Ulimbo
JF-Expert Member
- Aug 14, 2009
- 3,768
- 4,038
Niliamua kulima mwaka huu karanga nilipata fununu Kua karanga Zina pesa ndefu.. Tayari karanga zimekomaa nikafanya harakati za kuzivuna namshukuru Mungu zilikubali Sana nilipata debe 21 sawa na magunia 3
Nikaanza kuingia mtaani kusaka wateja unaenda anakumbia kaniletee MI najikaza narudi naenda beba namletea dah debe limejaa Adi kumwagika jamaa anasema bado tena anazinyambua kama mawe dah iliniuma Sana na anakuambia kama hujazi silipi inakubidi uende tena ukalete zingine uje kujazia khaa! Hapo na maneno ya ajabu utahisi anaongea na mtoto wake
Mteja mwingine anakuja kununua anataka nichague hataki zisizokomaa yani nikawaza huyu jamaa angejua ugumu wa kulima huyu!..
Mwingine nikajichanganya kumuachia debe mbili 1 alilipa 1 akasema Adi badae dah naenda badae namkuta binti yake eti yeye amesafiri atarudi Kesho nilichoka Sana nikawaza aisee mbona hali huku mtaani iko hivi?
Kuna umuhimu wa kuajiriwa tuheshimiane Sasa!
Sasa kwenye hiyo biashara mbona sijaona application ya vyeti? Hiyo ni biashara tu na si kumba wanakunyanyasa heti kwa sababu wana dhani ujasoma.