Nilipoingia mahabusu kwa kubambikwa kesi ya kuiba na kuvunja

Nilipoingia mahabusu kwa kubambikwa kesi ya kuiba na kuvunja

Umeweka sana msisitizo kwenye marinda, hadi napata wasiwasi huenda kweli yalitatuliwa.
 
Madongo ka yote Mara malinda yalikua salama ? Mara mambo mengi story zenye part2 zisitishwe OK fine
Tuendelee mida iyo ya usiku tukiwa tumelala na wengne wapo na story nikaamka nikajiunga kwenye story nilikua msikilizaji tu mladi muda uende lakini usingiz sio mchezo ukatupitia kuna muda watu wote kimya kabisa

Apo natamani kukuche waje wanitoe mida ya saa kumi na moja alafajiri ile azana akaja askari akauliza nani anataka kutoka jamaa flani wawili wakawai fasta mlangoni pale akasema nyie ndio wajanja akawatoa akafunga mlango.

Tukajiuliza unatokaje kirahisi ivi baadae wakarudishwa kumbe walienda kudekishwa na kufagia nje
asubhi kabisa purukushani zikaanza ndugu wanakuja kutoa jamaa zao mule
Majina yanaitwa kama ni kunywa chai utarudi kama kutoka ndio aurudi.

Ghafla nikasikia jina langu ibu bin flani fasta nikasogea mlangoni nikatolewa nikakuta mother yupo na mam mkubwa na yule dingi, dingi akauliza kwa askari sasa uyu ndio kesi ya kuiba na kuvunja afande akajibu mzee sio Mimi hii kesi ina wenyewe wakti nimesimama pale yule afande akasema dogo kesi yako ngumu
Mhmm nikashtuka ngumu kivipi

Akasema kuiba na kuvunja kesi kubwa na palipoibwa hapo sio poa nikaitwa kwa mmama mmoja ivi mwana sheria nikaongea nae nae nikawa simuelewi wala nini baada ya kumuelezea nae akaguna tu na kusema mungu atakusaidia usiwe na was wasi nikarudi lumande nikapewa na chai mule ndani kampani yote tunapunguziana kidogo kidogo fresh.

Nilikaa mule watu wengine wanatoka wengne wanabaki kuna jamaa mmoja dereva wa superfeo sijui alifanya nni kakaa wiki nzima akielewki akasema Leo sikubali
Akajitupa chini akaanza kugalagala kwamba anaumwa ila alikua anakojoa damu, mule ndani mazingira ni machafu sana aligaragara pale chini mpaka anaitwa askari akaja
Yule askari akasema mengne yatajifia humu yashaoza wakambeba mpaka nje wakampeleka hospital.

Sasa 7 azana sioni dalil ya kutoka saa kumi nayo azana kimya mhm nikaona hapa kuna hatari ya kulala tena itakuaje,nikawaza ikivuka Leo sijatoka kesho lazima niumwe nikalazwe hosptali uko potelea mbali ata nikifungwa pingu poa tu
Wale majambazi waliofungwa pingu na kuja nao kule gest nikawaona sasa walikua chumba kingne nikajua kabisa hawa ndio wamesababisha mim kulala humu kudadeki apo nipo kimya nawaza siku ya pili tena inikute humu ahaa kudadeki,

Akaja afande victor akaita Yale majamabaz ya kuvunja wakatoka wale jamaa wapo na pingu yao mkononi akaita na meneja nikatoka pale kaunta nikapewa simu yangu na vitu vyangu vyote tukaingizwa kwenye gari wote safari tena mhm sikujua tunaenda wapi pamoja na ma mother wangu na mzee nikaona akuna shida na hawa wapo sio ishu.

Tukaenda makao makuu ofisi ya upelelez karibu na kwa mkuu wa mkoa ghorofani mahojiano yakaanza askari anawauliza wale jamaa uyu mnamjua mmoja alikua mzee ivi sio sana mwngne kijana, mzee alikua mkaidi anapewa vitasa mhm yule mshkaji akasema mzee tuseme ukweli tutaumia hapa tukiulizwa tuanchojua tuseme

Ndio akawauliza uyu mnamjua wakasema atumjui nikasema afazali siku mlioenda pale gest mlimuona wakajbu atukumuona uyu.
Akaniuliza Mimi kwann unashirikiana na majambazi nikasema afande sijashirikiana na majambazi na si wajui hawa si umewasikia mwenyewe akasema kama wanakulinda si tutajuaje mmoja wao akasema uyu afande atumjui ile siku tumelala pale ni wahudumu tu ndio tunawakumbuka sio uyu atukumuona

Afande akasema kelele hapa nikatolewa nikapelekwa chumba kingne kutoa maelezo nikaanza kuhojiwa
iyo usiku ulikua wapi mpaka wanakuja nikawapa
A to Z maelezo yangu yaka andikwa yote karatasi mbili badae jioni saa kumi na mbili ndio nikatolewa kwa zamana na kupewa maagizo wahudumu waje watoe maelezo ili kusaidia ushahidi kwa polisi.

Nikaambiwa na nianze kuripoti kila baada ya siku tatu bila kukosa
Nikatoka mpaka home nikaoga kutoa nuksi wenyewe wanasema na nguo kufua.
Siku ya pili wahudumu nao walienda kuhojiwa sasa maelezo ya wahudumu ndio yalikua safi kwao polisi ila yangu ayakua na msaada sababu sikuwaona na ata wao awanijui.

Jama kesi yao walivunja stoo ya bia ya kampun ya breweries songea ipo maeneo ya masamala karibu na stendi kuu ya zamani na kuiba pesa kuna mtu aliwachoreshea mchongo inasemekana ni mlinzi.

Sababu za Mimi kuambiwa kesi ngumu ni bosi alimwaga pesa hao watu walio husika washikiliwe na bosi uyo ni boss STRAM anaitwa mi namjua kwa jina ilo hata zile gari zao za bia zimeandkiwa stram
Na jamaa Walishikwa kwa njia ya simu waliwakamatia shinyanga uko kitu kama icho kushikwa kwao ilikua ni mlinzi ambae anasema alipigwa na kufungwa kamba mikono nyuma ila sasa akatuma meseji kwa mtu kupitia simu yake

kavamiwa ndipo akashikwa unatumaje mesj mikono ipo nyuma ndio akataja wenzake na namba yao waka wa track na kuwashka wawili mmoja walimkosa alikua tandahimba nafikir maeneo ya mtwara baadae awakumuona tena kwnye trace zao nahisi alishtuka.

Sijui ikawaje kama walimshika au vipi nikaanza kuripoti siku ya kwanza wakasema uje tena siku flani
Ikawadia iyo siku nikaenda wanauliza we nan na una kesi gani nawajbu Sawa tumekuona ondoka nasepa bila kusahini wala chochote ila wengne wakawa wakija kuripoti wanasaini.
Baadae ikawa wiki na hatimae kila mwezi ila sasa kwanin kila nikiifika sisaini na wengne wote wanasaini kingne mimi wanashangaa una kesi gani ukiwaambia wanasema Sawa ondoka siku nyingne wanasema afande wako ayupo Mara we ulipoti kwangu nenda kwa flani ukienda uko nako wanasema we nenda zako unatuletea kiwingu uje siku nyingne.

Nikaona hapa naonaekana msukule na sijulikani kwanza kesi sio yangu wenye kesi wapo nikaacha kuripoti
Nikimuona afande victor mitaani uku nalala mbele namkwepa ivyo ivyo

Kuna siku njian tukakutana uso kwa uso niakaona hapa Leo kimbembe akauliza meneja upo mbona uonekani nikamwambia nipo afande vipi ujaleta majamabz mengine nikamwambia nipo makini saiz tukapiga story akasepa apo ndio nikapata kibali cha kua huru sasa kumbe swala la kulipoti lilisha sahaulika.

Mwaka 2020 wale wahudumu waliitwa mahakamani kwenda kutoa ushahidi mi sikuitwa kama nilivyosema maelezo yangu ayakua na msaada ila ya wahudumu ndio yalikua sahihi sana wao ndio waliwauhudumia siku iyo kesi ilihairishwa na kupangwa tarehe nyingne

Siku waliokuja gesti kulala wale majambazi walitoka usiku na ndio walienda kufanya tukio la kuiba pesa.
Na kuna mtu alikua kama ndio mfazili wao aliwalipia chumba na kila kitu pale gest na vyumba walivyo lala vilifatana namba 9 na 10.

Hao wahudumu mmoja ni mtu mzima kidogo mwingine binti alihetimia yupo vizuri kweli wale maafande bana karatasi ya uyu muhudumu binti ilikua inachunguzwa sana kumbe kuchukua namba bana na walikua wana msumbua sana mala njoo kituoni kuna maelezo inabidi utoe amna kitu wanataka mzigo tu ila aliniambia kati yao kuna mzee alimpitia na aliniambia uyo mzee ana puling ya hatari sijui alimnywea viaga alisema arudii tena kwake na mpaka pale lodge akawa anakuja kumbembeleza ampe mzigo tena.

Uyu mzee nikikutana nae njiani lazima aniulizie yule muhudumu wako yupo lazma tu
na pia afande mwngne na yeye alipita sema uyu Dada nae achengeshi swala ni mpunga tu.


Kashaulo
Upande wa malinda wakuu mahabusu swala la kuondoana malinda halipo kwa nijuavyo Mimi sijui wengne aya yanakua uko magerezani kwa wafungwa ndio ninavyo elewa.
Mwisho
Wewe meneja ulienda central banah ukawekwa lock up na sio magereza tofautisha hivi vitu
 
Wewe meneja ulienda central banah ukawekwa lock up na sio magereza tofautisha hivi vitu
Ni kweli mkuu central ila sijataja magereza au ndio mahubusu iyo iyo na gereza pia ? Na kama ni ivo basi mi nikajua mule mnaitwa mahabusu
 
Kweli lockup,mahabusu namuomba Mungu sana isinitokee na ndiyo maana ktk maisha yangu sijawahi kumshtaki mtu hata kwa balozi na si kwamba sikosewi,hata Sabaya pamoja na mabaya yake bado namuombea kwa Mungu amtoe mahabusu
 
Kuna ndugu yangu alishawahi kuwa katika mambo ya polisi,alisemaga tukiwa katika kikao yakuwa ukisikia nduguyo hapa amekamatwa na yupo kituoni mahabusu fanyeni hima mumtoe haraka sana palepale kabla ya kupelekwa mahabusu ya gerezani,alisema kule kuna hali mbaya tena alikazia ya kuwa kama nduguyo amekamatwa kama dhamani ni nyumba mtolee hapohapo awe huru uku mkishughulikia kesi yake
 
Back
Top Bottom