Cvez
JF-Expert Member
- May 19, 2018
- 4,405
- 13,411
Hahahaha hata kwenye kimasikhara kuna wadau wa nitaendeleanikija kusoma story za ITAENDELEA niiteni mbwaaaa
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hahahaha hata kwenye kimasikhara kuna wadau wa nitaendeleanikija kusoma story za ITAENDELEA niiteni mbwaaaa
Natia nukta hapaUMUGHAKA Lete Mambo Muraaaa
Umenikumbusha Operations ya Antiterrorism Musoma hapo 2017
Kuna Gaidi aliingia Mikononi
Duuh sawa ndo nasonga nayo hapa mdogomdogo kali kinoma[emoji848]Nenda jukwaa la Entitlement stori inaitwa Tulichomfanya yule mchawi.
Bravo brotherNilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 9.
Nilifunguliwa lile geti nikawa nimetoka mle ndani.Yule askari aliyenifungulia alinichukia mpaka kwenye kile chumba ambacho jana tulifikishiwa baada ya kufika hapo kituoni!.Sasa nilipofika hapo nilimkuja jamaa mmoja aliyekuwa amevaa suti nyeusi,pembeni yake alikuwa amekaa Gabriel ila shemeji ambaye ni mke wa Gabi sikumuona!.
Afande "Kaa chini bhana hapa huwa hatusimami!"
Afande aliyeniambia nikae chini ndiye yuleyule aliyekuwa akituhoji ile jana na ndiye niliyemkuta kule nyumbani kwa Gabriel!.Basi mle ndani kulikuwa na ukimya wa muda fulani ambapo yule askari yeye alikuwa akiendelea kuandika huku kila mmoja akiwa kimya akimtazama.
Afande "Mkuu nadhani sasa tutawasiliana"
Jamaa "Sawa,haina tatizo!"
Basi baada ya hapo nikaambiwa na yule afande niende pale mapokezi nikachukue vitu vyangu nilivyokuwa nimekabidhi kabla ya kuingizwa Selo!.Baada ya kukabidhiwa vitu vyangu nakutoka nje,ndipo Gabriel akanitaka nipande gari iliyokuwa imepaki kando ya hilo jengo la kituo cha polisi na ilikuwa ni Toyota Prado nyeupe!.Basi nilipoingia ndani ya ile gari nikamkuta na demu wa Gabriel.
Yule jamaa aliyekuwa amevaa suti yeye alikaa mbele kando ya dereva halafu na sisi watatu tukakaa nyuma!.Gari ile iliondoka na tukaelekea nyumbani kwa Gabriel maeneo ya Buhemba!.Tulipofika tulishuka na kuingia ndani ambapo kila mmoja aliingia bafuni kuoga na kubadili nguo,sasa kwakuwa mimi nguo zangu zilikuwa Sirari,Gabriel aliniazima nguo zake nikavaa ingawa aliniambia nisimrudishie amenipatia kama ndugu yake!.
Baada ya hapo yule Bosi wa Gabriel alisema tutoke tutafute sehemu iliyotulia ili tupumzishe akili,sasa wakati tunatoka Gabriel akasema mkewe abaki pale nyumbani,sasa yule bosi wake akasema inabidi twende wote lakini Gabriel akakataa akasema yeye abaki na kama ni chakula angeletewa!.Basi tukawa tumeondoka kuelekea mjini!.
Basi baada ya kufika hotelini ile gari ikapaki na sisi tukashuka kuingia ndani!,baada ya kupata msosi wa nguvu ndipo kila mmoja akaanza kushushia vitu vyake,baada ya kupiga vitu niliona sasa Gabriel akaanza kuchamngamka!.
Gabi "Unajua yule mwanamke ni mpumbavu sana Bosi!"
Bosi "Nani!,Mkeo?"
Gabi "Aah! yule si mke wangu hata hivyo mi napita tu!"
Bosi "Kwanini unasema hivyo!"
Gabi "Kila siku naongea lakini yanapitia huku yanatokea kule"
Aliendelea "Ukiachana na hii ishu lakini nadhani unakumbuka kipindi kile Babati ilivyokuwa kaka!"
Bosi "Yeah!,sasa inabidi uwe makini maana serikali sasa hivi wako makini sana,sema ndiyo hivyo tunabanana na hawa askari,lakini kama sivyo ni hatari sana!"
Sasa mimi sikutaka kabisa kuingilia yale mazungumzo lakini nilichokuja kugundua ni kwamba,yule demu wa Gabi ndiye yawezekana alisababisha yale majanga kwasababu Gabi alikuwa amechukia sana na sikujua alisababishaje maana mimi hakutaka kabisa kuniambia na inaonekana si mara moja,yeye na huyo bosi wake ndiyo walikuwa wakifahamu,mimi kazi yangu niliifanya kwa uaminifu kabisa na sikuwa na longo longo!.
Sasa mpaka tunatoka pale polisi aliyesababisha sisi kutoka ni huyo jamaa ambaye Gabi alikuwa akimuita bosi,sikujua amefanya fanyaje hadi sisi kutoka lakini niliamini ilikuwa ni fedha inaongea maana jamaa alionekana alikuwa na hela hatari,na kitu kingine nilichokuja kukigundua baadae ni kwamba yule jamaa ndiye alikuwa akimpatia Gabi zile fedha!.Hii nchi kuna dili haramu nyingi sana lakini huwezi kukuta watu wanaohusika wanawekwa ndani,siye vinyangarakata tusio na mbele wala nyuma ukizingua kidogo tu,utafia gerezani!.
Bosi "Hivi uliniambia huyu jamaa anaitwa nani!?"
Gabi "Huyu anaitwa umughaka"
Bosi "Ooh sawa!"
Aliendelea "Sawa bana nyie fanyeni kazi kwa umakini,najua kwasasa hakuta kuwa na wanoko maana wale wajinga tushamalizana!".
Sasa wakati nikiwa naendelea kukung'uta vyombo nilikuwa nawaza namna ya kuachana na ile biashara kichaa japo ilinipatia pesa ya kutosha lakini niliona inaweza kuniingiza kwenye matazizo makubwa!.Baada ya kupiga vyombo na kuona vimenitosha niliwaaga wao ili mimi nijikatae kwenda Sirari!.
Gabi "Unawahi wapi wewe,wewe kaa utatindike beer,kwako utaenda tu!"
Basi baada ya kila mtu kuridhika siku hiyo tuliondoka,Gabi alinishawishi sana hatimae sikwenda Sirari nikaamua kwenda kulala kwake ili asubuhi anipatie fungu niondoke nalo kuelekea Sirari!.
Baada ya kutufikisha pale nyumbani yule Bosi na dereva wake wao waliondoka.
Namshukuru asubuhi niliwahi kuamka na ndipo nikaelekea sebuleni kumsubiri Gabi aamke anikabidhi pesa haramu ili mimi niondoke zangu,sasa shemeji ndiye aliyetangulia kuamka na kuja pale sebuleni.
Mimi "Mambo vipi shemu"
Marieta "Safi,za tangu jana
Mimi "poa kabisa"
Mimi "Jamaa bado kalala?"
Marieta "Ngoja nimuamshe"
Basi baada ya dakika 10 jamaa akawa amekuja pale sebuleni.
Mimi "Nataka kuondoka kaka,unaweza kunipatia mzigo?"
Gabi "We nenda tu nitakuletea huko,pia kuna jambo nikija tutazungumza"
Mimi "Poa,basi acha mi niwahi"
Gabi "Mida ya saa 10 jioni nitakupigia simu tuonane mahali"
Mimi "Poa kaka"
Baada ya mazungumzo yale mi nikamuaga jamaa nikaondoka zangu,sikujua ni kwanini jamaa alibadili maamuzi ile asubuhi kwasababu jana yake tulikuwa tumeongea akawa amesema asubuhi angenipatia hela lakini alibadilika.Yeye na huyo demu wake kiukweli baada ya hilo sekeseke inaonekana kabisa hawakuwa sawa na sikufahamu tatizo lilikuwa ni nin!.Sikutaka sana kuchimba na kuuliza uliza mambo ya ndani kwani ningeonekana mjuaji!,nilichoshukuru mimi ni kutoka nje na ile kesi iliisha!.
Baada ya kufika pale Sirari wanangu walitaka kufahamu ni kitu gani kilisababisha hadi kujikuta nipo mikononi mwa mapongo.Sasa sikutaka kuwaeleza ukweli ikabidi nifanye siri kabisa,nilichowaambia ni kwamba kuna mtu alikuwa akinidai na hivyo aliamua kunipeleka polisi,wao wakaamini hivyo kumbe haikuwa hivyo!.
Sasa ilipofika mida hiyo ya saa 10 alasiri,Gabi akawa amepigia simu na kweli akawa yupo pale Sirari na akaniambia tuonane kwenye ile bar tuliyokutana ile siku ya kwanza.
Ningekuwa mim ningenda mwaza kwa mtatiro Gabi ningemtua sitaki shida mimiHuko mbele ya safari unaelekea kula kipigo mura bila Shaka hilo hukuacha baada ya kutoka rumande
Weeh sema kweliUmughaka is back again!!!!!!!!!