Niliacha chuo ili nifanye biashara, sasa mtaji umekatika sijui nifanye nini?

Dogo cha kwanza biashara lazima uwe na maleng. Pili, kama mtaji umekata tafuta kazi inayoendana na mtaji ulionao. Hapo ungekuwa upo mkoa Mwanza ningekwambia biashara moja inayolipa huku na mtaji wake ni chini ya 30k afu unafanya masaa labda 6 tu unaondoka na 10000 yako au zaidi.

Vijana kazi zipo nyingi mno ila shida tunazionea aibu. Lakini kingine kama hujawahi kufanya biashara jaribu kuulizia kwanza, wewe ulifikiri huwezi kuuza nguo huku unasoma? Mbona wengine tunafanya umachinga na chuo hatuachi? Dogo fanya maamuzi sasa
 
Binadamu hashindwi kitu jamaa, fanya hata udalali. Nenda Bagamoyo kule watu hawajasoma ukawape shule. Vijijini hapo pwani kuna malofa kibao, nenda kawapige. Unaeza ukaopoa hata mtumishi akawa anakulisha huku unatafuta mdogo mdogo
 
Mkuu unajua bei ya kupata nafasi ya kutandika vitu pale kariakoo? Sio mchezo
 
Umefika ile hatua ya kujiuliza kwanini nobody can stop reaggae... pole sana mkuu...
 
Binadamu hashindwi kitu jamaa, fanya hata udalali. Nenda Bagamoyo kule watu hawajasoma ukawape shule. Vijijini hapo pwani kuna malofa kibao, nenda kawapige. Unaeza ukaopoa hata mtumishi akawa anakulisha huku unatafuta mdogo mdogo
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ we jamaa mjanja kweliii!!
 
Naona wengi wakiku tukana hapa jukwaani, wakikashifu hasa kuhusu suala la shule sijui una sup 4, sijui ni kilaza, sijui hujui biashara na vyote hivi.

Mkuu hata biashara ukizingatia huwezi kulala njaa, fanya biashara ya kuchuhuza kwanza upate nguvu ya kurudi au relief.
Changamoto kama hizi hupitii wewe tu hata mimi napitia sana, simama tu kwenye line jiamini na biashara ipo siku.

wengi hapa wanaongea shule shule shule umeacha university umeacha university sijui serikali inakupa boom hayo yote ni makwazo unawekewa tu ili uone umeshashindwa lakini sio kweli pambana bado.
 
namba ya simu iko wapi upate michongo..
 
Hukutakiwa kuacha masomo wewe kijana...

Hela uliyolipwa na serikali ungevumilia na kuikusanya kidogo kidogo hadi unamaliza chuo ungekuwa na mtaji na wazo thabiti...

Ushauri kwa sasa, tafuta namna ya kurejea chuo
 
Usirudi chuo, usirudi chuo na usirudi chuo
Hukua na wazo baya ila ulikua na mategemeo mabaya, kwahiyo we jitathmini upya uanze kazi, usirudi chuo.
 
Dont be defeated by a temporary defeat......Kaka hayo ni ya muda tu.....kubali tu kwamba kwa sasa unapitia kipindi kigumu,usikubali kuwa umeshindwa kwa sababu umepitia kikwazo cha muda.....pambana mkuu......pambana boss wang najua mwanga upo mbele.......ukiwa unajifunza kuendesha baiskeli mara ya kwanza lzm utaanguka,utaumia,marafiki zako watakucheka na kukukebehi lkn kesho utakuwa more determinant usianguke tena,na utakapoweza kuendesha nakuhakikishishia utaendesha hata bila kufikiria na ikitokea umeanguka utajua ni vipi na kwanini umeanguka so haitakupa shida kusahihisha kosa lako.......keep going dont quit!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…