Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mogabiri.....umenikumbusha mbali sana aisee, hiyo barabara kwenda nyamwaga hadi nyamongo siku moja ilitaka kutuuaNisikuchoshe na usinichoshe,tusichoshane!.
Kwenye haya maisha kuna wakati huwa ninakaa chini na kusema "Kama sikufa kipindi kile,basi siwezi kufa mpaka Mungu atakaporuhusu".
Nadhani wengi mtakumbuka ni siku chache tu zimepita nimeandika kisa cha maisha ambayo nilikutana nayo wakati nikiwa nimekwenda kumsalimia baba yangu mdogo akiwa ni Headmaster, maisha yale yalikuwa ya kawaida ila washirikina walifanya tukakosa amani.
Sasa baada ya hapo nilifaulu vizuri tu kuelekea shule ya upili(advance)na nikapangiwa huko Tanga kwa mchepuo wa Sayansi wenye combination PCB.
Hali yangu ya maisha ya shule kiukweli ilikuwa mbaya sana mpaka nikajuta kwanini nilichukua hiyo combination, siyo kwamba sikuwa na akili, la hasha!, akili ilikuwepo ya kutosha kwasababu nilifaulu kwenda advance kwa divisheni 2, ni combination iliyohitaji kupiga msuli kana kwamba umetumwa na kijiji, haikutaka mchezo wala kujisahau hata kidogo,sasa mimi nilipofika huko nikajikuta naungana na makundi na kujanjaruka kuwashinda hata niliyowakuta!.
Mkurya mimi kutoka wilayani Tarime kijiji cha Mogabiri nikajikuta nazamia kwenye dimbwi la mapenzi ya mtoto wa kitanga ambaye alifanya hata kusoma nikaacha nikawa namuwaza yeye na utamu wa papuchi yake!.
(Shamima popote ulipo ulaaniwe mbwa wewe kwa kuniharibia maisha[emoji23][emoji23]). All in all ni kwamba napambana na maisha yanasonga japo ni kibishi!. Sasa haya ya kwanini nilifeli nadhani kwa leo si mahala pake,nitawaeleza tu kilichofuata baada ya mimi kufeli shule!.
Kiasili mimi ni mkurya kutokea wilaya ya Tarime huko kijijini Mogabiri,ingawa hatukuishi sana hapo kijijini lakini ndipo chimbuko letu lilipo hapo, kwa pale Tarime mjini nyumbani kwetu ni Rebu.Pia tunao ndugu wengi tu waliotapakaa karibu kila kona ya hii nchi!, hapa Dar es salaam wamejaa ila wanajifanya kama hawanioni vile!(Maisha ya sikuhizi yamekuwa yakipumbavu sana).Kwakuwa wanajifanya kukausha na mimi pia napiga mikausho ya hatari!,sitaki kumgasi mtu!.
Basi bana, nakumbuka ile nimemaliza skonga nikawa nashangaa shangaa pale nyumbani kusubiri tokeo la kuelekea chuo, sasa nilifahamu kabisa siwezi kufaulu kwa kile nilichokifanya kule skonga, Mzee yeye aliamini toto lake limemaliza shule na anajivunia kwasababu nilikuwa nina akili,hakuelewa kabisa kwamba baada ya kufika shule nilijanjaruka kuwazidi hata niliowakuta!. Baada ya matokeo kutoka na ikaonekana nimepata divesheni zero, mimi kwa upande wangu sikushituka ila Mzee alihamaki sana na kushangaa nilipatwa na nini hadi nifeli!.
Tangu nimeanza darasa la kwanza hadi darasa la saba, sikuwahi kuvuka namba 5,ingawaje sikuwahi kuwa namba 1 lakini nilikuwa nacheza kwenye namba 2-4. Nilipofika form 1 hadi form 4 wembe ukawa uleule! nashika namba 3 -5,sasa hadi nafaulu kuingia advance Mzee wangu hakushangaa maana alifahamu kabisa toto lake nilikuwa nina akili!
Mzee wangu kiukweli alikuwa mkali mno na ilikuwa ikitokea nimefanya kosa akanikamata, kiukweli nilikuwaga naimba Haleluya!.Yeye alikuwaga achapi kwa fimbo za miti ya kawaida,bali alikuwa anachapa kwa nyaya ya umeme! Aisee usiombe kukutwa!
Kuna muda nilikuwa nikifahamu nimefanya kosa siku hiyo najiwahisha kuoga na kuingia kulala na kujifanya naumwa!, sasa akija akikushika shingoni kama anakupima joto akakuta huna joto,aisee utaomba ardhi ipasuke ikumeze ili ikuepushe na kipigo kisichokuua ila chenye kukufanya ukajuta kwanini ulizaliwa!.
Kutokana na kutokuridhika kwa mzee na yale matokeo, kuna siku kadhaa sikumuona pale nyumbani nikajua uenda atakuwa kwenye mambo yake, sasa kumbe mzee amesafiri hadi Tanga kwenda kuonana na Headmaster kufahamu mwanae ni kwanini nimefeli kiasi kile na wenzangu kufaulu!
Alichoamini mzee ni kwamba sikustahili kufeli na nilipaswa nifaulu!. Ule mpango wa yeye kwenda Tanga kumbe hadi Maza nae alikuwa akifahamu ila aliamua kula buyu ili ukweli ufahamike!, Mama yangu alikuwa rafiki yangu mkubwa sana na yeye peke yake ndiye shida zangu zote nilikuwaga nikimwambia!.Ila safari hii na yeye aliukaza uso wake na hakutaka kabisa kucheka na kima!.
Mwanaume niliendelea kujinafasi na kujimwayamwaya kwa kipindi kile kifupi ambacho mzee hakuwepo nikiamini atakuwa ameenda kwenye shughuli zake, akili yangu iliamini kwasababu mzee wangu alikuwa akinimini basi angenipatia mtaji ili nianze biashara!.
Baada ya kama siku 5 mzee alirejea, sasa tukiwa tunapata chakula usiku alikuwa akiniangalia kwa jazba sana, sikuwa na tatizo nae kwasababu niliamini yeye kuwaga na hasira za karibu ndiyo ilikuwa kawaida yake!. Sasa ile naendelea kula sijui ili wala lile,nilishitukia amenipiga kofi ambalo lilifanya kuanza kuona maluweluwe!.
Mama "Tatigha omwana araghere!"(Muache mtoto ale)
Mzee "Amos hebu niletee waya hapo chumbani"
Sasa mdogo wangu aitwaye Amos akaagizwa waya akachukue waya ili viboko vichukue nafasi!.
Mzee "Leo nakuua mbwa wewe"
Kiukweli siku hiyo nilijua kabisa nakufa maana mzee wangu alikuwaga hana masikhara kabisa na maneno yake!. Basi mama alikuwa akijaribu kumtuliza mzee lakini bado ikashindikana, kwa wakati huo sikuelewa kabisa ni kitu gani kilimsibu mzee wangu ambaye alikuwa amerejea kutoka huko alikokuwa ameenda!.
Mzee alinyanyuka akatoka akaenda ndani ambako sikufahamu alikwenda kufanya nini,wakati huo kiukweli hata chakula sikuwa na hamu nacho tena kwasababu mabanzi na makwenzi niliyokuwa nimechezea yaliniharibia mudi kabisa!.Baada ya mzee kutoka chumbani alikuja na kamba ya katani akanisogelea akanifunga na kunibana miguu kana kwamba anataka kuchinja kuku!,sasa akauchukua ule waya uliyoletwa na dogo nikaanza kuchezea stiki! kiukweli nilipigika sana!. Baada ya kuona ameniadhibu vya kutosha alinilaza kifudi fudi wakati huo kanifunga mikono kwa nyuma kama vile jambazi au mwizi amepigwa pingu.
Mzee "Leo nakuua, sali sala yako ya mwisho!"
Aliendelea "Siwezi kuharibu pesa yangu halafu wewe uende shule kuwa mtoro!"
Baada ya kusikia ile kauli basi nikajiongeza kiakili na nikafahamu kabisa atakuwa alikwenda shuleni kuutafuta ukweli wa mimi kufeli!.Kiukweli nilikiona kifo kiko karibu yangu!.
Mzee "Yaani nakulipia karo wewe unaenda kuvuta bangi shule?"
Aliendelea "Hizo bangi ulianza kuvuta lini?"
Sasa nikaanza kushangaa ni nani alimwambia nilikuwa navuta bangi? Kiukweli kitu ambacho sikuwahi kukifanya kwenye maisha yangu ni huo uvutaji wa bangi alionieleza!.
Mimi "Hapana baba sivuti bangi!"
Mzee "Leo utanitambua mshenzi wewe"
Kiukweli kujitetea ilikuwa ngumu sana maana kila nilipojaribu kujitetea nilionekana muongo na kuishia kukandamizwa viboko visivyokuwa na idadi!
Sasa kumbe alipokwenda kule shuleni, walimu walimwambia ya kwamba mimi nilijiingiza kwenye kundi la waliokuwa wameshindikana na kuanza kujihusisha na uvutaji wa bangi!walimu pia hawakufahamu hicho hakikuwa chanzo cha mimi kufeli bali ilibidi wamwambie mzee kwasababu ya kuniona mimi kukaa na watu ambao pale shuleni walikuwa wameshindikana!
Na kwa kipindi kile walimu walikuwaga hawaangaiki na mtoto wa mtu,wao walikuwa wakituambia mwisho wa mambo yote ni pepa(mtihani)ndiyo utakaochuja nafaka halisi na magugu!.
Basi bana, baada ya kupigika sana na mzee kunishikia panga, ilibidi maza aingilie kati kwa kujifunga kibwebwe na kumkoromea mzee!.
Mama "Hivi baba Sarah unataka kumuua mtoto kisa kufeli shule!"
Aliendelea "Kama humtaki mtoto muache akatange tange huko!"
Basi baada ya mama kuingilia kati, mzee aliniacha na akanitaka nipotee pale nyumbani na nisije kumtambua kama baba yangu. Mama alinisogelea na kunifungua zile kamba mkononi na miguuni!. Kiukweli nilipigika sana.
Nilitoweka pale sebuleni nikaelekea chumbani kulala huku nikiendelea kulia kwa kwikwi, mwili wangu wakati huo ulikuwa umejaa alama ya nyaya za umeme zilizosababishwa na kile kipigo!.
Usiku huo kiukweli sikupata usingizi kabisa kutokana na maumivu ya viboko!.
Soma zaidi:
Unawajua wakurya au unawasikia tu hapa kwenye story, mie sio mkurya ila nimeishi nao, mkurya kushika fimbo na kumtandika mke, mtoto sijui shemeji, mdogo mtu tena hadharani ni jambo la kawaida kabisa haijalishi una umri ganiKijana aliyemaliza Form Six sio mtoto..ni mtu mzima..ana miaka zaidi ya 18..anajielewa..ni level ya kijana wa chuo kikuu...kushikiwa chini na kupigwa hivyo nadhani hapo kuna shida..hayo ni mambo ya watoto wa std iv to vii
Hakika huyu kijana apewe tozo hapa jf Ni mtu anajuwa ni maana ya fasihi andishi Ni mtaalamu haswa tumuombee mungu afike mbali manake anajuwa haswaUmekuwa mtu mmoja wa kutufikirisha sana,wengi wetu si wapenzi wa kutafuta vitabu,hakika unatenga muda wako wa kutunga,kuhariri na kutupostia sisi wadau ambao kuna muda hatuna Shukran,post zako zimezingatia Fasihi sahihi kabisa na wengi wetu inatufanya kupelekea lugha ya picha mjongeo akilini mwetu vile sura na mwili kwa ujumla wa Umughaka ulivyo,Gabi sura yake na mwili wake pamoja na wahusika wengine,pia shukran kwa uandishi ulio nyooka hakuna kukosea/kuchapia najua unatenga muda rafiki na muda wa kutosha kwa ajili ya wengi na wachache tusiojua kushukuru.
Hakika huyu kijana apewe tozo hapa jf Ni mtu anajuwa ni maana ya fasihi andishi Ni mtaalamu haswa tumuombee mungu afike mbali manake anajuwa haswa
Basi ndo mimi hujakosea!Hilo jina la Nyarusare umelichukua kutoka kwa yule Mzee Nyarusare msanii alikuwa mwana-ccm kindakindaki na anapiga sana zeze? Nakumbuka kuna sikukuu moja ya May Mosi alipiga wimbo unaitwa kazi ni kazi. Pamoja na kwamba nilikuwa mdogo lakini mpaka sasa kumbukumbu ipo
Nenda kamuone daktari [emoji56]Inawezekana mkuu,mi nilishakaa geto Moshi miaka 3 sikuwahi kuleta demu na wala sikuwa na demu moshi,kuanzia mwaka 2011 hadi 2014 nikiwa na umri zaidi ya miaka 21 ,inawezekana sana,mara nyingi mi nilikua naweza kukaa hata miezi 8 sijakutana na demu
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]yaani alikamatika kirahisi mnoKanuni ya kukamata mwanaume ni ile ile tangu shetani alipoitumia mpaka leo
Atoe namba tumchangie pesa ya mafuta
Hpn bhan moja tu inatosha [emoji23] kwa leoSawa kaka tumekuelewa,
Lakini tunakuomba leo shusha episode hata tano hivi, ili tuenjoy zaidi hii jumapili
[emoji4]
Kwa Nini mkuu??[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Dogo nakushauri hii stori usiendelee nayo pumzikia hapa inatosha
Kabisa tumchangie kidogo ya mafuta ya Bodaboda yake kwanza ili mambo yasiwe mengi maana anahadithia hadi mtu unakua teja hutamani story iishe
Mi sio mkurya ila kwenye hili nakubali kabisa, nawakubali sana sema nikileta posa msinitolee maparu 😂😂(jokin)Ukweli ni kwamba,jamii yangu ya kikurya ni jamii ambayo huwa ina upendo na kuwajali watu wengine pia,ukiachilia tu yale madhaifu madogo madogo kama wanadamu wengine lakini wakurya ni kabila bora sana miongoni mwa makabila bora kwenye hii nchi!,yale madhaifu madogo madogo ya kupiga mwanamke, kukeketa na kuchinjana ovyo yalikuwaga ni kwasababu ya ukosefu wa elimu tu,