Elections 2010 Nilikuwa mkereketwa wa CHADEMA lakini nimejitoa

Elections 2010 Nilikuwa mkereketwa wa CHADEMA lakini nimejitoa

Mnafki mkubwa! siasa za ccm ni unafki mtupu, eti Ngoda naye alikuwa CHADEMA, vp ulinyimwa viti maalum? Pole!
 
Kwako Zawadi
Nataka nikununulie zawadi ya lipstick, ili lips zako zipendeze.

Huwezi jua, soko lako likaongezeka mara dufu.
 
Uwe mkweli. Ulitumwa na mafisadi kutoka chama chao wanachokipenda ili uingine Chadema na kuvuruga. Inaonekana mbinu hiyo ilishindikana ndiyo maana ukaondoka.

Pipooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooz .............

Mwaka huu, mtasema mengi.
 
Mimi nakuunga mkono kujitoa chadema kwani inaonekana hata tanzania umejitoa kwani hujui umaarufu wa dr. Slaa.
Samahani mara ya mwisho kuwa tanzania ilikuwa lini?
 
Huyu anayejiita Zawadi gift what ever kwenda zako usitutishe hapa kwani ulipojiunga na chama ulituambia iweje leo uje kututangazia????? Nendeni bana kwani nani anawataka hapa.. Uongo wako umeonekana hahaha eti nimeamua kukihama chama cha CHADEMA yaani mnakuwa waongo mpaka siku mnarudi kwake yeye aliyewaleta. Tuondolee pumba zako hapa
 
cham hiyari yako kaka au dada! kajiunge na akina lowasa na rostamu la aziz kule kuna mgawo wa vitenge na kofia. huku tunagawa nafsi zetu kwa ajili ya Taifa letu

ROHO ZETU TUMEZIWEKA REHANI KWA AJILI YA TAIFA LETU KUPITIA KWAKO EWE DR SLAA, USIOGOPE TUPO NAWE
 
Nilipojua Kampeni za Mbowe na comany yake ya Chama kumuandaa Mh Slaa kuwa ndio Mgombea wa urais, nilishtushwa sana. Kwa vile sikuwa na uwezo wa kutengua uchaguzi wao (kwa ukilitimba wao ndani ya chama) niliamua kujitoa.

Mnajua huyu mtu namfahamu, hana uwezo kabisa wa kuongoza nchi hii yenye wakazi zaidi ya watu 35 milioni. Uwezo wake kuongoza jimbo tu, na hivyo alistahili kuwa mbunge mpaka atapostaafu mwenyewe.

Sababu tano zinazomfanya kutofaa kuwa Rais:

1. Ataigawa nchi vibaya sana.

2. Atarudisha nyuma Demokrasia (huyu ni dikiteta no 1)

3. Si maarufu Dar wala Dodoma. sijui atakaa ikulu ya wapi.

4. Ndie mbunifu wa mavadhi ya CHADEMA (ishara ya vurugu)

5. Hana sera yeyote ile ya uchumi.


Hayo ni machache tu lakini udhaifu wake ni mwingi mno.

Ni heri kubaki bila chama kuliko kumpigia debe Mh Slaa. Ndio maana niliamua kukihama chama.



Pole sana mkuu, Unfortunately, you have not communicated. There is no message
 
Nilikuwa mkereketwa wa CHADEMA



Wakereketwa wako Chama Cha Mafisadi, Kwanza mnakereketwa nini?

Katika CHADEMA hatuna wakereketwa bali wafuasi.
 
Nilipojua Kampeni za Mbowe na comany yake ya Chama kumuandaa Mh Slaa kuwa ndio Mgombea wa urais, nilishtushwa sana. Kwa vile sikuwa na uwezo wa kutengua uchaguzi wao (kwa ukilitimba wao ndani ya chama) niliamua kujitoa.

Mnajua huyu mtu namfahamu, hana uwezo kabisa wa kuongoza nchi hii yenye wakazi zaidi ya watu 35 milioni. Uwezo wake kuongoza jimbo tu, na hivyo alistahili kuwa mbunge mpaka atapostaafu mwenyewe.

Sababu tano zinazomfanya kutofaa kuwa Rais:
Post yako iko vague sana, unaona vipi utueleze kiundani zaidi?

1. Ataigawa nchi vibaya sana.
Ataigawa vipi nchi? Maelezo zaidi tafadhali.

2. Atarudisha nyuma Demokrasia (huyu ni dikiteta no 1)
Naomba utueleezee zaidi tafadhali.

3. Si maarufu Dar wala Dodoma. sijui atakaa ikulu ya wapi.
Kwani hapa wananchi wanachagua umaarufu ama uwezo wa kuongoza? Mwaka 1995 BWM hakuwa maarufu na bado alichaguliwa. Kweli watanzania tumeishiwa kiasi hiki mpaka tunachagua watu kwa vigezo vya umaarufu na sio utendaji wao wa kazi?

4. Ndie mbunifu wa mavadhi ya CHADEMA (ishara ya vurugu)
Mavadhi au mavazi?

5. Hana sera yeyote ile ya uchumi.
Slaa kama Slaa hana sera ya uchumi kwa sababu hagombei kama mgombea binafsi bali kwa kutumia ticket ya CHADEMA kwa hiyo nadhani mjadala unatakiwa uwe kuhusu sera ya uchumi ya chama chake.

Hayo ni machache tu lakini udhaifu wake ni mwingi mno.
Haya machache uliyoyaweka hayana mshiko tuongezee hayo mengine.
 
Zawadi ngonda pole kwa nadharia zako. Katika mambo uliyotaja ya kujitoa chadema ujaongea neno la maana ila tu umepangilia maneno vizuri kutoka katika kamusi ya kiswahili. Ni aibu kwa mtu mzima kusema maneno kama ayo. Ni bora ungezua tuhuma dhidi ya Mh. Dr wa kweli alaf ukafanya sababu ya kujitoa kuliko kuandika tu unachojisikia. Wenye akili timamu watashangaa mambo yako. Haukuwa mkereketwa kwani mkereketwa ina maana yake sio ili mradi kujiita mkereketwa tu. Zawadi wapo wengi kama wewe wasioweza siasa wamekaa kimya,sio lazima uwe ktk siasa waweza jaribu kitu kingne. Zawadi ukijitoa kabidhi kadi ili baada ya uchaguzi tujue Chadema imepoteza Mamluki wangapi. Ila usiseme umetimiza haki yako ya kisiasa au kidemokrasia,hamna haki yoyote inayosema kuwa ni haki ya 'kujitoa'. Huo ni uamuzi Zawadi wala sio demokrasia. Ushauri ntakupa bure,kumbuka Tanzania tuna maadui wanne: ujinga,maradhi,...na ufisadi. Jaribu kumfukuza adui aliyekujia Zawadi!
 
huyu Zawadi ngoda anahitaji medical attention ....as a medic nipo tayari kumtibu bure
 
Hoja zangu kujibu hoja zako kuhusu mabadikiko Tanzania ni kama ifuatavyo:
1. Ataigawa nchi vibaya sana: Nchi tayari imeshagawanyika vibaya kwa matabaka ya walio nacho na wasio nacho. Hii ni rahisi kuleta mapigano kwani wasio nacho watachoka kuona walio nacho tu ndio wanaongoza, wanaishi kitajiri na kupata huduma bora za afya (private hospitals), elimu (academy schools), mazoezi ili wawe na afya nzuri (gym), etc. Watanzania wengi kwa sasa wanakuwa ‘marginalized’ kitabaka na historia sehemu nyingine inaonesha, uki –marginalize watu baada ya muda wataanza mapambani ya mabadiliko (kama sasa Tanzania) na kama hakuna njia watatumia nguvu. Wapinzani wanatetea sera zinazoelekeza kuondoa hayo matabaka ya masikini na matajiri
2. Atarudisha nyuma Demokrasia (huyu ni dikiteta no 1): Demokrasia tayari iko nyuma kwa sasa kwani vyama nya upinzani havina uhuru chini ya msajili wa vyama na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi aliyechaguliwa na Rais. Vile vile mgawanyo wa mihimili mitatu ya dola: serikali, mahakama na bunge hauko wazi sababu rais ndio anateua jaji mkuu. Ili demokrasia idumishwe katiba yote ya sasa inabidi ipitiwe na kufanyiwa mabadiliko. Kwa sababu katiba hiyo ilitokana na chama tawala kwa siku zilizopita, kwa sasa inabidi ipitiwe kwa kushirikisha wananchi wote ‘referendum’ kama Kenya. Kwa hiyo si kweli kwamba chama cha CCM ndio kinaweza kudumisha demokrasia kwa sababu kwa sasa hatuna demokrasia chini katiba ya ki dikteta inayompa rais madaraka mengi
3. Si maarufu Dar wala Dodomasijui atakaa ikulu ya wapi: Are you a Great Thinker? - Hii si hoja ya kisomi kwa sababu tatu muhimu: Kwanza, walipokuwa wanatetea masuala ya kitaifia kwenye bunge na kufanikiwa kuleta mabadiliko, suala la kwamba wanakaa wapi halikuwa na maana; Pili hoja inatetea ubaguzi na ‘u- mkoa’ kwa maana ya kwamba ili mtu aweze kuwa kiongozi bora Tanzania ni lazima awe maarufu Dar na Dodoma. Je, wakati anagombea urais, Mkapa alikuwa na umaarufu kwenye hizo sehemu?; tatu, rais anaongoza serikali ambayo inaweza kuundwa na watu kutoka sehemu yoyote Tanzania ikijumuishwa Dar na Dodoma
4. Ndie mbunifu wa mavadhi ya CHADEMA (ishara ya vurugu): Are you a Great Thinker? Hii si hoja ya kisomi kwa sababu suala la kuhusisha mavazi na ishara ya vurugu halina uzito. Ni nani alikuambia yeye Slaa ndio kabuni hayo mavazi? Hata kama ni yeye kabuni, ni kwa namna gani hayo mavazi yanahusishwa na vurugu? Ni mavazi ya aina gani ambayo hayahusishwi na vurugu? Je, unaona ni sawa kwa mwanasiana wa sasa wa Tanzania kutembelea mwananchi masikini wa kutupwa akiwa amevaa suti ya shs. laki sita, kiatu cha laki mbili na gari la mamilioni?
5. Hana sera yeyote ile ya uchumi: Tatizo kubwa tulilo nalo ni ubadhilifu kwa maana ya kwamba viongozi wanafanya maamuzi yenye maslahi yao badala ya maslahi ya taifa. Sera nyingi za CCM kama za Mkukuta, Mkurabita, etc hazijaweza kubadilisha maisha ya Mtanzania wa kawaida. Hatutaki sera za kinadharia kwa sasa tunataka maamuzi yatakayobadilisha maisha ya watu wa chini na mabadiliko yakaonekana. Kwa miaka 15 sasa hali ya watu kijijini kwangu iko vile vile hakuna mabadiliko ingawa kumekua na sera nyingi tu zenye maneno matamu. Shule zimejengwa ndio lakini kwa wanakijiji kuweza kula mlo waliokuwa wanakula miaka 15 iliyopiwa kwa sasa ni ndoto. Mabadiliko tunayoyaona ni mijini tu kwenye watanzania wachache lakini vijjini hali ni mbaya. Kwa nini mpaka leo hatutumii maji ya Lake Victoria, Tanganyika, Nyasa kwa umwagiliaji Tanzania nzima? Mbona Egypt wanafaidika kwa Mto Nile? Haya mambo ni ‘practical’ yanahitaji watu wanaofanya matendo zaidi ya maneno maneno mengi. Kwa kipindi kirefu sera za CCM zimekuwa za maneno tu na tunaona kwa macho yetu wanaoneemeka ni wachache wa mijini. Kwa walio wengi umasikini uko pale pale

Haya ndio majibu yangu ya hoja zako. Sasa soma halafu utoe hoja kujibu majibu yangu kwa dondoo hizi hizi ili tuendelee na mjadala huu mzuri kama Great Thinkers
Kwanza nakupongeza sana, na kwa ukweli una alama 10/10 kwa upande wangu.

Sioni aibu kusema kwa siku mbili toka hii thread iwe hewani, hakuna aliyejibu hoja zangu. Mtu mwingine aliyekaribia kujibu hoja ni 'babadesi' kuhusu mavazi ambae yeye nilimpa alama 2/10. Waliobaki wengi wamenitisha na kuishia kutukana tu. Matu.si si asili yangu na hata kama utaniona nimetoka nje ni kuhusu kutofautiana kimtazamo tu na wala si ma.tusi

1. Nakubaliana nawe ila mgawanyo unaouzungumzia nimatokeo ya kukubali ubepari ambapo watanzania wote tumakubali reform hiyo. lakini Mh Slaa akiingia madarakani mgawanyo utazidi mara mbili kwa sababu hatapata support bungeni na atalazimisha kukaa na wabunge 30% kwa nguvu. Ktk nchi zilizooendele mambo yakienda kombo wanajiuzulu mfano(Baruso- Italy)- sasa huyu atafanya nini.

2. Na 30% hawezi kuleta demokrasia hilo sina haja hata ya kulijadili.

3. Umetoa mfano wa Mkapa, lakini unajua Mkapa aliua wangapi Dar. Wengine hata alikuwa hasalimiani nao kwa kushikana mikono, ukweli Makamba na Mahita ndio walikuwa wasemaji wakuu wa Mkapa Dar. Unaweza ukafikiri hilo Dogo, lakini hata Mwl alitumia mbinu nzuri sana ya kuishika Dar (ni mjadala mrefu huu staingia kiundani). UD walipoandamana wakati wa Mwinyi aliwaita wazee wa Dar na kuwa hutubia, halikadhalika Kikwete mambo yalipomuendea kombo na wafanyakazi. Gadafi alihamisha makao makuu kwenda Tripoli baada ya kuchukiwa kule makao makuu-fuatilia.

4. BabaDesi kashamaliza, mimi sina la kusema. Hivi unahisia gani ukiyaona mavazi ya fuatayo: Mgambo, JKT, Polisi, JWTZ. Tunaweza kuiwa katika hisia tofauti, lakini mimi huwa najua kuna jambo limetokea. Wahuni huwaita wazee wa kazi.

5. Nakubaliana nawe, lakini hapa kazi ipo. Kusema bungeni ni kitu kingine lakini kuwa katika utendaji ni jambo jingine kabisa. Hii ni jinsi mimi ninavyomuona huyu Mheshimiwa, na ndio maana nimesema mara nyingi kuwa bado ninamkosa kama mbunge. Hapa tunaweza tukatofautiana lakini si kitu na ndio maana ya kura.

Any way nimejibu kifupi sana ili nisiwachoshe wasomaji.
 
Kwanza nakupongeza sana, na kwa ukweli una alama 10/10 kwa upande wangu.

Sioni aibu kusema kwa siku mbili toka hii thread iwe hewani, hakuna aliyejibu hoja zangu. Mtu mwingine aliyekaribia kujibu hoja ni 'babadesi' kuhusu mavazi ambae yeye nilimpa alama 2/10. Waliobaki wengi wamenitisha na kuishia kutukana tu. Matu.si si asili yangu na hata kama utaniona nimetoka nje ni kuhusu kutofautiana kimtazamo tu na wala si ma.tusi

1. Nakubaliana nawe ila mgawanyo unaouzungumzia nimatokeo ya kukubali ubepari ambapo watanzania wote tumakubali reform hiyo. lakini Mh Slaa akiingia madarakani mgawanyo utazidi mara mbili kwa sababu hatapata support bungeni na atalazimisha kukaa na wabunge 30% kwa nguvu. Ktk nchi zilizooendele mambo yakienda kombo wanajiuzulu mfano(Baruso- Italy)- sasa huyu atafanya nini.

2. Na 30% hawezi kuleta demokrasia hilo sina haja hata ya kulijadili.

3. Umetoa mfano wa Mkapa, lakini unajua Mkapa aliua wangapi Dar. Wengine hata alikuwa hasalimiani nao kwa kushikana mikono, ukweli Makamba na Mahita ndio walikuwa wasemaji wakuu wa Mkapa Dar. Unaweza ukafikiri hilo Dogo, lakini hata Mwl alitumia mbinu nzuri sana ya kuishika Dar (ni mjadala mrefu huu staingia kiundani). UD walipoandamana wakati wa Mwinyi aliwaita wazee wa Dar na kuwa hutubia, halikadhalika Kikwete mambo yalipomuendea kombo na wafanyakazi. Gadafi alihamisha makao makuu kwenda Tripoli baada ya kuchukiwa kule makao makuu-fuatilia.

4. BabaDesi kashamaliza, mimi sina la kusema. Hivi unahisia gani ukiyaona mavazi ya fuatayo: Mgambo, JKT, Polisi, JWTZ. Tunaweza kuiwa katika hisia tofauti, lakini mimi huwa najua kuna jambo limetokea. Wahuni huwaita wazee wa kazi.

5. Nakubaliana nawe, lakini hapa kazi ipo. Kusema bungeni ni kitu kingine lakini kuwa katika utendaji ni jambo jingine kabisa. Hii ni jinsi mimi ninavyomuona huyu Mheshimiwa, na ndio maana nimesema mara nyingi kuwa bado ninamkosa kama mbunge. Hapa tunaweza tukatofautiana lakini si kitu na ndio maana ya kura.

Any way nimejibu kifupi sana ili nisiwachoshe wasomaji.

Wee interview ilikwendaje ile kazi ya housegirl kwa Mwaarabu wa JF?
 
nafkiri amesema alikuwa mkereketwa wa chadema na wala si mwanachama wa chadema.. sasa mnamuuliza uwanachama wake atoe ushahidi si wa waelewi.. kwani hata hao watu wachache watakaopigia kura chadema October 31st sio wote ni wanachama wenye kadi za chadema.

CHAGUWA KIKWETE CHAGUWA CCM ..
 
Nilipojua Kampeni za Mbowe na comany yake ya Chama kumuandaa Mh Slaa kuwa ndio Mgombea wa urais, nilishtushwa sana. Kwa vile sikuwa na uwezo wa kutengua uchaguzi wao (kwa ukilitimba wao ndani ya chama) niliamua kujitoa.

Mnajua huyu mtu namfahamu, hana uwezo kabisa wa kuongoza nchi hii yenye wakazi zaidi ya watu 35 milioni. Uwezo wake kuongoza jimbo tu, na hivyo alistahili kuwa mbunge mpaka atapostaafu mwenyewe.

Sababu tano zinazomfanya kutofaa kuwa Rais:

1. Ataigawa nchi vibaya sana.

2. Atarudisha nyuma Demokrasia (huyu ni dikiteta no 1)

3. Si maarufu Dar wala Dodoma. sijui atakaa ikulu ya wapi.

4. Ndie mbunifu wa mavadhi ya CHADEMA (ishara ya vurugu)

5. Hana sera yeyote ile ya uchumi.


Hayo ni machache tu lakini udhaifu wake ni mwingi mno.

Ni heri kubaki bila chama kuliko kumpigia debe Mh Slaa. Ndio maana niliamua kukihama chama.



1. Demokrasia imeshachakachuliwa na JK tayari - kungekuwa na demokrasia angewanyanyasa WAZEE wa watu kwa HAKI yao?? mbona MKAPA aliwapa kiasi?? ameshindwa nini kumalizia zilizobaki??? JK ni dictotor no. 1 aliyejificha kwenye nguo za rangi ya kijani

2. Eti Slaa sio maarufu Dar na Dodoma - ha ha haaaaaaaa - we unataka awe maarufu ki vipi??? na kwanini Dar na Dodoma tu??? yaani great thinker upeo wako wa kuwaza ni Dar na Dodoma - pole sana

3. Eti amebuni sare za chadema - whaaaaaaaaaat!!!! sie tunaongelea maendeleo ya nchi wewe unaongelea mavazi - sasa hiyo sare (tshirts na kofia za kijani na njano) ndio zinakusaidia nini???? mavazi sio TIJA wala HOJA - sie tunataka MABADILIKO period!!! na CCM imechemsha - imeshindwa kuyaleta - RUSHWA too much - UBADHIRIFU too much URASIMU too much - UONGO too much -

Hivi mtu unaandika eti mei nimeacha kuwa chama fulani - so what??????????????? thats your own business - UTAJIJUA MWENYEWE NA KUHANGAIKA KWAKO - wenzio ndio kwanza tunatoa michango kwa ajili ya CHADEMA - DR SLAA YUKO JUU - JUU - JUU ZAIDI!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kwanza nakupongeza sana, na kwa ukweli una alama 10/10 kwa upande wangu.

Sioni aibu kusema kwa siku mbili toka hii thread iwe hewani, hakuna aliyejibu hoja zangu. Mtu mwingine aliyekaribia kujibu hoja ni 'babadesi' kuhusu mavazi ambae yeye nilimpa alama 2/10. Waliobaki wengi wamenitisha na kuishia kutukana tu. Matu.si si asili yangu na hata kama utaniona nimetoka nje ni kuhusu kutofautiana kimtazamo tu na wala si ma.tusi

Useless..
1. Nakubaliana nawe ila mgawanyo unaouzungumzia nimatokeo ya kukubali ubepari ambapo watanzania wote tumakubali reform hiyo. lakini Mh Slaa akiingia madarakani mgawanyo utazidi mara mbili kwa sababu hatapata support bungeni na atalazimisha kukaa na wabunge 30% kwa nguvu. Ktk nchi zilizooendele mambo yakienda kombo wanajiuzulu mfano(Baruso- Italy)- sasa huyu atafanya nini.
Mi ni mtz na sijakubali hiyo reform..

Mushrikin..umekuwa sheikh Yahya?? lolz..hizo 30 % umezitoa wapi, na ataigawa nchi mara 2 umeitoa wapi? whats is ur supporting argument?

BTW, Baruso ndio kinyangarika gani..? bwe he he he..
2. Na 30% hawezi kuleta demokrasia hilo sina haja hata ya kulijadili.
Ni kweli huezi kujadili assumption kwa sababu ina-exists kwenye kichwa chako tu, it is not a real data.

3. Umetoa mfano wa Mkapa, lakini unajua Mkapa aliua wangapi Dar. Wengine hata alikuwa hasalimiani nao kwa kushikana mikono, ukweli Makamba na Mahita ndio walikuwa wasemaji wakuu wa Mkapa Dar. Unaweza ukafikiri hilo Dogo, lakini hata Mwl alitumia mbinu nzuri sana ya kuishika Dar (ni mjadala mrefu huu staingia kiundani). UD walipoandamana wakati wa Mwinyi aliwaita wazee wa Dar na kuwa hutubia, halikadhalika Kikwete mambo yalipomuendea kombo na wafanyakazi. Gadafi alihamisha makao makuu kwenda Tripoli baada ya kuchukiwa kule makao makuu-fuatilia.
Pointless..makazi ya rais hayana mafungamano yeyote na popularity ktk eneo la Ikulu, unless kama kiongozi mhusika aliingia Ikulu kwa mtutu au ujambazi wa kura. Kiongozi aliyechaguliwa kidemokrasia hana shaka kwenda popote,kuishi popote au kukutana na yeyote..and by the way huna empirical data kuthibisha kwamba ktk wagombea wetu ni yupi yupo popular wapi so far, unless utuambie wewe ni mfuga majini.
4. BabaDesi kashamaliza, mimi sina la kusema. Hivi unahisia gani ukiyaona mavazi ya fuatayo: Mgambo, JKT, Polisi, JWTZ. Tunaweza kuiwa katika hisia tofauti, lakini mimi huwa najua kuna jambo limetokea. Wahuni huwaita wazee wa kazi.
Pumba.

Kumbukumbu (verifiable) zinaonesha Chadema wameanza kuvaa hayo mavazi kitambo sana na si kutokana na msukumo wa Slaa kugombea urais. Kuifungamanisha hoja hii na Slaa kugombea urais dhahiri ni ukichaa. Btw, hata kama Chadema wangevaa kombati za kikomandoo, labda tuchungulie ni nani so far ameshamwaga damu?? wanajf watajibu kwa niaba yako.
5. Nakubaliana nawe, lakini hapa kazi ipo. Kusema bungeni ni kitu kingine lakini kuwa katika utendaji ni jambo jingine kabisa. Hii ni jinsi mimi ninavyomuona huyu Mheshimiwa, na ndio maana nimesema mara nyingi kuwa bado ninamkosa kama mbunge. Hapa tunaweza tukatofautiana lakini si kitu na ndio maana ya kura.
Thibitisha hoja yako ya awali kwamba Slaa hana sera ya Uchumi, usipaparike kama kuku kishingo alopigwa jiwe la utosini.
Any way nimejibu kifupi sana ili nisiwachoshe wasomaji.
..si lolote si chochote
 
Hoja zangu kujibu hoja zako kuhusu mabadikiko Tanzania ni kama ifuatavyo:
1. Ataigawa nchi vibaya sana: Nchi tayari imeshagawanyika vibaya kwa matabaka ya walio nacho na wasio nacho. Hii ni rahisi kuleta mapigano kwani wasio nacho watachoka kuona walio nacho tu ndio wanaongoza, wanaishi kitajiri na kupata huduma bora za afya (private hospitals), elimu (academy schools), mazoezi ili wawe na afya nzuri (gym), etc. Watanzania wengi kwa sasa wanakuwa ‘marginalized’ kitabaka na historia sehemu nyingine inaonesha, uki –marginalize watu baada ya muda wataanza mapambani ya mabadiliko (kama sasa Tanzania) na kama hakuna njia watatumia nguvu. Wapinzani wanatetea sera zinazoelekeza kuondoa hayo matabaka ya masikini na matajiri
2. Atarudisha nyuma Demokrasia (huyu ni dikiteta no 1): Demokrasia tayari iko nyuma kwa sasa kwani vyama nya upinzani havina uhuru chini ya msajili wa vyama na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi aliyechaguliwa na Rais. Vile vile mgawanyo wa mihimili mitatu ya dola: serikali, mahakama na bunge hauko wazi sababu rais ndio anateua jaji mkuu. Ili demokrasia idumishwe katiba yote ya sasa inabidi ipitiwe na kufanyiwa mabadiliko. Kwa sababu katiba hiyo ilitokana na chama tawala kwa siku zilizopita, kwa sasa inabidi ipitiwe kwa kushirikisha wananchi wote ‘referendum’ kama Kenya. Kwa hiyo si kweli kwamba chama cha CCM ndio kinaweza kudumisha demokrasia kwa sababu kwa sasa hatuna demokrasia chini katiba ya ki dikteta inayompa rais madaraka mengi
3. Si maarufu Dar wala Dodomasijui atakaa ikulu ya wapi: Are you a Great Thinker? - Hii si hoja ya kisomi kwa sababu tatu muhimu: Kwanza, walipokuwa wanatetea masuala ya kitaifia kwenye bunge na kufanikiwa kuleta mabadiliko, suala la kwamba wanakaa wapi halikuwa na maana; Pili hoja inatetea ubaguzi na ‘u- mkoa’ kwa maana ya kwamba ili mtu aweze kuwa kiongozi bora Tanzania ni lazima awe maarufu Dar na Dodoma. Je, wakati anagombea urais, Mkapa alikuwa na umaarufu kwenye hizo sehemu?; tatu, rais anaongoza serikali ambayo inaweza kuundwa na watu kutoka sehemu yoyote Tanzania ikijumuishwa Dar na Dodoma
4. Ndie mbunifu wa mavadhi ya CHADEMA (ishara ya vurugu): Are you a Great Thinker? Hii si hoja ya kisomi kwa sababu suala la kuhusisha mavazi na ishara ya vurugu halina uzito. Ni nani alikuambia yeye Slaa ndio kabuni hayo mavazi? Hata kama ni yeye kabuni, ni kwa namna gani hayo mavazi yanahusishwa na vurugu? Ni mavazi ya aina gani ambayo hayahusishwi na vurugu? Je, unaona ni sawa kwa mwanasiana wa sasa wa Tanzania kutembelea mwananchi masikini wa kutupwa akiwa amevaa suti ya shs. laki sita, kiatu cha laki mbili na gari la mamilioni?
5. Hana sera yeyote ile ya uchumi: Tatizo kubwa tulilo nalo ni ubadhilifu kwa maana ya kwamba viongozi wanafanya maamuzi yenye maslahi yao badala ya maslahi ya taifa. Sera nyingi za CCM kama za Mkukuta, Mkurabita, etc hazijaweza kubadilisha maisha ya Mtanzania wa kawaida. Hatutaki sera za kinadharia kwa sasa tunataka maamuzi yatakayobadilisha maisha ya watu wa chini na mabadiliko yakaonekana. Kwa miaka 15 sasa hali ya watu kijijini kwangu iko vile vile hakuna mabadiliko ingawa kumekua na sera nyingi tu zenye maneno matamu. Shule zimejengwa ndio lakini kwa wanakijiji kuweza kula mlo waliokuwa wanakula miaka 15 iliyopiwa kwa sasa ni ndoto. Mabadiliko tunayoyaona ni mijini tu kwenye watanzania wachache lakini vijjini hali ni mbaya. Kwa nini mpaka leo hatutumii maji ya Lake Victoria, Tanganyika, Nyasa kwa umwagiliaji Tanzania nzima? Mbona Egypt wanafaidika kwa Mto Nile? Haya mambo ni ‘practical’ yanahitaji watu wanaofanya matendo zaidi ya maneno maneno mengi. Kwa kipindi kirefu sera za CCM zimekuwa za maneno tu na tunaona kwa macho yetu wanaoneemeka ni wachache wa mijini. Kwa walio wengi umasikini uko pale pale

Haya ndio majibu yangu ya hoja zako. Sasa soma halafu utoe hoja kujibu majibu yangu kwa dondoo hizi hizi ili tuendelee na mjadala huu mzuri kama Great Thinkers

Heshima kwako admissionletter,

Good analysis.JF inahitaji watu kama wewe wenye uwezo wa kutoa majibu yanayoendana na hali hasi ya Tanzania.
 
Utakuwa Umenyimwa Viti Maalumu Umeanza Kuropoka sasa teh teh teh
Kuna Wakati Kukaa Kimya Ni Busara Kuliko Kuropoka ropoka
Hujaeleza Sababu Za Msingi Hapo Juu Umeweka Umbea Tu
:dance:
 
Tanzania hatutaki kuongozwa na Rais maarufu, tunataka kuongozwa na RAIS BORA.
 
Back
Top Bottom