Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua Nyumbani

Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua Nyumbani

Tunachokipinga hapa ni ujuaji wa kijinga, na most katika watu wa aina hii story hawaifatilii kiundani. Wanaosoma juu juu kutafuta cha kukosoa.

Na lau kama logic ingekua inatumika someone asinge hamaki, kupigiwa sim akakinbia kwenda alikopigiwa sim.

Kila kiumbe ana udhaifu wake, na udhaifu wake upo pale alipowekeza hisia zake. Mfano like family, mpenzi au rafiki wa kariiiibu sana! And you know what happen pale hisia zinaposhinda akili. Ni ku-act indecisively, sasa kama hilo mtu haezi ling'amua unajikutaje mchambuzi?


Of course na we pia bestie waonekana hufatilii story au msahaulifu... Sasa ukiwa na hizi sifa mbili don't judge ishia kua mtazamaji. Anyway kama kauli ni kali nisamehe bure ndugu yangu!

Nasema sio mfatliaji ama msahaulifu kwanini?

Ngoja nikukumbushe, baada ya uvamizi wao wa awali, unakumbuka baada ya kupewa chao 1.9M wagawane waliambiwa wakanunue sim zingine kisha gharama wampe boss wao kua atawareheshea kila kitu?

Sasa unasemaje kwamba walikua hawana mawasliano?

Again katika maisha yako hujawah kupoteza kifaa chako cha mawasiliano? Kama ndio, vipi ndio ulikuwa mwisho wako wa kufanya mawasiliano yako hadi leo?

Tuache mindset ya kibongo Movie 🤣, scenes ya kula tuanzie jikoni kuwasha moto... Maji yachemke... Ioneshwe mwiko ulio tumika en so so so so ndio kipakuliwe wahusika wale. Ilihali ile kukaa mezan kula ilitosha kuonesha kua watu wale wamekula chakula.

Tuchukue tulichojifunza kwenye story basi maisha yanedelee hatufanyi udahili wa uandishi hapa tupeane brake!

Mtajiuliza kwanini tunamkingia kifua, of course yes, Ni yeye na sio nyie aliye jitolea mda wake buuuuuure kabisa kwa ajili ya kufundisha na kuburudisha wengine. Kwa hayo machache tunaishia kumpongeza life liendelee!

Ila kama mnalipa kwa anachokifanya ruksa kukemea uwekazaji wenu 🖐️.
Tatizo la humu kujua kwingi....kiukweli mimi post za ujuaji sipotezi muda wangu kusoma. Uzuri Umughaka mwenyewe anawapotezea tu.
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 24.



Kamange ndiye aliyekuwa dereva kwenye ile Noah na mara zote alikuwaga hana kabisa stori na mtu!.Tulifanikiwa kufika Geita salama kabisa mida ya saa 6 usiku tukipitia njia ya Kahama,kwa mujibu wa malekezo ya Jipe ni kwamba,endapo tungepitia Kigongo/Busisi yawezekana kabisa tungeweza kugundulika kwenye ukaguzi,hivyo kwakuwa hatukuwa na haraka,jamaa akasema tupitie Kahama.

Baada ya kufika Geita usiku huo,aliyekuwa akituelekeza mahali pa kwenda alikuwa ni Jipe ambaye yawezekana aliifahamu vizuri ile mitaa ya Geita na viunga vyake,binafsi ukiacha siku tuliyoenda na Mtatiro kwenye mnada wa kuuza mitumba huko kwenye kijiji cha Nzera,sikuwahi tena kufika Geita hadi siku hiyo.Sasa Jipe alikuwa akimpatia yule demu dereva maelekezo namna ya kuifata njia yenye uelekeo sahihi wa kutufikisha tunakokwenda!.Haukupita muda tukawa tumefika kwenye nyumba ambayo haikuwa na fensi wala geti,sasa ile nyumba ilikuwa mbali kidogo kutokea pale mjini!.

Mimi,Mtatiro na Jipe tuliteremka wakati huo huo Gabi na Yule demu waliondoka na gari wakaahidi wangerudi kesho asubuhi!.Jipe alianza kugonga mlango wa ile nyumba hatimae mwenyeji akawa amefungua mlango.

Jipe "wachamawe sengi"

Yule mama "Wachatata"

Jipe "Mwasibhao"

Yule "Chasibhao lata,jendeyo"

Jipe "Ni jakisi sengi"


Jipe alinyanyua lile begi ambalo lilikuwa na silaha kwa chini na juu likiwa na nguo baadhi tukawa tumeingia ndani.

Jipe "Aisee huyu ni Shangazi yangu anaishi hapa Geita ni mwalimu,hivyo jisikieni huru"

Aliendelea "Shangazi,hawa ndiyo wale marafiki zangu ambao nilikwambia tunapita kulala hapa halafu kesho tunaelekea Nyarugusu"

Yule mama "Sawa baba,hapa ni kwenu,usijali"

Aliendelea "Mtalala kwenye hicho chumba wanangu"

Yule mama baada ya maongezi ya dakika kadhaa alituacha pale sebuleni akawa ameingia chumbani kwake kulala.

Jipe "Twendeni tukapige mbonji wazee"


Basi tuliingia chumbani tukawa kulala hadi asubuhi,ilipofika asubuhi Jipe aliamka akawa ameondoka pale kwa shangazi yake na akatutaka tusitoke hadi ile gari itakapokuja kutuchukua.Wakati tukiwa hapo kwa huyo mama,Mtatiro alianza kuniambia anajisikia vibaya sana na hali yake si nzuri!.

Mimi "Shida ni nini kwani?"

Mtatiro "Yaani nahisi tu baridi na najisikia kizinguzungu!"

Aliendelea "Ila niko poa wala usijali"

Mimi "Au nikakuchukulie panadol"

Mtatiro "Ngoja jamaa arudi umwambie"

Baada ya muda Jipe alirudi akatutaka tukapande gari tuondoke zetu,nilijaribu kumshirikisha hali ya mshikaji wangu Mtatiro akaniambia watamnunulia dawa tukifika tulikopaswa kwenda!.Tulipotoka nje,yule mama hatukumkuta bali tuliwakuta mabinti wawili wakubwa wakiwa wanaendelea na shughuli zao.

Jipe "Mi naondoka,mtamwambia Shangazi nitarudi"

Binti "Sawa kaka"


Tuliondoka na kushika njia kama tunarudi Mwanza,kuna mahali tulifika tukaikamata barabara ya vumbi iliyokuwa inatutoa nje ya ule mji wa Geita,baada ya kutembea kwa umbali mrefu kidogo hatimaye tukafika kwenye nyumba moja iliyokuwa na tofauli za kuchoma,ambapo Jipe alishuka akaenda kufungua ile nyumba kisha akatutaka tuteremke na kuingia ndani!.Baada ya kufika ndani Jipe akaanza kutoa maelekezo kwa kila mmoja!.

Jipe "Jamani hapa ndipo tutakaa mpaka usiku wa leo,na tukimaliza kufanya kilichotuleta tunaondoka leoleo!"

Aliendelea "Gabi nadhani nenda nilikokwambia"

Jipe "Kamange hakikisha hiyo gari ni nzima,kama kuna tatizo ipeleke gereji muda huu!"

Kamange "Gari inawasubiri nyinyi tu!"

Jipe "Ok,sawa"

Jipe alitoa hela kidogo akawa amempa yule demu aende pharmacy akamnunulie Mtatiro Panadol ili kuondoa ile hali ya sintofahamu aliyokuwa nayo.Sasa kwakuwa ile nyumba ilikuwa na vyombo vya kupikia,Jipe alishauri zikanunuliwe dagaa na unga tuje tukorofishe ili tuweze kupata chakula,na hivyo ndivyo tulivyofanya.Ilipofika mida ya Saa 1 usiku hali Mtatiro ilizidi kuwa mbaya hata baada ya kumeza vidonge,yeye kwa maelezo yake alikuwa akidai anaihisi baridi na kujisikia vibaya mwili mzima.

Jipe "Kwahiyo sa itakuwaje mwanangu"

Aliendelea "Chuma utaweza kushika?"

Mtatiro "Kwani tunaondoka sa hivi?"

Jipe "Mida inakaribia"

Mtatiro "Ngoja tuone"

Sasa ilipofika mida ya saa 4 usiku kuelekea saa 5,Jipe baada ya kuona hali ya Mtatiro haikuwa ya kuridhisha Jipe alinipatia maelekezo!.

Jipe "Umughaka utashika chuma ya Mtatiro"

Mimi "Sawa"

Jipe "Usifanye tofauti na nitakachokwambia"

Mimi "Sawa"

Baada ya nusu saa tukiwa tupo tayari kuondoka,simu ya Jipe ilikuwa ikiita,jamaa aliipokea akaanza kuzungumza. Aliyekuwa amepiga ile simu alikuwa Gabi ambaye yaelekea alikuwa akimpatia maelekezo Jipe.

Jipe "Kamange yuko wapi?"

Mimi "Nadhani atakuwa kwenye gari!"

Jipe "Twendeni"

Aliendelea "Tukitoka huko ni kuondoka tu kurudi Mwanza,hatuna muda wa kupoteza!"

Baada ya kutoka nje ya ile nyumba,Jipe alifunga kofuli kisha ufunguo akauweka juu ya mlango kwenye venti.Tuliondoka lile eneo kuelekea ambako walikuwa wakipafahamu Jipe na Gabi,sisi wengine ilikuwa ni wafuata maelekezo tu.Haukupita muda tukawa tumefika kwenye nyumba zilizokuwa mtaa wa kifahari kweli kweli.

Jipe "Umughaka ile nyumba yenye geti jeusi unaiona?"

Mimi "Ile ya mbele?"

Jipe "Ukiacha hiyo yenye paa refu,ile yenye geti jeusi siunaiona?"

Mimi "Ndiyo"

Jipe "Ok,hakikisha ukifika wewe gonga na wakiuliza nani waambie mimi respis geti,wakifungua tu hiyo kazi nyingine niachie mimi!"

Aliendelea "Kamange nyuma ya hii nyumba kuna njia isiyo rasmi,nenda kapaki hapo tunakukuta"

Kamange "Gabi yuko wapi?"

Jipe "Tutamkuta mbele"

Kamange "Mjulishe kabisa akae standby,sitaki lawama"


Mimi na jipe tulitelemka kwenye ile Noah huku tukiwaacha Kamange na Mtatiro ambaye hali yake haikuwa nzuri.Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuikamata silaha na kiukweli ilikuwa nzito kwa kiasi chake.

Nilichukua kitambaa cha kiujifunika nikakiweka mfukoni huku ile silaha nikiwa nimeiweka kwenye ndani ya koti.Nilipofika kwenye lile geti nilianza kugonga kwa nguvu mara kadhaa!.Wakati nilipokuwa nikigonga lile geti Jipe alikuwa pembeni huku akiwa makini sana.

Sauti ya mwanaume "Naniii !?"

Mimi "Mimi Respis"

Sauti "Nakuja"

Haukupita sekunde 20 lile geti lilifunguliwa kisehemu kidogo kile ch a watu kupita.Geti lilipofunguliwa tu Jipe alisukuma kwa nguvu huku akitoa silaha na kumuonyeshea yule jamaa.Jamaa alitaka kupiga kelele lakini Jipe alimdhibiti akamwambia akipiga kelele atamuua!.

Jipe "Ingia ndani fasta na ufunge hilo geti!"


Jipe alimchukua yule jamaa akiiingia nae ndani huku na mimi nikiwa nyuma nimeshika ile silaha iliyokuwa imenipatia kiburi kisichokua cha kawaida.

Jipe "Kaka yako yuko wapi?"

Yule jamaa "Braza amesafiri"

Jipe "Upo na nani humu ndani?"

Jamaa "Nipo na shemeji yangu pamoja na mdogo wake"

Jipe "Umughaka kaa tayari kwa lolote,ukiona hatari ruksa kuua"

Mimi "Sawa"

Jipe alimchukua yule jamaa ambaye alikuwa akitetemeka kama kashikwa na degedege kisa kuona ile SMG,baada ya muda Jipe alirudi na watu watatu pale sebuleni huku yule mwanamke akiwa ndani ya chupi tu.Alikuwa mwanamke,yule jamaa aliyetufungulia geti pamoja na dogo mmoja wa kiume ambaye kimuonekano alikuwa na miaka 12.

Jipe " Laleni chini mfunike sura zenu"

Aliendelea "wewe mume wako yuko wapi"

Mwanamke "Amesafiri"

Jipe "Kwenda wapi?"

Mwanamke "Ameenda Dar"

Jipe "Nataka pesa,ziko wapi?"

Mwanamke "pesa huwa tunapeleka benki,tafadhali msinifanye chochote twendeni benki nikawapatie"

Jipe "Wewe nitakupasua ubongo,nahitaji pesa wewe unaleta ujinga!"

Mwanamke "Hapa kipo kiasi kidogo,tafadhali usiniue"

Yule mwanamke alikuwa anaongea huku machozi yakimtoka kama mvua,wakati fulani huruma ilikuwa ikiniingia lakini sikuwa na namna!.

Jipe "Zipo shilingi ngapi wewe acha kutupotezea muda!"

Kabla mwanamke hajajibu swali,Jipe alimnyanyua akawa amerudi nae huko chumbani,wakati huo mimi pale sebuleni niliendelea kuwachunga wale madogo huku silaha ikiwa tayari kwa lolote.Baada ya muda Jipe alirudi pale sebuleni akiwa na kanga iliyokuwa imejaa pesa,ile kanga namna ilivyokuwa imefungwa ni kama furushi la nguo chafu.

Jipe aliwaambia wale madogo wasimame wote na tulielekea chumbani ambako aliwaambia waingie chini ya uvungu kisha akafunga mlango kwa nje na funguo.

Baada ya hapo tuliingia kwenye kile chumba cha yule mwanamke na kupekua kika mahali lakini hatukupata pesa nyingine.

Jipe "Ingia chini ya uvungu,ole wako upige kelele ndipo utajua mimi ni nan!"

Yule mwanamke aliingia chini ya uvungu kama kafukuzwa,ndipo jipe alichukua funguo akafunga mlango kwa nje akaniambia tusepe.Tulitoka ndani haraka kuifata ile Noah iliyokuwa imepaki nyuma ya ile nyumba,tuliingia ndani na kuondoka haraka sana lile eneo.

Baada ya mwendo mrefu kidogo huku tukiiacha Geita,kuna mahali tulifika Jipe akamwambia yule demu asimamishe gari.Jipe alitoa simu akaanza kupiga.

Jipe "Uko maeneo gani wewe?"

Aliendelea "Subiri hapo njiani tumekaribia"

Sasa kumbe alikuwa amempigia Gabi akitaka kujua yupo maeneo gani.Baada ya mwendo ambao haukuzidi dakika 3 tulimuona Gabi akiwa barabarani ndipo gari ikasimama akapanda tukaondoka zetu.

Jipe "Umefanikisha"

Gabi "Kama kawa"

Sikuelewa ni kitu gani ambacho Gabi alikuwa akikifanya muda huo huko alipokuwa,hiyo ilibaki ni siri yake yeye na Jipe.

Tulifanikiwa kufika Mwanza saa 11 alfajiri ambako moja kwa moja tulipitiliza hadi kwenye ile nyumba ambayo ndipo yalikuwa makazi yetu ya mipango mikakati. Ilipofika mida ya saa 2 asubuhi,Jipe alitupatia kila mmoja wetu mimi na Mtatiro laki 5,sikufahamu wale wengine walipewa kiasi gani maana sisi tuliondoka zetu.

Kiukweli ile pesa iliyokuwa imefungwa kwenye ile kanga sikufahamu ilikuwa kiasi gani maana kule Geita hatukuwa na muda wa kuhesabu,na hata tulivyofika hapo kwenye hiyo nyumba,Jipe na Gabi waliingia chumbani na lile furushi!.


Mtatiro "Hawa wasenge ngoja uje uone"

Mimi "Kwanini?"

Mtatiro "Wewe unaona makubaliano yetu yanatekelezwa?"

Aliendelea "Hawanijui vizuri,siwezi kuweka roho yangu rehani halafu unilipe laki 5"


Ile hela Mtatiro aliniambia tuiweke kwenye mtaji wa mitumba ili tuzidi kuizungusha .Sasa nakumbuka siku moja tukiwa pale Hungumahlwa kwenye harakati za kupambana na mitumba,ghafla hali ya mshikaji wangu mtatiro ilibadilika na akaniambia yeye inabidi arudi nyumbani akatafute dawa ameze ili hali itengemae,tulikubaliana tungeonana nyumbani!.

Ilipofika mida ya saa 8 mchana nilipigiwa simu,nilipotoa ile simu mfukoni nikakuta ilikuwa namba ya Mtatiro akinipigia,lakini baada ya kupokea nikakuta si yeye akiongea!.

Sauti "Hallo!"

Mimi "Hallo"

Sauti "Wewe bila shaka ni Umughaka"

Mimi "Ndiyo"

Sauti "Hebu kama unaweza njoo hapa Bugando"

Mimi "Niko mbali kidogo"

Sauti "Uko nje ya Mwanza?"

Mimi "Nipo Hungumalwa"

Sauti "Jitahidi ufike haraka"

Sikutaka kupoteza muda pale mnadani,nilichukua mzigo wangu nikaufunga nikaenda kuupakia kwenye fuso ambalo mara zote tulikuwaga tukipakia mizigo yetu kisha nikampatia dereva maagizo mahali pa kwenda kuushusha.Niliondoka hapo Hungumalwa na nikafanikiwa kufika Bugando mida ya saa 11 jioni.Sasa nilipofika niliipiga ile namba ya Mtatiro na hatimae ikapokelewa na yule yule mtu aliyekuwa amenipigia,alinielekeza mahali alipokuwa ndipo nikamfuata.Kumbe yule mtu alikuwa ni daktari na alitaka kunipatia taarifa ya Mtatiro.
Kiukweli nilianza kuingiwa na hofu sana kwasababu Mshikaji wangu Mtatiro aliondoka akiwa anajiweza kutembea sasa sikujia ni kitu gani kilikuwa kimempata.

Niliingia hadi kwenye chumba alichokuwa ameniambia niingie,nilipoingia nilimkuta Mtatiro pia yupo akiwa amekaa kwenye kiti,baada ya kumuona Mtatiro pale kwenye kiti angalau moyo wangu ulitulia.

Jamaa(Daktari) "Mambo vipi kaka"

Mimi "Safi kabisa kaka"

Jamaa "Karibu kiti kiti"

Aliendelea "Bila shaka huyu unamfahamu"

Mimi "Ndiyo"

Jamaa "Ni nani yako?"

Mimi "Ni rafiki zaidi ya ndugu"

Jamaa "Kwahiyo mnaaminiana?"

Mimi "Ndiyo"

Jamaa "Sasa mimi nimekuita hapa kwa ridhaa ya huyu ndugu yako,maana nilimwambia aniitie ndugu yake wa karibu ndipo akasema nikutafute wewe,bila shaka hali yake unaiona"

Aliendelea "Amewahi kukwambia kinachomsibu?"

Mimi "Hapana kwakweli"

Jamaa "Sawa,Bwana Mtatiro,ni vema rafiki yako akafahamu kinachokusibu atakuwa msaada kwako kama hutojali!"

Mtatiro "Haina tatizo dokta wewe mwambie huyu ni rafiki yangu tunapendana na kuheshimiana!"

Jamaa "Sawa,sasa bwana mimi nimekuita hapa kwa ajili ya huyu ndugu yako,ndugu yako ni muathirika wa virusi vya Ukimwi na kama ulivyoutaratibu mgonjwa anapopimwa na kugundulika na hilo tatizo huwa tunamuanzishia utaratibu wa kuanza matibabu"

Aliendelea "Ndugu yako huyu alianza dozi kama kawaida lakini kuna muda huwa anategea sana kuja kuchukua dawa mara zile tulizompa zinapokwisha,hivyo inamuondolea ufanisi wa afya yake,pia kwakuwa wewe upo hapa naomba uwe unamshauri asiwe mtu wa kunywa sana pombe,si nzuri kwa afya yake!"

Niliendelea kumsikiliza yule daktari kwa makini wakati huo moyo wangu ulikuwa unauma sana,sikutaka kuonyesha hadharani pengine ningemfanya mshikaji wangu aliyekuwa akiniamini Mtatiro ajisikie vibaya,nilikuwa makini sana ili nisije kuleta sintofahamu!.

Jamaa "Sasa naomba hizi dawa nazompatia hapa,hakikisha kila siku anameza kwa masaa yale yale atakayojipangia yeye ili kuweza kumjengea kinga imara dhibi ya mashambulizi nyemelezi"

Aliendelea "Naomba umsimamie awe anameza dawa kila siku na kama nimivyokwambia umshauri aache pombe,pia azingatie lishe bora!"


Baada ya mazungumzo tulitoka nje na Kuondoka zetu nyumbani,nilikuwa namlaumu sana rafiki yangu Mtatiro kwanini aliacha kuzingatia dawa wakati alilifahamu tatizo lililokuwa likimkabili,kiukweli sikumuonyesha chuki bali nilimpenda sana rafiki yangu na nilitaka afanye vema zaidi ili afya yake iendelee kuimarika.Sikumbagua bali niliendelea kumshauri na kumfanya awe na furaha muda wote kama rafiki yangu.


Itaendelea.............
Mkuu nimefurahi kuona mandhari ya Nhungumalwa kwenye hii story hata alhamis juzi nilikua pale mnadani[emoji4]
 
Shukran sana kaka UMUGHAKA

Kama kuna nyingine tunaomba tuletee. Mimi kama nilivyokwambia nitakuja bunju hapo Tupate beer mbili Tatu na Tupige story mbili tatu za akina Mwisse [emoji23][emoji23][emoji23]

Ila hadithi yako imejaa Mafunzo mazuri sana kwetu wapambanaji. Tumejifunza mengi

Stay Blessed [emoji2936][emoji2936]
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 25.



"Wewe ni mtu muhimu sana kwangu Mtatiro na umekuwa sehemu ya furaha katika maisha yangu,ulinipokea na kunisaidia wakati mzee aliponitimua nyumbani,hukuniacha katika matatizo bali ulinishika mkono kama kijana mwenzio hivyo na mimi sitokuacha rafiki yangu" ni maneno niliyokuwa nikimwambia rafiki yangu wa damu Mtatiro ili aendelee kuwa na amani kabisa.

USHAURI

Kuishi na Virusi vya Ukimwi si mwisho wa maisha na uhai,kama kuna kitu nakichukia katika maisha yangu ni ubaguzi unaofanywa kwa hawa ndugu zangu,haya ni maisha tu na tunapaswa kupendana,unaweza ukawa muaminifu na bado mumeo/mkeo akakuletea ugonjwa,hivyo hatupaswi kuwanyooshea wengine vidole kana kwamba ni wadhambi kuliko sisi,tuache dharau za kijuaji na kebehi zisizo na msingi.

Ndugu zangu pia niwaombe mzingatie dawa kwa wakati ili ziweze kuwafubaza virusi angalau unapokutana na mwenzako usimuambikize ili muendelee kufurahia maisha,jambo la msingi ni wewe mwenyewe kuacha kujibagua,jikubali na songa mbele.Acha starehe za kijinga,panga mipango yako na timiza ndoto zako,usiwe mlevi kupita kiasi na hakuna sababu ya kuwaambukiza wengine kwa makusudi,wapende watu wote.Pia achana na imani za mitume na manabii kwamba wakupatie maji au mafuta utumie kisha uache dawa,achana kabisa na hizo imani mfu,wewe muombe Mungu atakusikia,kama akipenda anaweza kuuondoa huo ugonjwa na kama akiona inafaa wewe kuendelea nao basi Mshukuru na endelea kuishi,hata kama ukimuomba Mungu na ugonjwa usitoke lakini Mungu bado atabaki kuwa mwema hivyo usikate tamaa.

NAWAPENDA SANA



Basi baada ya afya ya rafiki yangu kipenzi Mtatiro kuimalika tuliendelea na kazi yetu ya kuuza mitumba sehemu na vijiji mbalimbali vya kanda ya ziwa.Nakumbuka siku moja Gabi alimpigia simu Mtatiro akawa amemuambia inapaswa tuonane ili tupange mikakati ya kuelekea maeneo kama kawa.Kweli,tuliondoka siku iliyofuata kuelekea kule yalipokuwa makazi ya muda ilipokuwa inasukwa mipango kabla.Tulipofika pale ndani tulimkuta Gabi kama kawaida akiwepo Jipe na jamaa yule dereva tuliyeenda nae kwenye tukio kahama.

Jipe "Wanangu mko poa"

Mtatiro "Tuko fiti kaka"

Jipe "Sasa Kesho safari ni Kagera"

Aliendelea "Si mko vizuri?"

Mtatiro "Sisi tuko tayari hata leo kaka ni nyinyi tu!"

Jipe "Sawa,Gabriel atatangulia leo halafu sisi kesho jioni tutaondoka"

Basi baada ya yale mazungumzo Jipe akatutaka tujitayarishe kwa ajili ya safari kesho yake.Mimi na Mtatiro tuliamua kurudi nyumbani huku Mtatiro akiapa na kusema safari hii wakijidai kutudhurumu basi ama zake ama zao!.

Siku iliyofuata mida ya saa 7 mchana tulikuwa tushafika eneo la tukio na ndipo tukakamata Noah na kuianza safari ya kuelekea mkoa wa Kagera,kwenye gari nilikuwa mimi na Mtatiro wakati huo jipe akiwa amekaa kwa mbele pamoja na yule jamaa dereva!.Tuliingia Kagera mida ya saa 12 asubuhi siku iliyofuata,njia tuliyotumia ni ileile ya kupitia Kahama huku tukiwa makini kupita maelekezo,Jipe alikuwa ametoa maelekezo ya kwamba,yeyote atakaye jiingiza mkenge basi ingekuwa ni halali yetu!.Baada ya kufika Kagera,Jipe aliwasiliana na Gabi ambaye alimuelekeza maeneo ambayo tungemkuta,nakumbuka tuliikamata njia na uelekeo wa Bukoba mjini,nje kidogo ya mji tukamkuta Gabi.

Gabi "wazee kwa huku itabidi tuzunguke kidogo muda uende kwasababu hatuna makazi,na ikifika mida tutaitana tufanye kilichotuleta".

Kwakuwa mimi na Mtatiro ndiyo ilikuwa mara yetu ya kwanza kufika Kagera ilibidi tukae kwenye ile gari maana hatukutaka kucheza mbali tukajichanganya na ukizangatia hatukuwa na simu!.Dereva alitafuta maeneo ambayo hayakuwa na shughuli nyingi za watu akapaki gari hapo.

Ilipofika mida ya saa 10 jioni mvua ikaanza kunyesha kama masikhara lakini muda ulipozidi ndipo hali ilizidi kuwa mbaya,tangu nizaliwe sijawahi kuona radi zikipiga kama siku hiyo,ile mvua ilikuwa na radi si mchezo hadi uoga ukawa unaniingia!.Kadiri muda ulivyozidi ndivyo mvua nayo ilizidi kuongeza spidi na nilikuwa naona Jipe anaomba iendelee kunyesha vilevile isikatike.Sasa ikafika mida ya saa 12 ikapungua ikawa inanyesha kidogo sana,tulikuwa ndani ya gari wakati huo tukiendelea kuvuta muda.Ilipofika mida ya saa 3 usiku mvua ikaanza tena kunyesha kama mwanzo.

Jipe "Huu ni muda sasa"

Aliendelea "Aisee wewe utaenda kutusubiri mahali nitakapokuelekeza"

Jipe "Wengine wote tutaongozana na mtafanya kila nitakachowaambia"

Basi ile gari ikaanza kuondoka kuelekea uelekeo wa Bukoba Mjini,kuna mahali tulifika ambapo kwa umbali kama wa mita 500 kulikuwa na sheli(sitoitaja),dereva alitakiwa kuzima taa na kugeuza gari atusubiri hapo!.Kila mmoja alikuwa tayari kwa ajili ya makabiliano.Muda huo ilikuwa ni saa 4 usiku lakini kulikuwa na mvua kubwa sana,tulipofika kwenye ile sheli baada ya Jipe kuchomoa SMG kuna mlinzi alimuona akaanza kukimbia kama mwehu huku akiwa na gobole,Jipe hakutaka kumpotezea muda,alipiga risasi ya mgongoni yule mlinzi akawa amedondoka chini.

Jipe "Mtatiro kusanya hao wauza mafuta wote"

Jipe aliingia ndani kwenye vyumba vilivyokuwa kando ya ile sheli huku akiniambia niongozane nae.Pale nje Mtatiro na Gabi waliendelea kuwadhibiti wale wauza mafuta na kuchukua hela huku wakiwa chini ya ulinzi mkali.

Jipe "Toa pesa wewe la sivyo nitakuua"

Jipe alikuwa akimwambia dada mmoja kibonge ambaye tulimkuta mle ndani wakati huo akimnyooshea mtutu wa bunduki.Yule dada alifungua boksi moja lilikuwa la mbao na kulikuwa na noti za kutosha,sasa kulibeba lile boksi mwenyewe kidogo likawa zito,Jipe akamuamuru yule demu atupatie mfuko,yule demu alitoa mfuko mmoja ambao ulikuwa kama shuka ambao ulikuwa umechakazwa na rangi ya maoili!,niliukamata ule mfuko haraka nikaanza kuchukua zile hela haraka sana,sikutaka kabisa kuhangaika na silva maana jipe alisema nitemane nazo,baada kumaliza zile hela,Jipe alimuamuru yule demu alale chini na asijaribu kuinua kichwa kwani atamuua,tuliondoka chap mle ndani kuelekea nje ambapo tuliwakuta Gabi na Mtatiro wakiwa wanatusubiri!.

Tulikimbilia gari na tulipofika dereva aliondoka kwa spidi kali sana lile eneo,wakati huo bado mvua ilikuwa ikiendelea kunyesha sana.Wakati tupo njiani,Jipe alimpigia simu yule demu Kamange na kumtaka achukue ile gari Mark 2 atukute Geita.Ile Noah ilitembea vibaya mno usiku huo na tulifanikiwa kufika Geita mida ya saa 8 Usiku,Jipe akawa amemwambia Gabriel na dereva ya kwamba wao watangulie Mwanza halafu sisi tungeisubiri ile Mark 2.

Kweli,Kesho yake mida ya saa 4 asubuhi yule demu akawa amefika pale Geita kutuchukua tukawa tumeondoka,Tuliingia Mwanza mida ya saa 11 jioni.Tuliwakuta kina Gabi wao wameshafika,sasa tulipofika Mtatiro alimwambia Jipe ya kwamba pesa tulizopora ziletwe zihesabiwe ili kila mtu afe na chake,nadhani wao walidhani Mtatiro anatania lakini jamaa alikuwa serious sana,sikuwahi kufahamu kama Mtatiro akikasirika anakuwa vile aisee,mara zote mimi nimekuwa nikimuona akiwa kawaida nikawa namchukulia poa,siku hiyo ndiyo niliiona rangi halisi ya yule mkurya.

Mtatiro "Haiwezekani tupore pesa halafu nyie muwe mnagawana nyingi na sisi mnatupa kidogo,mkitaka damu leo imwagike ficheni hizo hela muone!"

Jipe "Hakuna atakayedhurumiwa hata mmoja"

Mtatiro "Mbona juzi mmetunyenga?"

Jipe "Yale yalikuwa ni maelekezo ya bosi"

Mtatiro "Basi mwambieni leo kila mtu anapata pasu,sitaki ufara!"

Baada ya jamaa kuona Mtatiro yuko serious,Jipe alimwambia Gabi walete zile pesa ili kila mmoja apewe haki yake.Kweli,mimi na Mtatiro kila mmoja alipata mioni 6,na wao pia walipata kama sisi.Tuliamua kuondoka zetu baada ya kupokea mgao wetu.

Mtatiro "Mwanangu kama ni hela ya mtaji tushapata,tuachane na hizi habari wao kama wanaendelea ngoja waendelee"

Aliendelea "Cha kufanya tukafungue duka la jumla tuachane na mitumba"

Mtatiro "Au wewe unaonaje mwanangu?"

Mimi "Kwanini tusifungue duka la vipodozi?"

Mtatiro "Eti eeeh,sawa?"

Baada ya kupata ile hela kweli tuliachana na biashara ya mitumba na tukafungua duka la vipodozi yale yale maeneo ya Usagara tukaanza kupambana,nakumbuka Mtatiro alikuwaga anafuata vipodozi Uganda kwasababu huko ndiko vilikuwa vinapatikana kwa bei ya chini,kiukweli tulipiga sana hela na maisha yetu yalianza kubadilika mdogo mdogo,ilifika sehemu tukahama pale kwa braza ake Mtatiro kila mmoja akaenda kupanga geto lake mwenyewe.

Nakumbuka siku moja Mtatiro akaja kuniambia kwamba Gabi anampigia simi twende kuna mchongo wenye hela kubwa tukapige.

Mimi "Umemwambiaje!"

Mtatiro "Mi nimemwambia kwasasa tunashughuli zetu,wao kama wanaendelea waendelee!"

Aliendelea "Jamaa baada ya kumwambia ananiambia kwamba tunataka kuwachoma,hivyo tujiangalie tutaumia"

Mimi "Sasa itakuwaje?"

Mtatiro "wale hawawezi kututisha we tulia"

Basi baada ya jamaa kuona hatuwapi tena ushirikiano wakaamua kutokutushirikisha kwenye michongo yao tena lakini walikuwa wamechukia sana baada ya sisi kuachana nao.Baada ya miezi kadhaa kupita,kuna siku Mtatiro akaja kuniambia amesikia habari mahali kuna majambazi wamedakwa wengine wameuawa huko Mbeya na mmoja wapo wa waliodakwa ni Gabi,sasa baada ya kuifatilia ile habari ni kweli kabisa ilikuwa Jipe na majambazi kadhaa wenzie waliuawa palepale eneo la tukio.

Kumbe walienda kumpora mfanyabiashara mmoja mwenye asili ya India ambaye ndani ya gari alikuwa na madini pamoja na pesa alizokuwa akizitoa huko Chunya kuelekea Mbeya,sasa wao hawakujua yule mfanyabiashara alikuwa na eskoti ya askari kadhaa,yawezekana walijua hilo ila wakajifanya wabishi kwakuwa walikuwa na silaha.Walikufa majambazi wawili na mmoja akiwa Jipe huku Gabi na mwingine mmoja wakisalimu amri.

Gabi alifungwa miaka the thelathini gerezani na mwaka juzi nimetoka kumuona pale gereza la Ruanda Mbeya.Jamaa amechoka sana na aliponiona mara ya kwanza alionyesha huzuni lakini hakuwa na namna ndo hivyo ishatokea.Aliniambia yule aliyekuwa bosi wake alikimbilia huko Kenya kuanzisha maisha huko.Huwa namtembelea jamaa nikipata nafasi,na siachi kumtia moyo na kumfariji,namwambia ashukuru akufa,maadam yuko hai basi atatoka tu gerezani na ataendelea na maisha yake ingawaje atakuwa amepoteza muda.

Mimi na Mtatiro lile duka la vipodozi tuliuza na kila mmoja akaendelea na biashara zake,Mtatiro aliondoka kwenda Uganda kwa anko wake hadi leo anaishi huko.Mimi niliamua kurudi Tarime Sirari nikafungua duka nikaanza kukimbiza,kuna mtoto wa dingi mkubwa anaishi Dar es salaam alikuwa anafanya biashara ya vyombo akaniambia nije tuungane tufanye biashara kwa kua inalipa sana,hivyo nikaondoka Tarime kuja Dar,kufika nikampatia jamaa zaidi ya milioni 9 akanidhurumu hadi leo,niliamua kumuachia Mungu nikaanza kupambana upya kutafuta mtaji,nilipopata mtaji nikanunua bodaboda yangu ambayo ndiyo inaniingizia kipato kwa hapa mjini.


Nawapenda sana.


MWISHO.
Lazima tuonane,mwamba
 
Stori nzuri sana ina mafundisho mengi,, lakini kilichonivutia zaidi jamaa ana roho flani ivi ya kusamehe sana na kupotezea vitu

imagine mtu anafanya kazi ya uvuvi halipwi na anaacha hasemi ata neno anaamua tu kuondoka.

Jamaa amedhulumiwa milion 9 na ndugu yake na bado amesema akaamua amwachie Mungu.

Hongera Mkuu una moyo wa tofauti sana amna kitu kinauma kama dhulma ni kitu kibaya sana,, nakumbuka kuna ukoo ulikua unazika mtu kila baada ya miezi mitatu sababu kuna walifanya dhulma ya mashamba kwenye ukoo mwingine.
 
UMUGHAKA


Baada ya kudhurumiwa zile pesa na ndugu yangu kiasi cha 9 mil,niliamua kurudi nyumbani na baba akanisaidia nikapata nafasi katika chuo cha polisi Moshi

Kwasasa mimi ni Pongo nipo Iringa

Jamaa kashindwa kumalizia hivi

Boda apate muda wa kwenda mbeya kutoka dar,unajua umbali uliopo dar-mbeya?
Kwani sh.ngapi?
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 18.



Muda si mrefu tulifika kwenye nyumba fulani ambayo ilikuwa ndani ya geti,geti lilifunguliwa ndipo tukazama ndani. Dereva yule aliteremka akawa anatuongoza kuelekea ndani.Mazingira yale yalikuwa yametulia sana na nyumba ile ilikuwa pembezoni mwa mlima!.


Gabi "Ooh wanaume wapambanaji wa kikurya!"

Gabi alipotuona alifurahi sana na kiukweli tulikumbatiana kwa furaha!.Nilimshangaa sana Gabi safari hii kwasababu alikuwa amebadilika sana tofauti na miezi michache iliyokuwa imepita,safari hii alikuwa ameachia ndevu kidevuni mwake na mashavuni kiasi kwamba kuficha uhalisia wake ambao nilikwisha kuuzoea!.

Gabi "Vipi wewe mbona hupatikanagi!?"

Mimi "Nilibadili namba kaka"

Gabi "Mambo yanakwendaje lakini!"

Mimi "Tupo tunapambana kaka"

Gabi "Jamaa bhana walinishikiria kwa siku kadhaa ila walitema nyongo!"

Mimi "Walikuja mpaka pale kwako au ilikuwaje kaka"

Gabi "By the way ni stori ndefu lakini niwaambie kitu,Kama huna hela utakufa njaa lakini mwenye hela huchelewa tu kula ila hafi njaa"

Aliendelea "Pesa ndo kila kitu"

Gabi "Vipi lakini mwanangu ule mzigo ilikuwaje?"

Mimi "Kaka ulivyoniambia mko njiani mnakuja mimi nilitoroka nao nikafika mahali nikauchoma moto!"


Gabi "Ahahaha ya kwamba Mkurya ulisanda,sio!"

Aliendelea "Wala usijali yale tuliyamaliza,tunachopaswa kufanya ni kuangalia yaliyoko mbele yetu!"


Gabi "Siku hizi mnafafanya shughuli gani aisee!"


Mtatiro "Braza tunapambana na mitumba"

Gabi "Sasa hiyo inawalipa kweli!?"

Aliendelea "Hebu ngoja kwanza niwaambie wawalete msosi mtandike wanangu!"


Baada ya muda chakula kililetwa na mama mmoja wa makamo ambaye kimuonekano alikuwa na miaka zaidi ya Hamsini,basi tulianza kula kile chakula wakati huo Gabriel hakiwa hayupo sebuleni,alirudi tukiwa tumemaliza kula na akatutaka tutoke kuelekea town tukapate bia mbili tatu!.
Tulipanda ile Land cruiser tukaondoka kuelekea mjini ambapo tulifikia Hotel ya kifahari ya Gold crest,Tulipofika pale tulipanda kwenye lift ambayo ilituvuta kwenda juu kabisa mwisho wa lile jengo,tuliingia kwa juu ambako nilikuta kuna uwazi wa kutosha huku watu wakiwa wanapata vyakula na vinywaji!.

Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuingia kwenye Hotel ya kifahari iliyokuwa hapo Mwanza,kiukweli nili enjoy sana maana mandhari yote ya jiji la Mwanza ilikuwa ikionekana hapo.Tulitafuta meza yetu tukawa tumekaa,Gabi aliagiza pombe Kali mchupa mkubwa na akawa ametutaka na sisi kila mmoja kuagiza tulichokuwa tunakunywa!.

Mtatiro akawa ameniambia tuagize li Jack Daniel chupa kubwa ili tulichape wawili,hivyo ndivyo tulivyofanya!.Hapo kabla sikiwahi kunywa pombe kali,nilikuwa nikinywa vibia vyangu kadhaa natulia,hiyo ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kunywa pombe kali!.Yule dereva yeye alikuwa akinywa maji muda wote tuliokuwa hapo.

Baada ya pombe kuanza kukolea,maongezi nayo yalichukua nafasi!.

Gabi "Wanangu mimi huwa nawakubali sana katika mapambano!"

Aliendelea "Nyie ni miongoni mwa marafiki zangu wakubwa na sitowaacha ndugu zangu!"

Gabi "Jioni kuna mahali nataka twende ndugu zangu!"

Mtatiro "Kuna dili jipya kaka?,wewe tupe dili sisi tupige tunachotaka ni hela!"

Gabi "Hilo wala msijali,nyie ni wanangu wa damu lazima kila dili niwe nawakumbuka!"

Baada ya kupiga mtungi kwa muda mrefu,Gabi alimwambia yule dereva aondoke atuache na sisi tungechukua taksi kwasababu tulikuwa na safari nyingine!.Baada ya yale mazungumzo nikiona Gabi anatoa pochi iliyokuwa imesheheni noti za elfu kumi kumi akachomoa elfu 50 akamkabidhi jamaa huku akimwambia atampigia simu!.


Gabi "Wanangu sikieni,huyo dogo ni mtoto wa dingi mdogo na pale alipowaleta ni nyumbani kwao,ingawaje pia wana nyumba nyingine Arusha ambako wanakaa ndugu zake na wadogo zake!"

Aliendelea "Dingi yake ni marehemu na baada ya kugawiwa pesa za urithi dogo akaona aje amalizie hiyo nyumba ya Mwanza aishi yeye na ile ya Arusha awaachie wadogo zake!"

Mtatiro "Anapiga ishu gani?"

Gabi "Dogo anasema anagereji ila sijajua ipo maeneo gani,alichezea sana hela dogo msimuone vile,hilo li cruiser alinunua tukamshauri alipeleke Arusha lipige kazi lakini naona kama haelewi!"


Basi baada ya mazungumzo hayo huku tukiendelea kukata maji machungu!,ilipofika mida ya saa 1 usiku tulionodoka kutafuta Taksi na kuelekea maeneo ambayo Gabi alikuwa akiyafahamu!.Tulifika kwenye nyumba moja ambayo ilikuwa kimya sana hata kabla nilidhani haikuwa na umeme kumbe taa zilikuwa zimezimwa!,baada ya ile Taksi kuondoka Gabi alipiga simu akazungumza na mtu mmoja ambaye bila kuchelewa alitufungulia geti tukazama ndani.

Tulipoingia ndani tulipelekwa hadi sebuleni ambapo nako hakukuwa na mwanga wa taa ila baada ya kukaa kwenye kochi ndipo taa ya sebuleni iliwashwa,sasa baada ya ile taa kuwashwa kulikuwa na jamaa wawili pale sebuleni ambao walikuwa wamejengeka vizuri mno kimisuli huku usoni mwao hakukuwa hata na chembe ya tabasamu!.Tulipoingia ndani,Gabi yeye moja kwa moja alipitiliza ndani huko vyumbani na hatukufahamu alienda kufanya nini!.

Baada ya muda alikuja Gabriel akiandamana na Jamaa mmoja aliyekuwa amenyoa upara,pia hakuwa na ndevu hata kidogo maana zote alikuwa amezipiga wembe!.

Gabi "Aisee mnaweza kutupisha kidogo tunamazungumzo"

Wale jamaa wawili tuliowakuta hapo walinyanyuka wakawa wameondoka kuelekea huko ndani!.

Gabi "Mkuu hawa ndio vijana niliokueleza tangu wiki iliyopita tukiwa Arusha!"

Aliendelea "Huyu anaitwa Mtatiro na huyu anaitwa Umughaka"

Gabi "Ni wakurya majasiri sana kama nilivyokwambia"
Aliendelea "Ndugu zangu huyu ni bosi wangu bila shaka pia atakuwa bosi wenu"

Gabi "Nadhani bosi karibu uzungumze chochote!"

Yule tuliyeambiwa ni bosi wa Gabi alianza kutuangalia kwa makini sana huku akitukazia macho kiasi kwamba kila mtu kama alianza kuingiwa na hofu!.


Bosi "Nyie ni Wakurya kutokea wapi bhana!"


Mtatiro "Tumetokea Tarime"

Bosi "Tarime ni kubwa"

Mtatiro "Wote tunatokea sehemu moja pale Tarime mjini"

Bosi "Ninaposema Tarime nahitaji kujua jina la kijiji au mtaa mnaotokea!"

Mtatiro "Tunatokea Rebu"

Bosi "Wewe una miaka mingapi?"


Mimi "Nina miaka 23"

Bosi " Na wewe?"

Mtatiro "Mi nina miaka 27"

Bosi "Mmewahi kufanya kazi gani ambayo ilitishia kuyakatisha maisha yenu uhai!?"


Baada ya hilo swali tulibaki kujiuma uma ndipo Gabi akaingilia kati kusaidia kujibu!.

Gabi "Bosi hawa wote nilikuwa nafanya nao ile kazi ndiyo maana nina waamini!"

Bosi "sawa,bila shaka umewaambia!"

Gabi "Hapana mkuu sijawaambia chochote"

Bosi "Ilipaswa uwaambie ili mwenye kuamua aamue,sitaki mtu mwenye roho ya kike kwenye kazi zangu!"

Aliendelea "Sasa nyie nisikilizeni kwa makini,naitwa Afande........,je mmewahi kutumia bunduki?"

Baada ya kutaja neno bunduki kiukweli akili yangu ilitaka kuchanganyikiwa,nilijikuta kale kapombe nilikokuwa nimekunywa kote kalikata!.Mimi niliitikia kwa kutikisa kichwa kuashiria hapana lakini Mtatiro alimjibu!.


Mtatiro "Hapana"

Bosi "Je mko tayari kutumia bunduki?"


Mimi nilisita kuitikia ila mwenzangu Mtatiro alikuwa na ujasiri sana kujibu like swali!.

Mtatiro "Ndiyo mimi nipo Tayari!"

Bosi "Na wewe je?"

Baada ya Mtatiro kujibu lile swali na mimi nikajikuta namfuatisha Mtatiro.

Mimi "Nipo Tayari!"

Bosi "Sasa nyie ndiyo wakurya ninao wafahamu,nimewapenda!"

Baada ya yale mazungumzo yule bosi aliondoka akarudi ndani akasema tumsubiri kwanza anarudi!

Muendelezo > Sehemu ya 19
Heheeeee..kumekucha.

#MaendeleoHayanaChama
 
Huu ndio ujuaji wa kijinga kila mda tunauzungumzia. Mbona mnajikuta ma-director sana kwenye kibwebwe kisicho wahusu. Mkiona ana puyanga si mkae muandike za kwenu kisha mziweke vile mnavyotaka ziwe?

Kwenye mtiririko wa story ake kuna mahala aliposema ye ni Jambazi konki? Kuna chuo amekwambia au amesimulia kua alienda kusomea ujambazi hivo keshakua Pro so hakupaswa kufanya mistake alizofanya?

Na namna mnavyoziona hizo mistake za kihalifu so mnataka kutushawishi tuone kua nyie ndio mijambazi mlio kubuhu so mnazijua mbinu zote au vp?

Waswahili tuna shida gani lakini? Mnachowashwa kitu gani kwani? Kama story mnaona ina chai nyingi si mpite tu kule kimya kimya [emoji1787]...

Em acheni ujuha wa kipumbafu, kaandikeni zenu basi zilizo 100% perfect. Mnaboa sana! Huo ujuaji wenu em uwekeni kwenye maisha yenu ya kila siku yawe perfect ili msikae jukwaani mnasubiri story za uongo!

Mijitu mizima ya hovyo kabisa, wakati wengine wanasoma kujiburudisha yenyewe yanasoma kutafuta makosa utafikiri yanafanya udahili wa waandishi. Hivi na huko mtaani kwenu mnaishije na jamii zenu watu wa aina yenu mmh?
Tatzo watu wameangalia movie sasa wanataka na jambazi wa kibongo awe kama wa kwenye movie zao
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 25.



"Wewe ni mtu muhimu sana kwangu Mtatiro na umekuwa sehemu ya furaha katika maisha yangu,ulinipokea na kunisaidia wakati mzee aliponitimua nyumbani,hukuniacha katika matatizo bali ulinishika mkono kama kijana mwenzio hivyo na mimi sitokuacha rafiki yangu" ni maneno niliyokuwa nikimwambia rafiki yangu wa damu Mtatiro ili aendelee kuwa na amani kabisa.

USHAURI

Kuishi na Virusi vya Ukimwi si mwisho wa maisha na uhai,kama kuna kitu nakichukia katika maisha yangu ni ubaguzi unaofanywa kwa hawa ndugu zangu,haya ni maisha tu na tunapaswa kupendana,unaweza ukawa muaminifu na bado mumeo/mkeo akakuletea ugonjwa,hivyo hatupaswi kuwanyooshea wengine vidole kana kwamba ni wadhambi kuliko sisi,tuache dharau za kijuaji na kebehi zisizo na msingi.

Ndugu zangu pia niwaombe mzingatie dawa kwa wakati ili ziweze kuwafubaza virusi angalau unapokutana na mwenzako usimuambikize ili muendelee kufurahia maisha,jambo la msingi ni wewe mwenyewe kuacha kujibagua,jikubali na songa mbele.Acha starehe za kijinga,panga mipango yako na timiza ndoto zako,usiwe mlevi kupita kiasi na hakuna sababu ya kuwaambukiza wengine kwa makusudi,wapende watu wote.Pia achana na imani za mitume na manabii kwamba wakupatie maji au mafuta utumie kisha uache dawa,achana kabisa na hizo imani mfu,wewe muombe Mungu atakusikia,kama akipenda anaweza kuuondoa huo ugonjwa na kama akiona inafaa wewe kuendelea nao basi Mshukuru na endelea kuishi,hata kama ukimuomba Mungu na ugonjwa usitoke lakini Mungu bado atabaki kuwa mwema hivyo usikate tamaa.

NAWAPENDA SANA



Basi baada ya afya ya rafiki yangu kipenzi Mtatiro kuimalika tuliendelea na kazi yetu ya kuuza mitumba sehemu na vijiji mbalimbali vya kanda ya ziwa.Nakumbuka siku moja Gabi alimpigia simu Mtatiro akawa amemuambia inapaswa tuonane ili tupange mikakati ya kuelekea maeneo kama kawa.Kweli,tuliondoka siku iliyofuata kuelekea kule yalipokuwa makazi ya muda ilipokuwa inasukwa mipango kabla.Tulipofika pale ndani tulimkuta Gabi kama kawaida akiwepo Jipe na jamaa yule dereva tuliyeenda nae kwenye tukio kahama.

Jipe "Wanangu mko poa"

Mtatiro "Tuko fiti kaka"

Jipe "Sasa Kesho safari ni Kagera"

Aliendelea "Si mko vizuri?"

Mtatiro "Sisi tuko tayari hata leo kaka ni nyinyi tu!"

Jipe "Sawa,Gabriel atatangulia leo halafu sisi kesho jioni tutaondoka"

Basi baada ya yale mazungumzo Jipe akatutaka tujitayarishe kwa ajili ya safari kesho yake.Mimi na Mtatiro tuliamua kurudi nyumbani huku Mtatiro akiapa na kusema safari hii wakijidai kutudhurumu basi ama zake ama zao!.

Siku iliyofuata mida ya saa 7 mchana tulikuwa tushafika eneo la tukio na ndipo tukakamata Noah na kuianza safari ya kuelekea mkoa wa Kagera,kwenye gari nilikuwa mimi na Mtatiro wakati huo jipe akiwa amekaa kwa mbele pamoja na yule jamaa dereva!.Tuliingia Kagera mida ya saa 12 asubuhi siku iliyofuata,njia tuliyotumia ni ileile ya kupitia Kahama huku tukiwa makini kupita maelekezo,Jipe alikuwa ametoa maelekezo ya kwamba,yeyote atakaye jiingiza mkenge basi ingekuwa ni halali yetu!.Baada ya kufika Kagera,Jipe aliwasiliana na Gabi ambaye alimuelekeza maeneo ambayo tungemkuta,nakumbuka tuliikamata njia na uelekeo wa Bukoba mjini,nje kidogo ya mji tukamkuta Gabi.

Gabi "wazee kwa huku itabidi tuzunguke kidogo muda uende kwasababu hatuna makazi,na ikifika mida tutaitana tufanye kilichotuleta".

Kwakuwa mimi na Mtatiro ndiyo ilikuwa mara yetu ya kwanza kufika Kagera ilibidi tukae kwenye ile gari maana hatukutaka kucheza mbali tukajichanganya na ukizangatia hatukuwa na simu!.Dereva alitafuta maeneo ambayo hayakuwa na shughuli nyingi za watu akapaki gari hapo.

Ilipofika mida ya saa 10 jioni mvua ikaanza kunyesha kama masikhara lakini muda ulipozidi ndipo hali ilizidi kuwa mbaya,tangu nizaliwe sijawahi kuona radi zikipiga kama siku hiyo,ile mvua ilikuwa na radi si mchezo hadi uoga ukawa unaniingia!.Kadiri muda ulivyozidi ndivyo mvua nayo ilizidi kuongeza spidi na nilikuwa naona Jipe anaomba iendelee kunyesha vilevile isikatike.Sasa ikafika mida ya saa 12 ikapungua ikawa inanyesha kidogo sana,tulikuwa ndani ya gari wakati huo tukiendelea kuvuta muda.Ilipofika mida ya saa 3 usiku mvua ikaanza tena kunyesha kama mwanzo.

Jipe "Huu ni muda sasa"

Aliendelea "Aisee wewe utaenda kutusubiri mahali nitakapokuelekeza"

Jipe "Wengine wote tutaongozana na mtafanya kila nitakachowaambia"

Basi ile gari ikaanza kuondoka kuelekea uelekeo wa Bukoba Mjini,kuna mahali tulifika ambapo kwa umbali kama wa mita 500 kulikuwa na sheli(sitoitaja),dereva alitakiwa kuzima taa na kugeuza gari atusubiri hapo!.Kila mmoja alikuwa tayari kwa ajili ya makabiliano.Muda huo ilikuwa ni saa 4 usiku lakini kulikuwa na mvua kubwa sana,tulipofika kwenye ile sheli baada ya Jipe kuchomoa SMG kuna mlinzi alimuona akaanza kukimbia kama mwehu huku akiwa na gobole,Jipe hakutaka kumpotezea muda,alipiga risasi ya mgongoni yule mlinzi akawa amedondoka chini.

Jipe "Mtatiro kusanya hao wauza mafuta wote"

Jipe aliingia ndani kwenye vyumba vilivyokuwa kando ya ile sheli huku akiniambia niongozane nae.Pale nje Mtatiro na Gabi waliendelea kuwadhibiti wale wauza mafuta na kuchukua hela huku wakiwa chini ya ulinzi mkali.

Jipe "Toa pesa wewe la sivyo nitakuua"

Jipe alikuwa akimwambia dada mmoja kibonge ambaye tulimkuta mle ndani wakati huo akimnyooshea mtutu wa bunduki.Yule dada alifungua boksi moja lilikuwa la mbao na kulikuwa na noti za kutosha,sasa kulibeba lile boksi mwenyewe kidogo likawa zito,Jipe akamuamuru yule demu atupatie mfuko,yule demu alitoa mfuko mmoja ambao ulikuwa kama shuka ambao ulikuwa umechakazwa na rangi ya maoili!,niliukamata ule mfuko haraka nikaanza kuchukua zile hela haraka sana,sikutaka kabisa kuhangaika na silva maana jipe alisema nitemane nazo,baada kumaliza zile hela,Jipe alimuamuru yule demu alale chini na asijaribu kuinua kichwa kwani atamuua,tuliondoka chap mle ndani kuelekea nje ambapo tuliwakuta Gabi na Mtatiro wakiwa wanatusubiri!.

Tulikimbilia gari na tulipofika dereva aliondoka kwa spidi kali sana lile eneo,wakati huo bado mvua ilikuwa ikiendelea kunyesha sana.Wakati tupo njiani,Jipe alimpigia simu yule demu Kamange na kumtaka achukue ile gari Mark 2 atukute Geita.Ile Noah ilitembea vibaya mno usiku huo na tulifanikiwa kufika Geita mida ya saa 8 Usiku,Jipe akawa amemwambia Gabriel na dereva ya kwamba wao watangulie Mwanza halafu sisi tungeisubiri ile Mark 2.

Kweli,Kesho yake mida ya saa 4 asubuhi yule demu akawa amefika pale Geita kutuchukua tukawa tumeondoka,Tuliingia Mwanza mida ya saa 11 jioni.Tuliwakuta kina Gabi wao wameshafika,sasa tulipofika Mtatiro alimwambia Jipe ya kwamba pesa tulizopora ziletwe zihesabiwe ili kila mtu afe na chake,nadhani wao walidhani Mtatiro anatania lakini jamaa alikuwa serious sana,sikuwahi kufahamu kama Mtatiro akikasirika anakuwa vile aisee,mara zote mimi nimekuwa nikimuona akiwa kawaida nikawa namchukulia poa,siku hiyo ndiyo niliiona rangi halisi ya yule mkurya.

Mtatiro "Haiwezekani tupore pesa halafu nyie muwe mnagawana nyingi na sisi mnatupa kidogo,mkitaka damu leo imwagike ficheni hizo hela muone!"

Jipe "Hakuna atakayedhurumiwa hata mmoja"

Mtatiro "Mbona juzi mmetunyenga?"

Jipe "Yale yalikuwa ni maelekezo ya bosi"

Mtatiro "Basi mwambieni leo kila mtu anapata pasu,sitaki ufara!"

Baada ya jamaa kuona Mtatiro yuko serious,Jipe alimwambia Gabi walete zile pesa ili kila mmoja apewe haki yake.Kweli,mimi na Mtatiro kila mmoja alipata mioni 6,na wao pia walipata kama sisi.Tuliamua kuondoka zetu baada ya kupokea mgao wetu.

Mtatiro "Mwanangu kama ni hela ya mtaji tushapata,tuachane na hizi habari wao kama wanaendelea ngoja waendelee"

Aliendelea "Cha kufanya tukafungue duka la jumla tuachane na mitumba"

Mtatiro "Au wewe unaonaje mwanangu?"

Mimi "Kwanini tusifungue duka la vipodozi?"

Mtatiro "Eti eeeh,sawa?"

Baada ya kupata ile hela kweli tuliachana na biashara ya mitumba na tukafungua duka la vipodozi yale yale maeneo ya Usagara tukaanza kupambana,nakumbuka Mtatiro alikuwaga anafuata vipodozi Uganda kwasababu huko ndiko vilikuwa vinapatikana kwa bei ya chini,kiukweli tulipiga sana hela na maisha yetu yalianza kubadilika mdogo mdogo,ilifika sehemu tukahama pale kwa braza ake Mtatiro kila mmoja akaenda kupanga geto lake mwenyewe.

Nakumbuka siku moja Mtatiro akaja kuniambia kwamba Gabi anampigia simi twende kuna mchongo wenye hela kubwa tukapige.

Mimi "Umemwambiaje!"

Mtatiro "Mi nimemwambia kwasasa tunashughuli zetu,wao kama wanaendelea waendelee!"

Aliendelea "Jamaa baada ya kumwambia ananiambia kwamba tunataka kuwachoma,hivyo tujiangalie tutaumia"

Mimi "Sasa itakuwaje?"

Mtatiro "wale hawawezi kututisha we tulia"

Basi baada ya jamaa kuona hatuwapi tena ushirikiano wakaamua kutokutushirikisha kwenye michongo yao tena lakini walikuwa wamechukia sana baada ya sisi kuachana nao.Baada ya miezi kadhaa kupita,kuna siku Mtatiro akaja kuniambia amesikia habari mahali kuna majambazi wamedakwa wengine wameuawa huko Mbeya na mmoja wapo wa waliodakwa ni Gabi,sasa baada ya kuifatilia ile habari ni kweli kabisa ilikuwa Jipe na majambazi kadhaa wenzie waliuawa palepale eneo la tukio.

Kumbe walienda kumpora mfanyabiashara mmoja mwenye asili ya India ambaye ndani ya gari alikuwa na madini pamoja na pesa alizokuwa akizitoa huko Chunya kuelekea Mbeya,sasa wao hawakujua yule mfanyabiashara alikuwa na eskoti ya askari kadhaa,yawezekana walijua hilo ila wakajifanya wabishi kwakuwa walikuwa na silaha.Walikufa majambazi wawili na mmoja akiwa Jipe huku Gabi na mwingine mmoja wakisalimu amri.

Gabi alifungwa miaka the thelathini gerezani na mwaka juzi nimetoka kumuona pale gereza la Ruanda Mbeya.Jamaa amechoka sana na aliponiona mara ya kwanza alionyesha huzuni lakini hakuwa na namna ndo hivyo ishatokea.Aliniambia yule aliyekuwa bosi wake alikimbilia huko Kenya kuanzisha maisha huko.Huwa namtembelea jamaa nikipata nafasi,na siachi kumtia moyo na kumfariji,namwambia ashukuru akufa,maadam yuko hai basi atatoka tu gerezani na ataendelea na maisha yake ingawaje atakuwa amepoteza muda.

Mimi na Mtatiro lile duka la vipodozi tuliuza na kila mmoja akaendelea na biashara zake,Mtatiro aliondoka kwenda Uganda kwa anko wake hadi leo anaishi huko.Mimi niliamua kurudi Tarime Sirari nikafungua duka nikaanza kukimbiza,kuna mtoto wa dingi mkubwa anaishi Dar es salaam alikuwa anafanya biashara ya vyombo akaniambia nije tuungane tufanye biashara kwa kua inalipa sana,hivyo nikaondoka Tarime kuja Dar,kufika nikampatia jamaa zaidi ya milioni 9 akanidhurumu hadi leo,niliamua kumuachia Mungu nikaanza kupambana upya kutafuta mtaji,nilipopata mtaji nikanunua bodaboda yangu ambayo ndiyo inaniingizia kipato kwa hapa mjini.


Nawapenda sana.


MWISHO.
Nimependa imani yako imeongezeka na umeujja ukweli na uhalisia wa maisha. Umetupa elimu kulingana na mpito yako toka mkasa ule wa kwanza hadi huu.
 
Mwamba Jipe hakutaka kufia kitandani we ndo shujaa wetu wa muda wote umu jf
Acha ujinga wewe kwahyo unaona Ni sahih kwenda kufamia watu kuwaua wasio na hatia ?.mbna hat umughaka Hapa pesa zote alizozipata zote zimezulumiwaa kak short cut is always a wrong cuts ,ona sas amekufa na umughaka Hapa pesa zote amezulumiwa na kuamua kuwa dereva boda boda, hi story siyo ya kufarahisha Ni ya kufindisha haswa
 
Back
Top Bottom