Uchaguzi 2020 Niliingiza jumla ya Tsh laki 8 kwa watia nia hawa Nkenge lakini nikawasaliti sandukuni

Uchaguzi 2020 Niliingiza jumla ya Tsh laki 8 kwa watia nia hawa Nkenge lakini nikawasaliti sandukuni

Riz king

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2018
Posts
276
Reaction score
549
1 Dr Mazima
huyu jamaa anaelimu ndogo yaani ni AMO lakini ni mbinafsi na roho ya ujuha sana nilikula laki mbili yake baada ya wapambe wake watatu walio nifata kwa nyakati tofauti na kunigea kitita hicho. Ila tabia zake za kudharau watu, shule ndogo kichwani na ujuha ndo vilisababisha nikaitafuna pesa yake kwa hasira sana

2Dr Kamala
huyu kasasemwa sana yeye nilitandika laki 3.5 nikiwa ndo miongoni mwa wagawaji wa pesa zake kwa wajumbe wenzangu huku akiamini ni timu yake lakini ujinga wake wa kupata madaraka na kuisahau Nkenge ndo kiliniudhi nikaila vyema hiyo pesa

3 Assumpita.
huyu alipojua nipo timu Kamala akaja kuzunja kwa fitna, nikajifanya namsapoti nikawa nauma huku na kule hatimaye nikala ela yake laki 2.5 ila kura nikampa Muungwana mmoja aitwaye Frolent Kyombo ingawa sikula pesa yake. Asanteni watia nia me naongezea kiasi kingine nikachukue bodaboda yangu ila msisahau kurudi 2025 tuzile tena
 
Waendelee kula hivi hivi mpaka waache kutia Nia
Pia Mkuu amesitisha mishahara mwezi huu mambo mazuri.
Acha waendelee wanaacha Udas, Uras, ukuu wa Wilaya plus Mkoa kukimbilia Ubunge
Wanyoosheni hawa mpaka wawe wanakuelewa Rais
Wawe wanaridhika jaman
 
Mmhhh laki 8 kwa watu watatu?? Huwa wajumbe si wanapewa elfu 20 mpaka 40?
 
Jiandae kuitwa kituo cha polisi kilichokaribu yako.
Alamsiki.
 
Watakukata mkua wewe! Umekula pesa ya Dr Kamala halafu namuona anakaribia kulia kwenye uchaguzi; kweli nyinyi wajumbe hamna maana mnaweza kumsababishia mtu kiharusi kwenye ukumbi wa mkutano.
 
Back
Top Bottom