Nikki wa Pili uko vizuri sana

GadoTz

JF-Expert Member
Joined
Nov 20, 2014
Posts
370
Reaction score
636
Na nimekusiliza kwenye kipindi cha siasa za siasa nimegundua mambo matano kuhusu wewe.

1. Una ufahamu mkubwa sana kuhusu mambo mengi.
2. Unasoma sana vitabu hivyo vinakujenga kifikra na kimtazamo
3. Una ujuzi wa kuwasiliana kwenye mazungumzo, unasikiliza, unatafakari ndipo unaongea
4. Una maono, mazungumzo yako yamejaa maono ya mbali ni aina ya watu wanaoifikiria kesho na kesho kutwa kila sekunde
5. Wewe ni hazina kubwa ya nchi hii, wanaokubeza wafikirie mara mbili kuhusu wewe.

WEWE NI INSPIRATION.

 
Wekeni Hayo Mahojiano Hapa Ili Mada Iwe Na Mashiko.Au 2pieni Link Ili 2we Na Vivid Proof!
 
GadoTz

Kuna tofauti kati ya Nikki Mbishi na Nikki wa Pili?
Na issue kuwa Nikki wa pili ni mdogo wa kuzaliwa wa Joh Makini ni kweli?
 
Last edited by a moderator:
Kuna tofauti kati ya Nikki Mbishi na Nikki wa Pili?
Na issue kuwa Nikki wa pili ni mdogo wa kuzaliwa wa Joh Makini ni kweli?

Ndio kuna tofauti kubwa..Niki mbishi ni msanii anaeimba hiphop ngumu anatokea Ukonga while Niki wa Pili ni msanii anaefanya hiphop shule anatokea Arusha.

Niki wa pili ni mdogo wa tumbo moja wa Joh Makini...

Mwisho kabisa Nikki wa Pili ni msanii msomi kuliko wasanii wote hapa Tanzania tokea tupate uhuru...Anafanya PHd ya development studies Mlimani .
 

Hakuna hip hop hizo ulizotaja hapa duniani, Labda huko mars.. Hip Hop ni Hip Hop haigawanyiki.

Kwingine uko sawa mkuu.
 
Kanifurahisha sana Leo anaulewa mzuri na ana hoja anaijibu shortly ikiwa imejitosheleza na usomi una msaidia kwa kiasi kwa kuwa na wider knowledge. Big up
Nimemkubali anajua coz ni wa moto katoka chuo juzi hata madaftari na pamphlets hajachoma moto bado
 

Kumbe ni ndugu... Sikuwahi kufahamu
 
Muda huo pia alikuwa EATV kwenye kipindi cha Siasa za siasa

Niki ni kichwa Haswa and cool human being.
 
Vip mkuu..ww ni unemployed nn..?? mbona umekukuna??
Ndio mkuu, nilishatafuta kazi kwa muda mrefu nikakosa, baada ya kuona umri wangu unazidi kwenda, ndipo nilipo amua kutafuta mtaji na kujiajiri mwenyewe. Wimbo wa sitaki kazi uliniongezea nguvu ya kukomaa na mishe zangu.
 
Ndio mkuu, nilishatafuta kazi kwa muda mrefu nikakosa, baada ya kuona umri wangu unazidi kwenda, ndipo nilipo amua kutafuta mtaji na kujiajiri mwenyewe. Wimbo wa sitaki kazi uliniongezea nguvu ya kukomaa na mishe zangu.

Hongera mkuu...mungu akujaze nguvu mkuu...utafanikiwa...
 
Anazingua na maswali yake ya kuchalenge kiuanafunz mpaka zito akawa anamaind anauliza swali hujamaliza kujibu anakukatisha kifupi ana maswali ya kuku na yai kipi kimeanza sometime jibu analijua lakin anauluza maswali ya kuleta majibu ya kichwan kwake
 

Siasa hawezi kabisa labda aendelee kujikita kwenye muziki kabisa!

Yani ana papara sana na wala hajui kuwa kuna wakati anatakiwa awaachie wenzie nafasi ya kuongea...! Tangu nianze kumfatilia pale 360 sijawai kuona cha maana kutoka kwake!

Nimekuwa nikijiuliza hivi Clouds TV huwa hawana watu wakualika zaidi ya Nick? Jana ndio kabisa..!

Mimi ninge mshauri abaki kwenye muziki kwenye siasa awaachie wengine!
 
Kusema ukweli yupo fresh labda tu kwa kuwa taaluma yake sio mwanahabari coz alikuwa hatoi nafasi kwa mh Zitto kujibu swali ambalo kauliza, yani anauliza swali hajajibiwa keshauliza lengine, so alikuwa anampa wakati mgumu sana mh Zitto.

Ushauri wangu kwa Nikki anatakiwa awe anatoa muda wa kusikiliza na kuhoji lakini kwa kweli jana niliona vurugu tu, hata mwandishi wa habari mwenyewe alichanganyikiwa alipokuwa akitaka kwenda break Nikki alikuwa bado anaendelea kuongea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…