Nilimkopesha mtaji akaenda kumwambia mke wangu yeye ni mke mwenza

Mamujay

Senior Member
Joined
Dec 24, 2022
Posts
149
Reaction score
345
Wazee hakuna binadamu amezaliwa na roho mbaya tunafundishana nimeamini.

Leo ndoa haikaliki kisa tu msaada na huruma yangu iliniponza, kiukweli nilimla siku 1 ila sasa anaharibu nyumbani. Hela yangu ameshanilipa sasa balaa ni hapo anasema nilimhonga na anatamba kwa mke wangu yeye ni mke mwenza na hatuna mawasiliano.

Hivi mtu kama huyu nimfanyaje?
 
Huyo alitaka umwachie hizo Ela, kurudisha kimemuuma ndomana maneno yamemtoka kutaka kuharibu ndoa yenu, mi ndomana siku hizi kumkopesha mgumu kweli, ukidai chako ugomvi tatizo.
 
Wanawake wa nje wako makini sana kutaka kuishi kindoa, Wanawake wa ndani hawatambui hilo, infacts wanawake wa ndani wangelitambua hili wangekuwa wanatulamba miguu,binafsi nimekoma hata kuwatania midada ya kitaa ilisha niletea dhahma, kibaya wanakuja na kugonga home bila hofu kabisa.
 
tumia akili mkuu, mwambie mkeo huyo demu anakutaka muda tu huna mpango nae hivyo kaona aje akuharibie, atapambana na mwanamke mwenzie,
 
Usiingilie ugomvi wa wanawake, utateseka.
Mpe mkeo mkasa ulivyo, mengine waachie wenyewe watamalizana wao.
 
Mkuu
Kaa kimya kwanza
Usimjibu kitu mkeo hadi atulie na kama anaona ndoa imemshinda mwambie afuate ushauri wa huyo aliyejipeleka kama mke mwenza kisha ishi zako kwa amani.

Hakuna kiumbe mwenye roho huru kama mwanamke. Akiamua lake hata kama si kweli atalisimamia.

Tibu ndoa ikishindikana usisubiri kufa taratibu kwa sumu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…