Nilijiapiza mjini nitarudi kutembea tu, lakini hapa nimelalia maboksi baada ya kuungua na maisha ya kijijini

Nilijiapiza mjini nitarudi kutembea tu, lakini hapa nimelalia maboksi baada ya kuungua na maisha ya kijijini

Ilikuwa ni mwezi wa saba sikumbuki tarehe ndo niliaga JF na kuelekea kijijini nikitokea Dar, baada ya kumaliza mafunzo ya ufundi, na nikijiapiza mjini ntarudi kutembea tu. Lakini hapa ninapoandika huu ujumbe nipo nimelalia maboksi kwenye geto la kupanga baada ya kuungua na maisha ya kijijini huku nikiwa na ujuzi wangu vizuri tu. Kwanza kabisa mimi ni fundi - simu, radio, umeme wa majumbani. Natengeneza video mbali mbali na vitu vingi vingi tu vinavyotumia umeme.

Changamoto za kijijini:
  • Upatikanaji haraka wa diode au spea za maredio tv nk.
  • Umbali wa kuvifikia nauli 12000 kwenda na kurudi.
  • Intaneti, unapokuwa unahitaji msaada wa kiufundi kupitia google
  • Kazi za msimu
  • Wateja wengi ni malialia n.k
Ndo vimenifanya leo hii nimelala kwenye mabox na vifaa vyangu vya kazi hapa Arussha mjini leo hii

Asanteni nawasilisha

We nae una ufundi huo unaenda kijijini kufanya si ungebaki hapa Dar ukakimbiza mdogo mdogo.

Anyways, kumbe Arusha ni kijijini, una taka ugomvi na machalii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kuna kaujinga fulani unako nilivo kusoma.
kijijini kutengeneza jina mpaka kufanikiwa kunachukua mda na mda ukifika basi kila mtu hata kupa kazi wewe na si mwingine.
kijijini unaweza kuanza na ziro na ukafikia kuwa hero.sababu mtaji utakuwa haraka mda unavozidi kwenda na utakuwa na ushindani mdogo.
kijijini unaweza kuwa wewe ndio muhasisi hapo nenda vijiji vingi utakuta walioanzisha kitu ndio matajiri wa hapo vijijini.
Tajiri wa kijiji?!!

Sasa ushindani si ndio kiwanda cha ubunifu, unaogopa ushindani uta excel vipi kazi zako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom