Nimeamkaa saa saba usiku kujisaidia haja ndogo nimesikia vishindo kama vya mtu anayezunguka nyumba yetu!

Vitu vidogo sana hivyo, nilishawahi kusikia kiumbe kinalia dirishani na kukwaruza dirisha Kwa kucha huku juu ya bati Kuna vishindo na mchanga unamwaga huko huko juu ya bati na niliendelea kulala safi tu japo waliniamsha usingizini...haya mambo yahitaji roho ya chuma.
 
Badala utoke nje ukaangalie ni nini we unaenda kujifunika blanket alafu ukute ndo mtoto wakiume unaetegemewa
 

😁😁😁
 
kwani siku hizi hamlali na filimbi ndani? au anza kupiga ngoma au ndoo huku ukioiga kelele za kuomba msaada majirani wakusikie. au tuma taarifa kwenye whatsapp group lenu hapo mtaani.
 
Toka nje acha uoga mwanaume.
Mimi huwa nikisikia hali ya tofauti nje lazima niamke nichungulie na ikiwezekana natoka nje kabisa.

Kitu naogopa usiku ni kusikia mlio wa bundi, huwa nikisikia usingizi unapotea kabisa nachukua earphones naplay music ili nisisikie.
 
Sasa mpaka mende mnawaogopa, mende usiku wa manane anakishindo kama cha wakoma(kibiblia zaidi), hii inatokana na eneo lote kuwa kimya.
 
usiogope wachawi!!!!...wewe amini MWENYE MBWA'usimwamini MBWA!!! manake usiogope mawakala wa shetani,mwogope MUNGU!!!
 
Ingawaje Watu wengi sana hapa wamechangia comments zao katika Hali ya mzaha na dhihaka, lakini ukweli mchungu sana ni kwamba thread hii ina 'content' ambayo ni nyeti sana kwa muktadha wa usalama na masuala ya 'public awareness' kuhusu suala zima la usalama kwenye makazi ya kuishi nyakati za usiku. Kwa kifupi kabisa ni kwamba, Operesheni nyingi sana za 'sabotage' huwa zinafanywa na wale 'jamaa' kuanzia muda wa saa 7 usiku au saa 8 usiku wa manane na kuendelea. Nyakati za asubuhi au mchana huwa zinatumika katika kujiandaa na operesheni zinazokuja au kwa ajili ya kutangaza matokeo ya operesheni zilizofanyika usiku.
 
mnaongea kishujaa wangese wakati humu nilileta uzi wa kutafuta wamba tuingie Somalia kulikua na kazi ya ulinzi hakuna aliyetokea. humu ni ma keyboard warrior mapimbi nyinyi.
 
Usiogope hao ni ccm walikuwa wanapitisha masanduku ya kura kwa ajili ya uchaguzi wa mwakani.
 
Wewe ni mwanaume au mwanamke, kama mwanamke sawa ila kama mwanaume basi hujakamilika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…