Hussein J Mahenga
JF-Expert Member
- Mar 5, 2012
- 750
- 656
Ngongo,Huyu ni Mgalatia Sheikh Mohamed Said hana muda nao.
Denis Phombeah alikuwa Meneja wa Ukumbi wa Arnautoglu.Enhee, sasa tuendelee nayo, Sheikh!
Habari wako ndugu yangu Mohamed Said,Denis Phombeah alikuwa Meneja wa Ukumbi wa Arnautoglu.
Ukumbi wa Atnautoglo uijengwa na Mgiriki George Arnautoglu.
Denis Phombeah alichukua nafasi hiyo kutoka kwa Chihota ambae alifariki Uingereza mwaka wa 1952.
Sikupata kulijua jina la kwanza la Mzee Chihota ingawa wanae nilifahamiananao.
Chihota alikuwa amekuja Tanganyika akitokea Southern Rhodesia (Zimbabwe) kuja kutafuta maisha Tanganyika.
Denis Phombeah alikuwa akipenda kula maisha na ile kazi yake ya kuwa meneja Arnautoglo ilimwenea vyema sana kwa kuwa kila Jumamosi Arnautoglo palikuwa pakipigwa dansi.
Ukumbi wa Arnautoglo ilikuwa haingii mtu dansini sharti awe amefunga tai.
George Arnautoglo alikuwa mtu tajiri sana katika nyakati zlle na mal yake alichuma yote Tanganyika.
Kwa kuonyesha shukurai kwa wananchi wa Tanganyika akajenga huo ukumbi kwa ajili ya Waafrika wawe na mahali ambapo wataweza kufanya shughuli zao na vilevile pawe mahali pa buruduani.
Lakini kikubwa alichokuwa kakiweka rohoni kwake ni kuwa George Arnautoglu akiwachukia Waingereza na alipata kuwapa fedha TANU kwa siri ziwasaidie katika shughuli zao za kudai uhuru.
Hili alinieleza Ali Mwinyi Tambwe ambae yeye ndiye aliyepokea fedha hizo.
Denis Phombeah kama walivyokuwa vijana wote wa nyakati zile walikuwa wanachama wa TAA.
TAA ilikuwa na wanachama ambao hawakuwa Watanganyika ilimuradi ni Mwafrika aliweza kujiunga na TAA.
Labda kama si kwa Denis Phombeah kujitokeza kumfanyia kampeni Julius Nyerere katika uchaguzi wa mwaka wa 1953 Nyerere alipogombea nafasi ya President wa TAA dhidi ya Abdul Sykes na historia hii yake ikaandikwa katika kitabu cha kwanza kueleza historia ya TANU pamoja na safari yake na Ally Sykes kwenda Salisbury, Southern Rhodesia kuiwakilisha Tanganyika katika mkutano ulioitishwa na Kenneth Kaunda, Phombeah asingekuwa sehemu ya historia ya uhuru wa Tanganyika.
Historia hii ipo kwa ufupi sana katika kitabu cha Judith Listowel, ''The Making of Tanganyika,'' (1965).
Historia hii nilikuja kuiandika kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes, ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924-1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika,'' (1998).
Niliweza kukieleza kisa chote kwa uhakika kwa kuwa Ally Sykes alinifungulia nyaraka za familia yao katika historia ya TAA/TANU na katika nyaraka hizi nikakuta nakala ya magazeti ya zamani yakieleza mkasa uliowafika Ally Sykes na Denis Phombeah, Salisbury wakiwa njiani kwenda Lusaka, Northern Rhodesia kuhudhuria mkutano uliokusudia kuwakutanisha wapigania uhuru wa nchi za Kiafrika chini ya Jangwa la Sahara.
Lakini kubwa ni kuwa Ally Sykes mwenyewe alinihadithia mkasa huu.
Mazungumza yangu yote na Ally Sykes yalikuwa kwenye cassette na tatizo la cassette ni shida kutunzika.
Ingekuwa starehe sana leo kama ningekuwekeeani audio clip mkamsika Ally Sykes na ile sauti yake ya kukwaruza kikuhadithieni historia yake na urafiki wake na Kenneth David kaunda.
Nimebahatika kusoma barua alizokuwa akiandikiana na Kaunda katika miaka ile ya 1950s.
Itaendelea In Shaa Allah...
Mr. Mzumbe,Habari wako ndugu yangu Mohamed Said,
Naomba unifahamishe, huu ukumbi wa Atnautoglo upo wapi huu kwasasa ? Au ndio atnautoglo uliopo karibu na hospital ya mnazi mmoja?
MashAllah,Denis Phombeah alikuwa Meneja wa Ukumbi wa Arnautoglu.
Ukumbi wa Atnautoglu ulijengwa na Mgiriki George Arnautoglu.
Denis Phombeah alichukua nafasi hiyo kutoka kwa Chihota ambae alifariki Uingereza mwaka wa 1952.
Sikupata kulijua jina la kwanza la Mzee Chihota ingawa wanae Raymond na Gershom nilifahamiananao.
Chihota alikuwa amekuja Tanganyika akitokea Southern Rhodesia (Zimbabwe) kuja kutafuta maisha Tanganyika.
Denis Phombeah alikuwa akipenda kula maisha na ile kazi yake ya kuwa meneja Arnautoglu Hall ilimwenea vyema sana kwa kuwa kila Jumamosi Arnautoglu palikuwa pakipigwa dansi.
Ukumbi wa Arnautoglu ilikuwa haingii mtu dansini sharti awe amefunga tai.
George Arnautoglu alikuwa mtu tajiri sana katika nyakati zlle na mal yake alichuma yote Tanganyika.
Kwa kuonyesha shukurai kwa wananchi wa Tanganyika akajenga huo ukumbi kwa ajili ya Waafrika wawe na mahali ambapo wataweza kufanya shughuli zao na vilevile pawe mahali pa buruduani.
Lakini kikubwa alichokuwa kakiweka rohoni kwake ni kuwa George Arnautoglu akiwachukia Waingereza na alipata kuwapa fedha TANU kwa siri ziwasaidie katika shughuli zao za kudai uhuru.
Hili alinieleza Ali Mwinyi Tambwe ambae yeye ndiye aliyepokea fedha hizo.
Denis Phombeah kama walivyokuwa vijana wote wa nyakati zile alikuwa mwanachama wa TAA.
TAA ilikuwa na wanachama ambao hawakuwa Watanganyika ilimuradi ni Mwafrika aliweza kujiunga na TAA.
Wakati waukoloni hii mipaka haikuwa na maana yoyote na ndiyo ilikuwa rahisi sana kwa wananchi wa nchi jirani kuingia nchi nyingine kutafuta kazi.
Labda kama si kwa Denis Phombeah kujitokeza kumfanyia kampeni Julius Nyerere katika uchaguzi wa mwaka wa 1953 Nyerere alipogombea nafasi ya President wa TAA dhidi ya Abdul Sykes na historia hii yake ikaandikwa katika kitabu cha kwanza kueleza historia ya TANU pamoja na safari yake na Ally Sykes kwenda Salisbury, Southern Rhodesia kuiwakilisha Tanganyika katika mkutano ulioitishwa na Kenneth Kaunda, Phombeah asingekuwa sehemu ya historia ya uhuru wa Tanganyika.
Uchaguzi huu ulifanyika Ukumbi wa Arnautoglu mwezi April, 1953.
Ajabu kubwa katika historia ya Julius Nyerere ni kuwa juu ya kuwa hili lilikuwa tukio kubwa sana katika maisha yake na ndilo liilomtia katika uongozi wa TAA kisha TANU hakupata hata siku moja kufungua kinywa chake kulizungumza.
Historia ya Denis Phombeah ipo kwa ufupi sana katika kitabu cha Judith Listowel, ''The Making of Tanganyika,'' (1965).
Historia hii nilikuja kuiandika kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes, ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924-1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika,'' (1998).
Niliweza kukieleza kisa chote kwa uhakika kwa kuwa Ally Sykes alinifungulia nyaraka za familia yao katika historia ya TAA/TANU na katika nyaraka hizi nikakuta nakala za magazeti ya zamani yakieleza mkasa uliowafika Ally Sykes na Denis Phombeah, Salisbury wakiwa njiani kwenda Lusaka, Northern Rhodesia kuhudhuria mkutano uliokusudia kuwakutanisha wapigania uhuru wa nchi za Kiafrika chini ya Jangwa la Sahara.
Lakini kubwa ni kuwa Ally Sykes mwenyewe alinihadithia mkasa huu.
Mazungumza yangu yote na Ally Sykes yalikuwa kwenye cassette na tatizo la cassette ni shida kutunzika.
Mikanda hii yote imepotea.
Ingekuwa starehe sana leo kama ningekuwekeeni ''audio clip'' mkamsika Ally Sykes na ile sauti yake ya kukwaruza akikuhadithieni habari za Denis Phombeah na historia yake na Kenneth David Kaunda.
Nimebahatika kusoma barua walizokuwa wakiandikiana miaka ile ya 1950s.
Itaendelea In Shaa Allah...
Shida ya huyu mzee amejawa udini na chuki dhidi ya wagalatia wa Tanganyika..ila akiondoa huo udini ni mzee maenye kontent.Mzee wangu Mohamed Said ninauhakika kwa nondo unazoziandika humu hata wale wanaokuchukia katika mioyo yao wanakukubali
Sent from my TECNO-L8 using JamiiForums mobile app
Ndio huu huu mkuu hata picha inajioneshaHabari wako ndugu yangu Mohamed Said,
Naomba unifahamishe, huu ukumbi wa Atnautoglo upo wapi huu kwasasa ? Au ndio atnautoglo uliopo karibu na hospital ya mnazi mmoja?
Mdukuzi,Huyu Phombeah alikuwa special branch wa waingereza kabla ya uhuru,hilo linajulikana mbona
wanaccm utawaweza wapenda Sana uwongo uhalisia hawautaki inaboa SanaMzee wangu Mohamed Said ninauhakika kwa nondo unazoziandika humu hata wale wanaokuchukia katika mioyo yao wanakukubali
Sent from my TECNO-L8 using JamiiForums mobile app
Hivi unafahamu kwann mufti wa Tanzania ikulu anashinda kuliko kiongozi wadini yeyote Tanzania kwa awamu zote......acheni umbululaShida ya huyu mzee amejawa udini na chuki dhidi ya wagalatia wa Tanganyika..ila akiondoa huo udini ni mzee maenye kontent.
Ona hata hii stori mgalatia wa Tanganyika mpaka ameombwa aandike ila anayo kaiminya tu yawezekana azipo nyingi za wagalatia kama hao ila kaziminya kwa sababu zake za udini.
Hapa ndio kinatufanya wengi tumpuuze na kumuona hafai.
#MaendeleoHayanaChama
Jiwe...Shida ya huyu mzee amejawa udini na chuki dhidi ya wagalatia wa Tanganyika..ila akiondoa huo udini ni mzee maenye kontent.
Ona hata hii stori mgalatia wa Tanganyika mpaka ameombwa aandike ila anayo kaiminya tu yawezekana azipo nyingi za wagalatia kama hao ila kaziminya kwa sababu zake za udini.
Hapa ndio kinatufanya wengi tumpuuze na kumuona hafai.
#MaendeleoHayanaChama
Mzee wangu Mungu akujaalie siha njema na busara kubwa, hakika tunanufaika na darsa zako!Jiwe...
Napenda sana hii, "Huyu mzee.''
Unasema nina, "Udini na chuki."
Unasahau kuwa historia ya uhuru kwa kuwa ni historia iloyojaa wazalendo wengi Waislam ilifanyiwa hujuma na watu ambao si Waislam.
Wewe huijui historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika lakini huna subra ya kuuliza unakuja hapa unanishambulia.
Denis Phombeah nimeandika historia yake katika kitabu Cha Abdul Sykes (1998).
Sijui una lipi la kusema?
Nasubiri jibu lako.
Sijapata kupuuzwa hata siku moja kwa kalamu yangu.
Kalamu yangu imeniingiza katika vyuo vingi kuzungumza.
Au hujui?
Fanya utafiti utaujua ukweli.
Unasema unanipuuza halafu uko hapa na mimi darsani kwangu?