# HABARI WANAFUNZI 28,037 KUKOSA MIKOPO.
Wanafunzi 28,037 watakosa mikopo kutoka bodi
ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya hivyo
watalazimika kusaka njia mbadala kama wanataka
kuendelea na masomo hayo. Hadi kufikia julai 31
wanafunzi 58,037 walikuwa wametuma maombi ya
mkopo na bodi hiyo imesema ina uwezo wa kutoa
mikopo kwa wanafunzi 30,000 tu.
Pia kuhusu madai ya wanafunzi wa vyuo vitano
kutaka wapewe bilioni 6.6 kwaajili ya mafunzo ya
vitendo, bodi ya mikopo imesema malipo hayo
yaandaliwa na kwamba hundi za malipo hayo
zinatarajiwa kupelekwa katika vyuo wiki ijayo.
Vyuo hivyo ambavyo havijapata fedha ni SAUT,
IFM, Teofilo Kisanji- Mbeya, Tumaini, SMUCCO na
Jordan cha Morogoro
hii habar hukuipata wewe?