Nilipopanga kila siku akina mama wanashindana kufua halafu bili ya maji tunalipa sawa

Habari zenu ndugu zangu,

Lengo la kuleta malalamiko yangu ni kuonya wapangaji vilaza. Kuhusu wapangaji wanao shindana kufua sijui mnavaa Nini maana daily kufua afu bill tunalipa wote sawa.

Panga nyumba ambayo hakuna share ya bills za maji wala umeme.

Wamama na matumizi ya maji ni pipa na mfuniko.

Wama matumizi ya umeme ni kwao ,anapiga pasi hadi jinzi ,akienda dukani hadi mtandio anapiga pasi,kublendi juisi kwao ni dakika 0 ,kuangalia tamthilia ni PIE ,anaweza akawa anapika TV akaiacha ON huku hakuna anayeangalia.

Hao watu kubana matumizi kwao ni mtihani.
 
Dawa ni kuhama bora hao wanafua mi wapangaji wenzangu ilikuwa wanawaachia watoto wanachezea maji halafu nalipa nao sao nikaona huu ujinga nikahama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…