. Marafiki zangu ambao hawako huku nawaambia kuhusu JF na wanajiunga na wanaijua ID yangu.
Sina jambo la kuigiza au kuogopa JF bado. Na hata wanaonijua nje ya JF kupitia JF wanajua siogopi kujulikana natumia JF.
Ungekuwa huna cha kuficha usingeziba sura yako.
 
Wote humu tuna ID na hatujuani ukiachilia mbali wale wanaojulikana yaani verified.. Nasemea ID za kujificha kama zetu hizi

Lakini mtaani haipiti siku tunaiongelea JF. Tabu ni kwamba kila tunapoongea mtaani hakuna anayeonyesha dalili kwamba yeye ni member.

Hivyo unaweza kujibizana na mtu humu kumbe mnakunywa naye beer kila jioni.

Nawapa stori moja.

Mtoto wa mjomba wangu mwaka 2011 niliona computer yake ina matatizo na nikamsaidia. Sasa ilikuwa wazi mno akajisahau akawa anatuma post humu JF, siisemi ID yake na nikaiona.

Hakujua nimeona ID yake na siku hiyo alikuwa anatuma kuonyesha matatizo ya chuoni kwake nacho sikitaji.

Basi nikaikariri ID yake nikawa nafuatilia post zake humu JF.

Kimsingi alifaulu sana kukisumbua kile chuo kupitia JF. Maana madai yao yalielezwa vizuri humu JF hadi watawala wa chuo wakanywea na Tanzania nzima ikajua matatizo ya chuo hicho.

Sasa baada ya mwaka mmoja nikamtumia message kwenye simu kumtania kwa kumuita kw ajina la ID yake ya humu JF.

Mfano, kama ID yake ni Chungasana, nikamwita "vipi Chungasana unasemaje?"

Eeeh bwana akaruka, akanijibu "Chungasana ndiye nani".

Sikutaka tena kumuuliza nikajua kuwa hata ndug yako akiwa na ID ya JF hataki umjue.

Je, wenzagu mlishawahi kumjua mwenzenu wa JF hata kwa kuhisia?
Hicho chuo ni The Law School of Tanzania.


Anyways any Tanzanian graduate is presumed to be a member of Jf
 
Kuna jamaa angu oficn kila akiona nimeingia JF anajidai anasogelea kompyuta yangu kuniuliza vitu...au utasikia naomba nitumie kompyuta yako mara moja...nawahi ku-log out

Swali ni Je inasaidia Nini??
Kumbe ndio I'd yako hii, nishakujua sasa[emoji854][emoji854]
 
Kazini baadhi ya tunaofanya nao kazi niliwashauri badala ya kuhangaika na facebook ambayo toka 2014 sijawahi kuitumia watumie Jamiiforum maana kuna mengi ya kujifunza zaidi, wengi niliwafungulia kwa kuwauliza wataje jina wanalipenda kutumia hivyo baadhi huwa nawaona wakichangia japo me si mchangiaji sana.

Wengine walipoona humu watu wasiri walibadili Id zao hivyo siwaoni tena japo wanatumia na sikupenda kuwafuatilia nijuwe Id zao maana kwangu mimi haina umuhimu.

Sasa kituko week kama mbili hivi tulikuwa na kikao na Boss wetu huku akituelekeza baadhi ya mambo ubaoni, sasa kuna mtu alikuwa akimpigia mara kwa mara..ndipo akanipatia simu huku akiniambia nisogee pembeni nipokee na nimweleze kuwa angempigia maana yupo katika kikao.

Baada ya simu kukata ndipo nikaona app ya Jf nilipofungua nikaona Id anayotumia, nilishituka kidogo maana kwa misimamo yake na alivyo serious nisingetegemea angekuwa hivi, yaani humu ni kituko na anapenda sana stori wa wanaume tena anajigamba yeye ni fundi awapi kitandani, Toka nijuwe najilaumu sana afadhali nisingejuwa.

Leo pia asubuhi nilishuhudia mwana Jf aki log in kuperuzi nikiwa katika daladala maana alikaa nami nilisimama kando yake ila sikutaka kufatilia sana na hata simkumbuki tena.
 
Back
Top Bottom