Chizi Maarifa
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 10,931
- 24,816
Una IDs nyingi.Aweke ata yote mimi fresh tu na akimaliza akaanza nyingine mpya sawa pia 😂
Uandishi wake unavutia
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Una IDs nyingi.Aweke ata yote mimi fresh tu na akimaliza akaanza nyingine mpya sawa pia 😂
Uandishi wake unavutia
Sijaisoma mkuukwani ilikupita ile riwaya ya "jirani yangu wa goba hakuwa mtu wa kawaida"?
[emoji23]‘Nehi nehi’[mention]SteveMollel [/mention]
YcSehemu ya Saba:
Sisi binadamu mwisho wetu ni nini kama sio kifo? Tutaruka turukavyo, twende tuendapo lakini mwisho wa siku makutano yetu ni pahali pamoja, napo si kwingine bali kaburini. Hili halijalishi hadhi wala cheo. Alimradi umezaliwa basi tayari muda wako wa kwenda umeshatiwa muhuri, kinachongojewa ni utelekezaji tu. Bwana ametoa na bwana ametwaa.
Maneno hayo yalinipatia faraja moyoni mwangu, nilikuwa nikiyatamka mwenyewe moyoni, kwenye kiti cha daladala, nilipokuwa nikielekea hospitali kule nilipopewa taarifa mbaya.
Niliyawaza mengi hapo njiani, mojawapo ni endapo nikipewa wasaa wa kusema neno ni nini nitaeleza, hapo ndo' nikaanza kujisema na kujitengenezea mwenyewe kauli na kauli, sijui akili yangu ilikuwa inawaza nini muda huo, saa hii ndo' naona ulikuwa ni ujinga tu, pengine ugeni wa misiba ulikuwa unanizuzua.
Mambo ya kutoa risala na mimi wapi na wapi?
Kwa mara ya kwanza, nilimwona Mgaya akiwa na macho mekundu ya uchungu, uchungu wa kumpoteza mama yake, japo sababu ni mwanaume alijikaza sana kumwaga chozi, kuna muda nilikuwa namwona aking'ata meno yake kwanguvu, sijui ni nini ila kitu kile, katika namna ya ajabu kabisa, kilinifanya moyo wangu kuwa wa bariidi kwa raha.
Kweli maisha ni mbio za vijiti, kukimbia na kupokezana zamu, jana yake ilikuwa ni mimi nikisaga meno kitandani, nararuka na moyo wangu mwenyewe, leo hii asubuhi zamu ya wengine, kijiti hakipo mikononi mwangu tena.
Bwana Mgaya, kwa uso ulolemewa na majonzi, alinambia yale yalotukia huku nyumbani baada ya mimi kuondoka kwenda shule.
Bwana huyo alimngoja mama yake atoke chumbani kwaajili ya kupata kifungua kinywa lakini mama hakutoka, hio haikuwa kawaida yake kukawia kiasi hiko chumbani kwani tangu amjue mama yake, hata akiwa aumwapo, ni mtu wa kuamka mapema kwenda kuota jua la asubuhi labda tu akiwa hajiwezi, na hilo ndo' lilimtisha.
Akiwa nje pamoja na Amiri, wanatazama ustawi wa mifugo, alitazama mara kwa mara pale nje kama atamwona mama yake lakini dakika zilikata asimwone katika upeo wa macho yake, hapo sasa akakata shauri kwenda kutazama.
Aliita mbele ya mlango ule ulokuwa wazi, mlango wa chumba alalacho mama yake, mara tatu kwa sauti kubwa lakini hakujibiwa, aliporusha macho yake ndani aliona mwili wa mama yake umetuama juu ya kitanda kana kwamba kisiwa katika bahari, mwili hauchezi wala kujigusa.
Upesi akamwita Amiri wakasaidiana kuubeba mwili huo mpaka kwenye gari na kutimka haraka hospitali, njia nzima mama hakusema kitu wala hakuomba hata maji, kufika hospitali haikupita hata dakika kumi, daktari akawaambia hamna mtu pale bali uwakilishi wake wa mwili tu.
Baada ya maelezo hayo, nilimkumbatia Mgaya kumpatia pole, nikasema maneno yangu ya faraja kwenye masikio yake, maneno ambayo angependa kuyasikia toka kwa mkewe, lakini maneno yale yalijawa na unafiki mtupu, hakuna hata moja nililomaanisha, walosema moyo wa mtu kichaka hawakukosea kabisa, hapa moyo wangu mimi ulikuwa pori kabisa.
Tena pori lenye giza totoro.
Watu wetu wa karibu, wale ambao wapo katika mkoa wa Dar na maeneo ya jirani, walifika nyumbani kutupatia pole kwa msiba ule. Walimu wenzangu walifika kunishika mkono wakiwa wanaongozana na meneja bwana Salum.
Miongoni mwa walimu hao alikuwamo Beatha. Mwanamke huyo ndiye alinikabidhi rambirambi ya walimu wenzangu kwa pamoja, alinipatia kama mwakilishi wa darasa lile ambalo mimi na yeye tunafundisha.
Lakini mbali na hapo, meneja Salum alinipatia pesa binafsi kutoka mfukoni mwake, kiasi cha kama laki mbili hivi ndani ya bahasha, akinambia itanisaidia kwenye safari ya kwenda na kurudi kwenye mazishi.
Pesa hiyo alinipatia kando, mbali kidogo na waombolezaji wengine, nami kwasababu hiyo niliitia pesa hiyo mahali pangu pa siri, sikutaka mtu mwingine ajue. Baada ya siku moja, tulisafirisha mwili kwenda Iringa, huko tukamzika mama yule mimi nikiweka shada kubwa juu ya kaburi lake, shada lililoandikwa kwa herufi kubwa - MAMA
Niliweka shada hilo machozi yakinishuka, sikufahamu kama nina uwezo mkubwa wa kuigiza kiasi kile, tabu ile ilinifanya nikatambua nina kipaji ndani yangu.
Baada ya mazishi, pale nyumbani kulifanyika kikao kidogo cha familia, bwana Mgaya pamoja na ndugu zake kujadiliana kuhusu mambo kadha wa kadha ukizingatia mama yule ndo' alikuwa mzazi pekee alobakia, baba yao alikwishafariki kitambo hata kabla sijaolewa na bwana Mgaya.
Katika kikao hicho kilichokuwa kinasimamiwa na kuongozwa na kaka mkubwa wa familia yao, bwana Mgaya alitambulika kama mume mwenye wake wawili, mimi na yule Momo alokuwepo pale.
Na katika mengi waliyojadiliana na kuafikiana katika kikao hicho, mojawapo lilikuwa ni la bwana Mgaya kuondoka na mkewe pale nyumbani kwani mama aliyekuwa anamuuguza hayupo tena.
Nilipokuja kuelezwa swala hilo na bwana Mgaya, sikuliafiki katukatu, sikuwa radhi nalo na nilimwambia bwana Mgaya mwanamke huyo ataingia ndani ya nyumba yangu mimi nikiwa mfu lakini si kwa uhai wangu huu.
Swala hilo likapelekea tafarani sana, sasa bwana Mgaya hakutaka kuonekana dhaifu mbele ya ndugu zake, kitendo cha maamuzi kufikiwa na kikao cha familia kisha yeye kushindwa kutimiza alikiona ni kama fedheha, tena fedheha zaidi kwa maana mwanamke ndo' amemshinikiza, ataambia nini ndugu zake? Mwanamke amempanda kichwani?
Tulipishana sana maneno hata kufikia mimi na mwanangu kuondoka wenyewe kurudi nyumbani, niliondoka hata pasipo kuaga. Nilipofika nikapokelewa na Amiri akinitua begi langu na kunipa pole ya msiba.
Baada ya siku mbili tangu nirejee ndo' bwana Mgaya akajileta nyumbani kama kifaranga kilichomwagiwa maji, mikono nyuma kama bwana mshauri, uso umeparwa na haya hawezi hata kunitazama usoni.
Nami, kama hakuna kilichotokea, sikuhangaika naye. Niliendelea na shughuli zangu tukisalimiana kama wapita njia mitaa ya mjini. Mwishowe, bwana huyo aliniangukia akiniomba msamaha kwa yalotokea. Alinitaka nitulie naye tujenge familia na nyumba yetu kama tulivyokuwa tunafanya hapo awali.
Kuhusu Momo, Mgaya alinieleza mwanamke yule amemrejesha nyumbani kwao, hayuko naye tena, na anachoshukuru mwanamke huyo amerejea kwao akiwa hana mtoto wala ujauzito wake.
Bila hiyana nikayaamini maelezo yake, sikuwa na budi nyingine, maisha yakarejea katika hali yake ya kawaida, hali ya amani, amani ambayo ililetwa kwa udhamini wa kifo cha yule mama mkwe. Kifo chake kilikuwa ni kama sadaka ya kutuliza tafarani ya familia muda ule.
Niliwasiliana na rafiki yangu Zai, sikuwa nimeonana naye muda kidogo kwani hata kwenye msiba hakufika sababu alikuwa anaumwa, hakuwa yuko sawa, alipewa 'bed-rest' hospitali fulani baada ya kuonekana anasumbuliwa na presha, hivyo nilivyorejea nilimpa taarifa kuwa nimerudi na tukakubaliana niende kumwona majira ya jioni kesho yake baada ya kutoka shuleni.
Kesho yake niliporejea shuleni baada ya siku zile chache za maombolezo, nilikuta shule nzima ina habari kuhusu pesa ile nilopewa kwa siri na meneja Salum.
Kumbe siku ile, mimi na meneja, hatukuwa peke yetu kama tulivyodhania, kuna macho ya wenye husda yalituona na kisha midomo ya wambea ikaenda kutenda kazi ya kusambaza taarifa, na hapa sikumdhania mtu mwingine isipokuwa Beatha. Hamna mtu mwingine bali yeye.
Hata nilipofika, alinikarimu kinafki akisema, "naona mke wa boss umewasili." Nami sikuhangaika naye nikaendelea na shughuli zangu, nilishakubali ana utindio wa ubongo hivyo kuhangaika naye niliona ni kujidhalilisha tu, kumbe pia kukaa kwangu kimya kukawa kunamuumiza, ama kweli hasidi hakosi sababu.
Kabla ya siku hiyo kuisha, nilionana na meneja Salum kwaajili ya kumshukuru.
Tuliongea naye mambo kadhaa, kama dakika kumi tu, kabla ya kumuaga na kwenda zangu kufungasha ili nielekee hospitali kuonana na Zai.
Nikiwa nafungasha, mara nikapata wito wa kufika ofisi ya mkuu wa shule mara moja. Ujumbe huo ulifikishwa kwangu na mwanafunzi mmoja wa madarasa ya juu, nami pasipo hiyana nikauitikia wito huo upesi ili nisikawie na ratiba yangu.
Ajabu nilipofika huko, nikakutana na malalamiko kwenye meza ya mkuu wa shule, Madam Bibiana, ya kwamba mimi nimekuwa nikipuuzia mamlaka yake pale shuleni.
Madam yule alinikumbusha ya kwamba kuna utaratibu wa kimamlaka kwenye taasisi yoyote ile na ni makosa kwa mwalimu kwenda kuonana na meneja moja kwa moja kana kwamba mhudumu wa mgahawani, kama kuna lolote linalonisibu basi natakiwa nianzie kwake kwanza kabla ya kugonga mlango wa meneja.
Hapo nikakumbuka yale matamko ya meneja kuhusu mimi kupunguziwa majukumu, lakini pia mawasiliano yangu naye kuhusu urefu wa likizo yangu ya uzazi, kumbe yote yale yalikuwa ni makwazo?
Nilimkubaliana mwanamke huyo kwa kila alichoongea maana nilikuwa na haraka zangu, hata mengine aloyaongea sikuyasikia vema, akili yangu haikuwepo hapo, nilipotoka tu humo ofisini nilinyookea moja kwa moja hospitali kumwona mgonjwa kabla muda haujanitupa mkono.
Bahati nilifika ndani ya muda. Nilimkuta Zai akiwa anaendelea vema kabisa hata akaniambia muda si mrefu ataondoka hapo hospitalini punde tu akikamilisha kulipia bili yake, kuna pesa fulani anaingoja atumiwe.
Tuliongea pale, mambo ya hapa na pale, tukielezana kwa uchache yale yalotukia wakati hatujaonana, kuanzia ya msiba mpaka yale ya kule Iringa, alipoyasikia hayo akacheka sana kwa songombingo zangu ila mwishowe akanipa pole akisema hayo ndo' maisha na changamoto zake.
Lakini kabla sijamuaga niende zangu, aliniuliza swali, swali ambalo lilifanya nikameza mate kwa ukavu wa koo langu.
Alisema;
"mara ya mwisho umeongea na Anwari lini?"
Nikasita kujibu, akatambua nimekwama, akanitazama kwa macho ya 'mwana mpotevu' kisha akasema kwa stara: "niambie ukweli, Magreth. Mimi ni rafiki yako."
Kwenye kufikiri kwangu, nikaona ni vema kukanusha taarifa ile. Mimi nilikuwa naamini hata rafiki yangu wa undani kabisa ni lazima awe na mipaka yake, si kila kitu ni cha kumshirikisha mtu, binadamu ndimi mbili, huwezi jua ni lini mambo hayo unayomjaza yatakuja kugeuka kuwa silaha ya kukuangamiza wewe mwenyewe. Nguruwe hukaangwa na mafuta ya mwilini mwake.
Hivyo,
Nikakataa, nikasema sikumbuki mara ya mwisho lini kuwasiliana na bwana huyo. Hapo Zai akatoa simu yake na kunionyesha ujumbe, ujumbe toka kwa Anwari, ujumbe mrefu uliokwangua sakafu ya moyo wangu na kuniachia majeraha.
Kwenye ujumbe huo Anwari alimlalamikia Zai ya kwamba ananitafuta sana hanipati hewani. Amefanya kila jitihada za kuniona lakini Zai hataki hata kumwambia sehemu yangu mpya ya kazi achilia mbali makazi yangu, sasa amechoka, kama sitaki kuonana naye basi angalau nimpe haki ya kumwona mwanae.
Hapo kwenye mwanae ndo' palitibua mzunguko wangu wa damu, nikahisi kizunguzungu na tumbo kunivuruga. Niliona kitanda cha hospitali kinaenda kaskazini kisha kinarudi kusini kwa haraka, ikanibidi nishike kingo zake kwanguvu kisije kikanivamia na kunilaza chini.
Na huo ndo' ukawa mwanzo mpevu wa safari ya kifo cha Anwari.
***
YcSehemu ya Tisa:
Anwari aliniambia anafahamu ya kwamba nina mtoto, mtoto wa kiume, na mtoto huyo umri wake unawiana sawa na muda tulokutana mimi na yeye.
Hapo nikamgomea, si kwamba hatukukutana, lah, bali nilimwambia muda huo nilishiriki tendo pia na mume wangu, hivyo yeye ana uhakika gani kama kweli mtoto yule ni wake?
Nilimuuliza nikiwa nayajenga yangu kichwani, bwana yule hajui ninapoishi wala wapi ninapofanya kazi, alitambuaje kama nina mtoto? Alitambuaje kama nilipata mimba?
Akili yangu ikanambia ni Zai. Hamna mtu mwingine isipokuwa yeye. Zai alimwambia Anwari kuwa mimi nina mimba na akamwambia nimepata mtoto.
Zai alimwambia kila kitu isipokuwa mahali ninapoishi na mahali ninapofanya kazi. Bila shaka angefanya hivyo, tayari Anwari angelifika getini kunigongea.
Lakini kwanini Zai aliyasema yale? ... Sikukaa nikajua.
Tuliendelea kuzozana na Anwari tusipate muafaka, na kwasababu muda ulinitupa mkono, nikamwambia nataka kwenda zangu nyumbani, siku nyingine tukionana panapo majaliwa basi tutaongea.
Bwana huyo akakataa.
Alinambia haniamini maana sikawii kum-block akahangaika tena kama hapo awali, kuhangaika mpaka kumhusisha Zai.
Na mimi kwasababu sikutaka aendelee kuwasiliana na Zai kuhusiana na lile jambo letu, nikaona ni vema nimpatie Anwari uhakika wa kunipata muda wowote atakaonitafuta.
Yale alokuwa anayajua Zai yanatosha, sikutaka azidishe tena hata punje.
Basi nikamwambia namba yangu nilompigia ndo' hiyohiyo itakayokuwa hewani milele. Akinihitaji anitafute aidha kwa kupiga ama kutume ujumbe, lakini nilimpa onyo asinitafute majira ya usiku, mimi ni mke wa mtu na sikuwa radhi kuivunja familia yangu kwa muda huo.
Baada ya hapo nikaondoka kurejea shuleni, nikamchukua mwanangu na kwenda naye moja kwa moja nyumbani.
Sikufahamu, kumbe Anwari alikuwa ananifuatilia nyendo zangu mpaka mwisho.
Kwasababu ya kujificha nisimwone na kumtambua, Anwari aliacha gari lake mahali fulani akanifuata kwa kutumia usafiri wa kukodi.
Hiyo ndo' sababu pekee sikufanikiwa kumwona siku ile, laiti angelitumia gari lake ambalo nalifahamu vema kama kiganja cha mkono wangu, isingenichukua macho mawili kumbaini.
Hata kama gari hilo lingekuwa limebadili rangi yake ya muda mrefu.
Nakumbuka gari lile lililombeba Anwari kunifuatilia, nilipata kulishuhudia kwa macho yangu kabisa lakini sikufikiria kwa muda huo kama gari lile lipo kwenye misheni maalum, nilidhani ni gari tu lenye shughuli zake, limembeba mtu ama watu wanaokaa katika mandhari yale, kuja kubaini nilikuwa nimeshachelewa.
Siku Anwari ananambia baada ya kumuuliza amepajuaje kwangu , maelezo anayonipa ndo' yananirejeshea kwenye fikra ya gari lile.
Gari dogo rangi ya fedha nililoliona kwa umbali wa mita kadhaa, muda mfupi tangu niliposhuka toka kwenye gari lile la shule linalonichukua na kunirejesha.
Basi siku ile niliyoonana na Anwari, nilifika nyumbani, kama ada, nikafanya kazi zangu na kuweka kila kitu sawa.
Nakumbuka siku hiyo nilimkuta mume wangu kesharudi nyumbani, yu pamoja na Amiri wakishughulikia mifugo.
Bwana huyo alinambia siku hiyo alirejea mapema nyumbani, majira ya mchana, maana alikuwa amechoka sana kwasababu ya ule ulevi wa jana yake usiku, alilalamika kichwa kilimsumbua kweli kazini achilia mbali uchovu hivyo akaona ni vema kurejea mapema.
Lakini mbali na hayo, alinambia habari mbaya alokuta pale nyumbani, matetea mawili ya kuku yalokuwa yanatamia mayai yamekutwa yamekauka huko bandani majira ya asubuhi.
Na chanzo cha matetea hayo kufa, hamna alokuwa anajua.
Habari hiyo ikanikumbusha upesi usiku ule wa jana, usiku ule niliposikia kuku wanalia na kuparura kule bandani.
Kumbe yale nilokuwa nawaza yalikuwa ni sahihi - ya kwamba kuna mdudu ama mnyama aliingia mule bandani?
Mume wangu alinambia wamekagua banda zima pamoja na Amiri lakini hawajaona sehemu yenye uwazi wa kuingiza hata nyoka, hawajui imekuaje kuku wale wakafa kwahiyo basi walihitimisha huenda ni ugonjwa hivyo kuku wapatiwe chanjo upesi.
Niliwatazama kuku wale walokufa, kweli walikuwa wamekauka kana kwamba mti mkavu, viungo vyao vimekakamaa mno, si mbawa wala miguu yao ilokuwa inajikunja, nikahamaki ule ni ugonjwa gani ulowapata?
Kwasababu sikuwa na ufahamu wowote na mambo ya mifugo, nilinyamaza kimya maisha yakaendelea.
Kesho yake, mapema asubuhi, niliwasiliana na rafiki yangu Zai kumjulia hali.
Alinambia ameshatoka hospitali, sasa yuko kwa ndugu yake kwasababu ya uangalizi mpaka pale atakapojihisi yuko sawa.
Nilimuuliza Zai kama alimwambia chochote Anwari kuhusu mimi, Zai akakataa katakata. Nilimweleza Anwari alikuwa anajua kuhusu ujauzito wangu na sasa anajua kama nina mtoto, habari hizo kazitoa kwa nani? Zai akasema hajui kitu.
Hajawahi kuongea jambo lolote na Anwari.
Basi nikampatia ujumbe kuwa kuanzia muda huo sitaki amwambie Anwari kitu chochote kile kunihusu mimi. Sitaki kabisa wanizungumzie huko watakapokutana ama kuongea.
Niliongea kwa kufoka na swala hilo likamkwaza Zai. Alinyamaza kunisikiliza nikiropoka mpaka mwisho wake pasipo kutia neno alafu akamalizia kwa ufupi, "sawa." Kisha akaniuliza, "umemaliza?"
Nikamwambia nimemaliza, hayo yamekwisha.
Akaniuliza, "naweza kukata simu?"
Kabla hajakata, nikamgusia kuhusu lile swala lake la kuonana na yule mama kwaajili ya tatizo lake la kupandwa na kusumbuka na maruwani.
Nilimwambia nimewasiliana na mama Miraji na tayari ameshanipatia muda na siku ya kuonana naye basi tufanye hima tukatimize wajibu wa kutafuta tiba, ajabu mwanamke huyo akanigomea katu, alinambia hana shida, na kama akiwa nayo basi atajua mwenyewe namna ya kuhangaika nayo.
Baada ya kusema hayo, alinikatia simu nikabaki na butwaa.
Zai alikuwa ameghafirika.
Sikuhangaika naye siku hiyo, nikamwacha na mimi nikandelea na mambo yangu. Baada ya kama siku mbili hivi, nilipigiwa simu na Anwari.
Sikutaka kupokea simu hiyo lakini sikuwa na budi kwasababu ya maagano niliyoyaweka. Nilipokea moja kwa moja nikamuuliza bwana huyo anataka nini, hapo akaniuliza mara yangu ya mwisho ni lini kuwasiliana na Zai, nikamweleza ni juzi, basi akanambia Zai amezidiwa sana, na hapo anapoongea na mimi yupo na Zai hospitalini!
Kutazama saa, ni jioni ya saa kumi na moja, tayari nisharudi nyumbani nipo kwenye maandalizi ya chakula cha jioni.
Sasa nafanyaje?
Niliharikisha mambo yangu kisha nikamwita Amiri na kumwambia aketi na mtoto pale nyumbani, mimi natoka kidogo ila nitarudi muda si mrefu.
Niliondoka na mwendo wa dharura, sikupata hata kugusa kile nilichokipika, niliona ni vema nikawahi kwanzan hospitali alafu nitarejea kuendelea na mambo yangu.
Nilikodisha bajaji mpaka huko ambako nilielekezwa, kufika nikamkuta Anwari pamoja na dada ambaye nilimtambua kama ndugu yake na Zai, yule ndugu ambaye kwake ndipo Zai alikuwa akiishi baada ya kutoka hospitali.
Dada yule aliniambia hali ya Zai ilibadilika majira ya jioni, akisema na kubwata maneno yasoeleweka, akipasua na kubamiza vitu alafu ghafla akaanguka chini na kupoteza fahamu!
Hapo ndo' akafanya jitihada za kumleta mwanamke huyo hospitali, moja kwa moja akaingizwa kwenye chumba cha dharura na hata sasa akiwa chini ya uangalizi wa madaktari.
Walipopata wasaa wa kusema na daktari waliambiwa mwanamke huyo anasumbuliwa na presha kali ya kupanda, moyo wake umetanuka, hivyo kwa muda kidogo watabaki naye mpaka pale watakapoona ni muda sahihi kumruhusu.
Gharama za siku hiyo, zote kuanzia usafiri mpaka vipimo vya Zai, bwana Anwari alivifunika kwa kuvilipia 'cash', pesa kutoka mfukoni mwake.
Bwana huyo alitoa pesa pasipo kugugumia wala kunung'una. Nilimtazama usoni akiwa anatoa pesa kweli nikaguswa na tukio lile.
Moyo wa kipekee kabisa.
Lakini jambo lile lilinipa mwanga ni kiasi gani Zai na Anwari walivyokuwa wameshibana. Nikajiaminisha moyoni mwangu kuwa kweli Zai alimpa maneno yale bwana Anwari. Maneno kunihusu mimi.
Baada ya kukaa hapo hospitali kwa takribani masaa mawili, niliona niage niende nyumbani maana muda ulishanitupa mkono.
Bahati haikuwa na mimi, muda wote n'lokaa hapo sikufanikiwa kumwona rafiki yangu Zainabu zaidi ya kuambiwa tu hali yake na vinywa vya watu wengine.
Niliahidi nitarejea tena kesho asubuhi, kwa muda huo waniache tu niende maana nimeacha mtoto mpweke na mume atakuwa yu njiani kurudi nyumbani.
Baada ya kueleza hayo, Anwari alisema;
"Naomba nikupeleke kama hutojali."
Sikukubali.
Nilimsihi abakie hapo pamoja na yule dada, ndugu yake na Zai, mimi nitaenda mwenyewe.
Lakini bwana yule hakukoma, aliendelea kusisitiza ya kwamba muda umepita na hivyo ni vema tukaenda wote ili anisogeze.
Kweli kutazama muda nikaona nimechelewa mno, nikamwambia bwana yule anisogeze mpaka mahali fulani, si mbali sana na nyumbani kwangu, hapo nitajua cha kufanya kufika ninapoishi.
Akaridhia.
Alinibeba na gari yake, na pasipo hata kumwelekeza makazi yangu yalipo, akanyoosha na njia kwenda mwelekeo sahihi.
Tulienda kilomita kadhaa, sikujua nini kilitokea, lakini nilianza kuhisi kichwa changu kizito, sioni vizuri na siwezi kuongea.
Nilijipapatua nikauliza; "Anwari, nini kina ..." Sikumalizia kauli yangu nikabebwa na usingizi mzito mno mno, nilikuja kupata ufahamu kesho yake nipo juu ya kitanda cha Anwari, sina nguo yoyote mwilini mwangu!
Shuka limenifunika upande mmoja tu, huko kwingine ni Mungu nisadie.
Kutazama saa ya simu yangu ni saa tatu ya asubuhi! 'Missed calls' kumi na tatu za bwana Mgaya, ujumbe ndo' usiseme, kweli nikajikuta napagawa na roho yangu.
Mungu wangu! Mungu wangu! Nini hiki?
Nilikurupuka pale kitandani nikaangaza huku na kule, sikuona nguo zangu, nilimtafuta Anwari naye sikumuona, niliita jina lake mara tatu lakini hakuna aliyenijibu, kimya nyumba nzima.
Sijakaa vema, simu ya Mgaya ikaita tena, sikuelewa nipokee ama niache.
Nikipokea nasema nini?
Nikiacha nitaenda kusema nini?
Sikuelewa nataka nini, sikuelewa nafanya nini?
Nikiwa nimeshikilia shuka langu kunisitiri, mara nikaona mlango wa chumba nilichomo unafunguliwa, kutazama ni Anwari.
Bwana huyo aliingia akiniuliza, "umeamkaje, mpenzi?"
Nikajikuta najisema mwenyewe rohoni...
Maneno ya ghadhabu,
K*mmmmmmk zako Anwari!
***
YcSehemu ya Kumi:
Nilikurupuka sana, kichwa kinaniwaka moto, nikavaa nguo zangu kama nakimbizwa lakini tena nikazivua.
Mwili ulikuwa umechunda kwa jasho. Harufu haieleweki. Vipi nikikutana na Mgaya nyumbani? Akihisi harufu hii haitakuwa tabu?
Nikakimbilia bafuni kuoga, nilijimwagia maji upesiupesi, hata sabuni haikutoka vizuri mwilini nikawa nishatoka na taulo kujifuta.
Nilijipakaa mafuta toka kwenye mkoba wangu, nikavaa upesi na kutengenezea nywele zangu vema, vilevile kama nilivyotoka nyumbani, nilipomaliza nikajipulizia marashi, yale aloniletea mume wangu kama zawadi, baada ya hapo nikawa tayari kuondoka.
Hapo nilitumia robo saa tu mpaka kuwa mkamilifu. Siku ile ndo' nilijua kumbe kujiandaa harakaharaka naweza, maana mimi desturi yangu ni kutumia si pungufu ya lisaa na kitu kwenye kujiandaa tu.
Muda wote huo nikiwa najiandaa, Anwari alikua amejilaza kitandani akinitazama, japo nilikuwa nafoka na kutusi juu, bwana yule hakuonekana kujali, ni kama vile alikuwa anafurahia yale yanayoendelea pale, namna mimi ninavyoteseka na kuhanyahanya.
Aliniuliza nikupeleke? Nikamjibu sitaki hata kuona sura yako, Anwari, achilia mbali kunipeleka.
Kwa hofu nilokuwa nayo, nilichuruza jasho japo nilitoka kuoga muda si mrefu na mule chumbani kulikuwa na kiyoyozi kinachoyoyoa hewa kwa mbali.
Anwari aliniambia; "sasa kama hutaki nikupeleke, utapata wapi usafiri haya maeneo yetu?"
Japo sikutaka kuzungumza naye wala kuongozana naye, ila alichokisema Anwari kilikuwa ni kweli, kule alipokuwa anaishi kulikuwa ni mbali na kituo cha magari na sikuwa na namba yoyote ya dereva aidha pikipikipiki au bajaji.
Kwahiyo hapa nikajikuta namrejea tena Anwari kama waswahil na baniani mbaya ...
Bwana huyo aliongozana na mimi, ndani ya gari yake, simu yangu nimeishikilia mkononi nawaza niandike nini ama nimpigie nani na ninwambie nini.
Niimtazama Anwari, nikayawaza mengi kichwani mwangu, Anwari ni nini umenifanyia? Nilimuuliza. Anwari, kwanini umenifanyia hivi?
Unajua kabisa nina familia nyumbani, mtoto na mume pia, hayo kwako hayakutosha?
Naye akanijibu kwa kuniuliza, kama ningekuambia ungenikubalia? Kisha akaongezea, si ungeanza kusema ngonjera zako za mimi ni mke wa mtu, nina mume wangu?
Bwana huyo akahitimisha akisema alikuwa ananihitaji na ndo' maana akafanya vile.
Akafanya ....?
Hapo ndo' fikra zangu zikakumbuka mchezo ulipoanzia.
Nikiwa pale kwenye benchi la kungojea, mimi pamoja na yule ndugu yake Zai, bwana Anwari alituomba radhi akatoka idogo kwenda mahali nisipopafahamu.
Baada ya dakika kadhaa, bwana huyo alirejea akiwa na chupa mbili za soda na 'foil' lillokuwa na nyama ya kukaanga ndani yake, akaniambia shika hii nimekuletea, najua una njaa.
Na ni kweli nilikuwa na njaa, nyumbani nilipika lakini ile dharura yangu ilin'tia pupa nikaondoka tumbo likiwa tupu, sikuwa nimekula tangu majira ya mchana, tena mchana wenyewe niligusagusa tu chakula cha shuleni maana nacho huwa cha hovyo.
Kwahiyo kwa ile njaa nilokuwa nasikia, 'foil' na kinywaji kile niliviona kama mkombozi.
Nilipovishika niliacha vinipe ahueni ya hali yangu, na kweli vikaninusuru, lakini kumbe vilitumwa kwa mkakati maalum.
Mkakati wa kunidhoofisha taratibu kadiri na muda.
Anwari alijua kunipata kweli, na alijua kunitumia. Makosa yale niliapa kutoyarudia kamwe katika mikono yake.
Huwezi kuamini alinambia, kama mimi nilivyokuwa namhitaji kipindi kile mpaka nikamrubuni akalala na mimi, basi naye ndivyo hivyo hivyo alivyofanya, hamna mwenye dhambi kumshinda mwenziwe.
Aliponifikisha maeneo fulani ambayo naweza nikapata usafiri kwa urahisi, nilimtaka anishushe niende zangu mwenyewe.
Niliposhuka nilinyookea moja kwa moja nyumbani nikitumia usafiri wa pikipiki, kufika Amiri ananipokea mkoba na pia ananipokea kwa maneno ya yale yalotukia pale nyumbani.
Alinambia bwana Mgaya hayupo, ametoka na mtoto kwenda asipopajua lakini alienenda akisema lengo lake ni kunitafuta mahali nilipo kwani simu zake hazipokelewi na hana habari yoyote ile.
Amiri alinambia bwana Mgaya alikuwa kama mtu alochanganyikiwa, anaongea mwenyewe na kufokea hewa, hata alipoingia kwenye gari lake alisahau funguo, alipoenda kuuchukua ufunguo akamsahau mtoto, alipomrejea mtoto akasahau simu!
Alienda akarudi akipiga honi nyingi, niletee simu yangu, niletee simu yangu!
Katikati ya masimulizi hayo ya Amiri, mara simu yangu ikaita, kutazama ni yuleyule tulokuwa tunamwongelea, yaani bwana Mgaya, nikapokea simu hiyo kwa mara ya kwanza na kumwambia niko nyumbani, nimeingia hapo muda si mrefu.
Alipotaka kuniparamia kwa pupa ya maswali, nikamwambia aje kwanza nyumbani, tutaongea kila kitu, haina haja ya kumaliza muda na salio la simu.
Basi nikiwa naongea na simu hiyo ya bwana Mgaya, bado hatujamalizana, mara simu nyingine ikawa inaingia na kuita 'diiii-diiii diii-diiii' kutazama naona jina la Anwari kwenye kioo!
Hii ndo' sababu sikuwa nataka kumpatia bwana huyu namba yangu, najua hana mipaka, hajui muda gani wa kutulia na muda gani wa kutenda, kweli anapiga muda huu na yale yote yalotokea?
Vipi kama ningemkuta bwana Mgaya pale nyumbani?
Mgaya alipokata simu, nilipokea ile simu ya Anwari nikafoka kumuuliza anataka nini? Anahangaika nini na mimi muda huo baada ya kunitenda yote yale? Ajabu bwana yule akawa anaongea mambo nisiyoyaelewa, alikuwa anabwata kama mtu alozidiwa na ulevi na mimi baada ya kuona huo ni upuuzi, nikakata simu yake.
Nilikata simu hiyo lakini nikaendelea kuongea mwenyewe kama mwehu. Nasonya kila mtindo.
Amiri aliyekuwa amesimama kando ananitazama kana kwamba bango, aliniuliza, "kuna tatizo?"
Sikumjibu, nikaingia zangu ndani moja kwa moja mpaka chumbani.
Muda si mrefu, bwana Mgaya akiwa ameongozana na mtoto wailifika nyumbani kikazuka kikao cha dharura.
Bwana Mgaya alikuwa amefura kwelikweli na mimi sikuwa na kingine cha kumweleza isipokuwa kumtumia mgonjwa Zai kama ngao yangu.
Nilimwambia rafiki yangu Zai yu hospitali amelazwa na mimi nilikimbilia huko kumwona baada ya kupewa taarifa hiyo mbaya.
Aliniuliza mbona sikuwa napokea simu yangu wala kurejesha jumbe zake lukuki? Nikasema simu yangu niliisahau nyumbani kwa zile haraka zangu, nilikuja kubaini sina simu nilipofika hospitali na sikuwa na namna tena.
Nilimwambia: "kumbe niliisahau simu jikoni ndani ya shelvu, nilivyorudi Amiri akanisaidia kupekua huku na kule maana simu yenyewe haikuwa na sauti, hata kuipiga isingesaidia."
Hapo nilimtazama Amiri, Amiri naye akajua kila jambo ndani yangu, sikuhitaji kumweleza kitu zaidi ya yale macho mangu, naye akashika hatamu kama vile tulikaa kitako kuyapanga yale mambo.
Akamweleza Mgaya namna tulivyotafuta simu mule ndani na namna mimi nilivyohamaki baada ya kuipata simu hiyo na kuona jinsi Mgaya alivyonitafuta.
Aliyaeleza mambo katika namna ambayo alinishangaza. Aliyasema kwa kujiamini pasipo kupepesa macho hata kunishinda mimi mtunzi wa wongo ule.
Alipomaliza hayo maelezo, Mgaya akabakiwa na hoja dhaifu, hakuwa na kingine cha kusema zaidi ya kukazia kwenye swali lake la kwanini usingechukua simu ya mtu mwingine ukanipa taarifa?
Alisema alikuwa na hofu sana juu ya usalama wangu kiasi cha kuanza kufikiria kupita vituo vya polisi ama kupita hospitalini kuniulizia.
Alisema laiti asingeniona siku hiyo nzima, basi angeanza zoezi hilo mara moja.
Baada ya hiko kikao, niliongozana na Mgaya kwenda naye chumbani, sasa nina amani maana kikwazo kile nimekikwatua.
Baadae nilipiga simu kule hospitali kwa ndugu yake Zai kumuuliza hali ya mgonjwa, nilipopata taarifa njema nikaendelea na ratiba yangu ya kawaida, nikipanga kesho ama keshokutwa nikitoka shule basi nipitie tena hospitali kumjulia hali rafiki.
Kweli baada ya siku mbili, kama nilivyopanga, nilifika hospitali na huko nikamkuta Zai anangoja kupewa bili yake ili apate kurejeshwa nyumbani, hali yake ilikuwa njema, si haba.
Bili ikatoka anadaiwa kama laki sita hivi kwa ujumla, achilia mbali bili ya siku ile ambayo Anwari alikuwa amemsaidia.
Sasa shida ikaja Zai hakuwa na pesa hiyo mfukoni, kwa maelezo yake alibakiwa na laki mbili tu kama akiba, akitoa hiyo hajui atadumu vipi na maisha mpaka kuja kuupata mwisho wa mwezi.
Hata yule ndugu yake anayekaa kwake hana kazi ya maana hivyo mbali na kumhudumia, kwenye swala la mambo ya pesa ni mtu dhoofu l'hali, pangu pakavu tia mchuzi.
Zai alisema; "Anwari aliniahidi atanisaidia kwenye hili janga langu mpaka mwisho wake lakini hata sasa simwoni."
Alisema amejaribu sana kumpigia Anwari pasipo mafanikio, mwanzoni simu yake ilikuwa inaita lakini sasa hivi imekuwa kimya. Ukipiga hapatikani.
Anawaza ni nini kimemkuta bwana huyo kwani si kawaida yake kupitisha siku asije kumwona, achilia mbali zimeshapita siku tatu sasa!
Alilalamika gharama za pale ni kubwa sana, kama ingekuwa ni kwa utashi wake mwenyewe asingekuja hospitali hiyo, angeenda zake hospitali za serikali, lakini Anwari alimsisitizia hapo maana anaamini pana huduma nzuri.
Sasa Anwari hapatikani, anafanyaje?
Nilitazama uwezo wangu binafsi wa kumsaidia rafiki Zai katika adha ile lakini bado sikufua dafu.
Kujikamua kote mifuko yangu niliambulia laki moja na alfu hamsini tu ya akiba ingali pesa inayohitajika pale hospitalini ni pomoni.
Nikajaribu kumpigia Anwari, simu haipatikani. Nikajaribu tena, bado haipatikani.
Nilijaribu kama mara tano lakini hamna nilichoambulia zaidi ya mhudumu kunihasa namba ya mteja ninayempigia hapatikani kwa muda huo.
Hapo akili yangu ikanikumbusha maongezi yangu ya mwisho na mwanaume yule.
Yale maongezi baada ya kuongea na Mgaya.
Yale maongezi niliyomfokea na kumtukana.
Nilichokumbuka katika maongezi hayo ni namna bwana huyo alivyokuwa anazungumza kana kwamba mwendawazimu mpaka mimi nikaikata simu yake.
Sasa leo hii hapatikani, na si tu leo ni tangu siku ile nilipoteta naye hewani.
Anwari, nini kimekukumba?
Sasa nikajiuliza na kichwa safi kisichokuwa na mawingu ya hasira.
Kwanini siku ile ulinipigia?
Ulikuwa unataka kuniambia nini ambacho sikuelewa? Na hicho ulichotaka kuniambia kina mahusiano na wewe kutokuonekana hospitali ama kutopatikana hewani?
Nikamwambia Zai acha niende nyumbani kwa Anwari nikatazame.
***
Pita hapa bossSijaisoma mkuu
Ila mbele ya safari Amir ana jambo lake..,Sehemu ya Kumi na Tatu: (EXTENDED)
Nilikitumia chumba changu vema kumshawishi bwana Mgaya, kesho yake tu Zai akanambia atafika nyumbani kwaajili ya kuweka kambi hapo kwa muda kama tulivyokubaliana.
Siku hiyo ya Zai kuja ilikuchwa kama kawaida, kama zilivyo siku zingine, lakini baadae ndo' mambo yalikuja kubadilika kufanya siku hiyo kuwa tofauti na siku zinginewe.
Siku hiyo ilikuwa ni mwisho wa juma, kwahiyo mimi nalikuwapo nyumbani kwaajili ya mapumziko yangu ya kawaida, na kwasababu hiyo niliutumia muda wangu kufanya kazi zangu za hapa na pale mathalani kufua nguo, kuosha vyombo, kusafisha uwanja na kadhalika.
Nikiwa nafyagia uwanja, kama kazi yangu ya mwisho ilobakia kabla sijarejea zangu ndani, Amiri alikatiza akiwa amebebelea nyasi kuelekea kule bandani.
Nilipomwona kijana huyo, niliongea naye mambo machache, mambo na maagizo madogomadogo ya pale nyumbani, nilipomaliza hayo akaniuliza jambo; "kuna mtu anakuja nyumbani leo hii?"
Sikujua kwanini aliniuliza hivyo, nilimuuliza akaniambia ameona baadhi ya maandalizi humo ndani, basi nikamwambia ni kweli, Zai yu njiani anakuja. Akaniuliza yule rafiki yako wa siku zile? Nikamjibu, ndio, hakusema tena akaniaga na kwenda zake.
Baadae katika majira ya jioni hivi, Zai alikuja nyumbani akiwa amebebelaa begi lake moja la mgongoni.
Mwanamke huyo alionekana dhoofu, nilipomtia tu machoni, nilimfuata na kumkubatia kisha nikamsaidia begi lake, begi alilokuwa ameweka humo nguo kadhaa za kuvaa akiwa pale nyumbani, nikamkarimu na kumwongoza mpaka ndani, huko tukaongea mambo machache kabla hatujaongozana kwenye chumba kile nilichomwandalia.
Kabla hajutaingia humo ndani, Zai alisimama akautazama mlango wa chumba kile anacholala Amiri, aliutazama mlango huo kana kwamba anasoma karatasi za kitabu, nikamuuliza kunani na jambo hilo?
Akanitazama kwa macho yake dhaifu kisha akaniuliza, si ni mlango huu? Sikumwelewa anachomaanisha, mlango huu nini? Akauliza tena, si ni mlango huu ndo' niliukanda na mikono yangu siku zile?
Hapo nikakumbuka ya kile kisa chake cha kupandwa maruwani, nami sikutaka ajisikie vibaya nikamwambia aachane na mambo hayo, yashapita, na hata hivyo si muda mrefu tutapata suluhu lake.
Ya nini Zai kuhangaika na doa na dawa yake iko njiani?
Tuliingia ndani akaweka begi lake kitandani kisha akalifungua na kutoa mfuko mdogo humo, akiwa anaufungua mfuko huo alinambia wasaa huu amejipanga kwa kiasi chake mpaka hapo atakapopata suluhu lake la kudumu.
Katika mfuko ule alitoa vijiti kadhaa vya udi, hivyo nilivitambua, lakini pia akatoa dawa fulani ndani ya chupa ndogo ya plastiki, chupa mithili ya hizi tunazoziona kwenye maduka ya madawa, chupa hiyo ilikuwa imebandikwa 'stika' yenye maelezo maelezo mengi, ya kiswahili na kiarabu, Zai akanieleza dawa hiyo ya ni ya ki-sunna, alipewa na bwana mmoja akimweleza itamsaidia na tatizo lake.
Alinieleza matumizi ya dawa hizo, vema, hatua moja baada ya nyingine, akisema siku au muda ikitokea akabanwa na tatizo basi nisisite kumsaidia haraka niwezavyo, hana mkono mwingine wa msaada isipokuwa wangu.
Nami niseme nini tena? Niliyakubali yote alonambia nikaondoka hapo nikiyabeba kifuani mwangu maana sikuwa na budi, alimradi nilimshawishi mwenyewe aje kuweka makazi pale basi niliwajibika na maamuzi yangu hayo.
Nilienda chumbani mwangu nikafanya kushika simu yangu upesi na kunakili sauti yangu kwa rikaa ya 'recorder', nilifanya hivyo ili nisije kusahau aya alizonipa Zai, aya chache ambazo natakiwa kuzisema punde nikiwa nahangaika na maelezo ya dawa zile alizonionyesha, nilipofanya hivyo sasa nikatulia.
Niliona kila kitu kipo sawa.
Kwasababu hiyo, nilienda zangu kuoga ili basi nipumzike kidogo kabla ya kushika majukumu mengine ya mwisho.
Nililala kama lisaa na nusu hivi, nilipoamka, kabla sijashika kitu chochote, nikapata hisia kuna jambo halipo sawa.
Tangu naongea na Zai, nikalala na sasa nimeamka, sijapata kumwona mwanangu.
Hiyo haikuwa kawaida.
Nilichungulia dirishani kutazama huko nje, nikarusha macho yangu kote pale panapoonekana, sikumwona mtoto.
Nilienda sebuleni, napo mtoto hakuwapo wala kule jikoni vilevile.
Nikaita kama mara mbili, mtoto hakuitika. Nikatoka nje kutazama, sikumwona mtoto. Nilienda hadi kule kwenye mabanda ya mifugo, sikumwona mtoto kabisa, sasa nikaanza kupagawa.
Sasa nikaanza kujihisi mzembe kwelikweli. Kwanini sikumtafuta mtoto muda ule? Vipi kama kaenda mbali? Vipi kama kapotea?
Tumbo lilinivuruga.
Kidogo Zai aliufungua mlango nilotokea, akaniita Mage Mage, nilipoitika na kumjongea aliniuliza namtafuta mtoto? Nilipomjibu ndio akanambia yeye alimwona kwa mbali mtoto wangu kule nje akiwa anaongozana na Amiri.
Hivyo kama namtafuta basi nimtafute kijana huyo.
Kusikia hivyo angalau moyo wangu ukatuama, niliamini mwanangu yuko salama kwenye mikono ya Amiri, haina haja ya kupanda presha.
Nikangoja kidogo, kweli Amiri akajiri pale getini akiwa na mwanangu, wanatembea wakiwa wameshikana mikono.
Amiri alinisalimu kisha akanieleza walipotokea, mkononi mwa mwanangu alikuwa amebebelea pipi kubwa ya kijiti, mbali na pipi hiyo usoni mwake alikuwa amepachika tabasamu pana, bila shaka alikuwa amefurahia 'kampani' ile ya Amiri na mimi sikuwa na hiyana na hilo, nilifurahi kumwona mwanangu ana furaha.
Nilijaribu kumtwaa kutoka kwa Amiri ili niende naye ndani, ajabu mtoto akakataa.
Mwanzoni nilidhani masikhara, labda tamu za pipi tu zinamzuzua, lakini kadiri nilivyotia jitihada kumchukua ndo' nikazidi kufeli na kufeli, mtoto alinikataa kana kwamba mimi sio mama yake mzazi.
Alinikana kana kwamba tumbo nililombebea sio lile ninalotembea nalo, nami nilipoona nimeshindwa basi nikamwomba Amiri amshawishi mtoto akubali kwani yampasa sasa akapate chakula cha jioni.
Yaani fikiria unamwomba mtoto wako kama pesa? Tena toka kwenye mikono ya mtu mgeni, unajisikiaje?
Amiri aliongea na mtoto na kweli mtoto akaridhia kuja upande wangu, kabla sijaondoka kwenda ndani pamoja na mtoto, Amiri alinitaka tuzungumze jambo kidogo kama nina muda.
Nami sikuona ubaya, nikasonga kando tukazungumza.
Amiri alinieleza jambo fulani ambalo kwa kiasi chake lilinishtua.
Kama haitoshi alinisisitiza kile akisemacho ni kweli, kweli kabisa iliyo uchi na hivyo nisipuuzie nichukue hatua.
Baada ya hapo, akaenda zake akiniacha natafakari.
Natafakari kile alichonieleza.
Ni kweli ama ni hekaya?
Nilikuja kuubaini ukweli si muda mrefu, Amiri hakuwa ananiongopea hata kidogo.
Sikuchukua sekunde nyingi pale nje, nikaingia zangu ndani kisha nikafanya mpango wa chakula, tukala kwa pamoja isipokuwa Amiri, na baada ya kumaliza Zai akaniambia ana habari njema anataka kunieleza.
Habari hizo alizihifadhi kifuani mwake akiningojea niamke na tutulie ili tupate kuzungumza.
Basi nikamwazima sikio.
Kwa furaha, Zai alinieleza kesho ama keshokutwa ataondoka pale nyumbani, kuna kazi amepata pahali na kazi hiyo ni ya pesa nzuri sana, hawezi kuacha fursa hiyo iende kombo.
Alinambia: "Mage, shule ile ni ya wazungu, mshahara wao si haba, hata nikifanya kazi miezi mitatu tu naweza nikamiliki biashara ya maana."
Kitu ambacho Zai hakujua, mimi nilikuwa namsikiliza nikiwa naujua ukweli wote, ukweli ya kwamba ananiongopea, hata macho yake yalikuwa yanamsaliti.
Nilimsikiliza mpaka mwisho wake, nikampa kongole zake alafu nikampa na ushauri juu yake, baada ya hapo nikaenda zangu chumbani maana sikuwa nahitaji msongamano, nalihitaji muda wangu wa pekee kwaajili ya tafakari.
Nilipofika huko, nilijilaza kitandani nikawianisha yale alonambia Amiri na yale alonambia Zai, niliona bayana ukweli uko wapi, nilipoyamaliza mambo hayo nikaona ni stara kwenda kuonana na Amiri kuyakiri yale alotamka.
Nilitoka nikaenenda na njia mpaka nje, huko kutazama kushoto na kabla sijamaliza kulia nikamwona Amiri upande wa mabanda.
Nilimwita nikamweleza vema kuwa yale alonambia yamejiri kama alivyoyatamka.
Mwanamke yule, yaani Zai, ameniambia anataka kuondoka muda si mrefu, kesho ama keshokutwa, na basi anishauri cha kufanya maana nahisi nachanganyikiwa.
Amiri alitikisa kichwa chake akanambia: "najua hakuniona, na ndo' maana aliyaongea mambo yale kwenye simu. Yule mwanamke anajua kila kitu kuhusu wewe na ubaya hizo taarifa anazitumia kama silaha aidha kukuangamiza wewe ama kujikwamua yeye na hali yake. Mimi ninachokushauri ni uongeze umakini zaidi kwake, la sivyo siri zako zitakuwa barabarani kila mtu akizitazama kisha anageukia upande wa pili maana ni chukizo!"
Aliponieleza hayo, nilitafakari kwa ghadhabu nikijiuliza ni nini niliwahi kumkosea Zai mpaka akafikia hatua ile, hatua ya kuamua kutoa siri zangu za ndani kwa watu anaojua wanaweza kuniumiza?
Hapa nikaelewa vema yale ya Yuda kumsaliti Yesu, haikuwa sababu nyingine bali vipande kadhaa vya fedha, vipande hivyo ndo' hivi sasa vinavyomwehusha Zai mpaka anasahau ya urafiki wangu wa dhati?
Pamoja na kumsaidia yote yale?
Sasa anataka shikana na ndugu za Anwari kunitokomezea familia?
Amiri aliniuliza ni kwanini mwanamke yule yuko hapo nyumbani, amefuata nini hapo, mimi nikamweleza ni shida yake ya kupandwa maruwani ndo' imepelekea tabu yote hiyo, shida hiyo imechochea mpaka mwanamke huyo kuwa na tatizo la presha ya kupanda kiasi kwamba moyo wake ukatanuka.
Anwari akasema vema, basi nitilie maanani yale alonambia, baada ya hapo akaenda zake na mimi nikaenda zangu.
Kila mmoja na shughuli zake.
Baadae bwana Mgaya alirejea nyumbani kwenye majira ya saa tatu au nne usiku hivi, nikamkutanisha na Zai kama mgeni wetu wa pale nyumbani, Zai akasalimiana na bwana huyo na wakateta mambo kadhaa.
Zai alisema, "nashukuru sana, shemeji. Ni muda mrefu kweli tangu siku ile ya harusi, nafurahi leo tumeonana."
Zai akamwambia bwana Mgaya angependa kukaa hapo nyumbani kwa muda mrefu lakini kuna dharura imemtokea hivyo basi hatodumu hapo kwa zaidi ya siku mbili, itambidi aondoke.
Bwana Mgaya akawa hana la zaidi la kusema, yote kwake yalikuwa kheri, alimkaribisha Zai kwa mara nyingine pale nyumbani kisha akala chakula chake na kwenda zake kulala.
Ulipowadia usiku wa manane, usiku mzito wenye utulivu mkubwa, ndipo visa vikaanza rasmi chini ya paa lile.
Nikiwa sina hili wala lile, niko ndani ya ulevi wa usingizi, nikasikia sauti ya mtu akiita, akiita vitu nisivyovielewa.
Awali nilidhani sauti hiyo ni ndoto ama inatokea mbali huko mashambani lakini ilipoendelea kuita nikahisi tofauti, nikahisi sauti hiyo inatokea mule ndani na si kwingine.
Niliamka nikaketi kitako kitandani, nasikiliza kwa umakini kuhakikisha kile nisikiacho, nilipopata uhakika nikafanya jitihada za kumwasha bwana Mgaya, kumwamsha asikie na tusaidizane.
Mgaya ... Mgaya ... Amka! .. we Mgaya!
Nikamwita nikimtikisa lakini hakuamka, aliendelea kukoroma kana kwamba hamna kinahojiri.
Sikukata tamaa, nikaita tena na tena, tena na tena, huko nje ya chumba sauti inazidi kumea na sasa si kuita tena, sauti ile inanguruma kana kwamba simba ama tuseme mbwa anayemtishia mvamizi, lakini bado Mgaya hakuamka.
Ni kama vile hakuwa katika usingizi huu wa kawaida tunaoujua, kwa mtu aliyekuwepo usingizini asingeweza kumudu pale kitandani pasipo kuamka kwa namna ile nilivyokuwa namwamsha.
Nilimsukumia huku na kule kazi yake ikawa kubadili tu mikao, lakini kuamka 'nehi nehi'. Alilala usingizi mkubwa ambao hata samaki pono haufahamu abadan!
Nilikuwa napoteza muda na nguvu yangu bure kuhangaika naye, na nilipobaini hilo niliachana naye nikanyaka simu yangu kisha nikaelekea mlangoni.
Sasa sauti inazidi kunifikia masikioni, tena vema sana, sauti ya mtu akinguruma kama mnyama, na mtu akipiga mayowe kama mfiwa.
Nilifungua mlango nikashika sakafu baridi ya korido, kitu cha kwanza kufanya, nikaelekea kwenye mlango wa Amiri nikabisha hodi kwa lengo aje kunisaidia na janga lile.
Nilibisha hodi nikiita Amiri Amiri, Amiri amka njoo upesi, Amiri njoo unisaidie, kweli kitambo kidogo mlango wa Amiri ukafunguliwa akatoka kijana huyo akiwa amevalia bukta tu, uso wake umejifinyanga na mang'amung'amu ya usingizi, macho yake yamefunikwa na ndita za sin'tofahamu.
Akaniuliza, kuna nini? Mbona majra haya mlangoni kugonga?
Nikastaajabu, ina maana mambo yale yananibughudhi peke yangu ama? Hawa wengine wanalalaje na songombingo zile? Ngurumo na mayowe?
Nilimweleza kuna tatizo, akaniambia anasikia, nikamwomba afuatane na mimi kwenda kumkabili mwanamke yule chumbani mwake, mimi najua kila kitu, 'ei to zedi' ya namna ya kuenenda naye maana alishanielekeza.
Amiri hakukataa, akiwa vilevile asichukue kitu wala kufanya jambo jingine, aliongozana na mimi moja kwa moja mpaka ndani ya chumba alichokuwemo Zai.
Humo tukamkuta mwanamke huyo, akiwa amevalia nguo ya ndani pekee, anahaha na kurandaranda huku na kule akijitutumua kama mpambanaji, tena mpambanaji mwenye nguvu kama Awafu, macho ameyatoa kama mtu aliyenigwa na tonge kubwa kooni.
Alivyotuona, alisimama akituangazia, kweli sijawahi kuona mapepo sijui maruwani kama yale, nalikuwa nashuhudia kwenye runinga vipindi mbalimbali vya maombi lakini sijawahi kutana na kitu halisi kama kile, kitu cha kutisha kweli, yani kama una roho ndogo huwezi kuhimili, aidha uzirai ama ukimbie.
Kufumba na kufumbua Zai alimkimbilia Amiri akipiga kelele, akamvaa wakapelekana mpaka chini, sasa ikawa mielekea aidha yeye ama Amiri, Amiri ama yeye.
Waligaragazana huku na kule kupishana nguvu, Zai anahangaika kumjeruhi Amiri na Amiri anahangaika kujizuia, yani ni kelele, ngurumo na miguno ya maumivu na jitihada za kujikwamua kutoka kwa mwingine.
Nilijaribu kumshika Zai lakini kamwe sikufanikiwa, mikono yangu ilikuwa kama ubua vile kwenye mwili wake, sikuweza hata kumsogeza msuli.
Amiri akaniambia, tena akipiga kelele ya mamlaka, fanya ile dawa!...fanya ile dawa! Mama, fanya ile dawa, fanya haraka!
Hapo ndo' nikakumbuka kumbe kuna jambo natakiwa kulifanya, tena jambo hilo ndo' limelileta humo ndani, basi upesi nikaangaza hapa na pale, kwenye kona ya chumba kile nikaona begi la Zai, upesi nikaliendea na kulifungua kutoa ile chupa ya dawa na vijiti vya ubani.
Nikakimbilia jikoni kuwasha ubani ule na pia kubeba kisosi kwaajili ya dawa, nilipofika chumbani nikafanya yale ambayo Zai alinielekeza pale awali, hatua kwa hatua, lakini nilipofika kwenye kunuwia yale maneno ya lugha nyingine, maneno ambayo niliyarekodi kwenye simu yangu, sikuweza kabisa!
Kila nilipojaribu nilikwama, ulimi mzito, ulimi una ukakasi, maneno hayatamkiki kabisa, wakati huo bado pambano la Amiri na Zai linapamba moto, hakuna anayekubali kuzidiwa na mwenziwe.
Nikiwa nahangaikahangaika, bado sijajimudu na maneno lakini mazingira nimeyaweka sawa, Amiri akaanza kutamka maneno ambayo binafsi sikuyaelewa, maneno hayo yalikuwa machache tu lakini aliyatamka kwa marejeleo, marejeleo ambayo yalinifanya nikayashika maneno hayo kwa upesi sana.
Kidogo akanambia, kwa sauti ileile ya mamlaka huku aking'ang'ana na Zai, tamka hayo maneno, Mama, tamka hayo maneno kama mimi! Fanya upesi!
Nikafanya hivyo, sikuwa na budi, nilifanya nikiwa nauzungusha ule udi kwenye kichwa cha Zai mara tatu kwenda, mara tatu kurudi, mara tatu kwenda na tena tatu kurudi.
Ajabu, Zai akanitazama kwa macho makali, kabla sijafanya kitu, akamwachia Amiri kisha akanirukia mithili ya paka, sikuweza kumhimili tukaenda wote mpaka chini, nilifikia mikono nikajiumiza sana.
Zai alinikaba kwanguvu mno nikawa natapatapa kujikwamua lakini kila nilivyojifaragua sikuweza kumshinda, alikuwa na nguvu mno mno, nilitumia mikono na miguu yangu kujiokoa lakini sikuweza kabisa.
Amiri alikuja kunisaidia kwa kumvuta mwanamke huyo kwanguvu, nami nikamsaidia kwa kutumia miguu yangu kumsukumia Zai mbali na mimi.
Nilitumia nguvu kubwa kiasi nikamtupa Zai kwenye kingo ya kitanda.
Aliruka akakita hapo kwanguvu akitoa kishindo kikubwa - KIH! kisha akatulia tuli, tuli sana.
Amiri alimsogelea kwa karibu akamtazama kwa umakini, alimshika nyuma ya kisogo akaona damu vidoleni mwake, akanitazama na kunambia, amekufa.
Hapo moyo wangu ukararuka, nikauliza unasemaje, Amiri? Amiri akarudia tena, Zai amekufa.
Jasho likaongezeka kunitiririka, nikanyanyuka upesi kwenda kumtazama Zai, nikamwita mara tatu nikimpigapiga makofi, hakuamka wala hakuitika hata kwa kuguna, nikaamini kweli mwanamke yule amekufa.
Sasa inakuaje? Nikajiuliza mimi mwenyewe, sasa inakuaje, nikamuuliza Amiri.
Nilihisi akili imeniruka kwakweli, kwa muda kidogo nikawa kama mtu alochanganyikiwa, Amiri alijaribu kunituliza akinambia sasa yatupasa kufikiri na sio kuwehuka, ikanichukua muda kidogo kurejea katika fahamu zangu za kawaida.
Amiri alinambia: "sasa tuubebe huu mwili tukaufukie mashambani, hamna atakayejua!"
Nikamuuliza ana uhakika, akasema ndio, ninyanyuke tufanye hilo zoezi upesi.
Basi kwa kusaidiana, tukaubeba mwili wa Zai mpaka jikoni, tukafungua mlango kisha tukaongozana mpaka nje ya uzio, huko tukaulaza mwili wa Zai chini kisha Amiri akaendea chepe ndani kwaajili ya kuja kuchimba ardhi tumfukie Zai.
Nilisimama hapo shambani nikiwa naogopa sana, kweli tuko wenyewe? Hamna mtu anayetuona? Nilitazama huku na kule kila saa, mwili unatetemeka, si kwa baridi bali kwa hofu.
Kidogo Amiri alifika akiwa amebebelea chepe mkononi, jasho lamtiririka kwenye paji lake la uso, akanambia, "sikia, wewe kazi yako imekwisha. Huku niachie mimi. Nenda ndani kahakikishe mazingira yanakuwa sawa."
Nikaenda ndani upesi, kuanzia pale mlango wa jikoni mpaka ndani chumbani alimokuwamo Zai kulikuwa na matone na michirizi mingi ya damu.
Nikaanza kufuta damu hizo upesi kwa kutumia tambara na ndoo ndogo, nilipomaliza jikoni nilishika korido ya kuelekea chumbani, kabla sijamaliza korido hiyo, nikasikia mlango unafunguliwa.
Upesi nikarusha macho mwisho wa korido, hapo moyo unalipuka vipande vipande, ni nani huyo?
Sauti ikaita, mama! ... Kumbe alikuwa mtoto, upesi nikamkimbilia na kuingia naye chumbani nikimuuliza mbona hajalala? Anafanya nini macho muda huo? Nilimuuliza nikihofia kama atakuwa ameona chochote.
Lakini kumbe yeye hakuwa shida pale, shida ilikuja pale nilipoingia naye ndani nikamkuta bwana Mgaya akiwa amesimama anatazama nje ya dirisha, nikahisi haja zote kwa pamoja! Sikujua nianze na ipi nifuatie na ipi.
Nilijikuta nasema mwenyewe kama mwehu, "Mgaya, ngoja nitakueleza, tafadhali nisikilize."
Mgaya hakusumbuka na mimi, aliendelea kusimama pale dirishani, alisimama kama mwanasesere, hajigusi wala hasogei, nikamsogelea nikimuita, bado kimya, sijui alikua anawaza nini, sijui alikuwa amepanga nini.
Nilipomkaribia kabisa nilisimama nyuma yake, kidogo nikahisi kishindo cha miguu, kutazama kule mlangoni nikamwona Amiri amesimama, chepe lake mkononi.
Akanambia, "tayari nimeshamaliza."
Kurudisha uso kwa Mgaya nikamkuta mwanaume huyo ananitazama kwa macho ya woga, mdomo wake unatetemeka.
Amiri akasema, "na huyo ndo' afuataye."
Mimi nikadakia, "hapana, hapana! Sio hivyo, Mgaya. Mgaya, ngoja nikueleze."
"UNIELEZE NINI?"
Nikakurupuka kitandani kama mwivi, macho yamenitoka, kutazama pembeni yangu namwona Mgaya akiwa amejilaza, nusu ya mwili wake umemezwa na shuka, ananiangalia kwa macho ya wasiwasi na kuchanganyikiwa.
Kutazama dirishani bado giza, nikamuuliza bwana Mgaya saa hii ni saa ngapi? Akaniambia saa kumi na moja sasa.
Haraka nikakurupuka kitandani, nikakimbilia chumba cha Zai.
Sikuamini ile ilikuwa ni ndoto, nilijikuta nakumbuka yale ya mama mkwe na yale yalotokea baada ya ndoto ile.
Nilipofika huko wala sikubisha hodi nikazama moja kwa moja, kutazama kitandani sioni mtu. Zai hakuwapo.
Ndani humo kunanukia ubani si utani.
Nilitazama kwenye kingo za dirisha nikaona vijiti vya ubani vikiishilia, na pale juu ya meza ya chumba hicho kuna kisosi chenye dawa, kisosi kilekile nilichokiona katika ndoto yangu.
Basi upesi nikatoka humo nikimbilie nje, bwana Mgaya ananifuata akinistaajabu nimepatwa na nini, nilipofika jikoni, hamaki, nikamkuta Zai akiwa anakunywa maji.
Mwanamke huyo alinitazama akaniuliza, "vipi, Mage? Kuna shida?"
Sikuelewa kitu.
Nilimsogelea nikamkagua mwili wake mzima kwa macho na vidol vyangu, alikuwa yu mzima mtupu, hana hata mchubuko, nikarudi koridoni upesi kwenda kwenye chumba cha Amiri.
Hapo nikagonga mara tatu na kuita, Amiri, Amiri!
Kimya.
Niliendelea kuita lakini Amiri hakuitika wala hakutoka ndani.
Bwana Mgaya akanisogelea na kunambia, Amiri yuko nje kitambo, ameshadamka kukamua maziwa.
Nikasema mwenyewe hapana, hapana, haiwezekani.
Akili yangu ikanambia sasa nielekee kule shambani tulipoupeleka mwili wa Zai kuufukia.
Niende huko nikatazame.
***
Thanks mkuu.Pita hapa boss
[emoji116]
Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida
Jirani Yangu wa kule Goba Hakuwa Mtu wa Kawaida. Sasa ni miaka miwili imepita, nimehamia na ninaishi kwengine, lakini yale ya kule Goba nayakumbuka vema kana kwamba yametokea jana yake, na huenda mambo hayo nikayakumbuka hata na milele maana ni moja ya visa ambavyo vilinishangaza sana. Mwaka...www.jamiiforums.com
Thanks a lot bossthe glassroof hii hapa
Soga kama hizi ulizoandika wewe😀Hii simulizi imekosa wazeee wa mizozo au wapiga soga unakuta uzi umetembea kwa kupiga umbea tu🤣😄
Karib ...humo ndio utamjua mtu m bad BIG😂Thanks mkuu.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Nimekaa hapa kuangalia uongo upo wapi katika story hii. Unapotunga uzingatie sana vigezo vya utungaji. Yaani usidanganye sana utaniudh. Mugaka anafahamu habari yangu vizuri na moderators. So nakutahadhalisha uwe makini na utulie sana.
Kuna namna fulan inamake sense,,,,kuna malalamiko kuwa wanachama wanasema unawacheleweshea story.. kama vipi kaa chini tunga maliza ndo uje upost kuliko kuwacheleweshea. tutaanza kugombana mimi na wewe. mimi nasimamia sana ustawi wa wasomaji. sipendi wawe na hasira au manung'uniko. kama umeshindwa kazi acha siyo kutaka waanze kukubembeleza. hadithi nyepesi kama hii unashindwaje itunga kwa haraka tu ukamaliza? angalia sana dogo usije sema mimi mbaya hakikisha kila siku unaleta episodes za kutosha.
NzuriSehemu ya Kumi na Mbili:
Yule alikuwa wa pili katika orodha.
Orodha hii ya vifo vitano, kila kifo na mkasa wake.
Nilivyopokea habari ya msiba wa Anwari, sasa ikanibidi nisitishe habari za kwenda kuonana na Zai kwaajili ya tiba yake kule kwa mama Miraji.
Nilichokifanya nilipiga simu kwa mama Miraji nikampa taarifa ya udhuru, sasa taarifa hii ikiwa ni ya pili kwa udhuru, kila tukiyapanga, mambo yanatibuka, mambo yanaibukia kasi ama kusi, yakiambatana na mawimbi yake.
Mama yule aliniambia basi hakuna tabu, tufanye tu siku nyingine lakini ni mpaka atakaponiambia maana ana safari karibuni akienda kwao Mtwara, mimi nikaona kheri.
Baada ya hapo, nilimtafuta Zai pia naye nikampa taarifa ya msiba, kweli akapokea taarifa hiyo kwa uchungu mrefu na mpana, akauliza ana nini ana nini, mbona kuandamwa na taarifa mbaya kila kukuchwa kwa jua?
Aliumia sana, Anwari kwake alikuwa zaidi ya shemeji tu, alikuwa ni mtu anayemkirimu na changamoto zake kila anapomuhitaji, hivyo kumpoteza haikuwa kama jani kuning'inia mtini tu, bali pengo kubwa lililoachwa kinywani kwa kuondolewa jino muhimu.
Nilimpa habari tukutane sehemu fulani ili tuongozane kwenda msibani, akaridhia, japo kwa kwikwi nyingi na mafua mepesi ya kilio, nilipomalizana naye nikaenda ofisini kutoa taarifa ya msiba huo, nikiomba udhuru wa siku kama mbili hivi kuhani na kukirimu msiba wa mtu wangu wa karibu.
Kwasababu ya urahisi, kukwepa maelezo mengi na taratibu lumbesa za kiofisi, nilienda moja kwa moja kuonana na meneja Salum.
Nilijua jambo hilo lingeleta utata kwa mkuu wa shule lakini kweli sikujali, mimi nilitaka kutimiza adhma ya kuharakisha shughuli yangu tu, hayo yaliyo kwenye makapu mengine sikuyatilia maanani wala sikutaka hata kuyachungulia.
Nilibisha hodi mara moja mbele ya mlango wa mkurugenzi kabla ya kuingia na kuwa na maongezi naye mafupi.
Nilimweleza haja yangu, haja ilonileta pale, naye akanieleza haja yake akinikumbushia mambo ambayo alinieleza kwenye makutano yetu ya mwisho.
Alisema, "mimi sina shida na hilo madam Magreth, take your time, shida mimi nilonayo unaifahamu na bado nangojea utatuzi wake."
Nikamwambia haina tabu, ngoja kwanza nikabiliane na hili lililopo mbele yangu kisha tutayaganga yanayokuja.
Hivyo tu, nikaondoka zangu kukutana na Zai kisha kiguu na njia mpaka nyumbani kwa Anwari. Huko tulikutana watu baadhi, watu wa karibu na bwana huyo marehemu, hawazidi kumi kwa idadi, wakatueleza yanayojiri na yalokwishajiri.
Mosi, mwili wa Anwari ulikuwa tayari hospitalini kwaajili ya hifadhi, pili, ratiba ya msiba katika siku hizo za maombolezo pale nyumbani, tatu, siku wanayoenda kuupumzisha mwili na utaratibu wake.
Mimi na bwana Adrian tulisonga kando kwaajili ya kupeana mawili matatu, ilinipasa kujongea huko na Zai lakini hali yake haikuwa nzuri, tangu nilipokutana naye na zaidi tulipofika eneo la msibani, hakuwa kwenye mandhari njema kabisa, alikuwa anahema juu juu akidai pia anaishiwa na nguvu mwilini.
Yote hayo ni sababu ya ugonjwa wake unaomsibu, ugonjwa wa presha ya kupanda ulopeleka moyo wake kutanuka.
Adrian alinieleza namna alivyomkuta Anwari pale nyumbani baada ya kumtafuta mara kadhaa kwenye simu pasipo kuzaa matunda.
Alipomkosa ndipo akatia shaka, shaka kwasababu ya yale yalotukia vile karibuni, na kwavile alikuwa akikatiza maeneo ambayo si mbali sana na makazi ya Anwari basi akaona ni vema sana apitie hapo kumjulia hali bwana huyo.
Kufika kuhamaki,
Pale sebuleni, juu ya makochi, bwana Anwari alikuwa amelala mfu. Mwili wake hausemi, mwili wake hausogei.
Mwili wake umedaka na kushika baridi, baridi la kifo.
Mkononi sindano iliyotoboa mwili wake inaning'inia. Sindano iliyomnyang'anya pumzi yake.
Alinambia baada ya siku ile, mimi na yeye kumkuta Anwari akiwa hajitambui sababu ya kujidunga madawa mwilini, aliweka nadhiri na bwana huyo, kule hospitalini, ya kwamba hatokaa akarejea tena kwenye ule uraibu.
Uraibu huo unamtesa.
Atatafuta namna nyingine ya kukabiliana na msongo wa mawazo na changamoto zake za maisha mbali na kuweka kemikali haribifu mwilini.
Kemikali ambazo zinampa ahueni ya masaa tu kisha anarejea tena, mikono nyuma, katika dimbwi lake la matatizo.
Lakini bado ... bado hakushinda pambano hilo.
Adrian aliniuliza kama nafahamu chochote kile kilichokuwa kinamsumbua Anwari kipindi hiko kifupi kabla ya umauti wake, mimi nikaapa sijui, kwanza sikuwa nawasiliana naye mara kwa mara tangu tuyavunje mahusiano yetu zama za pontio pilato.
Siku ile kunikuta pale nyumbani kwake ni kwasababu ya Zai tu, si kingine. Nilimwambia ni muda mrefu sana ulipita bila kuonana na bwana huyo.
Uongo uongo mtupu ...
Nayasema hayo lakini ndani yangu najua kweli yote na kweli hiyo inanisuta kifuani mwangu.
Lakini nifanyaje sasa? Ebu sema.
Nimwambie Adrian kuwa mimi ni miongoni mwa watu walomtia Anwari msongo wa mawazo kwa kumnyima kumwona mwanae?
Nani anataka kadhia hiyo? Anwari inabidi aende na siri hiyo kwenye kifua chake.
Kifua cha marehemu.
Kifua hicho hakihemi wala hakitoi maneno, nami nitabaki kuwa salama na familia yangu. Familia ambayo furaha yake imeanza kumea kwa mbolea ya kifo cha Mama mkwe.
Basi baada ya maongezi hayo na Adrian, tulirejea kuungana na wengine katika sakafu ya msiba, hapo tulikaa mpaka majira fulani ya jioni ndipo tukaondoka baada ya kushughulika na kukamilisha kila kitu pale msibani ikiwamo pia kupika chakula.
Keshokutwa yake, mapema tu, mwili wa Anwari ulifika pale nyumbani kwaajili ya kumuaga, siku hiyo watu walikuwa lukuki ukilinganisha na siku zingine, na siku hiyo, naikumbuka vema kabisa, mimi kuja kuisahau itaniwia ugumu kweli, nilikumbwa na matukio mawili matata, kila tukio na kijimambo chake.
Siku hiyo, Zai alizirai kama mara tatu hivi, yani kuona jeneza tu linaingia akazirai, kuona tena mwili kwenye kuaga, akazirai. Kuona jeneza linashuka ardhini, puh, akazirai tena.
Yani nilipata taabu kwelikweli maana niligeuka kuwa mtumishi wa msalaba mwekundu pale msibani, kuokota mtu na kupepea, kuokota mtu na kupepea.
Sijasahau siku ile,
Ndo' ilikuwa siku yangu niloweka shada langu la maua juu ya kaburi la Anwari, shada lililoandikwa kwa maneno makubwa meupe: RAFIKI.
Shada hilo nililiweka nikiongozana na watu kama wanne hivi, nao wakiwa wamebebelea ya kwao.
Lakini kubwa zaidi siku ile, mimi Magreth, nilijikuta napatwa na jaka kubwa la roho pale ndugu yake na Anwari aliposimama mbele ya waombolezaji kusoma wasifu ule wa marehemu.
Mimi sikuwa na shida na elimu ya Anwari, elimu iliyosomwa kwenye wasifu wake, wala sikuwa na shida na kazi yake aliyokufa huku akiifanya wala historia ya maisha yake aloyaishi, mimi nilishtuka tu pale msomaji aliposema marehemu Anwari ameacha mtoto mmoja wa kiume, tena mtoto huyo akitajwa na umri wake ambao unawiana vema na wa mwanangu.
Nikajiuliza haya ni masikio yangu ama ya jirani kaniazima tu kwa muda? Nilichosikia nimesikia ama nimeshikia? Sikuelewa.
Tokea hapo akili yangu ikawa kama imeacha mwili hivi, nipo hapo kwenye msiba kama kivuli, kichwani kuna mtafaruku wa mawazo na marejelea.
Baadae nilimuuliza Zai, tukiwa tunarejea kutoka maeneo ya mazishi, yule mtoto wa Anwari aliyetajwa pale kwenye wasifu anamfahamu? Zai akanambia hamjui, nami nikaona nisimsumbue sana maana hakuwa katika hali nzuri, ila mimi ndani yangu nilikosa raha kweli.
Nilienda nyumbani na niliishi na mawazo hayo siku nzima, kuna muda nilikuwa napata maruweruwe kabisa nahisi kuna watu wanabisha hodi lakini nikitazama simwoni mtu.
Bwana Mgaya alinikuta katika hali hiyo, hali ya sintofahamu, akahisi nipo katika maombolezo ya kumpoteza rafiki, akae asijue namwaza baba wa mtoto tuliye naye ndani.
Mambo mengine ni kheri yakabakia kizani milele, inabidi yawe hivyo kama gharama ya kudumisha amani. Si kila kitu cha kufahamu, Mgaya, na sijali nitatembea kilomita ngapi kukufanya usijue hili, mimi niko radhi na moyo wangu wote.
Basi usiku huo, nilimpigia Zai kumuuliza hali yake, aliponieleza nikamuuliza tena kuhusu mtoto yule, yule aliyetajwa kwenye wasifu, je, amjua? Zai akakataa kwa mara nyingine, hamjui mtoto huyo, ila hapa akaniuliza mbona nataka sana kufahamu hilo, sikumjibu cha maana tukahitimisha maongezi yetu.
Siku iliyofuata niliripoti kazini kama kawaida, lakini kabla sijaanza majukumu yangu, mwalimu mkuu alinita ofisini kwake, kwenda ananiuliza nilikuwa wapi siku zile za kazi na ingali sikupata ruhusa?
Nilipomwambia meneja alinipatia ruhusa hiyo nikawa nimetia chumvi kwenye jeraha bichi, aliniwakia na kunimwagia maneno kweli kweli kiasi kwamba nikashangaa, katika maneno yote hayo, hili nililishika zaidi.
Alinambia: "nitakuonyesha kati yako na mimi nani alimkuta mwenziwe hapa, na n'takuonyesha nani ni mkuu wa shule hapa!"
Mie baada ya kushindiliwa maneno hayo nikaenda zangu, wala sikurudisha hata nukta, nikaendelea na majukumu yangu mpaka jioni nilipofunga na kurejea nyumbani pamoja na mwanangu.
Kesho ama keshokutwa yake, Zai alinipigia simu kunambia ana shida ya kuonana na mimi, shida ya dharura, kama nikipata muda basi nifanye kuonana naye kesho yake baada ya kutoka kazini.
Kweli nikafanya hivyo, nilimtafuta mara moja baada ya kumaliza kazi zangu, tukakutana mgahawa fulani ambapo mimi nilisimamia kila kitu kwasababu hali ya Zai kiukweli haikuwa nzuri, sio tu kiafya bali pia kifedha.
Pesa zake za akiba alikuwa amezimaliza kwenye matibabu alafu kurudi kazini anafukuzwa, na mpaka muda huo tunakutana, hakuwa amepata ajira popote pale, bado alikuwa anabangaiza.
Hata kula yake tu ilikuwa mushkeli.
Siku hiyo tuliongea mambo kadhaa, yote muhimu, kuanzia utafutaji wake wa ajira akinisihi nimsaidie kutafuta fursa, pia hali yake ya afya ilivyokuwa muda huo, na vilevile habari za ndugu yake kule anapoishi mpaka kufikia kwenye kitovu cha wito wake ambao ulimsukuma yeye kuniita pale.
Alinambia, siku hiyo mapema asubuhi, mama yake Anwari alimpigia simu akimtaka waonane mahali fulani siku za usoni kwani ana mambo machache wanataka kuzungumza.
Hajui mama huyo alitoa wapi namba yake na kwanini amemtafuta lakini yeye anahisi jambo hilo ni muhimu kunishirikisha, na swala lililomfanya akahisi kuna ulazima huo ni kitendo cha mama huyo kumwambia swala lake hilo ni nyeti sana na endapo akimsaidia basi bila hiyana atamkabidhi donge nono la pesa.
Sasa swala hilo ni lipi? Linamhusu vipi marehemu Anwari? Na lina mahusiano gani na yeye? Hapo hakutambua.
Mimi aliponieleza hayo, moja kwa moja kichwani mwangu nilona sasa ni muda mwafaka wa kumsogeza Zai karibu zaidi na mimi.
Nilianza kuamini umbali wetu unaweza geuka kuwa silaha ya kuangamiza uhai wa familia yangu, kwahiyo basi nillitumia mwamvuli wa ugonjwa wake, ukata unaomkumba kwa muda huo na hitilafu iliyopo baina yake na ndugu yake kumshawishi kuja kwenye makazi yangu na swala hilo likafaulu vema.
Kuhusu habari ya kumweleza mume wangu, bwana Mgaya, kamwe haikuwahi kunipa shida, upendo wake na uaminifu wake kwangu ulikuwa ni nyenzo yangu muhimu, na mimi niliitumia ipasavyo kwenye kukamilisha lengo langu.
Kwahiyo,
Siku ya siku Zai akahamia nyumbani kwangu, chumba chake kilekile alichokuwa analalia mama mkwe wangu, chumba cha wageni.
Hivyo,
Mimi nikawa nimenasa kwenye mtego wake wa uongo na unafiki, na yeye akajikuta amenasa kwenye kwenye mtego wangu wa kifo.
Kifo kile cha Zai kikiwa ndo' kifo kilichoniweka matatani zaidi kuliko vifo vingine vyote.
Kama vidole na macho vingekuwa vinaua basi nisingeishi kuja kuhadithia kisa hiki hapa.
****