ephen_
JF-Expert Member
- Oct 28, 2022
- 14,949
- 54,485
- Thread starter
- #401
SEHEMU YA 8
Nikafanikiwa kutoroka hadi jikoni, kule maeneo mengi giza ndo maana sikubambwa
Nikanunua maandazi nikanywa na chai haraka, sasa nikawa naona kuruta wanakimbia wameruhusiwa kwenda kulala
Sasa nikawa nasuuza kikombe fasta na mimi nikalale
Kwa mbali namuona bakabaka anakuja na service man ( wanaojitolea) wetu
Basi service man akasema "Ephen mwenyewe yule pale" moyo ulishtuka ukaenda kasi sana
Nilipokea mvua ya matusi kutoka kwa yule bakabaka halafu mwanamke "Wenzako wapo kombania wewe huku unafanya nini? Nikaongezewa bao la mgongo
"Kuruta naongea unanitizama badala ya kupunguza urefu?'
"Punguza urefu haraka!"
Basi nikachuchumaa ndo kupunguza urefu.
Pembeni kulikua na bomba la maji nikapelekwa pale yakafunguliwa nikaloa chapachapa
"Aya roll uelekeo kombania"
Ilikua ngumu kwangu njia ya kuroll ina kokoto, mimi nina kidonda kibichi gotini kinaniuma na nimefungwa bandage.
"Afande naomba unibadilishie adhabu nina kidonda kibichi"
kuruta unanidindia?
Nikaona huyu anataka kukuza mambo! Nikaanza kuroll goti maumivu kama yote damu zikaanza kutoka na afande hanionei huruma
Kulikua na umbali hadi kombania ila nikafika!
Wenzangu walivyoniona wakaanza kunisonya wanalalamika.
Kombania zipo A hadi D kama sijakosea, A, C na D wakaruhusiwa kwenda kulala muda mrefu tu.
Na kombania B wanaume waliruhusiwa pia kasoro wasichana ndo hawakuruhusiwa sababu hawakutimia
Nani hakutimia ni mimi hapa.
Jeshini ikitokea kuruta ametoroka kwenye kombania hamuendi kulala hadi apatikane.
Muda huo saa 7 usiku damu zinatoka gotini maumivu hadi nalia.
"Sasa sikieni! Leo mnakesha na mimi hapa! mpaka asubuhi!
Nyie si hamjaiva, mlimtuma mwenzenu akanywe chai muda wa kombania haya wote kichurachura mnaenda na kurudi hadi kukuche, Wazii kuruta?
Kuruta wenzangu wakaanza kulia "Afande sisi hatujamtuma! Tunaomba tukalale"
Nauliza tena "Wazii kuruta?"
Tukaitikia waziii Afande!
Huku wenzangu wananitukana nimewaponza hawaendi kula utawala (kula utawala- kupumzika)
Bakabaka sasa "Kila mtu akachukue ndoo ya maji mje kumwaga hapa na poda ya kutosha mje mumpake usoni" (Poda-Vumbi)
Nililia sana basi wakaenda kuchukua poda wakanipaka, maji yakamwagwa kwenye vumbi kukawa na tope nikaambiwa,
"Wewe siumekuja hapa kula! Aya twende kama kambare"
Nikaanza kuroll kwenye tope.
Yule afande alikua na roho ngumu sanaaa
"Aya kuruta simama hapo uanze kupiga makofi wao wanafatisha"
Nikaanza nikipiga kofi wanasimama nikipiga wanalala chini! Ngoma ilienda hadi afande akasema nasimama pale nyie endeleeni!
Kumbe aliondoka sisi tukaendelea tukidhani anatuangalia, tumeshtuliwa na filimbi ya alfajiri
Tulikesha tena na wenzangu!!
Walinichukia! siku hio nikawa na kazi ya kuwaomba msamaha. Niliwafanya wasilale tena kwa usiku mwingine ukijumlisha na siku 7 za mwanzo.
Itaendelea.......
Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini
Nikafanikiwa kutoroka hadi jikoni, kule maeneo mengi giza ndo maana sikubambwa
Nikanunua maandazi nikanywa na chai haraka, sasa nikawa naona kuruta wanakimbia wameruhusiwa kwenda kulala
Sasa nikawa nasuuza kikombe fasta na mimi nikalale
Kwa mbali namuona bakabaka anakuja na service man ( wanaojitolea) wetu
Basi service man akasema "Ephen mwenyewe yule pale" moyo ulishtuka ukaenda kasi sana
Nilipokea mvua ya matusi kutoka kwa yule bakabaka halafu mwanamke "Wenzako wapo kombania wewe huku unafanya nini? Nikaongezewa bao la mgongo
"Kuruta naongea unanitizama badala ya kupunguza urefu?'
"Punguza urefu haraka!"
Basi nikachuchumaa ndo kupunguza urefu.
Pembeni kulikua na bomba la maji nikapelekwa pale yakafunguliwa nikaloa chapachapa
"Aya roll uelekeo kombania"
Ilikua ngumu kwangu njia ya kuroll ina kokoto, mimi nina kidonda kibichi gotini kinaniuma na nimefungwa bandage.
"Afande naomba unibadilishie adhabu nina kidonda kibichi"
kuruta unanidindia?
Nikaona huyu anataka kukuza mambo! Nikaanza kuroll goti maumivu kama yote damu zikaanza kutoka na afande hanionei huruma
Kulikua na umbali hadi kombania ila nikafika!
Wenzangu walivyoniona wakaanza kunisonya wanalalamika.
Kombania zipo A hadi D kama sijakosea, A, C na D wakaruhusiwa kwenda kulala muda mrefu tu.
Na kombania B wanaume waliruhusiwa pia kasoro wasichana ndo hawakuruhusiwa sababu hawakutimia
Nani hakutimia ni mimi hapa.
Jeshini ikitokea kuruta ametoroka kwenye kombania hamuendi kulala hadi apatikane.
Muda huo saa 7 usiku damu zinatoka gotini maumivu hadi nalia.
"Sasa sikieni! Leo mnakesha na mimi hapa! mpaka asubuhi!
Nyie si hamjaiva, mlimtuma mwenzenu akanywe chai muda wa kombania haya wote kichurachura mnaenda na kurudi hadi kukuche, Wazii kuruta?
Kuruta wenzangu wakaanza kulia "Afande sisi hatujamtuma! Tunaomba tukalale"
Nauliza tena "Wazii kuruta?"
Tukaitikia waziii Afande!
Huku wenzangu wananitukana nimewaponza hawaendi kula utawala (kula utawala- kupumzika)
Bakabaka sasa "Kila mtu akachukue ndoo ya maji mje kumwaga hapa na poda ya kutosha mje mumpake usoni" (Poda-Vumbi)
Nililia sana basi wakaenda kuchukua poda wakanipaka, maji yakamwagwa kwenye vumbi kukawa na tope nikaambiwa,
"Wewe siumekuja hapa kula! Aya twende kama kambare"
Nikaanza kuroll kwenye tope.
Yule afande alikua na roho ngumu sanaaa
"Aya kuruta simama hapo uanze kupiga makofi wao wanafatisha"
Nikaanza nikipiga kofi wanasimama nikipiga wanalala chini! Ngoma ilienda hadi afande akasema nasimama pale nyie endeleeni!
Kumbe aliondoka sisi tukaendelea tukidhani anatuangalia, tumeshtuliwa na filimbi ya alfajiri
Tulikesha tena na wenzangu!!
Walinichukia! siku hio nikawa na kazi ya kuwaomba msamaha. Niliwafanya wasilale tena kwa usiku mwingine ukijumlisha na siku 7 za mwanzo.
Itaendelea.......
Muendelezo soma Niliyoyashuhudia Jeshini