Nilivyonusurika kifo juu ya mti

Nilivyonusurika kifo juu ya mti

Mbute na chai

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2012
Posts
564
Reaction score
593
Tukio lililonitokea nikiwa darasa la tatu.

Ikiwa muda wa masomo umemalizika, nikiwa na wanafunzi wenzangu, tunapita jirani na mti wa mzambarao. Mti ule ulikuwa umesheheni zambarao zilizoiva na nono zaidi, wale waliyopitia maisha haya nadhani wananielewa vizuri. Mti huo ulikuwa mrefu mithili ya futi 60 hivi za urefu basi, kwakuwa nilikuwa mtundu nikasema ngoja nikwee nikajiangulie yaliyo mazuri zaidi. Nilimkabidhi rafiki yangu mfuko wangu wa madaftari uliyojulikana kama sport enzi hizo, nikamwambia nikidondosha zambarao unanihifadhia. Nilipofika mtini nikasema ngoja nile kwanza halafu nitashusha zingine. Baada ya kutosheka kula nikaanza kuangua na kumdondoshea rafiki yangu ahifadhi.

Nilipokuwa nadondosha zile zambarao nilisikia huko chini wakibishana na yule rafiki yangu akiwaambia ‘mimi ndiye ninayemkusanyia.’ Juu ya mti zambarao zile nono huwa zinatabia ya kuwa kwenye matawi membamba ya pembezoni nikajisemea isiwe tabu, basi nikashika tawi nene mkono wa kushoto huku mkono mwingine nikijinyoosha kufikia hizo zambarao na kumbe lile tawi nene lilikuwa na wadudu ambao tulikuwa tunawaita nyugi (wasp) jamii kama ya nyuki. Kumbe nilivyokuwa najinyoosha ndivyo nilivyokuwa natingisha kile kijumba chao na nilipokaribia kukamata kitawi chenye zile zambarao nikasikia kama mtu kanidunga sindano ya sikio, kwa wenge nikaachia lile tawi nene, mama yangu!!!! Nilisikia pwaaaaaach, parapataaaaa, kurukunguuu…… nikiwa katika hali ya taharuki nasikia huko chini zinakuja nyingi naomba na sisi tukuokotee bila kujua kuwa nilikuwa mimi mwenyewe ndiye naporomoka kama jackie chan kwenye movie ya who am I. Mungu saidia nikanasa kwenye matawi ya katikati huku jasho uchafu ule unaotoka kwa kujificha vyote vimenienea. Ile kama napata hafueni lile tawi lililonikwamisha pale likavunjika bahati nzuri nikawa nimekanyaga mti wenyewe. USIOMBE YAKUKUTE.
 
Tukio lililonitokea nikiwa darasa la tatu.

Ikiwa muda wa masomo umemalizika, nikiwa na wanafunzi wenzangu, tunapita jirani na mti wa mzambarao. Mti ule ulikuwa umesheheni zambarao zilizoiva na nono zaidi, wale waliyopitia maisha haya nadhani wananielewa vizuri. Mti huo ulikuwa mrefu mithili ya futi 60 hivi za urefu basi, kwakuwa nilikuwa mtundu nikasema ngoja nikwee nikajiangulie yaliyo mazuri zaidi. Nilimkabidhi rafiki yangu mfuko wangu wa madaftari uliyojulikana kama sport enzi hizo, nikamwambia nikidondosha zambarao unanihifadhia. Nilipofika mtini nikasema ngoja nile kwanza halafu nitashusha zingine. Baada ya kutosheka kula nikaanza kuangua na kumdondoshea rafiki yangu ahifadhi.

Nilipokuwa nadondosha zile zambarao nilisikia huko chini wakibishana na yule rafiki yangu akiwaambia ‘mimi ndiye ninayemkusanyia.’ Juu ya mti zambarao zile nono huwa zinatabia ya kuwa kwenye matawi membamba ya pembezoni nikajisemea isiwe tabu, basi nikashika tawi nene mkono wa kushoto huku mkono mwingine nikijinyoosha kufikia hizo zambarao na kumbe lile tawi nene lilikuwa na wadudu ambao tulikuwa tunawaita nyugi (wasp) jamii kama ya nyuki. Kumbe nilivyokuwa najinyoosha ndivyo nilivyokuwa natingisha kile kijumba chao na nilipokaribia kukamata kitawi chenye zile zambarao nikasikia kama mtu kanidunga sindano ya sikio, kwa wenge nikaachia lile tawi nene, mama yangu!!!! Nilisikia pwaaaaaach, parapataaaaa, kurukunguuu…… nikiwa katika hali ya taharuki nasikia huko chini zinakuja nyingi naomba na sisi tukuokotee bila kujua kuwa nilikuwa mimi mwenyewe ndiye naporomoka kama jackie chan kwenye movie ya who am I. Mungu saidia nikanasa kwenye matawi ya katikati huku jasho uchafu ule unaotoka kwa kujificha vyote vimenienea. Ile kama napata hafueni lile tawi lililonikwamisha pale likavunjika bahati nzuri nikawa nimekanyaga mti wenyewe. USIOMBE YAKUKUTE.
Hiyo miti ya zambarau sio imara
Wengi wameanguka na kuumia walipopanda
 
Wasp kama sikosei ni dondola tulikuwa tukiwaita hivyo, dah mizambarau mikwaju mipera kwa kule dom kuna susuna na mifuru hii miti nimeikwea sana ila nashkuru nilipita salama ngwe hiyo.
 
Tukio lililonitokea nikiwa darasa la tatu.

Ikiwa muda wa masomo umemalizika, nikiwa na wanafunzi wenzangu, tunapita jirani na mti wa mzambarao. Mti ule ulikuwa umesheheni zambarao zilizoiva na nono zaidi, wale waliyopitia maisha haya nadhani wananielewa vizuri. Mti huo ulikuwa mrefu mithili ya futi 60 hivi za urefu basi, kwakuwa nilikuwa mtundu nikasema ngoja nikwee nikajiangulie yaliyo mazuri zaidi. Nilimkabidhi rafiki yangu mfuko wangu wa madaftari uliyojulikana kama sport enzi hizo, nikamwambia nikidondosha zambarao unanihifadhia. Nilipofika mtini nikasema ngoja nile kwanza halafu nitashusha zingine. Baada ya kutosheka kula nikaanza kuangua na kumdondoshea rafiki yangu ahifadhi.

Nilipokuwa nadondosha zile zambarao nilisikia huko chini wakibishana na yule rafiki yangu akiwaambia ‘mimi ndiye ninayemkusanyia.’ Juu ya mti zambarao zile nono huwa zinatabia ya kuwa kwenye matawi membamba ya pembezoni nikajisemea isiwe tabu, basi nikashika tawi nene mkono wa kushoto huku mkono mwingine nikijinyoosha kufikia hizo zambarao na kumbe lile tawi nene lilikuwa na wadudu ambao tulikuwa tunawaita nyugi (wasp) jamii kama ya nyuki. Kumbe nilivyokuwa najinyoosha ndivyo nilivyokuwa natingisha kile kijumba chao na nilipokaribia kukamata kitawi chenye zile zambarao nikasikia kama mtu kanidunga sindano ya sikio, kwa wenge nikaachia lile tawi nene, mama yangu!!!! Nilisikia pwaaaaaach, parapataaaaa, kurukunguuu…… nikiwa katika hali ya taharuki nasikia huko chini zinakuja nyingi naomba na sisi tukuokotee bila kujua kuwa nilikuwa mimi mwenyewe ndiye naporomoka kama jackie chan kwenye movie ya who am I. Mungu saidia nikanasa kwenye matawi ya katikati huku jasho uchafu ule unaotoka kwa kujificha vyote vimenienea. Ile kama napata hafueni lile tawi lililonikwamisha pale likavunjika bahati nzuri nikawa nimekanyaga mti wenyewe. USIOMBE YAKUKUTE.
Mie niliwahi ng'atwa madondola nikiwa juu ya mwembe nilijikuta niko chini sema huo mwembe haukua mrefu sana,hii ya zambarau ilimuua kijana wa jirani yetu alianguka toka kwenye mzambarau akafa,pumzika kwa amani Deus
 
Nimecheka kama mazuri vile, pole sana mkuu unanikumbusha enzi zetu na age mates 2 watundu hao, ila mimi wala hata kupanda kwenye miti nilikua sijui so nakua muokotaji wenzangu wakipanda kuchuma.

Kuna siku huyo mwenzangu kapanda kuchuma mapera(guavas) juu kabisa mimi nikiwa chini nasubiri adondoshe niokote , kachuma wee sijui ilikuaje anasema alishika tawi vibaya akateleza, dah niliskia kishindo cha ajabu mtu yupo chini, sijui kuchanganyikiwa kule nilikimbia home nikamuacha analia hapo,naye akaja home kateguka mkono analia. Dah now tumekua wakubwa nikimkumbusha anacheka na ananiona nna tabia mbaya kumkimbia😀😀

Juzi hapa mdogo wangu wa kiume kang'atwa na nyigu sikioni akiwa shamba dah alilia kama mdada nilicheka vibaya😂 na ile kakimbilia home kumbe kuna nyigu alibaki kwenye shati hee si akamng'ata tena shingoni dah😂
 
Mizambarau inatabia ya kuteleza na miti yake rahisi sana kukatika, hasa kipindi cha mvua

Udogoni nilikua na dance sana juu ya matawi, hadi mwenzetu alipokata moto kwa kuanguka juu ya mzambarau pale kijijini mang'ula (mwaya )
 
Mie niliwahi ng'atwa madondola nikiwa juu ya mwembe nilijikuta niko chini sema huo mwembe haukua mrefu sana,hii ya zambarau ilimuua kijana wa jirani yetu alianguka toka kwenye mzambarau akafa,pumzika kwa amani Deus
Duh mti ulikua mrefu sana eeh, maskini hadi kufa ni maumivu gani hayo aliyapitia😪
 
Mizambarau inatabia ya kuteleza na miti yake rahisi sana kukatika, hasa kipindi cha mvua

Udogoni nilikua na dance sana juu ya matawi, hadi mwenzetu alipokata moto kwa kuanguka juu ya mzambarau pale kijijini mang'ula (mwaya )
Hii miti ni mirefu sana? Na inaonesha ni rahisi kukatika ama kuteleza, hadi mtu afe aisee
 
Kuna miti ya mizambarau nimekata miezi iliyopita ,maana kesi za watoto wakitoka shule haziishi,nimeona heri nizitengenezee mbao zitakuja kumwua mtoto siku moja maana washavunjika sana
 
Hii miti ni mirefu sana? Na inaonesha ni rahisi kukatika ama kuteleza, hadi mtu afe aisee
Mazambarau mazuri yanakaa juu sana na mwishoni mwishoni
Ukichukulia na umri wa mtoto (8-14), kufa ni swala dogo sana ukianguka kutoka kwenye mti

Niliwai kukutana na NYIGU juu ya mti, wakaanza kunigonga
Akili ilicheza fasta, nikasema hapa nikiachia mti tu, basi nimekufa
Ilibidi nishuke kwenye mti kwa speed ya light, kukaribia na chini nikajiachia jumla
Nikatoka Mbio umbali flani ndio nikaanza kujikagua, michubuko na manundu ya dondola[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]


When I was kid, nilikua mtundu sana[emoji119][emoji119][emoji119]
 
Mazambarau mazuri yanakaa juu sana na mwishoni mwishoni
Ukichukulia na umri wa mtoto (8-14), kufa ni swala dogo sana ukianguka kutoka kwenye mti

Niliwai kukutana na NYIGU juu ya mti, wakaanza kunigonga
Akili ilicheza fasta, nikasema hapa nikiachia mti tu, basi nimekufa
Ilibidi nishuke kwenye mti kwa speed ya light, kukaribia na chini nikajiachia jumla
Nikatoka Mbio umbali flani ndio nikaanza kujikagua, michubuko na manundu ya dondola[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]


When I was kid, nilikua mtundu sana[emoji119][emoji119][emoji119]
Aisee pole, hadi unajiachia kwani hao dondola walikua bado wanakufata? Au ni maumivu yake tu hadi watu wanaachia mti na kuanguka? Kama nakuonà ulivobakiwa na manundu ya dondola😂😂
 
Back
Top Bottom