Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua Nyumbani

Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua Nyumbani

Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 20.



Gari ilitembea tukaikamata njia ya Sirari,sasa tukawa kama tunaelekea Musoma.Yule jamaa akamwambia yule demu aliyekua akiendesha gari ya kwamba inapaswa tuweke kituo kwanza Lamadi tukapate msosi kisha ndiyo tuondoke.

Baada ya kufika lamadi na kupata Msosi tuliondoka kuelekea Bariadi,sikuwahi kufika bariadi ni hiyo ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika huko,sasa baada ya kuiacha bariadi tulianza kuingia vijijini huko ndani ndani ambako sikuvifahamu kwa haraka maana sikuwa mwenyeji huko.

Kituo chetu cha mwisho kilikuwa kwenye kijiji cha Mwanaungu ambako baada ya kushushwa hapo,yule jamaa alimwambia yule demu kwamba amsubiri kwanza atupeleke halafu waondoke!.

Mtatiro "Mwanangu kwahiyo mnatuacha?"

Jamaa "Tutarudi kuwachukua ondoa shaka!"

Tulitembea kwa umbali mrefu kidogo hatimaye tukafika kwenye mji mmoja ambao ulikuwa umezungushiwa minyaa ya kutosha,baada ya kufika hapo tulikuta kuna vijumba vingi vya nyasi huku kukiwa na watu ambao wengine walikuwa wamelala kwenye majamvi huku wengine wakiendelea na shughuli zao!.Kuna mwanamke akaja kutupokea kwa salamu ya kisukuma huku akipiga magoti,sasa mimi kwakuwa nilikaa usukumani kwa kipindi fulani wakati baba yangu mdogo akiwa headmaster,ile salamu haikunipa taabu kabisa!,na siyo salamu tu,naweza kukizungumza kisukuma ingawaje cha kuombea maji!.

Baada ya ile salamu yule mwanamke alituletea viti ambavyo havikuwa na watu kwa wakati huo.Basi baada ya muda mfupi yule mwanamke akaja na daftari akatutaka kila mmoja wetu kutaja jina lake na kuandikwa,sasa tulipoandikwa akatuchania vikaratasi vikiwa na namba,mimi nilipewa namba 16 na Mtatiro akapewa namba 17,yule jamaa yeye akamwambia yule mwanamke kwamba anahitaji kuonana na Mwami(Ng'wana Mwami).Yule mwanamke akamtaka asubiri kwanza.

Baada ya muda yule mwanamke akaja akamuita yule jamaa akampeleka mpaka kwenye kinyumba cha nyasi kilichokuwa kikubwa kati ya vile vinyumba tulivyovikuta pale.Baada ya muda yule jamaa akatoka akaja akatuambia angerudi baada ya siku mbili,hatukujua alipoingia mle ndani alienda kuzungumza kitu gani na huyo aliyekuwa humo ndani!.Jamaa aliondoka akatuacha pale,hiyo ilikuwa mida ya mchana saa 7.

Ilipofika mida ya saa 10,kuna mwanamke alitoka kwenye kile kijumba huku akijinyoosha kana kwamba alikuwa amechoka sana!.Alianza kuwazungukiwa watu kadhaa waliokuwa pale nje huku akiongea nao kisukuma na kiswahili!.Alipofika kwetu alitusalimia kisukuma na kama kawaida nami nilimuitikia kisukuma,sasa Mtatiro halikuwa haelewi kabisa hata salamu ndipo nilimwambia yule mama ya kwamba mwenzangu haelewi kisukuma,aliamua kumsalimu kiswahili kisha akaendelea na watu wengine!.Yule mama ndiye aliyekuwa mwenyeji wetu na alikuwa mganga!.

Mtatiro "Mwanangu kisukuma kumbe unakipiga fresh"

Mimi "Nimekaa nao,dingi yangu mdogo alikuwa headmaster shule moja huko Tabora hivyo nilikinyaka kiasi fulani"

Ilipofika mida ya saa 12 jioni kuna watu takribani 7 ambao walikuwa wanaume 3 na wanawake 4 waliingia pale nyumbani huku wakiwa wamebeba majembe,mimi nilidhani ni ndugu tu wanaoishi hapo kumbe walikuwa wateja wa huyo mama.Sasa utaratibu ulikuwa ni kwamba,unapofika kwa huyo mama unapewa namba kama sisi tulivyopewa,wakati ukiendelea kusubiri ili namba yako iitwe ilipaswa kila kunapokucha ukamate jembe umfuate mwenyeji akakuelekeze shamba la kulima na ulikuwa unapewa kipande chako ili upambane nacho,na kipande chenyewe hakikuwa cha kitoto,yaani kama ukimaliza kile kipande ndipo unaambiwa sasa umekolifai kupatiwa matibabu na yule mama.Sasa wakati unasubiri matibabu ndipo mnaitwa kwa namba ambazo hata sisi tulipewa.(Yule mganga alikuwa mjanja sana,badala ya kulima mashamba yake,sisi wapumbavu ambao tulifahamika kama wateja wake ndio tuliomlimia wakati yeye akiwa ametulia nyumbani,Daaah![emoji23][emoji23],na kila mtu aliyefika hapo kwake ni lazima ilikuwa akamatishwe jembe aingie shambani![emoji23][emoji23]).

Mimi na Matatiro tulikomaa na vipande vyetu ambavyo tulivianza siku iliyofuata kwasababu siku tuliyofika tulikuwa tumechelewa,bahati nzuri ilikuwa ni palizi na hakukuwa na nyasi sana!.Siku hiyo tulipomaliza kupalilia lile shamba ilikuwa mida ya saa 9 alasiri,tuliporudi hapo nyumbani kiukweli tulikuwa tumechafuka miguu na kunuka majasho hatari,sasa nilimfuata yule mama aliyetupokea siku ile nikawa nimemwambia atupatie maji ili tuoge,alituambia inapaswa tuwasubiri wenzetu ambao nao walikuwa hawajamaliza sehemu zao ili tupate chakula kwa pamoja kisha ndio tuoge!.

Wale walipotoka huko shambani,tulitengewa ugali wa udaga kwa na furu wa kuchemsha.Sasa tulipaswa kukaa watu watatu watatu kwa ajili ya chakula,mimi nilikaa na Mtatiro kama kawaida pamoja na jamaa mmoja ambaye alikuwa mteja kama sisi!.Siku hiyo ikapita kapa bila kuitwa namba lakini kuna watu wao waliitwa wakaendelea kupewa huduma kama kawaida!.

Siku iliyofuata tukaitwa majina watu kama wanne,sasa kwakuwa mimi na Mtatiro tulikuwa na shida moja ilibidi tuambiwe tusubiri kwanza amalizane na wale wa wawili.Zamu yetu ilifika na tukaitwa ndani kwa yule mama,hatukujieleza hata kidogo bali tulipoingia ndani alitutaka tuvue shati ili kitendo cha kupigwa chale kuchukue nafasi!.

Yule mama alitupiga chale kwa kutumia kisu kilichokuwa kikali kama wembe,alituchanja kila sehemu aliyoona yeye inafaa,baada ya hapo alituchanja pia kwenye ulimi kila mtu!.Alipomaliza kutuchanja na kutupaka dawa,alichukua kitu kilichokuwa kimefungwa na kukazwa sana na kutakiwa kila mmoja akivae kiunoni,ile alituambia ni irizi na asije akatokea mtu akaivua,alisema endapo ikitokea ukaivua basi usije ukamlaumu!.

Mpaka wakati huo hatukufahamu kwa huyo mganga tulipelekwa kufanya nini,ingawa tuliambiwa tunakwenda kutengenezwa ili hatukujua utengenezwaji ulikuwa na faida gani katika ile kazi yetu mpya ambayo tungeianza siku chache zilizokuwa mbele yetu!.

Yule mama alituambia ya kwamba,ile irizi haikupaswa kabisa kutolewa kiunoni hata iweje. Basi baada ya kumaliza ile shughuli tulitoka nje tukaendelea kumsubiri jamaa aliyetuambia angekuja kutuchukua!.Ile siku jamaa hakutokea kabisa,hivyo ikatubidi tulale tena kwa yule mama.

Yale mazingira yalikuwa ya hovyo sana lakini ilibidi tukubaliane na hali kwasababu tuliitamani pesa!.Ilipofika mida ya saa 5 asubuhi ya siku iliyofuata yule jamaa alirudi kutuchukua na kisha tukaondoka,sasa tulipoingia kwenye ile Noah tulikuta kuna mabegi kadhaa na kulikuwa na jamaa mmoja akiwa amekaa siti za abiria,dereva alikuwa ni yuleyule demu ambaye alikuwaga azungumzi na mtu!.

Jamaa "Wanangu safari ni moja kwa moja Arusha"

Mtatiro "Kaka mngeturudisha kwanza tukachukue nguo"

Jamaa "Nguo sio sehemu ya kuwazia,utazikuta huko"

Hatukuwa na swali,tuliamua kukausha na safari kuanza.Tulitembea sana na hatimaye tukaikamata lami kuelekea Musoma,baada ya kuivuka lamadi kwa mbele,tukaikamata geti la Ndabaka linaloingia Serengeti.
Wanaume kazini..

#MaendeleoHayanaChama
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 21.



Haikuwa safari ya kitoto hata kidogo,tuliingia pale Arusha saa 3 usiku.Hii haikuwa mara yangu ya kwanza kufika Arusha,japo nimefika mara kadhaa lakini sikuwahi kuwa mwenyeji,mara zote wakati naenda shule Tanga nilikuwa nikipita Arusha.Baada ya kufika Arusha mjini yule jamaa akawa ametuambia inapaswa tupate chakula mahali fulani ili tukimaliza tuondoke kwakuwa tulipokuwa tukienda hakukuwa na chakula wala mtu wa kukipika!.

Tulipomaliza kula tuliondoka zetu kuelekea ambako mimi na Mtatiro tulikuwa hatupajui.Baada ya muda ile gari ikaanza kupiga honi baada ya kufika mbele ya nyumba ambayo ilikuwa na geti;geti lile lilifunguliwa kisha gari ikaingia ndani.Tuliteremka huku tukiendelea kushangaa shangaa ndipo yule jamaa akaja akatuambia tumfuate,tulielekea ndani ambako tulionyeshwa chumba cha kulala ambacho kilikuwa na vitanda 2.

Wakati ule kiukweli hakuna mtu tuliyemkuta pale kwenye ile nyumba zaidi ya yule mtu aliyetufungulia lile geti,sasa kumbe baada ya ile Noah kutuacha pale wao waliondoka na hakuelewa walienda kulala wapi.Asubuhi mida ya saa 2 yule jamaa tuliyetoka nae Mwanza alikuja kutuchukua na kutuambia inapaswa tuondoke!.Tuliondoka kuelekea Tengeru hatimaye tukafika kwenye nyumba moja ambayo tulimkuta yule bosi wake na Gabi akiwa na jamaa wawili,miongoni mwa wale jamaa tulikuwa nae Mwanza ila yule mmoja sikumfahamu,sasa ilifanya idadi yetu kuwa watu wanne ukimuondoa yule Bosi.Yule bosi alimuita yule jamaa tuliyekuja nae wakaanza kuzungumza kitu ambacho hatukukilewa,sasa baada ya yale mazungumzo jamaa alitoka akawa ameondoka,baada ya muda kuna jamaa mmoja miongoni mwa wale tuliowakuta alikuja akawa ametuuliza mimi na Mtatiro tunavaa viatu namba ngapi kila mmoja.

Baada ya kumueleza size ya namba ya viatu tulizokuwa tunavaa,jamaa aliondoka.Haukupita muda akawa amerudi na viatu aina ya safari boot ambazo kila mtu alipaswa kuchukua size yake!.Sasa ilipofika mida ya jioni yule jamaa tuliyetoka nae Mwanza alirudi akiwa kwenye gari aina ya Mark 2 nyeupe iliyokuwa na tinted,ile gari iliingia mpaka pale ndani kisha jamaa akawa ametelemka na begi jeusi ambalo lilionekana lilikuwa zito.

Jamaa "Aisee hebu njoeni ndani mara moja"

Baada ya kufika ndani,jamaa hakutaka kupoteza muda,alifungua lile begi ambalo lilikuwa na nguo kadhaa akawa amezitoa na kututaka kila mmoja ajaribu itakayo mtosha.Mimi zilizonitosha ilikiwa ni jeans mbili pamoja na cadet moja iliyokuwa nzito,Mtatiro yeye kwakuwa alikuwa na mwili mkubwa kidogo,alipata nguo ambazo ziliendana na mwili wake vizuri.

Sasa baada ya hapo jamaa alituambia tukae chini kisha akawa ametoa bunduki iliyokuwa kwenye lile begi!.Sikufahamu ile bunduki ilikuwa ni aina gani kwasababu sikuwa mtaalamu wa bunduki kwa wakati huo,ile bunduki ilikuwa ni fupi kisha ikawa imekazwa kwa mapira katikati.Sasa baada ya kuitoa ile bunduki yule jamaa alituambia tumsubiri yule aliyekuwa bosi wa Gabi anakuja.

Yule bosi baada ya kurudi na yeye hiyo mida ya saa 2 usiku pia alikuwa na bunduki ambayo niliifahamu ilikuwa SMG.

Bosi "Msiogope bhana haya ni mambo ya kawaida"

Aliendelea "Jamaa yenu mtamkuta Kahama anawasubiri,pale kuna mtu ana hela zangu itapaswa mkazichukue"

Aliendelea "Hii Mashine ningekupatia wewe(Mtatiro)lakini nahitaji kwanza muda"

Aliendelea "Jipe atawapa hiyo nyingine mtaondoka nayo kwenda Kahama halafu hii kuna mtu mtaongozana nae ndiyo atakuwa nayo"

Aliendelea "Sasa naomba simu zenu mziache hapa maana huko hampaswi kwenda na simu"

Basi tulichukua zile simu tukawa tumemkabidhi yule aliyeitwa Bosi.Kumbe muda huo ambao sisi tulikuwa hapo Arusha,Gabi yeye alikuwa Kahama mkoani Shinyanga ambako hatukufahamu alikwenda kufanya shughuli gani!.

Bosi "Nyie mtaondoka kesho kutwa,kaeni hapa mpumzike kwanza"

Baada ya yale mazungumzo,yule Bosi aliondoka na yule jamaa tuliyetoka nae Mwanza wakawa wametuacha pale kwenye ile nyumba tukiwa pamoja na wale jamaa wawili tuliowakuta.

Kweli!,baada ya siku mbili tuliondoka asubuhi na mapema,ilikuwa mida ya saa 10 usiku ndipo tuliianza safari kuelekea Kahama mkoani Shinyanga,mimi kiukweli sikuelewa kilichokuwa kimetupeleka Arusha ilikuwa ni kitu gani maana hata bunduki zenyewe hatukupewa kwa muda huo bali tuliishia tu kuonyeshwa na kupewa maelekezo,sikuweza kuhoji sana niliamua tu kutulia maana nilikubali mwenyewe kujiingiza kwenye genge la ujambazi!.
Tuliondoka na ile Toyota Mark 2 ambayo tulikuwa mimi na Mtatrio pamoja na yule jamaa tuliyetoka nae Mwanza ambaye alifahamika kwa jina la Jipe,sikujua kama ndilo jina lake halisi lakini hata sisi baada ya kuzoeana tulikuwa tukimuita hivyo!.Dereva aliyekuwa akiendesha ile gari kiukweli alikuwa jamaa fulani wa kawaida sana na mwembamba lakini alikuwa dereva mzuri sana,nakumbuka ile gari ilikuwa ikitembea mpaka unahisi inapaa!.

Baada ya safari ndefu hatimaye tukafika Kahama,sasa tulipofika maeneo ya mgodi wa buzwagi,tuliingia kushoto tukaikamata barabara ya vumbi kuelekea Mwendakulima kwa ndani ndani huko.

Haukupita muda tukawa tumefika kwenye nyumba moja ambayo haikuwa na geti lakini ilikuwa imejitenga mbali na nyumba nyingine,sasa tulipofika hapo ndipo tukakutana na Gabriel ambaye baada ya sisi kuteremka kwenye ile gari alimchukua pembeni yule jamaa wakaanza kuzumngumza!.

Baada ya yale mazungumzo Gabi alituambia tuingie ndani huku yule jamaa akibeba lile begi lililokuwa na silaha kuingia nalo ndani!.Tulipiga stori na Gabi huku yeye akiendelea kutupa moyo kwamba yale mambo yalikuwa ni kawaida tu na hatukupaswa kuwa na hofu!.

Siku iliyofuata ilipofika saa 6 usiku,yule jamaa alituambia mimi na Mtatiro tutaongozana nae kuelekea mahali fulani,sasa alimpatia Mtatiro ile bunduki iliyokuwa imefungwa na mapira kwa nguvu sana na yeye akachukua ile SMG.

Jipe "Mtakuwa manafuata maelekezo yangu kila nitakachokuwa nawaambia!"

Mtatiro "Sawa"
Jipe "Hiyo silaha tayari risasi iko chemba,hivyo kuwa makini!"

Aliendelea "Gabriel atabaki hapa kuweka mambo sawa,sisi tutaondoka na tutawahi kurudi,kule tukifika hakuna kusubiri,tunaenda kufata kilichotupeleka!"

Jipe "Wewe jamaa(mimi)utakuwa kando yetu na utafanya nitakachokuwa nakwambia"

Mimi "Sawa"

Mtatiro alivyokuwa ameishika ile silaha ungemuangalia kwa haraka haraka ungezani uenda alikuwa askari mwenye uzoefu wa miaka mingi,jamaa alikuwaga jasiri sana alikuwa mtu ambaye ulikuwa ukimpatia maelekezo mara ya kwanza basi hurudii tena maana alikuwa na kichwa chepesi!.Mpaka muda huo ukweli ni kwamba,Mtatiro ndiye aliyenishawishi hadi na mimi kujikuta naingia mkenge!,sikuwa na namna ilipaswa nitafute pesa!.
Nitarudi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Namba mbili umeharibu, so bodaboda hapaswi kuwa akili. Kuna watu wana masters wanapiga hizo mishe sembuse form6 failure???
Masters anaepiga mishe ya ubodaboda ni MJINGA kabisa.

KWANINI?

Yani umemaliza digrii ya kwanza uakawa jobless (maana unapoamua kuwa bodaboda obvious wewe ni jobless), halafu kwa kuonyesha kabisa hazikutoshi unaamua kuongeza elimu kwa lengo la kuwa BODABODA, hivi inaingia akilini kweli?[emoji23]

Wasomi wengi ni bodaboda ila sio masters holders, labda tusemee hao wenye digrii moja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: ARV
Masters anaepiga mishe ya ubodaboda ni MJINGA kabisa.

KWANINI?

Yani umemaliza digrii ya kwanza uakawa jobless (maana unapoamua kuwa bodaboda obvious wewe ni jobless), halafu kwa kuonyesha kabisa hazikutoshi unaamua kuongeza elimu kwa lengo la kuwa BODABODA, hivi inaingia akilini kweli?[emoji23]

Wasomi wengi ni bodaboda ila sio masters holders, labda tusemee hao wenye digrii moja.

Sent using Jamii Forums mobile app
Duh... Yaani mtu anayeamua kuendesha Bodaboda yeye ni Jobless? Kwahiyo ile Bodaboda sio JOB?

Na Kwa msingi huo tuseme nyinyi wasomi elimu yenu haijawasaidia nyinyi na Taifa Kwa ujumla maana mmeshindwa kutatua tatizo la ajira kabisa maana boda boda ni wengi kuliko nyinyi waajiliwa!
 
imefungwa

Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 25.



"Wewe ni mtu muhimu sana kwangu Mtatiro na umekuwa sehemu ya furaha katika maisha yangu,ulinipokea na kunisaidia wakati mzee aliponitimua nyumbani,hukuniacha katika matatizo bali ulinishika mkono kama kijana mwenzio hivyo na mimi sitokuacha rafiki yangu" ni maneno niliyokuwa nikimwambia rafiki yangu wa damu Mtatiro ili aendelee kuwa na amani kabisa.

USHAURI

Kuishi na Virusi vya Ukimwi si mwisho wa maisha na uhai,kama kuna kitu nakichukia katika maisha yangu ni ubaguzi unaofanywa kwa hawa ndugu zangu,haya ni maisha tu na tunapaswa kupendana,unaweza ukawa muaminifu na bado mumeo/mkeo akakuletea ugonjwa,hivyo hatupaswi kuwanyooshea wengine vidole kana kwamba ni wadhambi kuliko sisi,tuache dharau za kijuaji na kebehi zisizo na msingi.

Ndugu zangu pia niwaombe mzingatie dawa kwa wakati ili ziweze kuwafubaza virusi angalau unapokutana na mwenzako usimuambikize ili muendelee kufurahia maisha,jambo la msingi ni wewe mwenyewe kuacha kujibagua,jikubali na songa mbele.Acha starehe za kijinga,panga mipango yako na timiza ndoto zako,usiwe mlevi kupita kiasi na hakuna sababu ya kuwaambukiza wengine kwa makusudi,wapende watu wote.Pia achana na imani za mitume na manabii kwamba wakupatie maji au mafuta utumie kisha uache dawa,achana kabisa na hizo imani mfu,wewe muombe Mungu atakusikia,kama akipenda anaweza kuuondoa huo ugonjwa na kama akiona inafaa wewe kuendelea nao basi Mshukuru na endelea kuishi,hata kama ukimuomba Mungu na ugonjwa usitoke lakini Mungu bado atabaki kuwa mwema hivyo usikate tamaa.

NAWAPENDA SANA



Basi baada ya afya ya rafiki yangu kipenzi Mtatiro kuimalika tuliendelea na kazi yetu ya kuuza mitumba sehemu na vijiji mbalimbali vya kanda ya ziwa.Nakumbuka siku moja Gabi alimpigia simu Mtatiro akawa amemuambia inapaswa tuonane ili tupange mikakati ya kuelekea maeneo kama kawa.Kweli,tuliondoka siku iliyofuata kuelekea kule yalipokuwa makazi ya muda ilipokuwa inasukwa mipango kabla.Tulipofika pale ndani tulimkuta Gabi kama kawaida akiwepo Jipe na jamaa yule dereva tuliyeenda nae kwenye tukio kahama.

Jipe "Wanangu mko poa"

Mtatiro "Tuko fiti kaka"

Jipe "Sasa Kesho safari ni Kagera"

Aliendelea "Si mko vizuri?"

Mtatiro "Sisi tuko tayari hata leo kaka ni nyinyi tu!"

Jipe "Sawa,Gabriel atatangulia leo halafu sisi kesho jioni tutaondoka"

Basi baada ya yale mazungumzo Jipe akatutaka tujitayarishe kwa ajili ya safari kesho yake.Mimi na Mtatiro tuliamua kurudi nyumbani huku Mtatiro akiapa na kusema safari hii wakijidai kutudhurumu basi ama zake ama zao!.

Siku iliyofuata mida ya saa 7 mchana tulikuwa tushafika eneo la tukio na ndipo tukakamata Noah na kuianza safari ya kuelekea mkoa wa Kagera,kwenye gari nilikuwa mimi na Mtatiro wakati huo jipe akiwa amekaa kwa mbele pamoja na yule jamaa dereva!.Tuliingia Kagera mida ya saa 12 asubuhi siku iliyofuata,njia tuliyotumia ni ileile ya kupitia Kahama huku tukiwa makini kupita maelekezo,Jipe alikuwa ametoa maelekezo ya kwamba,yeyote atakaye jiingiza mkenge basi ingekuwa ni halali yetu!.Baada ya kufika Kagera,Jipe aliwasiliana na Gabi ambaye alimuelekeza maeneo ambayo tungemkuta,nakumbuka tuliikamata njia na uelekeo wa Bukoba mjini,nje kidogo ya mji tukamkuta Gabi.

Gabi "wazee kwa huku itabidi tuzunguke kidogo muda uende kwasababu hatuna makazi,na ikifika mida tutaitana tufanye kilichotuleta".

Kwakuwa mimi na Mtatiro ndiyo ilikuwa mara yetu ya kwanza kufika Kagera ilibidi tukae kwenye ile gari maana hatukutaka kucheza mbali tukajichanganya na ukizangatia hatukuwa na simu!.Dereva alitafuta maeneo ambayo hayakuwa na shughuli nyingi za watu akapaki gari hapo.

Ilipofika mida ya saa 10 jioni mvua ikaanza kunyesha kama masikhara lakini muda ulipozidi ndipo hali ilizidi kuwa mbaya,tangu nizaliwe sijawahi kuona radi zikipiga kama siku hiyo,ile mvua ilikuwa na radi si mchezo hadi uoga ukawa unaniingia!.Kadiri muda ulivyozidi ndivyo mvua nayo ilizidi kuongeza spidi na nilikuwa naona Jipe anaomba iendelee kunyesha vilevile isikatike.Sasa ikafika mida ya saa 12 ikapungua ikawa inanyesha kidogo sana,tulikuwa ndani ya gari wakati huo tukiendelea kuvuta muda.Ilipofika mida ya saa 3 usiku mvua ikaanza tena kunyesha kama mwanzo.

Jipe "Huu ni muda sasa"

Aliendelea "Aisee wewe utaenda kutusubiri mahali nitakapokuelekeza"

Jipe "Wengine wote tutaongozana na mtafanya kila nitakachowaambia"

Basi ile gari ikaanza kuondoka kuelekea uelekeo wa Bukoba Mjini,kuna mahali tulifika ambapo kwa umbali kama wa mita 500 kulikuwa na sheli(sitoitaja),dereva alitakiwa kuzima taa na kugeuza gari atusubiri hapo!.Kila mmoja alikuwa tayari kwa ajili ya makabiliano.Muda huo ilikuwa ni saa 4 usiku lakini kulikuwa na mvua kubwa sana,tulipofika kwenye ile sheli baada ya Jipe kuchomoa SMG kuna mlinzi alimuona akaanza kukimbia kama mwehu huku akiwa na gobole,Jipe hakutaka kumpotezea muda,alipiga risasi ya mgongoni yule mlinzi akawa amedondoka chini.

Jipe "Mtatiro kusanya hao wauza mafuta wote"

Jipe aliingia ndani kwenye vyumba vilivyokuwa kando ya ile sheli huku akiniambia niongozane nae.Pale nje Mtatiro na Gabi waliendelea kuwadhibiti wale wauza mafuta na kuchukua hela huku wakiwa chini ya ulinzi mkali.

Jipe "Toa pesa wewe la sivyo nitakuua"

Jipe alikuwa akimwambia dada mmoja kibonge ambaye tulimkuta mle ndani wakati huo akimnyooshea mtutu wa bunduki.Yule dada alifungua boksi moja lilikuwa la mbao na kulikuwa na noti za kutosha,sasa kulibeba lile boksi mwenyewe kidogo likawa zito,Jipe akamuamuru yule demu atupatie mfuko,yule demu alitoa mfuko mmoja ambao ulikuwa kama shuka ambao ulikuwa umechakazwa na rangi ya maoili!,niliukamata ule mfuko haraka nikaanza kuchukua zile hela haraka sana,sikutaka kabisa kuhangaika na silva maana jipe alisema nitemane nazo,baada kumaliza zile hela,Jipe alimuamuru yule demu alale chini na asijaribu kuinua kichwa kwani atamuua,tuliondoka chap mle ndani kuelekea nje ambapo tuliwakuta Gabi na Mtatiro wakiwa wanatusubiri!.

Tulikimbilia gari na tulipofika dereva aliondoka kwa spidi kali sana lile eneo,wakati huo bado mvua ilikuwa ikiendelea kunyesha sana.Wakati tupo njiani,Jipe alimpigia simu yule demu Kamange na kumtaka achukue ile gari Mark 2 atukute Geita.Ile Noah ilitembea vibaya mno usiku huo na tulifanikiwa kufika Geita mida ya saa 8 Usiku,Jipe akawa amemwambia Gabriel na dereva ya kwamba wao watangulie Mwanza halafu sisi tungeisubiri ile Mark 2.

Kweli,Kesho yake mida ya saa 4 asubuhi yule demu akawa amefika pale Geita kutuchukua tukawa tumeondoka,Tuliingia Mwanza mida ya saa 11 jioni.Tuliwakuta kina Gabi wao wameshafika,sasa tulipofika Mtatiro alimwambia Jipe ya kwamba pesa tulizopora ziletwe zihesabiwe ili kila mtu afe na chake,nadhani wao walidhani Mtatiro anatania lakini jamaa alikuwa serious sana,sikuwahi kufahamu kama Mtatiro akikasirika anakuwa vile aisee,mara zote mimi nimekuwa nikimuona akiwa kawaida nikawa namchukulia poa,siku hiyo ndiyo niliiona rangi halisi ya yule mkurya.

Mtatiro "Haiwezekani tupore pesa halafu nyie muwe mnagawana nyingi na sisi mnatupa kidogo,mkitaka damu leo imwagike ficheni hizo hela muone!"

Jipe "Hakuna atakayedhurumiwa hata mmoja"

Mtatiro "Mbona juzi mmetunyenga?"

Jipe "Yale yalikuwa ni maelekezo ya bosi"

Mtatiro "Basi mwambieni leo kila mtu anapata pasu,sitaki ufara!"

Baada ya jamaa kuona Mtatiro yuko serious,Jipe alimwambia Gabi walete zile pesa ili kila mmoja apewe haki yake.Kweli,mimi na Mtatiro kila mmoja alipata mioni 6,na wao pia walipata kama sisi.Tuliamua kuondoka zetu baada ya kupokea mgao wetu.

Mtatiro "Mwanangu kama ni hela ya mtaji tushapata,tuachane na hizi habari wao kama wanaendelea ngoja waendelee"

Aliendelea "Cha kufanya tukafungue duka la jumla tuachane na mitumba"

Mtatiro "Au wewe unaonaje mwanangu?"

Mimi "Kwanini tusifungue duka la vipodozi?"

Mtatiro "Eti eeeh,sawa?"

Baada ya kupata ile hela kweli tuliachana na biashara ya mitumba na tukafungua duka la vipodozi yale yale maeneo ya Usagara tukaanza kupambana,nakumbuka Mtatiro alikuwaga anafuata vipodozi Uganda kwasababu huko ndiko vilikuwa vinapatikana kwa bei ya chini,kiukweli tulipiga sana hela na maisha yetu yalianza kubadilika mdogo mdogo,ilifika sehemu tukahama pale kwa braza ake Mtatiro kila mmoja akaenda kupanga geto lake mwenyewe.

Nakumbuka siku moja Mtatiro akaja kuniambia kwamba Gabi anampigia simi twende kuna mchongo wenye hela kubwa tukapige.

Mimi "Umemwambiaje!"

Mtatiro "Mi nimemwambia kwasasa tunashughuli zetu,wao kama wanaendelea waendelee!"

Aliendelea "Jamaa baada ya kumwambia ananiambia kwamba tunataka kuwachoma,hivyo tujiangalie tutaumia"

Mimi "Sasa itakuwaje?"

Mtatiro "wale hawawezi kututisha we tulia"

Basi baada ya jamaa kuona hatuwapi tena ushirikiano wakaamua kutokutushirikisha kwenye michongo yao tena lakini walikuwa wamechukia sana baada ya sisi kuachana nao.Baada ya miezi kadhaa kupita,kuna siku Mtatiro akaja kuniambia amesikia habari mahali kuna majambazi wamedakwa wengine wameuawa huko Mbeya na mmoja wapo wa waliodakwa ni Gabi,sasa baada ya kuifatilia ile habari ni kweli kabisa ilikuwa Jipe na majambazi kadhaa wenzie waliuawa palepale eneo la tukio.

Kumbe walienda kumpora mfanyabiashara mmoja mwenye asili ya India ambaye ndani ya gari alikuwa na madini pamoja na pesa alizokuwa akizitoa huko Chunya kuelekea Mbeya,sasa wao hawakujua yule mfanyabiashara alikuwa na eskoti ya askari kadhaa,yawezekana walijua hilo ila wakajifanya wabishi kwakuwa walikuwa na silaha.Walikufa majambazi wawili na mmoja akiwa Jipe huku Gabi na mwingine mmoja wakisalimu amri.

Gabi alifungwa miaka the thelathini gerezani na mwaka juzi nimetoka kumuona pale gereza la Ruanda Mbeya.Jamaa amechoka sana na aliponiona mara ya kwanza alionyesha huzuni lakini hakuwa na namna ndo hivyo ishatokea.Aliniambia yule aliyekuwa bosi wake alikimbilia huko Kenya kuanzisha maisha huko.Huwa namtembelea jamaa nikipata nafasi,na siachi kumtia moyo na kumfariji,namwambia ashukuru akufa,maadam yuko hai basi atatoka tu gerezani na ataendelea na maisha yake ingawaje atakuwa amepoteza muda.

Mimi na Mtatiro lile duka la vipodozi tuliuza na kila mmoja akaendelea na biashara zake,Mtatiro aliondoka kwenda Uganda kwa anko wake hadi leo anaishi huko.Mimi niliamua kurudi Tarime Sirari nikafungua duka nikaanza kukimbiza,kuna mtoto wa dingi mkubwa anaishi Dar es salaam alikuwa anafanya biashara ya vyombo akaniambia nije tuungane tufanye biashara kwa kua inalipa sana,hivyo nikaondoka Tarime kuja Dar,kufika nikampatia jamaa zaidi ya milioni 9 akanidhurumu hadi leo,niliamua kumuachia Mungu nikaanza kupambana upya kutafuta mtaji,nilipopata mtaji nikanunua bodaboda yangu ambayo ndiyo inaniingizia kipato kwa hapa mjini.


Nawapenda sana.


MWISHO.
Part hii imeniumiza Sana dah
 
Nimepita Hapa NYASURA, alikoshukia [mention]UMUGHAKA [/mention] wakati akielekea Mgodini alikoenda kumuona Mtatiro
 
Mwamba kalazimisha kuimaliza story mapema kuna matukio ameyaruka kwa makusudi Ila siyo kwa kupenda.
Ila ni kwa sisi tuliosomea Cuba tumesanuka.
Umegundua kama Mimi. Kwa kweli aanzishe Whatsapp group atupie huko.

Jf Ina maibilis na mapoyoyo wengi. Yaani MTU anamapenzi ya kuwapostia mna mzingua. Masenge majitu tunaita ma monster 👹

Hii story niliona inakwenda mpaka mtatiro alivyoaga dunia.

Umughaka alivyoamua kuwa boda hapo kati mengi ameyaacha
 
Nilichojifunza!
1. Usifanye dili haramu na mwanamke hususani mpenzi
2. Rafiki anamuchango mkubwa kukutengeneza au kukuharibu tabia
3. Hakuna aliyemkamirifu ( mapongo walimwibia OMUGHAKA Pesa zake) na Bosi zao mapongo WALIWAACHIA kwa Kupokea RUSHWA ...
4. Kumfukuza mtoto nyumbani nikutaka kumpoteza! Omghaka ni mwanaume vipi kwa dadazetu si angekuwa KAHABA!
5. Elimu ya secondary kwa mtoto ni chimbuko la kuinuka au kuanguka kimaadili
6. Tamaa mbele mauti nyuma
7. Maisha ni vita
8. Pesa nyingi zinatokana na dili haramu, Rushwa, TOZO, magendo na sadaka feki Zilizo pambwa majina mazuri kuhalalisha! Lakini msingi wake mkubwa ni HARAMU
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 25.



"Wewe ni mtu muhimu sana kwangu Mtatiro na umekuwa sehemu ya furaha katika maisha yangu,ulinipokea na kunisaidia wakati mzee aliponitimua nyumbani,hukuniacha katika matatizo bali ulinishika mkono kama kijana mwenzio hivyo na mimi sitokuacha rafiki yangu" ni maneno niliyokuwa nikimwambia rafiki yangu wa damu Mtatiro ili aendelee kuwa na amani kabisa.

USHAURI

Kuishi na Virusi vya Ukimwi si mwisho wa maisha na uhai,kama kuna kitu nakichukia katika maisha yangu ni ubaguzi unaofanywa kwa hawa ndugu zangu,haya ni maisha tu na tunapaswa kupendana,unaweza ukawa muaminifu na bado mumeo/mkeo akakuletea ugonjwa,hivyo hatupaswi kuwanyooshea wengine vidole kana kwamba ni wadhambi kuliko sisi,tuache dharau za kijuaji na kebehi zisizo na msingi.

Ndugu zangu pia niwaombe mzingatie dawa kwa wakati ili ziweze kuwafubaza virusi angalau unapokutana na mwenzako usimuambikize ili muendelee kufurahia maisha,jambo la msingi ni wewe mwenyewe kuacha kujibagua,jikubali na songa mbele.Acha starehe za kijinga,panga mipango yako na timiza ndoto zako,usiwe mlevi kupita kiasi na hakuna sababu ya kuwaambukiza wengine kwa makusudi,wapende watu wote.Pia achana na imani za mitume na manabii kwamba wakupatie maji au mafuta utumie kisha uache dawa,achana kabisa na hizo imani mfu,wewe muombe Mungu atakusikia,kama akipenda anaweza kuuondoa huo ugonjwa na kama akiona inafaa wewe kuendelea nao basi Mshukuru na endelea kuishi,hata kama ukimuomba Mungu na ugonjwa usitoke lakini Mungu bado atabaki kuwa mwema hivyo usikate tamaa.

NAWAPENDA SANA



Basi baada ya afya ya rafiki yangu kipenzi Mtatiro kuimalika tuliendelea na kazi yetu ya kuuza mitumba sehemu na vijiji mbalimbali vya kanda ya ziwa.Nakumbuka siku moja Gabi alimpigia simu Mtatiro akawa amemuambia inapaswa tuonane ili tupange mikakati ya kuelekea maeneo kama kawa.Kweli,tuliondoka siku iliyofuata kuelekea kule yalipokuwa makazi ya muda ilipokuwa inasukwa mipango kabla.Tulipofika pale ndani tulimkuta Gabi kama kawaida akiwepo Jipe na jamaa yule dereva tuliyeenda nae kwenye tukio kahama.

Jipe "Wanangu mko poa"

Mtatiro "Tuko fiti kaka"

Jipe "Sasa Kesho safari ni Kagera"

Aliendelea "Si mko vizuri?"

Mtatiro "Sisi tuko tayari hata leo kaka ni nyinyi tu!"

Jipe "Sawa,Gabriel atatangulia leo halafu sisi kesho jioni tutaondoka"

Basi baada ya yale mazungumzo Jipe akatutaka tujitayarishe kwa ajili ya safari kesho yake.Mimi na Mtatiro tuliamua kurudi nyumbani huku Mtatiro akiapa na kusema safari hii wakijidai kutudhurumu basi ama zake ama zao!.

Siku iliyofuata mida ya saa 7 mchana tulikuwa tushafika eneo la tukio na ndipo tukakamata Noah na kuianza safari ya kuelekea mkoa wa Kagera,kwenye gari nilikuwa mimi na Mtatiro wakati huo jipe akiwa amekaa kwa mbele pamoja na yule jamaa dereva!.Tuliingia Kagera mida ya saa 12 asubuhi siku iliyofuata,njia tuliyotumia ni ileile ya kupitia Kahama huku tukiwa makini kupita maelekezo,Jipe alikuwa ametoa maelekezo ya kwamba,yeyote atakaye jiingiza mkenge basi ingekuwa ni halali yetu!.Baada ya kufika Kagera,Jipe aliwasiliana na Gabi ambaye alimuelekeza maeneo ambayo tungemkuta,nakumbuka tuliikamata njia na uelekeo wa Bukoba mjini,nje kidogo ya mji tukamkuta Gabi.

Gabi "wazee kwa huku itabidi tuzunguke kidogo muda uende kwasababu hatuna makazi,na ikifika mida tutaitana tufanye kilichotuleta".

Kwakuwa mimi na Mtatiro ndiyo ilikuwa mara yetu ya kwanza kufika Kagera ilibidi tukae kwenye ile gari maana hatukutaka kucheza mbali tukajichanganya na ukizangatia hatukuwa na simu!.Dereva alitafuta maeneo ambayo hayakuwa na shughuli nyingi za watu akapaki gari hapo.

Ilipofika mida ya saa 10 jioni mvua ikaanza kunyesha kama masikhara lakini muda ulipozidi ndipo hali ilizidi kuwa mbaya,tangu nizaliwe sijawahi kuona radi zikipiga kama siku hiyo,ile mvua ilikuwa na radi si mchezo hadi uoga ukawa unaniingia!.Kadiri muda ulivyozidi ndivyo mvua nayo ilizidi kuongeza spidi na nilikuwa naona Jipe anaomba iendelee kunyesha vilevile isikatike.Sasa ikafika mida ya saa 12 ikapungua ikawa inanyesha kidogo sana,tulikuwa ndani ya gari wakati huo tukiendelea kuvuta muda.Ilipofika mida ya saa 3 usiku mvua ikaanza tena kunyesha kama mwanzo.

Jipe "Huu ni muda sasa"

Aliendelea "Aisee wewe utaenda kutusubiri mahali nitakapokuelekeza"

Jipe "Wengine wote tutaongozana na mtafanya kila nitakachowaambia"

Basi ile gari ikaanza kuondoka kuelekea uelekeo wa Bukoba Mjini,kuna mahali tulifika ambapo kwa umbali kama wa mita 500 kulikuwa na sheli(sitoitaja),dereva alitakiwa kuzima taa na kugeuza gari atusubiri hapo!.Kila mmoja alikuwa tayari kwa ajili ya makabiliano.Muda huo ilikuwa ni saa 4 usiku lakini kulikuwa na mvua kubwa sana,tulipofika kwenye ile sheli baada ya Jipe kuchomoa SMG kuna mlinzi alimuona akaanza kukimbia kama mwehu huku akiwa na gobole,Jipe hakutaka kumpotezea muda,alipiga risasi ya mgongoni yule mlinzi akawa amedondoka chini.

Jipe "Mtatiro kusanya hao wauza mafuta wote"

Jipe aliingia ndani kwenye vyumba vilivyokuwa kando ya ile sheli huku akiniambia niongozane nae.Pale nje Mtatiro na Gabi waliendelea kuwadhibiti wale wauza mafuta na kuchukua hela huku wakiwa chini ya ulinzi mkali.

Jipe "Toa pesa wewe la sivyo nitakuua"

Jipe alikuwa akimwambia dada mmoja kibonge ambaye tulimkuta mle ndani wakati huo akimnyooshea mtutu wa bunduki.Yule dada alifungua boksi moja lilikuwa la mbao na kulikuwa na noti za kutosha,sasa kulibeba lile boksi mwenyewe kidogo likawa zito,Jipe akamuamuru yule demu atupatie mfuko,yule demu alitoa mfuko mmoja ambao ulikuwa kama shuka ambao ulikuwa umechakazwa na rangi ya maoili!,niliukamata ule mfuko haraka nikaanza kuchukua zile hela haraka sana,sikutaka kabisa kuhangaika na silva maana jipe alisema nitemane nazo,baada kumaliza zile hela,Jipe alimuamuru yule demu alale chini na asijaribu kuinua kichwa kwani atamuua,tuliondoka chap mle ndani kuelekea nje ambapo tuliwakuta Gabi na Mtatiro wakiwa wanatusubiri!.

Tulikimbilia gari na tulipofika dereva aliondoka kwa spidi kali sana lile eneo,wakati huo bado mvua ilikuwa ikiendelea kunyesha sana.Wakati tupo njiani,Jipe alimpigia simu yule demu Kamange na kumtaka achukue ile gari Mark 2 atukute Geita.Ile Noah ilitembea vibaya mno usiku huo na tulifanikiwa kufika Geita mida ya saa 8 Usiku,Jipe akawa amemwambia Gabriel na dereva ya kwamba wao watangulie Mwanza halafu sisi tungeisubiri ile Mark 2.

Kweli,Kesho yake mida ya saa 4 asubuhi yule demu akawa amefika pale Geita kutuchukua tukawa tumeondoka,Tuliingia Mwanza mida ya saa 11 jioni.Tuliwakuta kina Gabi wao wameshafika,sasa tulipofika Mtatiro alimwambia Jipe ya kwamba pesa tulizopora ziletwe zihesabiwe ili kila mtu afe na chake,nadhani wao walidhani Mtatiro anatania lakini jamaa alikuwa serious sana,sikuwahi kufahamu kama Mtatiro akikasirika anakuwa vile aisee,mara zote mimi nimekuwa nikimuona akiwa kawaida nikawa namchukulia poa,siku hiyo ndiyo niliiona rangi halisi ya yule mkurya.

Mtatiro "Haiwezekani tupore pesa halafu nyie muwe mnagawana nyingi na sisi mnatupa kidogo,mkitaka damu leo imwagike ficheni hizo hela muone!"

Jipe "Hakuna atakayedhurumiwa hata mmoja"

Mtatiro "Mbona juzi mmetunyenga?"

Jipe "Yale yalikuwa ni maelekezo ya bosi"

Mtatiro "Basi mwambieni leo kila mtu anapata pasu,sitaki ufara!"

Baada ya jamaa kuona Mtatiro yuko serious,Jipe alimwambia Gabi walete zile pesa ili kila mmoja apewe haki yake.Kweli,mimi na Mtatiro kila mmoja alipata mioni 6,na wao pia walipata kama sisi.Tuliamua kuondoka zetu baada ya kupokea mgao wetu.

Mtatiro "Mwanangu kama ni hela ya mtaji tushapata,tuachane na hizi habari wao kama wanaendelea ngoja waendelee"

Aliendelea "Cha kufanya tukafungue duka la jumla tuachane na mitumba"

Mtatiro "Au wewe unaonaje mwanangu?"

Mimi "Kwanini tusifungue duka la vipodozi?"

Mtatiro "Eti eeeh,sawa?"

Baada ya kupata ile hela kweli tuliachana na biashara ya mitumba na tukafungua duka la vipodozi yale yale maeneo ya Usagara tukaanza kupambana,nakumbuka Mtatiro alikuwaga anafuata vipodozi Uganda kwasababu huko ndiko vilikuwa vinapatikana kwa bei ya chini,kiukweli tulipiga sana hela na maisha yetu yalianza kubadilika mdogo mdogo,ilifika sehemu tukahama pale kwa braza ake Mtatiro kila mmoja akaenda kupanga geto lake mwenyewe.

Nakumbuka siku moja Mtatiro akaja kuniambia kwamba Gabi anampigia simi twende kuna mchongo wenye hela kubwa tukapige.

Mimi "Umemwambiaje!"

Mtatiro "Mi nimemwambia kwasasa tunashughuli zetu,wao kama wanaendelea waendelee!"

Aliendelea "Jamaa baada ya kumwambia ananiambia kwamba tunataka kuwachoma,hivyo tujiangalie tutaumia"

Mimi "Sasa itakuwaje?"

Mtatiro "wale hawawezi kututisha we tulia"

Basi baada ya jamaa kuona hatuwapi tena ushirikiano wakaamua kutokutushirikisha kwenye michongo yao tena lakini walikuwa wamechukia sana baada ya sisi kuachana nao.Baada ya miezi kadhaa kupita,kuna siku Mtatiro akaja kuniambia amesikia habari mahali kuna majambazi wamedakwa wengine wameuawa huko Mbeya na mmoja wapo wa waliodakwa ni Gabi,sasa baada ya kuifatilia ile habari ni kweli kabisa ilikuwa Jipe na majambazi kadhaa wenzie waliuawa palepale eneo la tukio.

Kumbe walienda kumpora mfanyabiashara mmoja mwenye asili ya India ambaye ndani ya gari alikuwa na madini pamoja na pesa alizokuwa akizitoa huko Chunya kuelekea Mbeya,sasa wao hawakujua yule mfanyabiashara alikuwa na eskoti ya askari kadhaa,yawezekana walijua hilo ila wakajifanya wabishi kwakuwa walikuwa na silaha.Walikufa majambazi wawili na mmoja akiwa Jipe huku Gabi na mwingine mmoja wakisalimu amri.

Gabi alifungwa miaka the thelathini gerezani na mwaka juzi nimetoka kumuona pale gereza la Ruanda Mbeya.Jamaa amechoka sana na aliponiona mara ya kwanza alionyesha huzuni lakini hakuwa na namna ndo hivyo ishatokea.Aliniambia yule aliyekuwa bosi wake alikimbilia huko Kenya kuanzisha maisha huko.Huwa namtembelea jamaa nikipata nafasi,na siachi kumtia moyo na kumfariji,namwambia ashukuru akufa,maadam yuko hai basi atatoka tu gerezani na ataendelea na maisha yake ingawaje atakuwa amepoteza muda.

Mimi na Mtatiro lile duka la vipodozi tuliuza na kila mmoja akaendelea na biashara zake,Mtatiro aliondoka kwenda Uganda kwa anko wake hadi leo anaishi huko.Mimi niliamua kurudi Tarime Sirari nikafungua duka nikaanza kukimbiza,kuna mtoto wa dingi mkubwa anaishi Dar es salaam alikuwa anafanya biashara ya vyombo akaniambia nije tuungane tufanye biashara kwa kua inalipa sana,hivyo nikaondoka Tarime kuja Dar,kufika nikampatia jamaa zaidi ya milioni 9 akanidhurumu hadi leo,niliamua kumuachia Mungu nikaanza kupambana upya kutafuta mtaji,nilipopata mtaji nikanunua bodaboda yangu ambayo ndiyo inaniingizia kipato kwa hapa mjini.


Nawapenda sana.


MWISHO.
Pole kiongozi.... ila kwanin umemuacha huyo jamaa aliekudhulum?
 
Dah! Nimesoma hii habari kama vile naangalia movie. Jamaa Mungu akupe maisha marefu,sawa umeumiza watu kwenye hiyo background yako na wenzako lakini nimekuelewa,hii nayo ni side B ya maisha yako.

Ni hustler haswa, rafiki yako Mtatiro dah! Ameniuma naye aisee. Sema alikuwa rafiki wa kweli aisee. Hii story nimejifunza mengi haswa.
Haya maisha ukitoboa kw shortcut basi ujue umebarikiwa,shortcut is such a long cut then.

Wewe hata mtu akija akaseme umfundishe maisha atatoboa maana ugumu wote wa life umeupitia haswa
 
Duh... Yaani mtu anayeamua kuendesha Bodaboda yeye ni Jobless? Kwahiyo ile Bodaboda sio JOB?

Na Kwa msingi huo tuseme nyinyi wasomi elimu yenu haijawasaidia nyinyi na Taifa Kwa ujumla maana mmeshindwa kutatua tatizo la ajira kabisa maana boda boda ni wengi kuliko nyinyi waajiliwa!
Unalazimisha ionekane kama nimewadharau ila msingi wa hoja yangu ni kwamba, HAKUNA BODABODA mwenye masters.

Ikiwa kwa degree moja mtu kakosa shughuli nyingine (akawa jobless) mpaka kaamua kujikita kwenye bodaboda (ambayo kimsingi sijaidharau), hiyo degree ya pili (Masters) ataenda kuitafuta ili iweje? Unless awe ni mtu asiyejitambua.

HIYO NDIO ILIKUWA HOJA YANGU, hakuna bodaboda mwenye MASTERS.
 
Unalazimisha ionekane kama nimewadharau ila msingi wa hoja yangu ni kwamba, HAKUNA BODABODA mwenye masters.

Ikiwa kwa degree moja mtu kakosa shughuli nyingine (akawa jobless) mpaka kaamua kujikita kwenye bodaboda (ambayo kimsingi sijaidharau), hiyo degree ya pili (Masters) ataenda kuitafuta ili iweje? Unless awe ni mtu asiyejitambua.

HIYO NDIO ILIKUWA HOJA YANGU, hakuna bodaboda mwenye MASTERS.
Aiseee.
 
Nilivyonusurika Kifo baada ya Mzee kunitimua nyumbani - 23.



Baada ya gari kuingia ndani ya ile nyumba,Gabi alishuka na zile hela kwenye lile gunia na Jipe alifunua zile siti akatoa silaha kisha tukaingia wote ndani,baada ya kufika ndani yule dereva hakukaa sana akawa ameondoka!.Kiukweli zile hela zilikuwa nyingi mno zaidi ya milioni 50,maana tangu nilivyoanza kushika hela japo nilizoshika nyingi zilikuwa za bandia lakini nilikuwa ninafahamu bunda likiwa na milioni 1 au zaidi,zile za kwenye ule mfuko kiukweli zilikuwa nyingi na nina hakika zilizidi milioni hamsini.

Tuliamua kukaa kimya kwenye ile nyumba huku kila mmoja akitafakari kivyake kichwani mwake!,hakukuwa kabisa na muda wala hamu ya kupata usingizi!.

Sasa ilipofika mida ya saa 1 asubuhi alitokea yule bosi wake na Gabi ambaye hakuwepo hapo nyumbani na nakumbuka alikuja na kale kadada kalikokuwa kadereva tulipoenda Arusha.Baada ya kufika alikuja moja kwa moja hadi sebuleni ambapo mimi na Mtatiro tulikuwa tumejiegesha kwenye makochi.

Bosi "Jipe yuko wapi?"

Mtatiro "watakuwa huko ndani!"

Basi yule bosi aliingia ndani vyumbani huko na baada ya muda akawa ametoka akiwa ameongozana na Gabi pamoja na Jipe aliyekuwa amebeba lile fuko lililokuwa na hela!.
Bosi "Mlizihesabu?"

Jipe "Hapana bosi hatukuwa na muda huo na tumefika muda si mrefu"

Bosi "Kwanini mlimpiga jamaa risasi?"

Jipe "Alitaka kuleta ubishi bosi na sisi tulitaka kuwahi!"

Bosi "Sawa ni jambo jema ila niliwahi kukwambia uwe unaangalia na mazingira Jipe,usiwe unatumia tu risasi hata ambapo unaona hakuna uhitaji,hizo risasi nazipata kwa gharama sana!"

Aliendelea "Tukiwa Namanga nimewahi kukwambia ikiwezekana risasi itumike kwa wabishi tu na wasenge(Askari)lakini hao watu wa kawaida unaweza ukatumia kuwatishia tu wakatoa mzigo"

Bosi "Utawapa maelekezo hawa marafiki zangu pia namna ya kutumia risasi,si kila mahali!"

Baada ya yale mazungumzo yule bosi alizimwaga zile hela chini,hakika zilikuwa hela nyingi sana kama nilivyosema zilikuwa zaidi ya milioni 50.Sasa baada ya kuzihesabu zile hela alimwambia Gabi alete begi waweke zile hela,Gabi aliingia chumbani akaleta begi ambalo waliziweka zile hela.

Bosi "Kamateni hizo mtagawana wewe na mwenzio"

Aliendelea "Niliwaambia siri kwetu ni kitu muhimu kuliko hii pesa,bila shaka mnakumbuka!".

Mtatiro "Tunakumbuka bosi"

Bosi "Sawa,nawaamini sana"

Basi Mtatiro akachukua zile hela akaanza kuzihesabu na kupata jumla yake milioni 1.9 aambazo ilipaswa tuzigawane mimi na yeye.Nilimwambia Mtatiro azitie mfukoni na tungezigawana baadae.Baada ya kuchukua zile hela,Gabi alituambia wao walikuwa wanatoka kuna mahali wanaelekea na alitutaka tuondoke kurudi maskani ili tukapumzike na wakirudi angetushitua kwenye simu.

Mtatiro alimwambia simu zetu tuliziacha Arusha na hivyo hatukuwa na mawasiliano kwa wakati huo.Gabi alimuuliza yule bosi kuhusu mawasiliano na bosi wake akasema tununue simu mpya kisha tumwambie gharama tutakayoitumia kununulia hizo simu ili aturejeshee,sasa nakumbuka Gabi alimwandikia Mtatiro namba yake akasema tukishanunua simu Mtatiro ampigie.

Walipoondoka na ile Noah na sisi tuliamua kuondoka zetu kurejea kule Usagara kwenye nyumba ya braza ake na Mtatiro walipokuwa wakikaa.

Mtatiro "Hivi jamaa si alituambia tukipata pesa tutakuwa tunagawana pasu kwa pasu!"

Aliendelea "Sasa mbona wametupa milioni 1.9?"

Mimi "Mwanangu siungemuuliza Gabi?"

Mtatiro "Mimi nilidhani labda wamekosea hivyo nilitaka kuona labda wangetuongeza nyingine"

Mimi "Hata hivyo hii ni siku ya kwanza Mtatiro pia siunakumbuka alisema hela niya kwake"

Mtatiro "wewe ngoja tukanunue simu,nitamuuliza Gabi"


Baada ya muda ndipo nilikuja kugundua kumbe yule jamaa ambaye tulienda kwake kufanya tukio alikuwa mfanyabiashara wa madini hapo Kahama.Kiukweli niliumia sana moyo kwa kile kitendo tulichokuwa tumekifanya lakini tayari nilikuwa mikononi mwa watu wabaya wasiokuwa na huruma!.

Baada ya kuwa tumenunua zile simu,Mtatiro alimpigia Gabi simu na akamwambia wao wako Arusha wangerejea baada ya siku 3,hivyo alimwambia jamaa akifika tutaonana tuzungumze mambo mengi!.Kweli!,Baada ya wiki kupita tangia tufanye lile tukio,Gabi alimtafuta Mtatiro akawa amesema tunapaswa kuonana nae!.Tuliondoka tukaelekea mjini pale tulipokutana siku ya kwanza Golden Crest.

Gabi "Wanangu si mko lakini!"

Mtatiro "Tuko poa kaka"

Gabi "Tulienda Arusha mara moja,nimerudi mimi na Jipe ila mkuu kabaki atakuja wiki ijayo"

Mtatiro "Vipi nyie mlipewa chenu?"

Gabi " Yeah kila mtu alipewa chake!"

Mtatiro "Lakini bosi alisema tutakuwa tunatoka pasu kaka"

Gabi "Mwanangu pesa bado zipo nyingi mno,hiyo ni rasha rasha tu!"

Aliendelea "Unajua yule Magige waliwahi kufanya na mkuu biashara,sasa nadhani kuna udhurumaji ulifanyika ndiyo maana mkuu alitaka tuzifate pesa zake"

Gabi "Pesa bado zipo nyingi kaka wala hata usiwaze kwa hilo!"

Basi baada ya yale mazungumzo ya Gabi ni kama alituliza presha ya Mtatiro.Tulimaliza pale yale mazungumzo kisha tukaanza kupata beer ambapo tuliondoka mida ya saa 3 usiku.
Nakumbuka tulikaa mtaani wiki 2 bila kazi,na wiki ya tatu ilipoanza,Gabi alitutafuta kwenye simu akatuambia tuelekee kule mjengoni ili kuona tunajipangaje namna ya kutoka kuelekea kwenye uvamizi tena!.

Tulipofika pale kama kawaida tulimkuta Gabi,Jipe pamoja na jamaa mmoja ambaye ndiye alikuwaga akibaki pale kwenye ile nyumba,sasa baada ya muda alikuja yule demu aliyekuwa akiendesha ile Noah.

Jipe "Mko poa wanangu"

Mtatiro "Si tuko poa kaka,umetutenga sana"

Jipe 'Safari hii tutatoka wote jamaa zangu"

Aliendelea "Nyie ndio wanangu siwezi kuwatupa"

Mtatiro "Sawa,tupe mchongo"

Jipe " Tutaondoka leo usiku kuelekea Geita tutaenda kupitia Kahama ndiko hakuna hakuna wakuda,tukifika kuna nyumba tutafikia kisha tutapumzika hapo halafu kesho tutaifanya kazi itakayotupeleka hapo"

Aliendelea "Simu zote tutaziacha hapa na pia kama kuna mtu anavyo vitambulisho itabidi aviache hapa,kule tutaenda kama tulivyoenda Kahama,hatupaswi kuwa na chochote zaidi ya masihine!"

Jipe "Gabi wewe nadhani una maelekezo kutoka kwa bosi hivyo unajua cha kufanya"

Aliendelea "Wewe Kamange unaijua kazi yako,nimemaliza!"

Basi baada ya yale maelekezo kila mmoja alisubiri ifike usiku ili tuianze safari!.
Mkurya kama mkurya.

#MaendeleoHayanaChama
 
Moja ya kitu watu wengi hasa wenye viburi vya kitaluuma za kukariri wajifunze kwa Dogo Umughaka hana degree kama wao ila alisoma fasihi andishi akaelewa Na akiamua kutumia kalamu kuwa tajiri anaweza, ukiacha usimuliaji ni mwandishi mzuri sana .
Mkuu,unamfahamu huyu UMUGHAKA ? Ni kweli ni "Dogo" kwako? Ni kweli hana "Degree"?
 
Back
Top Bottom