Niliyoyashuhudia Jeshini

Niliyoyashuhudia Jeshini

SEHEMU YA 8
Nikafanikiwa kutoroka hadi jikoni, kule maeneo mengi giza ndo maana sikubambwa
Nikanunua maandazi nikanywa na chai haraka, sasa nikawa naona kuruta wanakimbia wameruhusiwa kwenda kulala
Sasa nikawa nasuuza kikombe fasta na mimi nikalale

Kwa mbali namuona bakabaka anakuja na service man ( wanaojitolea) wetu
Basi service man akasema "Ephen mwenyewe yule pale" moyo ulishtuka ukaenda kasi sana

Nilipokea mvua ya matusi kutoka kwa yule bakabaka halafu mwanamke "Wenzako wapo kombania wewe huku unafanya nini? Nikaongezewa bao la mgongo
"Kuruta naongea unanitizama badala ya kupunguza urefu?'
"Punguza urefu haraka!"
Basi nikachuchumaa ndo kupunguza urefu.

Pembeni kulikua na bomba la maji nikapelekwa pale yakafunguliwa nikaloa chapachapa
"Aya roll uelekeo kombania"
Ilikua ngumu kwangu njia ya kuroll ina kokoto, mimi nina kidonda kibichi gotini kinaniuma na nimefungwa bandage.

"Afande naomba unibadilishie adhabu nina kidonda kibichi"
kuruta unanidindia?
Nikaona huyu anataka kukuza mambo! Nikaanza kuroll goti maumivu kama yote damu zikaanza kutoka na afande hanionei huruma

Kulikua na umbali hadi kombania ila nikafika!
Wenzangu walivyoniona wakaanza kunisonya wanalalamika.
Kombania zipo A hadi D kama sijakosea, A, C na D wakaruhusiwa kwenda kulala muda mrefu tu.
Na kombania B wanaume waliruhusiwa pia kasoro wasichana ndo hawakuruhusiwa sababu hawakutimia
Nani hakutimia ni mimi hapa.

Jeshini ikitokea kuruta ametoroka kwenye kombania hamuendi kulala hadi apatikane.
Muda huo saa 7 usiku damu zinatoka gotini maumivu hadi nalia.

"Sasa sikieni! Leo mnakesha na mimi hapa! mpaka asubuhi!
Nyie si hamjaiva, mlimtuma mwenzenu akanywe chai muda wa kombania haya wote kichurachura mnaenda na kurudi hadi kukuche, Wazii kuruta?

Kuruta wenzangu wakaanza kulia "Afande sisi hatujamtuma! Tunaomba tukalale"

Nauliza tena "Wazii kuruta?"
Tukaitikia waziii Afande!
Huku wenzangu wananitukana nimewaponza hawaendi kula utawala (kula utawala- kupumzika)

Bakabaka sasa "Kila mtu akachukue ndoo ya maji mje kumwaga hapa na poda ya kutosha mje mumpake usoni" (Poda-Vumbi)
Nililia sana basi wakaenda kuchukua poda wakanipaka, maji yakamwagwa kwenye vumbi kukawa na tope nikaambiwa,
"Wewe siumekuja hapa kula! Aya twende kama kambare"
Nikaanza kuroll kwenye tope.

Yule afande alikua na roho ngumu sanaaa
"Aya kuruta simama hapo uanze kupiga makofi wao wanafatisha"

Nikaanza nikipiga kofi wanasimama nikipiga wanalala chini! Ngoma ilienda hadi afande akasema nasimama pale nyie endeleeni!

Kumbe aliondoka sisi tukaendelea tukidhani anatuangalia, tumeshtuliwa na filimbi ya alfajiri

Tulikesha tena na wenzangu!!
Walinichukia! siku hio nikawa na kazi ya kuwaomba msamaha. Niliwafanya wasilale tena kwa usiku mwingine ukijumlisha na siku 7 za mwanzo.

Itaendelea.......

Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini
 
Ni kudeka.

Mtu anadeka kwa anaemdekeza, ndio maana kuna msemo kua "yatima hadeki" hiyo ni kwakua mdekezaji anakua hayupo.

Huoni kuna watoto akiwepo mama/baba yake analilia kila kitu basi tu apewe attention.
Hakika,, kuna vitoto viko hivyo. Lakini binafsi siioni katika kudeka, sijui ni mazoea ya makuzi.
Mfano mdogo, nimekulia kwenye nyumba ambayo haina ndoo za lita 20. Ni tank, majaba na vindoo vya lt 10.

Nimemaliza heka heka za kusoma, nikapata tempo mkoani. Mshua akagoma nisitoke nyumbani kwenda kuishi mwenyewe ama laa niende huo mkoa nikakae kwa ndugu flani, nikakubali kwenda kwa huyo ndugu.

Hilo eneo nikakuta maji kukatika week nzima ni kawaida tu na hawana tank. Wana madumu na mandoo kibao ya Lt20, mimi siwezi kuyabeba.. yule mtu anapiga simu home kunisemelea kwamba najifanyisha. Home wananitetea kidizain aendelee kunizoesha kidogo kidogo.

So hapo napo ni kudeka? Hapana ni mazoea ya makuzi.
Nachukia kuumwa, ile moment mwili unakuwa unconfortable uwa siipendi. So najikuta ndio nimeshalia.

Mazoea ya kusindikizana pia, sijui umeagizwa wapi unaenda na mdogo wako, ama unaenda wapi umeenda na mama. Haya yalinifikia mpaka huku utu uzimani.. nikitoka job imetokea ninaondoka mwenyewe, nashindwa kutembea mwenyewe, naangalia contact list nimpigie nani mpk nifike stand.

kuna mtu humu anaitwa Lenie, nimemsumbua sana. Nikitoka nampigia tustorike mpaka navyopanda hiace. 😂

So ni mazoea na sio madeko… mtoto kamzoea baba ake, akimuona lazima amgande gande. Nyie ndo mnaona madeko? Hapana 😂😂😂
 
BONUS
Mwanzoni wiki 6 mjeda namesake alinifata kuniaga, kwa kumwangalia hakua sawa kama amelia muda mrefu.

"Mimi naondoka kwaheri"
Sababu gani nikamuuliza
"Kuna nafasi za kwenda course ya kuajiriwa migration zilitoka, nikapata nafasi, lakini nimepimwa nina mimba hivyo safari yangu imeishia hapa"

NIlimuonea huruma katika kumchimba ndo nikagundua
Alipata mimba ya yule bakabaka yeye akawa anaficha, nafasi zilivyotoka jina lake lipo ilibidi amwambie mchumba ake.

Bakabaka akamwambia unaitoa ili upate nafasi ya kwenda mafunzoni au unabaki nayo?
Yeye akachagua kubaki nayo akose jeshi!
Alikua ameshajitolea zaidi ya miaka miwili.

Nilimuonea huruma, nilimuona ana moyo mzuri sana! Mwingine angeitoa ili akamilishe ndoto yake ya kua mwanajeshi.

Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini
 
BONUS
Mwanzoni wiki 6 mjeda namesake alinifata kuniaga, kwa kumwangalia hakua sawa kama amelia muda mrefu.

"Mimi naondoka kwaheri"
Sababu gani nikamuuliza
"Kuna nafasi za kwenda course ya kuajiriwa migration zilitoka, nikapata nafasi, lakini nimepimwa nina mimba hivyo safari yangu imeishia hapa"

NIlimuonea huruma katika kumchimba ndo nikagundua
Alipata mimba ya yule bakabaka yeye akawa anaficha, nafasi zilivyotoka jina lake lipo ilibidi amwambie mchumba ake.

Bakabaka akamwambia unaitoa ili upate nafasi ya kwenda mafunzoni au unabaki nayo?
Yeye akachagua kubaki nayo akose jeshi!
Alikua ameshajitolea zaidi ya miaka miwili.

Nilimuonea huruma, nilimuona ana moyo mzuri sana! Mwingine angeitoa ili akamilishe ndoto yake ya kua mwanajeshi.
Bakabaka hayuko serious
Kamwaribia mwenzake… kwani box la condom sh ngapi?

Yan ni sawa makuruti mpendanee.. mapenzi moto moto, mmoja amwambie mwenzake nichore tattoo ya jina langu wakati anajua fika tattoo haziruhusiwi.
 
Kwa jinsi nilivyosoma uzi wake mpaka hapa unacomment huyu sio mwanaume ni mwanamke! Soma vizuri mkuu, hadi anasema Kuna mwanajeshi wa kike aliyemuonea huruma wanafanana majina.
kuna shida kubwa mno ya uelewa kwa watu wengi. Hasa kwa kizazi cha 2000. Kina access kubwa ya maarifa, ila uelewa ni mdogo sana. Sijui shida nini.
 
[emoji445]Nasikia raha utamu, Tena raha utamuuuuu....

Weeeh! Siku ya kwanza alisemaje, Mama Naumiaaaaa.....

Siku ya pili akasemaje, Mdogomdogo inaingiaaaaa.....

Siku ya tatu akasemaje, Lini utarudiaaaa....

Siku ya nne akasemaje, Nasikia raha utamuuuuu....

Jamani raha utamuuuuu.....[emoji445]
 
Nimekumbuka Oljoro JKT tulikuwa tukijongo Ijumaa tunatokea Unga Ltd na kurudi Jumapili na tunaanzia mahabusu.Mara zingine tunatoroka kwa kutumia magari ya mkaa kupitia Olasiti.Nilikaa kambini kwa mujibu wa sheria miezi 6 ya ukuruta na kuhamia Mgambo kumalizia miezi 6.Maisha mazuri hasa.
unapakumbuka mnadani...!

unaukumbuka ugomvi wa wamasai na askari...!
 
Back
Top Bottom