Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua Nyumbani

Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua Nyumbani

Vitu viwili vya kufikirisha;
1. Siku zote nimekaa pale Sorari sikuwa na demu wala sikuwahi kwenda kulala na demu guest na pale nilopopanga sikuwahi kuleta demu. Inawezekanaje mwanaume kukaa muda wote huo bila kupiga demu?

2. Mwanangu Nyamori aliniambia nishuke hapo Bunda kuna kijiji kuna mgodi unatema sana madini, baada ya kufika huyo huyo Nyamori anamuambia hapa hakuna kitu tunapoteza tu muda.
Just enjoy and move on brother,

HUJAMLIPA.
 
Kwani kuchambua Kuna shida gani? CCM imewaharibu Sana.
Akili za vijana wa tanzania mda wote wanawaza siasa. Tatizo ujuaji unawaponza. Mtu kaandika story yake napo unataka uje ujifanye makamo wake we ndo ulimzaa?

Sasa akudanganye kwenye hadithi ambayo haikuingizii hata mia seriously? Nyie kwenye chama chenu mmekaririshwa kubishana kwenye kila kitu? Kha
 
Akili za vijana wa tanzania mda wote wanawaza siasa. Tatizo ujuaji unawaponza. Mtu kaandika story yake napo unataka uje ujifanye makamo wake we ndo ulimzaa? Sasa akudanganye kwenye hadithi ambayo haikuingizii hata mia seriously? Nyie kwenye chama chenu mmekaririshwa kubishana kwenye kila kitu? Kha
Kaka, siku hizi watu wengi hawapo timamu, wanatafuta ubishani kwenye kila jambo ili wajione wapo sawa... wapotezee
 
ANGALIZO


Episode kadhaa zinazofuata zinaukakasi,uenda zikakuudhi na zikakukera!.

Naomba mniwie radhi maana hapa nasema kile nilichokipitia na huko nilishaacha muda mrefu,mimi kwasasa ni raia mwema kama mlivyo nyie,hivyo msinihukumu kwa yaliyopita!.

Nia na madhumuni ni kujifunza na kuwatahadharisha vijana wenzangu kuachana na maisha ya starehe ya muda mfupi.

Nawapenda sana.
Nikimkumbuka Analyze,Elvis Musiba aka Willy Gamba Holy him na Sasa Umghaka napenda kusema,mkoa wa Mara una good story tellers.
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 18.



Muda si mrefu tulifika kwenye nyumba fulani ambayo ilikuwa ndani ya geti,geti lilifunguliwa ndipo tukazama ndani.Dereva yule aliteremka akawa anatuongoza kuelekea ndani.Mazingira yale yalikuwa yametulia sana na nyumba ile ilikuwa pembezoni mwa mlima!.


Gabi "Ooh wanaume wapambanaji wa kikurya!"

Gabi alipotuona alifurahi sana na kiukweli tulikumbatiana kwa furaha!.Nilimshangaa sana Gabi safari hii kwasababu alikuwa amebadilika sana tofauti na miezi michache iliyokuwa imepita,safari hii alikuwa ameachia ndevu kidevuni mwake na mashavuni kiasi kwamba kuficha uhalisia wake ambao nilikwisha kuuzoea!.

Gabi "Vipi wewe mbona hupatikanagi!?"

Mimi "Nilibadili namba kaka"

Gabi "Mambo yanakwendaje lakini!"

Mimi "Tupo tunapambana kaka"

Gabi "Jamaa bhana walinishikiria kwa siku kadhaa ila walitema nyongo!"

Mimi "Walikuja mpaka pale kwako au ilikuwaje kaka"

Gabi "By the way ni stori ndefu lakini niwaambie kitu,Kama huna hela utakufa njaa lakini mwenye hela huchelewa tu kula ila hafi njaa"

Aliendelea "Pesa ndo kila kitu"

Gabi "Vipi lakini mwanangu ule mzigo ilikuwaje?"

Mimi "Kaka ulivyoniambia mko njiani mnakuja mimi nilitoroka nao nikafika mahali nikauchoma moto!"


Gabi "Ahahaha ya kwamba Mkurya ulisanda,sio!"

Aliendelea "Wala usijali yale tuliyamaliza,tunachopaswa kufanya ni kuangalia yaliyoko mbele yetu!"


Gabi "Siku hizi mnafafanya shughuli gani aisee!"


Mtatiro "Braza tunapambana na mitumba"

Gabi "Sasa hiyo inawalipa kweli!?"

Aliendelea "Hebu ngoja kwanza niwaambie wawalete msosi mtandike wanangu!"


Baada ya muda chakula kililetwa na mama mmoja wa makamo ambaye kimuonekano alikuwa na miaka zaidi ya Hamsini,basi tulianza kula kile chakula wakati huo Gabriel hakiwa hayupo sebuleni,alirudi tukiwa tumemaliza kula na akatutaka tutoke kuelekea town tukapate bia mbili tatu!.
Tulipanda ile Land cruiser tukaondoka kuelekea mjini ambapo tulifikia Hotel ya kifahari ya Gold crest,Tulipofika pale tulipanda kwenye lift ambayo ilituvuta kwenda juu kabisa mwisho wa lile jengo,tuliingia kwa juu ambako nilikuta kuna uwazi wa kutosha huku watu wakiwa wanapata vyakula na vinywaji!.

Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuingia kwenye Hotel ya kifahari iliyokuwa hapo Mwanza,kiukweli nili enjoy sana maana mandhari yote ya jiji la Mwanza ilikuwa ikionekana hapo.Tulitafuta meza yetu tukawa tumekaa,Gabi aliagiza pombe Kali mchupa mkubwa na akawa ametutaka na sisi kila mmoja kuagiza tulichokuwa tunakunywa!.

Mtatiro akawa ameniambia tuagize li Jack Daniel chupa kubwa ili tulichape wawili,hivyo ndivyo tulivyofanya!.Hapo kabla sikiwahi kunywa pombe kali,nilikuwa nikinywa vibia vyangu kadhaa natulia,hiyo ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kunywa pombe kali!.Yule dereva yeye alikuwa akinywa maji muda wote tuliokuwa hapo.

Baada ya pombe kuanza kukolea,maongezi nayo yalichukua nafasi!.

Gabi "Wanangu mimi huwa nawakubali sana katika mapambano!"

Aliendelea "Nyie ni miongoni mwa marafiki zangu wakubwa na sitowaacha ndugu zangu!"

Gabi "Jioni kuna mahali nataka twende ndugu zangu!"

Mtatiro "Kuna dili jipya kaka?,wewe tupe dili sisi tupige tunachotaka ni hela!"

Gabi "Hilo wala msijali,nyie ni wanangu wa damu lazima kila dili niwe nawakumbuka!"

Baada ya kupiga mtungi kwa muda mrefu,Gabi alimwambia yule dereva aondoke atuache na sisi tungechukua taksi kwasababu tulikuwa na safari nyingine!.Baada ya yale mazungumzo nikiona Gabi anatoa pochi iliyokuwa imesheheni noti za elfu kumi kumi akachomoa elfu 50 akamkabidhi jamaa huku akimwambia atampigia simu!.


Gabi "Wanangu sikieni,huyo dogo ni mtoto wa dingi mdogo na pale alipowaleta ni nyumbani kwao,ingawaje pia wana nyumba nyingine Arusha ambako wanakaa ndugu zake na wadogo zake!"

Aliendelea "Dingi yake ni marehemu na baada ya kugawiwa pesa za urithi dogo akaona aje amalizie hiyo nyumba ya Mwanza aishi yeye na ile ya Arusha awaachie wadogo zake!"

Mtatiro "Anapiga ishu gani?"

Gabi "Dogo anasema anagereji ila sijajua ipo maeneo gani,alichezea sana hela dogo msimuone vile,hilo li cruiser alinunua tukamshauri alipeleke Arusha lipige kazi lakini naona kama haelewi!"


Basi baada ya mazungumzo hayo huku tukiendelea kukata maji machungu!,ilipofika mida ya saa 1 usiku tulionodoka kutafuta Taksi na kuelekea maeneo ambayo Gabi alikuwa akiyafahamu!.Tulifika kwenye nyumba moja ambayo ilikuwa kimya sana hata kabla nilidhani haikuwa na umeme kumbe taa zilikuwa zimezimwa!,baada ya ile Taksi kuondoka Gabi alipiga simu akazungumza na mtu mmoja ambaye bila kuchelewa alitufungulia geti tukazama ndani.

Tulipoingia ndani tulipelekwa hadi sebuleni ambapo nako hakukuwa na mwanga wa taa ila baada ya kukaa kwenye kochi ndipo taa ya sebuleni iliwashwa,sasa baada ya ile taa kuwashwa kulikuwa na jamaa wawili pale sebuleni ambao walikuwa wamejengeka vizuri mno kimisuli huku usoni mwao hakukuwa hata na chembe ya tabasamu!.Tulipoingia ndani,Gabi yeye moja kwa moja alipitiliza ndani huko vyumbani na hatukufahamu alienda kufanya nini!.

Baada ya muda alikuja Gabriel akiandamana na Jamaa mmoja aliyekuwa amenyoa upara,pia hakuwa na ndevu hata kidogo maana zote alikuwa amezipiga wembe!.

Gabi "Aisee mnaweza kutupisha kidogo tunamazungumzo"

Wale jamaa wawili tuliowakuta hapo walinyanyuka wakawa wameondoka kuelekea huko ndani!.

Gabi "Mkuu hawa ndio vijana niliokueleza tangu wiki iliyopita tukiwa Arusha!"

Aliendelea "Huyu anaitwa Mtatiro na huyu anaitwa Umughaka"

Gabi "Ni wakurya majasiri sana kama nilivyokwambia"
Aliendelea "Ndugu zangu huyu ni bosi wangu bila shaka pia atakuwa bosi wenu"

Gabi "Nadhani bosi karibu uzungumze chochote!"

Yule tuliyeambiwa ni bosi wa Gabi alianza kutuangalia kwa makini sana huku akitukazia macho kiasi kwamba kila mtu kama alianza kuingiwa na hofu!.


Bosi "Nyie ni Wakurya kutokea wapi bhana!"


Mtatiro "Tumetokea Tarime"

Bosi "Tarime ni kubwa"

Mtatiro "Wote tunatokea sehemu moja pale Tarime mjini"

Bosi "Ninaposema Tarime nahitaji kujua jina la kijiji au mtaa mnaotokea!"

Mtatiro "Tunatokea Rebu"

Bosi "Wewe una miaka mingapi?"


Mimi "Nina miaka 23"

Bosi " Na wewe?"

Mtatiro "Mi nina miaka 27"

Bosi "Mmewahi kufanya kazi gani ambayo ilitishia kuyakatisha maisha yenu uhai!?"


Baada ya hilo swali tulibaki kujiuma uma ndipo Gabi akaingilia kati kusaidia kujibu!.

Gabi "Bosi hawa wote nilikuwa nafanya nao ile kazi ndiyo maana nina waamini!"

Bosi "sawa,bila shaka umewaambia!"

Gabi "Hapana mkuu sijawaambia chochote"

Bosi "Ilipaswa uwaambie ili mwenye kuamua aamue,sitaki mtu mwenye roho ya kike kwenye kazi zangu!"

Aliendelea "Sasa nyie nisikilizeni kwa makini,naitwa Afande........,je mmewahi kutumia bunduki?"

Baada ya kutaja neno bunduki kiukweli akili yangu ilitaka kuchanganyikiwa,nilijikuta kale kapombe nilikokuwa nimekunywa kote kalikata!.Mimi niliitikia kwa kutikisa kichwa kuashiria hapana lakini Mtatiro alimjibu!.


Mtatiro "Hapana"

Bosi "Je mko tayari kutumia bunduki?"


Mimi nilisita kuitikia ila mwenzangu Mtatiro alikuwa na ujasiri sana kujibu like swali!.

Mtatiro "Ndiyo mimi nipo Tayari!"

Bosi "Na wewe je?"

Baada ya Mtatiro kujibu lile swali na mimi nikajikuta namfuatisha Mtatiro.

Mimi "Nipo Tayari!"

Bosi "Sasa nyie ndiyo wakurya ninao wafahamu,nimewapenda!"

Baada ya yale mazungumzo yule bosi aliondoka akarudi ndani akasema tumsubiri kwanza anarudi!.
Unaenda kucheka nao na zakichwa za kichwa
 
Akili za vijana wa tanzania mda wote wanawaza siasa. Tatizo ujuaji unawaponza. Mtu kaandika story yake napo unataka uje ujifanye makamo wake we ndo ulimzaa? Sasa akudanganye kwenye hadithi ambayo haikuingizii hata mia seriously? Nyie kwenye chama chenu mmekaririshwa kubishana kwenye kila kitu? Kha
Kwa taarifa yako,kubishana ndiyo msingi wa maendeleo.Jamii isiyobishana ni jamii mfu,jamii ambayo haifikiri bali jamii ya ndiyo Mzee.
 
Umekuwa mtu mmoja wa kutufikirisha sana,wengi wetu si wapenzi wa kutafuta vitabu,hakika unatenga muda wako wa kutunga,kuhariri na kutupostia sisi wadau ambao kuna muda hatuna Shukran,post zako zimezingatia Fasihi sahihi kabisa na wengi wetu inatufanya kupelekea lugha ya picha mjongeo akilini mwetu vile sura na mwili kwa ujumla wa Umughaka ulivyo,Gabi sura yake na mwili wake pamoja na wahusika wengine,pia shukran kwa uandishi ulio nyooka hakuna kukosea/kuchapia najua unatenga muda rafiki na muda wa kutosha kwa ajili ya wengi na wachache tusiojua kushukuru.
Wewe ni mmoja wa watu wachache sana wenye ustaarabu uliotukuka humu most of members humu Wana majibu ya kijinga sana
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 18.



Muda si mrefu tulifika kwenye nyumba fulani ambayo ilikuwa ndani ya geti,geti lilifunguliwa ndipo tukazama ndani.Dereva yule aliteremka akawa anatuongoza kuelekea ndani.Mazingira yale yalikuwa yametulia sana na nyumba ile ilikuwa pembezoni mwa mlima!.


Gabi "Ooh wanaume wapambanaji wa kikurya!"

Gabi alipotuona alifurahi sana na kiukweli tulikumbatiana kwa furaha!.Nilimshangaa sana Gabi safari hii kwasababu alikuwa amebadilika sana tofauti na miezi michache iliyokuwa imepita,safari hii alikuwa ameachia ndevu kidevuni mwake na mashavuni kiasi kwamba kuficha uhalisia wake ambao nilikwisha kuuzoea!.

Gabi "Vipi wewe mbona hupatikanagi!?"

Mimi "Nilibadili namba kaka"

Gabi "Mambo yanakwendaje lakini!"

Mimi "Tupo tunapambana kaka"

Gabi "Jamaa bhana walinishikiria kwa siku kadhaa ila walitema nyongo!"

Mimi "Walikuja mpaka pale kwako au ilikuwaje kaka"

Gabi "By the way ni stori ndefu lakini niwaambie kitu,Kama huna hela utakufa njaa lakini mwenye hela huchelewa tu kula ila hafi njaa"

Aliendelea "Pesa ndo kila kitu"

Gabi "Vipi lakini mwanangu ule mzigo ilikuwaje?"

Mimi "Kaka ulivyoniambia mko njiani mnakuja mimi nilitoroka nao nikafika mahali nikauchoma moto!"


Gabi "Ahahaha ya kwamba Mkurya ulisanda,sio!"

Aliendelea "Wala usijali yale tuliyamaliza,tunachopaswa kufanya ni kuangalia yaliyoko mbele yetu!"


Gabi "Siku hizi mnafafanya shughuli gani aisee!"


Mtatiro "Braza tunapambana na mitumba"

Gabi "Sasa hiyo inawalipa kweli!?"

Aliendelea "Hebu ngoja kwanza niwaambie wawalete msosi mtandike wanangu!"


Baada ya muda chakula kililetwa na mama mmoja wa makamo ambaye kimuonekano alikuwa na miaka zaidi ya Hamsini,basi tulianza kula kile chakula wakati huo Gabriel hakiwa hayupo sebuleni,alirudi tukiwa tumemaliza kula na akatutaka tutoke kuelekea town tukapate bia mbili tatu!.
Tulipanda ile Land cruiser tukaondoka kuelekea mjini ambapo tulifikia Hotel ya kifahari ya Gold crest,Tulipofika pale tulipanda kwenye lift ambayo ilituvuta kwenda juu kabisa mwisho wa lile jengo,tuliingia kwa juu ambako nilikuta kuna uwazi wa kutosha huku watu wakiwa wanapata vyakula na vinywaji!.

Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuingia kwenye Hotel ya kifahari iliyokuwa hapo Mwanza,kiukweli nili enjoy sana maana mandhari yote ya jiji la Mwanza ilikuwa ikionekana hapo.Tulitafuta meza yetu tukawa tumekaa,Gabi aliagiza pombe Kali mchupa mkubwa na akawa ametutaka na sisi kila mmoja kuagiza tulichokuwa tunakunywa!.

Mtatiro akawa ameniambia tuagize li Jack Daniel chupa kubwa ili tulichape wawili,hivyo ndivyo tulivyofanya!.Hapo kabla sikiwahi kunywa pombe kali,nilikuwa nikinywa vibia vyangu kadhaa natulia,hiyo ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kunywa pombe kali!.Yule dereva yeye alikuwa akinywa maji muda wote tuliokuwa hapo.

Baada ya pombe kuanza kukolea,maongezi nayo yalichukua nafasi!.

Gabi "Wanangu mimi huwa nawakubali sana katika mapambano!"

Aliendelea "Nyie ni miongoni mwa marafiki zangu wakubwa na sitowaacha ndugu zangu!"

Gabi "Jioni kuna mahali nataka twende ndugu zangu!"

Mtatiro "Kuna dili jipya kaka?,wewe tupe dili sisi tupige tunachotaka ni hela!"

Gabi "Hilo wala msijali,nyie ni wanangu wa damu lazima kila dili niwe nawakumbuka!"

Baada ya kupiga mtungi kwa muda mrefu,Gabi alimwambia yule dereva aondoke atuache na sisi tungechukua taksi kwasababu tulikuwa na safari nyingine!.Baada ya yale mazungumzo nikiona Gabi anatoa pochi iliyokuwa imesheheni noti za elfu kumi kumi akachomoa elfu 50 akamkabidhi jamaa huku akimwambia atampigia simu!.


Gabi "Wanangu sikieni,huyo dogo ni mtoto wa dingi mdogo na pale alipowaleta ni nyumbani kwao,ingawaje pia wana nyumba nyingine Arusha ambako wanakaa ndugu zake na wadogo zake!"

Aliendelea "Dingi yake ni marehemu na baada ya kugawiwa pesa za urithi dogo akaona aje amalizie hiyo nyumba ya Mwanza aishi yeye na ile ya Arusha awaachie wadogo zake!"

Mtatiro "Anapiga ishu gani?"

Gabi "Dogo anasema anagereji ila sijajua ipo maeneo gani,alichezea sana hela dogo msimuone vile,hilo li cruiser alinunua tukamshauri alipeleke Arusha lipige kazi lakini naona kama haelewi!"


Basi baada ya mazungumzo hayo huku tukiendelea kukata maji machungu!,ilipofika mida ya saa 1 usiku tulionodoka kutafuta Taksi na kuelekea maeneo ambayo Gabi alikuwa akiyafahamu!.Tulifika kwenye nyumba moja ambayo ilikuwa kimya sana hata kabla nilidhani haikuwa na umeme kumbe taa zilikuwa zimezimwa!,baada ya ile Taksi kuondoka Gabi alipiga simu akazungumza na mtu mmoja ambaye bila kuchelewa alitufungulia geti tukazama ndani.

Tulipoingia ndani tulipelekwa hadi sebuleni ambapo nako hakukuwa na mwanga wa taa ila baada ya kukaa kwenye kochi ndipo taa ya sebuleni iliwashwa,sasa baada ya ile taa kuwashwa kulikuwa na jamaa wawili pale sebuleni ambao walikuwa wamejengeka vizuri mno kimisuli huku usoni mwao hakukuwa hata na chembe ya tabasamu!.Tulipoingia ndani,Gabi yeye moja kwa moja alipitiliza ndani huko vyumbani na hatukufahamu alienda kufanya nini!.

Baada ya muda alikuja Gabriel akiandamana na Jamaa mmoja aliyekuwa amenyoa upara,pia hakuwa na ndevu hata kidogo maana zote alikuwa amezipiga wembe!.

Gabi "Aisee mnaweza kutupisha kidogo tunamazungumzo"

Wale jamaa wawili tuliowakuta hapo walinyanyuka wakawa wameondoka kuelekea huko ndani!.

Gabi "Mkuu hawa ndio vijana niliokueleza tangu wiki iliyopita tukiwa Arusha!"

Aliendelea "Huyu anaitwa Mtatiro na huyu anaitwa Umughaka"

Gabi "Ni wakurya majasiri sana kama nilivyokwambia"
Aliendelea "Ndugu zangu huyu ni bosi wangu bila shaka pia atakuwa bosi wenu"

Gabi "Nadhani bosi karibu uzungumze chochote!"

Yule tuliyeambiwa ni bosi wa Gabi alianza kutuangalia kwa makini sana huku akitukazia macho kiasi kwamba kila mtu kama alianza kuingiwa na hofu!.


Bosi "Nyie ni Wakurya kutokea wapi bhana!"


Mtatiro "Tumetokea Tarime"

Bosi "Tarime ni kubwa"

Mtatiro "Wote tunatokea sehemu moja pale Tarime mjini"

Bosi "Ninaposema Tarime nahitaji kujua jina la kijiji au mtaa mnaotokea!"

Mtatiro "Tunatokea Rebu"

Bosi "Wewe una miaka mingapi?"


Mimi "Nina miaka 23"

Bosi " Na wewe?"

Mtatiro "Mi nina miaka 27"

Bosi "Mmewahi kufanya kazi gani ambayo ilitishia kuyakatisha maisha yenu uhai!?"


Baada ya hilo swali tulibaki kujiuma uma ndipo Gabi akaingilia kati kusaidia kujibu!.

Gabi "Bosi hawa wote nilikuwa nafanya nao ile kazi ndiyo maana nina waamini!"

Bosi "sawa,bila shaka umewaambia!"

Gabi "Hapana mkuu sijawaambia chochote"

Bosi "Ilipaswa uwaambie ili mwenye kuamua aamue,sitaki mtu mwenye roho ya kike kwenye kazi zangu!"

Aliendelea "Sasa nyie nisikilizeni kwa makini,naitwa Afande........,je mmewahi kutumia bunduki?"

Baada ya kutaja neno bunduki kiukweli akili yangu ilitaka kuchanganyikiwa,nilijikuta kale kapombe nilikokuwa nimekunywa kote kalikata!.Mimi niliitikia kwa kutikisa kichwa kuashiria hapana lakini Mtatiro alimjibu!.


Mtatiro "Hapana"

Bosi "Je mko tayari kutumia bunduki?"


Mimi nilisita kuitikia ila mwenzangu Mtatiro alikuwa na ujasiri sana kujibu like swali!.

Mtatiro "Ndiyo mimi nipo Tayari!"

Bosi "Na wewe je?"

Baada ya Mtatiro kujibu lile swali na mimi nikajikuta namfuatisha Mtatiro.

Mimi "Nipo Tayari!"

Bosi "Sasa nyie ndiyo wakurya ninao wafahamu,nimewapenda!"

Baada ya yale mazungumzo yule bosi aliondoka akarudi ndani akasema tumsubiri kwanza anarudi!.

Ooooh my God UMUGHAKA sasa umeyakanyaga aiseee[emoji56][emoji56][emoji56][emoji56][emoji56][emoji56][emoji846]
 
Aisee huyu Mtatiro ni Tommy Higan kabisa! Yani hapo Umughaka umedandia mtubwi wa vibwengo aiseeee ...mtatiro bwege sana..[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Weeee mm japo sipigi dili haram lkn akija boss na gari ya style hio ofisini sipand namwambia tangulia nakufata nyuma na pkpk
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom