Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua Nyumbani

Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua Nyumbani

Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 10.




Niliondoka mdogo mdogo nikaelekea kwenye ile bar ambayo aliniambia ningemkuta hapo.Kweli,baada ya kufika hapo nilimkuta Gabi akiwa amekaa huku akiendelea kupiga beer yake pendwa ya Safari!.

Gabi "Uko poa?"

Mimi "Niko poa kaka"

Basi na mimi nikaagiza beer nikaanza kunywa huku tukiendelea kupiga stori za hapa na pale.Gabi bado alionekana kabisa kutokuwa na furaha tofauti na siku nyingine nilivyokuwa nimemzoea,yaani baada ya hilo sakata la sisi kukamatwa ni kama alikuwa hana mudi kabisa!.

Gabi "Mwanangu kwanza kabisa nikuombe samahani,maana jana tulishindwa kuzungumza kabisa kwasababu sikutaka kuzungumza mambo yetu mbele ya Eric(Bosi)"

Aliendelea "Vipi lakini uko Good?"

Mimi "Mimi niko Good kaka wala usijali"

Gabi " Unajua mwanangu asubuhi nimeshindwa kukupa hela kwasababu yule mwanamke amenikwaza sana"

Aliendelea "Hivi unajua yeye ndiye chanzo cha sisi kukaa ndani kaka!"

Mimi "Acha usiniambie kaka"

Gabi "Huwezi amini umughaka!"

Aliendelea "Usimuone na mitako ile ukadhani kichwani kuna akili,kichwani kabeba kamasi tu!"

Mimi "Mimi nilishangaa tu ananipigia simu ile juzi na akataka nije home kwako,lakini nilipokupigia simu yako kujiridhisha nikaona upo kimya kaka ndiyo ikabidi nije"

Gabi "Simu yako nilikuwa naiona lakini sikuweza kupokea kutokana ile hali ambayo nadhani uliikuta,isingekuwa rahisi!"

Aliendelea "Jambo la kushukuru tupo uraiani kaka,hayo mengine sidhani kama niyakutuumiza kichwa sana!"

Gabi "Unajua hiyo juzi nilikuwa nimetoka kuna mtu nilienda kuonana nae,sasa nikiwa huko nashangaa ananipigia simu akiwa analia,nikamuuliza kuna nini?,hasemi!"

Aliendelea "Ikabidi niwashe gari kurudi nyumbani maana nikadhani uenda wakurya wamemfanya kitu mbaya!"

Gabi "Ile nimefika ndani nashangaa nawekwa chini ya ulinzi,mwanangu hakuna siku nimemchukia yule mwanamke kama juzi!"


Aliendelea "Unajua mwanangu mimi nilikuwa mwalimu huko Babati sehemu moja inaitwa Haidomu,sasa kuna mambo mengi yalijitokeza hapo katikati hivyo nikawa nimetemana na uticha!"

Gabi "Sasa yule demu mimi nilifahamiana nae kipindi hicho hapo Haidomu,nikajikuta tunafahamiana na hatimae kuwa wapenzi!"

Gabi "Tumeishi kwa muda mrefu tu mpaka mimi kuja kufahamiana na Eric na ndiye akanipa mchongo huu ambao umenipa kila ninachokitaka,na huyu mwanamke anaelewa kila kitu kaka,siyo kwamba hajui!"

Aliendelea "Tukiwa pale babati,kuna siku sikachukua hela kaenda benki eti atumiwe kwenye akaunti yake!"

Mimi wakati huo naendelea kumsikiliza Gabriel tu na wala sikuwa mchangiaji!.


Gabi " Kibaya zaidi alichukua laki 5"

Mimi "Mbona zilikuwa nyingi sana"

Gabi "Kaka ninapokwambia hana akili siyo kwamba namdharau,hapana!,ni mwanamke wangu hilo nakubali lakini tatizo lake huwa hajiongezi,kila siku namwambia lakini haelewi!"

Aliendelea "Sasa alichokifanya Babati ndicho juzi ametaka kukifanya hapa,nimemuuliza ilikuwaje ananiambia eti alichukua laki moja kwenda kumtumia mtu kwa wakala,sasa inavyoonekana yule wakala baada ya kuzitambua zile pesa alipiga simu polisi"

Gabi "Na lenyewe lisivyokuwa na akili likabaki palepale mpaka wakalidaka!"

Mimi "Sasa kaka tutafanya kazi kweli kwa mazingira hayo?"

Gabi "Kaka nina mzigo!,we acha tu!"

Aliendelea "Sema tu kwamba hii ishu inamtandao mpana hivyo hata ukikamatwa kukaa ndani ni sekunde tu unakuwa umetoka"

Gabi "Sasa kitu ambacho nataka ufanye,nimekuja na mzigo na nitakukabidhi wote,wewe pambana mdogo mdogo na utakuwa unafanya kama tulivyokubaliana mwanzo!".

Basi ilipofika mida ya saa 1 usiku,Gabi akawa amenichukua kwenye ki-Corolla chake hadi nyumbani nilipokuwa naishi!,aliamua kushuka kabisa ili aingie ndani aone ninapoishi!.Sasa wakati anashuka akafungua buti ya gari akatoa begi ambalo siku zote alikuwa akihifadhia zile hela!.

Gabi "Kaka hapa kuna usalama kweli"

Mimi "Hapa kaka kila mtu na time yake,hakuna wakuda"

Gabi "Kama ndivyo basi hakuna shaka,jambo la muhimu ni wewe kuwa makini tu"

Basi baada ya mazungumzo,yeye akawa ameondoka na nikamsindikiza kisha akaniacha pale kijiweni na yeye akawa ameondoka kuelekea Tarime.Basi baada ya kuniacha hapo niliamua kurudi zangu geto kuzitathimini zile hela na kuzipangia mpango mkakati namna ya kuziingiza mtaani,nilianza kuzihesabu usiku ule ndipo nikapata jumla yake milioni 9.Asubuhi kama kawaida kazi ya kuzingiza mtaani ikaendelea na nilikuwa nafanya kwa usiri mkubwa sana.Tangu lile jambo la kuswekwa ndani litokee sikutakaga kabisa kumwambia mshikaji wangu Mtatiro,niliamua kukaa nalo moyoni!.

Nakumbuka kila nilipokuwa nafanya kazi ikifika milioni 1,nilikuwa nampelekea jamaa chake na mimi kubaki nacha kwangu!.Kiukweli ile pesa japo ilikuwa haramu lakini ilikuwa tamu!.Kwa kipindi kile sikuona kabisa kazi nyingine ya kunipatia fedha nyingi na kwa haraka kama ile ya kubadili noti feki,japo nilijua ni kazi hatari lakini ilikuwa imenikolea mno!.

Sasa nakumbuka baada ya miezi kama miwili kupita huku nikiwa naendelea kukimbizana na zile hela hili ziishe niletewe nyingine,nikiwa pale kijiweni nikiendelea na kazi yangu ya upiga debe,kuna meseji ziliingia kwenye simu yangu kwa mfululizo!.Nilipochukua simu mfukoni na kutazama zilikuwa sms zilizokuwa zimetumwa na Gabriel!,basi ikabidi nifungue sms moja baada ya nyingine.

Sms 1 " Umughaka uko wapi?"

Sms 2 "Hizo hela unaweza kuzichoma moto muda huu?"

Sms 3 "Kama unaweza hebu ondoka kabisa hapo kwako na hizo hela"


Sasa baada ya kusoma zile sms kiukweli nilishituka sana,sasa nikakimbia kuweka vocha na kuanza kumpigia Gabriel lakini simu ikawa inaita tu haipokelewi!,baada ya kupiga sana akanitumia sms nyingine tena.

Sms "Nimekwambia kimbia kaka mambo yameharibika,tupo njiani tunakuja kwako!"


Aisee baada ya jamaa kuniambia wanakuja kwangu niliondoka nikikimbia kuelekea nyumbani kama kichaa,nilivuta picha umbali wa kutoka pale Tarime hadi Sirari nikaona kabisa kama gari ilikuwa na spidi kali,basi watakuwa wamebakiza hatua chache!.Nilipofika nyumbani nilifungua mlango kama vile mwizi,nilichukua lile begi nikavaa viatu nakutoka kisha nikaufunga mlango na kukimbia!.

Sasa kuna njia ilikuwa inakupeleka moja kwa moja mpaka mpakani(Mpaka wa Tanzania na Kenya),mimi nikaamua kuipita hiyo na sikutaka kwenda na ile njia kubwa ambayo ingetokezea kwenye lami kisha kijiweni.Nilikuwa nakimbia kama kichaa vile.

Baada ya mwendo mrefu kidogo nikajikuta nimeingia upande wa pili wa Kenya na sikutaka kabisa kuzubaa maana nilikuwa nimechanganyikiwa kabisa!.Sasa baada ya kufika ng'ambo ya pili ya upande wa Kenya pale mpakani Isebania,nilijaribu kuipiga ile namba ya Gabriel ikawa haipatikani!.Nilichokifanya nilichukua elfu 50 ya Tanzania nikaibadili pale mpakani kisha nikaenda stage(stand) nikapanda shuttle zilizokuwa zinakwenda Migori.

Sikufahamu nakwenda Migori kufanya nini lakini niliona bora kukimbia kuliko kukamatwa nikaozee gerezani,nilifahamu kile kitendo cha Gabriel kuniambia nikimbie kilikuwa ni kitendo cha hatari na uenda yeye tayari alikuwa mikononi mwa ndata!.
Yaani hapa mwisho unapoelezea kuwa ulikuwa ukikimbia na huku mapigo yangu ya moyo yalikuwa yakienda kasi. Kiongozi unajua kuandika. Hongera sana
 
Baada ya wiki Mungu akijaalia ntakuja kuisoma tena..i hope itakuwa imesogea sogea.

Nakumbuka niliwahi kusoma kitabu cha story za shigongo chenye page kama 500 na ushee kwa muda wa siku mbili tu. Au ww umughaka ni shigongo uliyejificha ktk fake id??
 
Yani mtuhumiwa yupo mikononi mwa polisi na bado anachatiii....hiiii bangosha nehene loloo
 
Wakati mansubiria mwendelezo pitieni hapa kwa mzee wa JF. Simulizi yake inasisimua kwelikweli
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 11.




Nililipa kiasi cha Ksh 50 kwenye Hiace(Shuttle) iliyokuwa ikielekea Kisumu na niliwaambia waniache Migori.Migori ni mji ambao ulikuwa ni mkubwa tu na hapo kabla sikuwahi kufika lakini katika stori za washikaji walikuwa wakidai ni mji ambao ulikuwa jirani sana na Isebania,nilichokua nimepanga ni kwamba nikifika hapo mji wa Migori nitajua cha kufanya,jambo la msingi ni kutoka kwanza hapo Sirari ambapo hali ya hewa ilikuwa imechafuka!.

Nikiwa kwenye gari nilikuwa nimekumbatia kile kibegi ambacho hakikuwa kizito na kiukweli nilikuwa kama nimepagawa na kuduwazwa na ile hali ya hofu niliyokuwa nayo!.Tulitumia takribani nusu saa mpaka dakika arobaini kufika hapo mjini Migori!.

Nilipofika nilishuka na nilitembea kuelekea juu kama narudi tena Sirari,sasa nilipofika kwa mbele nilikutana na jamaa nikamuuliza anielekeze ilipo Guest House ili niende nikapumzike,sasa kwa wale jamaa wao walikuwa wanaita Lodge,ulikuwa ukiuliza neno Guest House kidogo wanakushangaa,basi jamaa akawa amenionyesha Lodge moja ambayo haikuwa mbali na ile stage(stand).

Nilifika pale nikauliza vyumba nikaambiwa ni Ksh 350,nilichomoa hela nikawa nimempa kisha nikaonyeshwa chumba changu!.Kiukweli baada ya kuingia chumbani akili yangu ilitulia sasa!,niliingia bafuni kuoga na nilipomaliza nililala sana na nimekuja kushituka ikiwa mida ya 12 jioni!,basi nikaamua kuamka ili niende kutafuta mahali walipokuwa wanauza msosi ili nitwange nirudi ndani,sasa nilijaribu kumuuliza yule jamaa wa pale mapokezi akawa amenionyesha kimgahawa ambacho hakikuwa mbali na lile eneo,sasa baadae nilikuja kufahamu kumbe mwenye ule mgahawa ndiye aliyekuwa mwenye ile Lodge!.

Nilipofika hapo Migori kiukweli kilichonichanganya ni namna ya kuitumia hela ya Kenya kiusahihi,kuna muda nadhani nilikuwa naibiwa kwasababu sikuwa na muda wa kuanza kuhesabu hesabu vichenji vilivyokuwa vinabaki!.

Sasa wakati natoka Sirari,kwenye lile begi nilikuwa na kiasi cha Tsh milioni 5,na sikufahamu nitazifanyia nini nikiwa hapo Migori!,Sasa asubuhi kulipokucha niliamka mida ya 4 asubuhi nikanawa uso na kupiga mswaki kisha nikaondoka kuelekea pale kwenye kile ki-mgahawa ili kupata chai!.Ule mgahawa ilionekana kwa lile eneo ulikuwa unauza sana kwasababu ile jioni na hata asubuhi nilipoingia nilikuta kuna watu wengi wakipata vyakula mbalimbali,sasa wakati nimeagiza chai na chapati nikiwa nasubiria,ghafla waliingia jamaa wawili wakiwa wamevaa makoti ya kijeshi na suruali za kijani huku wakiwa na bunduki!,nilipata hofu sana lakini nikawa mtulivu,sasa kumbe wale jamaa walikuwa ni askari wa Kikenya na ndivyo walivyokuwa wakivaa,haukupita muda waliongezeka na wengine wawili wakiwa na silaha kama wenzao!.Basi nao walikaa wakawa wameagiza chai wakaendelea kunywa!.

Muda huo nilijikausha kama sina habari na mtu,namshukuru Mungu pia na wao hawakuwa na habari na mtu!,walipomaliza walinyanyuka wakawa wameondoka,sasa nilikuja kugundua kumbe lile eneo nililokuwepo halikuwa mbali na kituo cha polisi hapo Migori na kituo chenyewe kilikuwa barabarani kabisa,niliona lile eneo si sahihi kwangu,hivyo nikapanga ikifika mchana niondoke lile eneo nikatafute Lodge nyingine ambayo itakuwa mafichoni kidogo!. Kiukweli ile hela niliyokuwa nimebadili ilimalizika siku hiyo baada ya kutafuta Lodge nyingine iliyokuwa pembeni ya mji kama unaelekea Kisumu,sasa hofu ilianza kunijaa namna nitakavyoweza kusavaivu kwa kipindi chote nitakachokuwa huko!.

Ilipofika mida ya jioni nilitoka nikaelekea pale stendi kwa mguu na nilipofika jamaa walidhani ni abiria wakaanza kunichangamkia na niliwaeleza mimi si abiria,nilikaa pembeni kujaribu kuangalia namna wanavyofanyakazi lakini kila nikijaribu kuangalia mdau angalau nilete mazoea lakini hola!,kiukweli sikufahamu nitaishije yale mazingira ambayo sikuyazoea!.Utofauti niliuona pale stendi ni kwamba jamaa walionekana kujitahidi kuchangamka lakini bado washikaji na wahuni niliokuwa nikifanya nao kazi pale Sirari walikuwa wamewazidi wale wajaluo kwa uchangamfu!.Basi siku hiyo niliamua kurudi zangu pale Lodge ambako nililala mpaka asubuhi,ilipofika mida ya saa 3 asubuhi nilitoka zangu nikarudi pale stendi kushangaa,sasa nikasogea zilipokuwa zinapaki gari za kuelekea Isebania,pale niliwakuta jamaa wanaongea kikurya hivyo nikajiona kabisa kama nipo Sirari,sasa kuna dogo alikuwa konda akiita abiria kwenye zile shuttle na alikuwa amevaa tisheti iliyokuwa na picha ya Chege na Temba huku ikiwa imeandikwa TMK WANAUME,sasa baada ya kumcheki kwa muda mrefu yule dogo ni kama alinivutia kwa namna alivyokuwa mchangamfu!,sasa baada ya kuitia ile shuttle na kujaza,nilimsogelea kutaka angalau mazoea nae ili ikiwezekana yeye ndiye aifanye ile kazi ya kubadili zile hela wakati nikiwa kule!.

Mimi "Mwanangu mambo niaje?"

Dogo "Ni bomba bro!"

Mimi "Una muda mrefu sana hapa eeh!"

Dogo "Yes bro tuko hapa kitambo!"

Sasa wakati naongea nae hakusita kuniuliza kama mimi ni Mtanzania maana ongea yangu na yake ilikuwa tofauti kabisa!.

Mimi "Unaitwa nani mwanangu?"

Dogo "Mimi naitwa Joe lakini wengi huniita Mkamilifu!"

Dogo "Na wewe bro majina yako nani?"

Mimi " Mimi naitwa Umughaka"

Dogo "Its your first time hapa Migori?"

Mimi "Hapana,huwa nakuja mara kibao tu!"

Dogo "Mi pia huwa nakwenda Sirare kwa jamaa zangu"

Sasa wao kwa kule badala ya kuita Sirari,wao walikuwa wakiita Sirare na hata shuttle zao zote za kuelekea Sirari zilikuwa zimeandikwa Sirare,nadhani ilikuwa ni lafudhi tu lakini walikuwa wakimaanisha Sirari!.Sasa dogo alionekana kupafahamu vizuri Sirari na hata maeneo baadhi niliyomtajia alionekana kuyafahamu!.Pia nilimdanganya kwamba hapo Migori mimi sikuwa mgeni ili isije akawa mkora akatafuta genge la kihalifu wakanifanya kitu mbaya!.

Sikutaka stori nyingi kwasababu sikuwa na hela ya kunivusha siku itakayofuata,nilitaka yeye ndiye akawe chambo wa kubadili zile hela na nilipanga endapo kikinuka basi ningechafua hapo Migori kuendelea kusonga mbele!.


Mimi "Hivi hapa ni maeneo gani wanabadili hela"

Dogo "Ooh kwani una haraka sana bro,huwezi subiri nimalize hii job then nikuonyeshe!"

Mimi "Sawa haina noma"

Basi dogo akaendelea kupambana na ile kazi ya kuita abiria mpaka akawa amejaza tena gari ya pili,hiyo ilikuwa mida ya saa 7 mchana!.

Dogo "Naweza kukuelekeza sasa"

Basi dogo akawa amenichukua mpaka kwenye jengo moja ambalo tukaingia ndani tukakuta maduka kibao,sasa mimi baada ya kuingia mle ndani kiukweli niliona siwezi kubadili zile hela kwenye mazingira yale kwasababu ningedakwa tu!.Sasa nilimchukua dogo nikatoka nae nje nikamwambia twende mpaka kwenye ile Lodge niliyofikia kisha nikamwambia nitamlipa hela ili kufidia muda wake!.Tulipofika kwenye ile Lodge nilimuacha dogo pale mapokezi nikamwambia anisubiri,nilifungua lile begi nikatoa laki moja kisha nikaitia mfukoni nikawa nimefunga kile chumba na kutoka nje!.

Mimi "Nakupa hizi hela naomba ukabadili sehemu nyingine tofauti na pale pa mwanzo kwasababu wale jamaa wanakata hela kubwa"

Dogo "Ok bro kuna jamaa mmoja yupo hapo ng'ambo nampelekea huwa ana-exchange pesa ya Tz,nikukute basi hapa"

Mimi "Nitakulipa vizuri ukifanya vizuri!"

Dogo "Sawa bro nikukute hapa,sa hii tu nakuja!"

Mimi "Uwe muaminifu"

Dogo "Ahahaha bro ndiyo maana nikaitwa Mkamilifu,we uliza watu wote kwa pale stage hakuna ambae hanijui!"

Mimi "Sawa nakusubiri".


Basi dogo alitoka akikimbia akielekea kwa huyo jamaa kubadili ile hela niliyompatia,ile hela kama nilivyosema hapo awali ya kwamba,ulikuwa ukiiangalia kiukweli hakukuwa na shaka yeyote kwamba ilikuwa ni pesa halali kwa matumizi,uenda kama ungeiweka kwenye mashine au ungekuwa na utambuzi wa hela feki ndipo ungeifahamu!.Nilipompa dogo ile hela nilikuwa nina mambo niliyokuwa nayafikiria kichwani,kama angekimbia basi kwangu isingeniuma kwasababu nilikuwa nazo za kutosha,na kama angefanikiwa kubadili basi ndiye angekuwa rafiki yangu kwa kipindi ambacho ningekuwa hapo,lakini pia kama wangemdaka nilipanga kutoweka kama kipanga!.

Basi baada ya kama nusu saa nikiwa pale nje,nilimuona dogo kwa mbali akiwa anakuja!.

Safi sana itasonga leo ama kesho?
 
Back
Top Bottom