Nimeamua kujiuzulu ushabiki wa Yanga ili kuiunga mkono Mbao Fc kwa sababu inafanya kile tulichotaka kufanya

Nimeamua kujiuzulu ushabiki wa Yanga ili kuiunga mkono Mbao Fc kwa sababu inafanya kile tulichotaka kufanya

Mbao wachawi wamemzika mbuzi mzima pale katikati ya uwanja juzi usiku kabla ya mechi

Hatukuliona hilo kaburi la mbuzi badala yake tumeshuhudia soka safi na matokeo halali ndiyo yamepatikana! Haji Habibu Kiyombo ndiye kasababisha yote haya@
 
Mbao zimekaza wakuu,hivyo isiwe taabu Leo najiuzulu rasmi ushabiki wa Yanga.Lengo ni kuunga mkono juhudi za mbao ambazo nasi ndizo tulizozitaka
Ilitakiwa umuunge mkono Mwenyekiti Wa timu
 
kwakweli ni jambo la kusikitisha sana kuona JITU kubwa linalazimishwa kujisaidia hadharani na mtoto mdogo ,,
 
Mbao ndio wanaoifuta aibu ya Toto Africa kwa Yanga. Viongozi wa Mbao FC wasikubali kufanywa tawi na timu za Yanga na Simba kama yule kiongozi wa Toto aliyejitokeza hadharani kuiunga mkono Yanga wakicheza na Toto.

Vv
 
demigod halloooo mkuu network inasumbua?


hahahahah niko eneo shwari kabisa..


bado natafakari ni kwa namna gani vijana wa mwanza wanaweza kutuotea kwa namna hii...?

Naona mleta Uzi kaamua kujiuzulu ushabiki wa yanga kwa na kuunga mkono mbao kwa kuwa mbao wanafanya kile ambacho yeye anakitaraji kuwa yanga wanataka kufanya....(Nimecheka sana hii hapa).

Nina wasiwasi na ushabiki wake! sidhani kama Yanga wanataka kushinda mechi tu kama lengo lao kuu. Bali kwao kutwaa Ubingwa ndio shabaha kuu!
 
Hivi ni Yanga tuu ndo mtashindaga siyo na wengine ,VUMILIA MCHEZO HUU HAUTAKI HASIRA
 
Kumbe wachezaji wa yanga karibu wote wanadai hela za usajili namsikitikia Sana Ajibu maana ni Kama amepishana na Hari la mshahara kutoka simba kwenda tanga. Ajibu ni km ngasa tu ni watu wanaocheza mpira bila malengo wanapendana kuwafurahisha watu bila kujua mpira ni Maisha.
 
Hivi we ulikua mshabiki kindakindaki sababu ya mbao kuwafunga ndio ufanye maamuzi hayo kila la heri
 
Nami pia nilitamani kuanzisha uzi kuhusu ushindi wa Mbao dhidi ya Yanga.

Ukweli sisi watu wa Mwanza ni watu tunaoamini tunaishi katika mji mashuhuri hivyo tunaamini tunaweza kuwa na kila kitu japo nyuma kidogo ya Dar sasa linapokuja swala la soka sisi kuwa watumwa wa timu za Dar hili hunishangaza sana.

Miaka ya nyuma tulipokuwa na Pamba nusu ya washabiki wa soka wa hapa tulikuwa wafuasi wa Pamba na timu za Dar ziligawana ile nusu iliyobaki eti leo Mbao ya hapa inaisambaratisha timu ya Dar alafu nashangaa nusu ya mashabiki wa soka wa hapa wanatembea kama wamenyeshewa mvua huo ni upumbavu wa hari ya juu, si waende tu kule Dar wakasaidiane na wenzao kuwa wanajaza uwanja.

Binasfi sitokaa niziunge mkono timu za Dar na timu yao ya taifa stars/ kilimanjaro stars kama haina sura ya vilabu vyote vya ligi kuu bara.

Eti huwa mnanchukuwa hao wa Dar kwakuwa ndio huonekana kulijua soka sasa toka muanze kuwa mnawachukua hao mmeshapata mafanikio yapi katika medani za kimataifa. Sibora mgekuwa mnachukua kutoka vilabu karibu vyote ili tunavyokuwa tunaambulia vichapo tuwe nanajisikia tumefungwa wote kuliko hivi inavyokuwa mmefungwa nyinyi.
 
Nami pia nilitamani kuanzisha uzi kuhusu ushindi wa Mbao dhidi ya Yanga.

Ukweli sisi watu wa Mwanza ni watu tunaoamini tunaishi katika mji mashuhuri hivyo tunaamini tunaweza kuwa na kila kitu japo nyuma kidogo ya Dar sasa linapokuja swala la soka sisi kuwa watumwa wa timu za Dar hili hunishangaza sana.

Miaka ya nyuma tulipokuwa na Pamba nusu ya washabiki wa soka wa hapa tulikuwa wafuasi wa Pamba na timu za Dar ziligawana ile nusu iliyobaki eti leo Mbao ya hapa inaisambaratisha timu ya Dar alafu nashangaa nusu ya mashabiki wa soka wa hapa wanatembea kama wamenyeshewa mvua huo ni upumbavu wa hari ya juu, si waende tu kule Dar wakasaidiane na wenzao kuwa wanajaza uwanja.

Binasfi sitokaa niziunge mkono timu za Dar na timu yao ya taifa stars/ kilimanjaro stars kama haina sura ya vilabu vyote vya ligi kuu bara.

Eti huwa mnanchukuwa hao wa Dar kwakuwa ndio huonekana kulijua soka sasa toka muanze kuwa mnawachukua hao mmeshapata mafanikio yapi katika medani za kimataifa. Sibora mgekuwa mnachukua kutoka vilabu karibu vyote ili tunavyokuwa tunaambulia vichapo tuwe nanajisikia tumefungwa wote kuliko hivi inavyokuwa mmefungwa nyinyi.
Kupenda ni hiari ya mtu. Hakuna anayelazimishwa nini apende, lini, vipi na wapi. Endelea kupenda ulichoamua kupenda, lakini usiwahoji wengine kwa nini wanaprnda wanachopenda. Kama wa Mwanza ni haramu kupenda cha Dar, vipi Watanzania wanaopenda vya Ulaya? Kwa hivyo masafa, nasabu wala asili havipaswi kuwa ndio sababu ya mtu kupenda apendacho. Wache wengine wapende wavipendavyo ili nawe wasikubughudhi kupenda upendacho. Ila tukumbuke tu kwamba duniani hakijaumbwa wala hakitaumbwa kizuri kisicho kasoro. Kwa hivyo hata hicho ukipendacho nacho hakijakosa wala hakitakosa dosari. Tena inawezekana ni nyingi na kubwa kuliko za hicho unachokichukia.
 
Tena usihasau kugombe urais wa mbao kama wale mabwana wanao hamia fisiem
 
Back
Top Bottom