Niliwahi kutoa wazo kama hili kwenye mkutano wa kijiji, watu wakaishi kucheka. Sasa natoa mfano!

Gaddaf i06

JF-Expert Member
Joined
Nov 14, 2022
Posts
1,770
Reaction score
2,841
Habari za wakati huu expert mwenzangu[emoji4]
siku moja nitauliza ni kwanini tunaitwa "experts"
isije kuwa ni maexperts wa kuandika nyuzi[emoji23][emoji119]


..mnaokaa karibu na bahari, maziwa na mito, jamani mungu awape macho, hiyo ni fursa.

ninaishi sehemu ambayo upatikanaji wa maji ni shida sana, kwahyo nawaza na kuwazua jinsi gani ya kukabiliana na changamoto hii.

wazo:
kwa sababu nipo nje ya mji,eneo kubwa nk, nataka ninunue cement ya kutosha, nijenge tank ambalo litahifadhi maji angalau lita mil. 1 (one million litres of water) na nitahakikisha linajaa kabla msmu wa mvua haujaisha..
lengo nipate maji ya kutosha kumwagilia bustani zangu.
maana
ninapata matokeo hasi kwa kutegemea mvua zisizoeleweka.
niko serious kabisa. Nataka niwaonyeshee mfano walionicheka, naamini hii wataipenda tu[emoji4]


rafiki yangu hapo, unasemaje/ unauonaje mpango huu?[emoji4]
unaweza kuniongezea wazo au maarifa zaidi?

karibu sana
 
Mvua za kujaza tenki la lita millioni moja utazipata wapi kwa hi Tanzania labda uwe sehemu za ya mkoa wa kagera
 
Ongeza ifike lita 1.5ml
 
Kwa mvua znazonyesha lazima lijae tu nitaangalia namna ya kuyadaka!
 
Tank/shimo la lita 1,000,000 ni kubwa sana. Ni sawa na tank za lita 1,000 ziwe 1,000 au tank za lita 10,000 ziwe 100.

Gharama ya kujenga hilo tank/shimo ni kubwa sana, unahitaji materials nzuri kuliimarisha na ufundi madhubuti wenye usimamizi wa kitaalam kabisa. Otherwise utakuwa unalifanyia ukarabati kila msimu.

NB: Nina shimo la lita kama 50,000, linajaa kwa maji ya bati tu, tena mvua zikinyesha kubwa mara tano linafurika. Likijaa situmii maji ya dawasa, nililijenga kipindi hakukuwa na maji, ila linanisaidia hadi leo maji ya dawasa yakiwepo.
 
mkuu ERoni, una akili sana aisee umenipa hamasa zaidi!

nina hekala 4 ambazo nataka zipate maji kila siku msimu hadi msimu.
unaonaje nipunguze litres?
 
Kila la kheri, achana na wapumbavu waliokucheka. Matanki hayo yapo kabla hata ya Yesu kuzaliwa. Kiingereza wanayaita Cisterns
 
Watu wanasemaga hesabu nitatumia wapi? Hapa sasa hesabu za kutafuta ujazo wa mcheduara ndiyo zinahusika.
 
Hii weather ilivyo itajaza kweli kwa ujazo unaotarajia ,mvua zimekua sio nyingi
 
Mkuu naona kama utatumia gharama kubwa sana aisee, Cha msingi chimba kisima tu , pia tafuta solar pannel za kutosha na betttery uwezo mkubwa , utazalisha umeme mwingi tu ambao utakusaidia kuvuta maji ya kisima na utapata maji mengi tu kwa ajili ya matumizi yako ya Kila siku
 
Mimi nasema wewe genius ila mzee Makamba yeye sijui atasemaješŸ˜‚
 
Hii weather ilivyo itajaza kweli kwa ujazo unaotarajia ,mvua zimekua sio nyingi
mabwawa ya karibu yanajaa maji lakin yanakauka mapema kwahyo mvua zkiwa hazieleweki, uwezekano wa kuyavuta hayo unakuwepo
 
wazo zuri sana hili! niliwahi kuwatafuta hao jamaa wanaodrill visima wakaniambia malipo milioni kumi

asante sana mkuu sayoo nitalinganisha gharama na faida
 
Sehemu zinine maji ya kisima yana chumvi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…