Niko Njia Panda... Msaada Please

mapenzi hayahitaji ushauri...fuata moyo wako..hapa watu wanajaribu kukudadavulia tu principles according to their experiences ila ujue kuwa sio suluhisho la kudumu, mwenye uchaguzi na suluhisho la swala hili ni WEWE TU!! sali sana na kaa chini uungalie kwa undani hawa jamaa yupi anayekufaa..Kumbuka..ni WEWE TU!!
 

Mzee mwenzangu Asprin,

Hawa wajukuu sijui tuwaelezeje...Nimeona mahali eti RR anajaribu kutafuta tafsiri ya ndoa.....Hili jambo liko wazi.

Mwenza wa kufa na kuzikana siyo lazima awe na mapenzi ya egoli egoli au bongo movies...Haya huwa hayadumu hata kidogo.

Kama kuna mtu anabisha, basi anambie anaweza kula pilau mara ngapi kwa mwezi? Ila ugali na maharage au kauzu tunakula mwaka mzima...na hatuchoki. Binti awe makini kama hataki kuishia kwenye vikao vya usuluhishi kila siku..!!

Halafu The Boss kampa ushauri mzuri sana...Peter anaweza kuendelea kumpa raha na matumaini ya kuishi duniani. Ila siyo mume hata kidogo!!.....Vinginevyo, apige wote chini na kuazan safari upya!

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
Mkongwe Dark City mzee mwenzangu umenena vema...

Hilo la kupiga chini aanze moja kwa hali halisi itakuwa ngumu. Kwanza ukizingatia umri unakimbia na ni vigumu mwanamke kutongoza. Maadam ameshatokewa na wawili na inavyoonyesha tatizo lake ni uchaguzi wa kati yao.

Ndo maana sisi wenye busara zetu, tunamwambia..... Go For Johnnie!!
 
Last edited by a moderator:
Ile sauti uisikiayo moyoni ndo njia ya kweli
 
Ile sauti uisikiayo moyoni ndo njia ya kweli

Punguzeni kujidanganya,

Hata wanoolewa na vibaka au serial killers huwa wanadai waliwapenda sana...

Unapofikia point ya kuchagua mume au mke, hutakiwi kusikiliza kiungo kimoja..Kinyume cha hapo ni kujitafutia kiama!!

Babu DC!!!
 
Well,Da asia ushauri wangu kwako ni 'FOLLOW UR HEART' coz huwezi amua kuishi na mtu just bcoz anakupenda 2 bt wewe huna 'appetite nae' huna stim,not compatible,not same hobby,interests,zenyewe haziendani m-baba....hutakuwa unaitendea nafsi yako haki...huwezi nunua 'amani,furaha ya moyo wako na maisha' kwa pesa...co money at times iz not everything...we mwenyewe unazo za kwako...kaa chini na peter mwelimishe mpange maisha...that's all...
 
Nyumba kubwa kukufafanulia tu ni kuwa wote wana watoto. John anaishi na watoto wake. Peter nae ana watoto lakini wanaishi na mama yao. kwa sasa yeye anaishi mwenyewe ila anasomesha watoto wake wakiwa kwa mama yao, pamoja na matumizi anatoa.

Kwani umekwenda umri sana maana ndoa sio mchezo wa kuigiza...unaweza kuwa mzigo usiobebeka wakati mwingine.
 

Mkuu Asprin; nimeshatia timu DSM. Ni-PM Mkuu kupata mshiko wako. Au toa maelekezo nini cha kufanya.
 
Last edited by a moderator:

Mkuu Kongosho, huna haja ya kwenda Sumbawanga, nimeshatia timu Bongo. Tuwasiliane na Winners wote!
 
Last edited by a moderator:

Maneno yako yametulia sana...Mie binafsi siwezi kuwa na mtu ambaye yeye ananipenda sana lakini moyoni mwangu hayuko hata chembe. Sina hata raha tunapokuwa pamoja au kumkosa pale ambapo hatuko pamoja. Naona kama nitakuwa napoteza muda wangu. Mapenzi ukiyapata pale ambapo wewe unapenda na kujua unapendwa yanaleta furaha kubwa sana. Umesema Peter ana elimu sasa mshawishi atafute kazi ya kuajiriwa na huku aendelee na mishe mishe...hata kama mishe mishe zikikwama bado atakuwa na kazi yake ambayo inawaingizia kipato cha kuweza kumudu gharama za maisha...Kwa hiyo ushauri wangu mpe nafasi nyingine Peter. Kila la heri

 
Last edited by a moderator:

Mi najua akitulia na kumsahau peter ataweza kumpenda john na ikiwa john hatampa makhashikashi ila akimpa upendo atampenda sana hata yeyd atashangaa ni yeye ajaamua tu kumpa moyo
 
Last edited by a moderator:

Naam pesa hutafutwa...na mkiweka nia na kujituma basi hazitawapiga chenga....kwenda kujilazimisha kuolewa na mtu ambaye huna hata chembe ya mapenzi naye ni adhabu ya aina yake baada ya muda ndani ya ndoa utamtafuta Peter na kumwambia huna raha ndani ya ndoa umefanya makosa makubwa sana kuolewa na John, Peter naye si ajabu ana mke mwingine....mnabaki kukutana nje ya ndoa zenu na kuwasaliti wenzenu.


 
Last edited by a moderator:
bado una mtihani wa kimaisha mahana hapa upo njia panda ila ushauri wangu kama utojali ni vema ukamkubali unaye mpenda kuliko kujiingiza kwenye maisha ambayo ktk maisha yako hutaishi kwa amani itakuwa ni ndoa ndoano hambayo yawezekana ikawa na kila kitu ila ukajiona huna dhamaini ktk maisha yako kwa kawaida usiangalie uwezo angalia upendo wa thati upo upande upi japo ni ngumu kufanya mahamuzi ya haraka kuliko ujiingize kwenye jambo ambalo hutalifurahia ktk maisha yako yote ya ndoa
 
Naamini kuwa unawafahamu vema sana watu hao........Jaribu kufuata moyo wako pamoja na ushauri uloupata kutoka kwa wajumbe wengine
 

What is Love to you?

Nashauri pamoja na hisia zako za kimapenzi waweke wote katika mizania ya vigezo vyote ulivyonavyo vya mume unayemtaka.

Ila kumbuka kuwa Mapenzi ni zaidi ya feelings. katika ndoa inafika mahali feelings na hata mapenzi ama yanapungua au yanakwisha. ask yourself utabaki na nini katika ndoa hali hiyo itakapotokea? Pia kumbuka wakati mwingine unaweza kujifunza kumpenda mtu kwa kumfanyia mambo mazuri hadi unampenda kweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…