Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua Nyumbani

Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua Nyumbani

FfMw6VaXgAEHvyd.jpeg
kudadadeki
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 6.



Maisha kwa upande wangu yalikuwa mazuri na hata yale majuto ya mzee wangu kunitimua nyumbani hayakuwepo tena,zaidi ni mimi ndiye niliyetamani nifanikiwe ili nikamringishie ajute kunifukuza nyumbani kwa kunidharirisha!.Nilikuwa nafanya kazi mbili kwa wakati mmoja,kazi yangu ya upiga debe ilikuwa ikinipatia pesa ya kula kila siku,kuhusu kula kwakweli nilikuwa siwazi kabisa!,ile pesa ya kubadili fedha haramu yenyewe ilifanya nikavaa vizuri,nikanunua samani za ndani na kupiga starehe!.

Marafiki na wadau wangu wa pale Sirari wao waliamini mimi ni mjanja mjanja na uenda nilikuwa najiongeza kutokana na elimu yangu kumbe pasipo kufahamu kijana mwenzao nilikuwa nafanya dili haramu.

Niliendelea kumsubiri bwana Gabi(Gabriel) ili atakapo rudi basi tuendelee na kazi yetu ambayo tayari ishanitia uchizi!.Sasa ndani ya mwezi mmoja baada ya kusubiri jamaa alirudi na alipofika tu alikuwa amenipigia simu akinitaka niende nikachukue hela niziingize mtaani ili kila mtu afe na chake!.Kiukweli pesa zilikuwa nyingi sana na sikuwahi kufahamu yeye alikuwa akizitoa wapi!. Kitu cha kumshukuru Mungu kwa upande wangu tangu nianze kujihusisha na ile biashara haramu,sikuwahi kushitukiwa na mtu yeyote na nilikuwa nimesema endapo siku nikashitukiwa basi mimi ningekufa na mtu yeyote kwa kumsingizia uongo ili nichomoke!.

Sasa nikiwa naifanya kazi ile kwa umakini mkubwa huku nikiendelea kuzuga kwenye kazi yangu ya upiga debe,mpaka muda huo nadhani mtaani nilikuwa nishaingiza si chini ya milioni 10.kuna siku mida ya saa 5 asubuhi mke wa jamaa akawa amenipigia simu huku akihitaji kufahamu niko maeneo gani.Sikuwahi kabisa kuwasiliana na yule mwanamke ijapokuwa namba yangu yeye alikuwa nayo na mimi pia ya kwake nilikuwa nayo,sasa kitendo cha kuniuliza niko wapi sikujua lengo lake ni lipi maana hata mumewe hakuwahi kuniuliza kwamba niko wapi!,nakumbuka ilikuwa ni ile siku ya kwanza tu ndiyo jamaa aliniuliza nipo maeneo gani ili aje tuzungumze!,sasa huyu mkewe lile swali lake la "Uko wapi" na namna alivyouliza ni kama Jamii yetu ya kikurya mwanaume kuambiwa na mkewe kwamba "Nitakupiga".Ikifika hatua hiyo basi unaweza kumkung'uta mwanamke na ukamuua kabisa!.Sasa kitendo cha kuniuliza uko wapi tena bila hata salamu kilinikera na kuniudhi sana lakini niliamua kukausha tu!.

Yeye "Marieta hapa naongea"

Aliendelea "Uko wapi?"

Mimi "Kuna shida?"

Yeye "Wewe niambie uko wapi?"

Mimi "Kwani siku zote huwa napatikana wapi shemu!?"

Basi baada ya kumwambia vile akakata simu,nilifahamu kama kungekuwa na tatizo angenipigia simu yeye,mimi niliendelea na kazi yangu bila presha!.Sasa baada ya kama dakika 10 kupita akawa amenipigia simu.

Yeye "Njoo nyumbani Gabi anakuita"

Mimi "Ok sawa,mwambie nitakuja jioni"

Yeye "Njoo muda huu kama unaweza ni ishu ya haraka!".

Mimi "Shemu kuna shida?"

Yeye "Hapana ni kawaida tu!".

Basi baada ya mazungumzo akawa amekata tena ile simu,sasa yule mwanamke alikuwaga anaongea kwa kisirani sana na kwa mkato,sikufahamu uenda ndivyo walivyokuwa wanawake kutoka huko Arusha au ilikuwa ni tabia yake tu!,kiukweli mimi alikuwa akiniudhi sana kama kijana wa kikurya niliyekuwa sipendi dharau na ndiyo maana hata nilikuwa sipandishi nae stori!.

Niliamua kumpigia simu bwana Gabriel mimi mwenyewe kama ni kweli alikuwa akinihitaji wakati ule pale nyumbani ama la!,sasa niliipiga sana ile simu ya jamaa ikawa inaita tu bila kupokelewa,nikaendelea kupiga lakini nikaona holaa!.Sasa akilini mwangu nikaanza kuwaza mambo ya kijinga,nikawa nasema uenda mtoto wa kike anahitaji kupelekewa moto na ile ilikuwa ni Zuga tu kujisemesha naitwa na jamaa ili niende pale nyumbani kwao!,lakini pia kilichonipa ujasiri ni kwamba kama jamaa angekuwa ananihitaji angenipigia simu mwenyewe!,sasa mawazo yakanipeleka mbali sana nikaingia tamaa ya moyo ghafla yule mwanamke akajaa usoni nikaanza kumvutia picha namna alivyo na namna nitakavyo mkung'uta shipa lenye ladha ya kikurya!.Basi nikaamua kumpigia simu ili kujiridhisha tena!.

Yeye "Umefika wapi?"

Mimi "Ndo nadandia usafiri nakuja"

Mimi "Nampigia jamaa simu naona hapokei"

Yeye "Mi sijui bana we njoo"

Basi mwanaume nikadandia mchomoko iliyokuwa ikielekea Tarime mjini nikaondoka!.Baada ya kufika pale Tarime niliingia stendi kule ambako kulikuwa na wanangu wenye magari ya kuelekea Musoma,nikadandia Hiace ikanishusha maeneo ya Buhemba yalipokuwa makazi ya Gabriel na huyo mkewe!.

Basi nilipofika getini nilikuta geti liko wazi nami nikalifungua na kuingia ndani,nilibisha hodi na hatimaye yule mwanamke alikuja kunifungulia mlango,sasa wakati anafungua mlango alionekana ni kama hana amani kabisa tofauti na siku zote!.

Mimi "Shwari?"

Yeye "Shwari,vipi!"

Sasa ile natia tu mguu ndani,kumbe kuna jamaa alikuwa amejificha nyuma ya mlango akawa amenivuta kwa ndani kisha akaufunga ule mlango na funguo akachomoa! .Basi yule jamaa akaniambia kwa ishara niongozane na yule mwanamke kuelekea sebuleni!.

Baada ya kufika sebuleni nikawakuta jamaa 3 na yule aliyefunga mlango walikuwa jumla 4,pia nikamkuta Gabriel amekaa kwenye kochi akiwa hana raha kabisa!.Basi miongoni mwa wale jamaa akaniongelesha kwa ukarimu kabisa!.

Jamaa "Umughaka mambo vipi kaka"

Mimi "Shwari kaka"

Jamaa "Vipi lakini mambo yako!"

Mimi "Mimi niko poa kabisa kaka"

Jamaa "Ooh sawa,sirari wanasemaje kaka"

Mimi "Tupo tu tunapambana"

Jamaa "Hivi pale Sirari huwa unaishi maeneo gani?"

Sasa kabla hata sijajibu,yule jamaa ambaye yeye kwa wakati huo akiwa amekaa na wenzie wamesimama kama milingoti,akaniambia nisimame nimsogelee alipokuwa amekaa!.

Jamaa "Hebu tuangalie humu mfukoni umeweka nini bwana Umughaka"

Jamaa moja kwa moja baada ya kumsogelea alizama mfukoni mwangu akatoa simu na hela nilizokuwa nazo!.

Jamaa "Hii simu ya nani?"

Mimi "Ya kwangu"

Jamaa "Na hii hela!"

Mimi "Ni yangu kaka"

Jamaa "Kumbe unaweza kufanya tu kazi zako vizuri na bado ukapata hela nzuri tu bwana Umughaka"

Sasa ile hela niliyokuwa nayo mfukoni muda huo ilikuwa ni elfu 16 na vichenji kadhaa!.

Jamaa "Huyu bwana unamfahamu?"

Mimi "Ndiyo,ni brother angu"

Jamaa "Mtu wa Arusha na mkurya ni ndugu wapi na wapi Umughaka wewe acha hizo bwana!"

Kiukweli yule jamaa alikuwa anaongea kama mtu fulani mnyenyekevu sana lakini kiuhalisia alionekana asiyekuwa na huruma hata chembe!,sasa mpaka wakati huo nilifahamu kabisa mambo yameshaharibika na sikupata tabu kuamini wale walikuwa ni mapongo (Askari).

Jamaa "Mbona jamaa anasema yeye hakujui!"

Sasa wakati jamaa anaongea na mimi alikuwa akiendelea kukipekua kiswanswadu changu.

Jamaa "Wewe unasema jamaa ni brother wako lakini jamaa nimemuuliza anasema hakujui"

Basi nilimtazama Gabriel nikadhani uenda ataniangalia ili anipatie ishara yeyote lakini jamaa akawa ameangalia chini tu huku akichezea vidole!.Baada ya kuona jamaa aniangalii mimi ikabidi nikomae kwamba jamaa ni brother angu!.

Jamaa "Sawa bwana umughaka naona mnateteana Mkurya na muarusha!"

Aliendelea "Jamaa mpaka sasa ameshakupatia shilingi ngapi bwana Umughaka!"

Lile swali kiukweli lilifanya nikakosa pozi nikaanza kujiuma uma hata kujibu nikashindwa!,na kibaya zaidi jamaa alikuwa anauliza kama utani lakini alionyesha yuko serious sana!.

Jamaa "Huna haja ya kuficha kaka wewe kuwa mkweli tu ili ukaendelee na shughuli zako".

Mimi "Kiukweli nikihesabu haraka haraka inaweza kufika milioni 1"

Jamaa "Hebu kuwa serious kidogo kaka uache utani,yaani miezi takribani mitano mnafanya kazi awe amekupa milioni 1 tu!"

Aliendelea "Acha hizo mambo bhana,wewe eleza ukweli ili uondoke ukafanye shughuli zako"

Mimi "Kaka hiyo ndiyo nayo ikumbuka"

Jamaa "Haya bhana!"

Aliendelea "Marco hebu nendeni na jamaa mpaka kwake huko nadhani atawaeleza vizuri,pengine hapa anaona aibu"

Basi baada ya jamaa kusema vile,kuna jamaa kati ya wale waliokuwa wamesimama akanishika shingoni akaniambia nisimame tuondoke!,kiukweli nilichanganyikiwa sana siku hiyo na nilifahamu kabisa mambo si mambo,nilijua tu kuna namna Gabriel na mkewe watakuwa waliharibu mahali na mimi sasa ndiyo kujikuta nimo kwenye msafara!.

Tulipotoka nje wale jamaa waliniambia nitembee pasipo kuwa na hofu yeyote na wala nisije kujaribu kukimbia maana wangenipiga mpaka waniue!.Basi tukaanza kutembea kuelekea barabarani kutafuta Hiace ili twende mpaka mjini tukapande mchomoko kuelekea sirari.
Sasa wakati tunatembea,jamaa wao walikaa kushoto na kulia,mimi nikawa katikati yao!.Muda huo tulikuwa tunapiga stori za kwaida kabisa kana kwamba hakuna tatizo huku mimi nikionyesha Kicheko feki kilichojaa majuto ndani yake! .
Dili Dirisha
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 6.



Maisha kwa upande wangu yalikuwa mazuri na hata yale majuto ya mzee wangu kunitimua nyumbani hayakuwepo tena,zaidi ni mimi ndiye niliyetamani nifanikiwe ili nikamringishie ajute kunifukuza nyumbani kwa kunidharirisha!.Nilikuwa nafanya kazi mbili kwa wakati mmoja,kazi yangu ya upiga debe ilikuwa ikinipatia pesa ya kula kila siku,kuhusu kula kwakweli nilikuwa siwazi kabisa!,ile pesa ya kubadili fedha haramu yenyewe ilifanya nikavaa vizuri,nikanunua samani za ndani na kupiga starehe!.

Marafiki na wadau wangu wa pale Sirari wao waliamini mimi ni mjanja mjanja na uenda nilikuwa najiongeza kutokana na elimu yangu kumbe pasipo kufahamu kijana mwenzao nilikuwa nafanya dili haramu.

Niliendelea kumsubiri bwana Gabi(Gabriel) ili atakapo rudi basi tuendelee na kazi yetu ambayo tayari ishanitia uchizi!.Sasa ndani ya mwezi mmoja baada ya kusubiri jamaa alirudi na alipofika tu alikuwa amenipigia simu akinitaka niende nikachukue hela niziingize mtaani ili kila mtu afe na chake!.Kiukweli pesa zilikuwa nyingi sana na sikuwahi kufahamu yeye alikuwa akizitoa wapi!. Kitu cha kumshukuru Mungu kwa upande wangu tangu nianze kujihusisha na ile biashara haramu,sikuwahi kushitukiwa na mtu yeyote na nilikuwa nimesema endapo siku nikashitukiwa basi mimi ningekufa na mtu yeyote kwa kumsingizia uongo ili nichomoke!.

Sasa nikiwa naifanya kazi ile kwa umakini mkubwa huku nikiendelea kuzuga kwenye kazi yangu ya upiga debe,mpaka muda huo nadhani mtaani nilikuwa nishaingiza si chini ya milioni 10.kuna siku mida ya saa 5 asubuhi mke wa jamaa akawa amenipigia simu huku akihitaji kufahamu niko maeneo gani.Sikuwahi kabisa kuwasiliana na yule mwanamke ijapokuwa namba yangu yeye alikuwa nayo na mimi pia ya kwake nilikuwa nayo,sasa kitendo cha kuniuliza niko wapi sikujua lengo lake ni lipi maana hata mumewe hakuwahi kuniuliza kwamba niko wapi!,nakumbuka ilikuwa ni ile siku ya kwanza tu ndiyo jamaa aliniuliza nipo maeneo gani ili aje tuzungumze!,sasa huyu mkewe lile swali lake la "Uko wapi" na namna alivyouliza ni kama Jamii yetu ya kikurya mwanaume kuambiwa na mkewe kwamba "Nitakupiga".Ikifika hatua hiyo basi unaweza kumkung'uta mwanamke na ukamuua kabisa!.Sasa kitendo cha kuniuliza uko wapi tena bila hata salamu kilinikera na kuniudhi sana lakini niliamua kukausha tu!.

Yeye "Marieta hapa naongea"

Aliendelea "Uko wapi?"

Mimi "Kuna shida?"

Yeye "Wewe niambie uko wapi?"

Mimi "Kwani siku zote huwa napatikana wapi shemu!?"

Basi baada ya kumwambia vile akakata simu,nilifahamu kama kungekuwa na tatizo angenipigia simu yeye,mimi niliendelea na kazi yangu bila presha!.Sasa baada ya kama dakika 10 kupita akawa amenipigia simu.

Yeye "Njoo nyumbani Gabi anakuita"

Mimi "Ok sawa,mwambie nitakuja jioni"

Yeye "Njoo muda huu kama unaweza ni ishu ya haraka!".

Mimi "Shemu kuna shida?"

Yeye "Hapana ni kawaida tu!".

Basi baada ya mazungumzo akawa amekata tena ile simu,sasa yule mwanamke alikuwaga anaongea kwa kisirani sana na kwa mkato,sikufahamu uenda ndivyo walivyokuwa wanawake kutoka huko Arusha au ilikuwa ni tabia yake tu!,kiukweli mimi alikuwa akiniudhi sana kama kijana wa kikurya niliyekuwa sipendi dharau na ndiyo maana hata nilikuwa sipandishi nae stori!.

Niliamua kumpigia simu bwana Gabriel mimi mwenyewe kama ni kweli alikuwa akinihitaji wakati ule pale nyumbani ama la!,sasa niliipiga sana ile simu ya jamaa ikawa inaita tu bila kupokelewa,nikaendelea kupiga lakini nikaona holaa!.Sasa akilini mwangu nikaanza kuwaza mambo ya kijinga,nikawa nasema uenda mtoto wa kike anahitaji kupelekewa moto na ile ilikuwa ni Zuga tu kujisemesha naitwa na jamaa ili niende pale nyumbani kwao!,lakini pia kilichonipa ujasiri ni kwamba kama jamaa angekuwa ananihitaji angenipigia simu mwenyewe!,sasa mawazo yakanipeleka mbali sana nikaingia tamaa ya moyo ghafla yule mwanamke akajaa usoni nikaanza kumvutia picha namna alivyo na namna nitakavyo mkung'uta shipa lenye ladha ya kikurya!.Basi nikaamua kumpigia simu ili kujiridhisha tena!.

Yeye "Umefika wapi?"

Mimi "Ndo nadandia usafiri nakuja"

Mimi "Nampigia jamaa simu naona hapokei"

Yeye "Mi sijui bana we njoo"

Basi mwanaume nikadandia mchomoko iliyokuwa ikielekea Tarime mjini nikaondoka!.Baada ya kufika pale Tarime niliingia stendi kule ambako kulikuwa na wanangu wenye magari ya kuelekea Musoma,nikadandia Hiace ikanishusha maeneo ya Buhemba yalipokuwa makazi ya Gabriel na huyo mkewe!.

Basi nilipofika getini nilikuta geti liko wazi nami nikalifungua na kuingia ndani,nilibisha hodi na hatimaye yule mwanamke alikuja kunifungulia mlango,sasa wakati anafungua mlango alionekana ni kama hana amani kabisa tofauti na siku zote!.

Mimi "Shwari?"

Yeye "Shwari,vipi!"

Sasa ile natia tu mguu ndani,kumbe kuna jamaa alikuwa amejificha nyuma ya mlango akawa amenivuta kwa ndani kisha akaufunga ule mlango na funguo akachomoa! .Basi yule jamaa akaniambia kwa ishara niongozane na yule mwanamke kuelekea sebuleni!.

Baada ya kufika sebuleni nikawakuta jamaa 3 na yule aliyefunga mlango walikuwa jumla 4,pia nikamkuta Gabriel amekaa kwenye kochi akiwa hana raha kabisa!.Basi miongoni mwa wale jamaa akaniongelesha kwa ukarimu kabisa!.

Jamaa "Umughaka mambo vipi kaka"

Mimi "Shwari kaka"

Jamaa "Vipi lakini mambo yako!"

Mimi "Mimi niko poa kabisa kaka"

Jamaa "Ooh sawa,sirari wanasemaje kaka"

Mimi "Tupo tu tunapambana"

Jamaa "Hivi pale Sirari huwa unaishi maeneo gani?"

Sasa kabla hata sijajibu,yule jamaa ambaye yeye kwa wakati huo akiwa amekaa na wenzie wamesimama kama milingoti,akaniambia nisimame nimsogelee alipokuwa amekaa!.

Jamaa "Hebu tuangalie humu mfukoni umeweka nini bwana Umughaka"

Jamaa moja kwa moja baada ya kumsogelea alizama mfukoni mwangu akatoa simu na hela nilizokuwa nazo!.

Jamaa "Hii simu ya nani?"

Mimi "Ya kwangu"

Jamaa "Na hii hela!"

Mimi "Ni yangu kaka"

Jamaa "Kumbe unaweza kufanya tu kazi zako vizuri na bado ukapata hela nzuri tu bwana Umughaka"

Sasa ile hela niliyokuwa nayo mfukoni muda huo ilikuwa ni elfu 16 na vichenji kadhaa!.

Jamaa "Huyu bwana unamfahamu?"

Mimi "Ndiyo,ni brother angu"

Jamaa "Mtu wa Arusha na mkurya ni ndugu wapi na wapi Umughaka wewe acha hizo bwana!"

Kiukweli yule jamaa alikuwa anaongea kama mtu fulani mnyenyekevu sana lakini kiuhalisia alionekana asiyekuwa na huruma hata chembe!,sasa mpaka wakati huo nilifahamu kabisa mambo yameshaharibika na sikupata tabu kuamini wale walikuwa ni mapongo (Askari).

Jamaa "Mbona jamaa anasema yeye hakujui!"

Sasa wakati jamaa anaongea na mimi alikuwa akiendelea kukipekua kiswanswadu changu.

Jamaa "Wewe unasema jamaa ni brother wako lakini jamaa nimemuuliza anasema hakujui"

Basi nilimtazama Gabriel nikadhani uenda ataniangalia ili anipatie ishara yeyote lakini jamaa akawa ameangalia chini tu huku akichezea vidole!.Baada ya kuona jamaa aniangalii mimi ikabidi nikomae kwamba jamaa ni brother angu!.

Jamaa "Sawa bwana umughaka naona mnateteana Mkurya na muarusha!"

Aliendelea "Jamaa mpaka sasa ameshakupatia shilingi ngapi bwana Umughaka!"

Lile swali kiukweli lilifanya nikakosa pozi nikaanza kujiuma uma hata kujibu nikashindwa!,na kibaya zaidi jamaa alikuwa anauliza kama utani lakini alionyesha yuko serious sana!.

Jamaa "Huna haja ya kuficha kaka wewe kuwa mkweli tu ili ukaendelee na shughuli zako".

Mimi "Kiukweli nikihesabu haraka haraka inaweza kufika milioni 1"

Jamaa "Hebu kuwa serious kidogo kaka uache utani,yaani miezi takribani mitano mnafanya kazi awe amekupa milioni 1 tu!"

Aliendelea "Acha hizo mambo bhana,wewe eleza ukweli ili uondoke ukafanye shughuli zako"

Mimi "Kaka hiyo ndiyo nayo ikumbuka"

Jamaa "Haya bhana!"

Aliendelea "Marco hebu nendeni na jamaa mpaka kwake huko nadhani atawaeleza vizuri,pengine hapa anaona aibu"

Basi baada ya jamaa kusema vile,kuna jamaa kati ya wale waliokuwa wamesimama akanishika shingoni akaniambia nisimame tuondoke!,kiukweli nilichanganyikiwa sana siku hiyo na nilifahamu kabisa mambo si mambo,nilijua tu kuna namna Gabriel na mkewe watakuwa waliharibu mahali na mimi sasa ndiyo kujikuta nimo kwenye msafara!.

Tulipotoka nje wale jamaa waliniambia nitembee pasipo kuwa na hofu yeyote na wala nisije kujaribu kukimbia maana wangenipiga mpaka waniue!.Basi tukaanza kutembea kuelekea barabarani kutafuta Hiace ili twende mpaka mjini tukapande mchomoko kuelekea sirari.
Sasa wakati tunatembea,jamaa wao walikaa kushoto na kulia,mimi nikawa katikati yao!.Muda huo tulikuwa tunapiga stori za kwaida kabisa kana kwamba hakuna tatizo huku mimi nikionyesha Kicheko feki kilichojaa majuto ndani yake! .
Hahaaaa, mwamba ulikamatwa kiboya sana. Yaani ulishindwa kujua kama kuna mtego mbele.
 
Back
Top Bottom