Nimeamua kumpeleka Shemeji yangu Mahakamani!

Nimeamua kumpeleka Shemeji yangu Mahakamani!

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
NIMEAMUA KUMPELEKA SHEMEJI YANGU MAHAKAMANI

Anaandika, Robert Heriel.

Haki lazima ikatendeke!
Mbwembwe zangu zote lakini naishi Kwa Shemeji. Kuna wakati nakaa nawaza Kama nisingekuwa na Dada ingekuwaje, maana ndugu zangu wote wa kiume Hali zetu dhoofu ilhali Kama Yukreini. maisha yametupiga makombora, tumepigika tukachakaa!

Ukinikuta nyumbani utafikiri ndio Mimi ninayeandika huku mitandaoni Kwa kujiamini mwenye misimamo na kujitia Great Thinker, Thubutu! Ooh! Huku nimepoa Kama Uji wa Mgonjwa wa malaria Kali. Hasa Shemeji yangu akirudi kutoka kazini,

Taikon taabani maji kidevuni, Sister angu yeye alishanichoka miaka nenda Rudi licha ya kuniwekea Sanctions za kutosha ili niondoke lakini niliapa nitakomaa na vikwazo vyao mpaka kieleweke. " Mimi nirudi kijijini Mimi" mpaka najicheka kwenye kioo nijitazamapo.

"Ooh! Taikon kanenepea Kwa Shemeji"
Mara "Ooh! Unachezea Rimoti ya TV Kwa Mume WA Dadaako" Hayo maneno hata Kama yanakera lakini mvumilivu hula mbivu hata kama za uvivu. Endeleeni tuu na kelele zenu za chura, Mimi tembo hazinitishi.

Ninakaba penati Kama nipo ligi ya mpira za arabuni, Chenchi nikutumwa sirudishi nipo Radhi nikane kwa ubishi; nilikupa! nilikupa!
Nitawezaje kujiunga bando nifurahie maisha ya Mtandaoni. Nina washikaji kibao Mtandaoni, wapo wanaoniheshimu na kuniona mtu wa maana, ndio niwashikaji zangu hata kama hatujawahi kuonana. Sitishwi na maneno ya wanaonikera Mtandaoni kwani maneno Yao wala hayafui dafu mbele ya maneno ya Shemeji yangu huyu na Sister angu.

Shemeji yangu anamaneno ya kejeli na Dharau katu sitosahau.
Lakini sikumtuma aniite nyumbani kwake, nilikuwa zangu kijijini Makanya huko na maisha yangu yasiyo na mbele wala nyuma baada ya kumaliza University lakini niliridhishwa nayo. Yeye ndio aliyeniita Mjini ati atanitafutia kazi.

Nafika mjini siku zaidi ya tisini hakuna kwenda kazini labda kunipa vijikazi vya pale nyumbani. Hiyo ni baada ya Housegirl kufukuzwa pale nyumbani kisa nilileta uroho wa kutaka Kula kimasikhara Kama Rikiboy. Ugomvi ukazuka na uhasama ukaibuka. Japo sio vizuri kusema mambo binafsi hata Mimi Nafsi inanisuta lakini maji yameshavuka ukingo wa shingo na sasa yanaelekea puani, Acha niseme kabla ya pumzi yangu kuzima.

Kama ninakula, ninakunywa, ninaafya iweje nisichakate mchakato wa Katiba iliyopendekezwa. Lakini Shemeji yangu akazuia Katiba mpya na kumfukuza Housegirl. Analeta Siasa za UCCM na UCHADEMA kwenye maisha, looh!

Nilimshamsomea kila risala naye bila Sala akaniona Kula kulala, ati sina fikra wala maarifa, elimu yangu ati msalaba nilioubeba kwenda kunisulubisha. Mimi nikamuuliza kwani ulivyonitoa huko kijijini Kwetu Makanya hukujua hayo yote. Nikamuona anarapu rapu na kunitolea shit motherfanta.
Nikasema huyu hanijui, ndimi Taikon Master mwenye Mkanda mwekundu wa kuganda Kama ruba.

Juzi nimetimiza miaka mitano tangu nifike Kwa Shemeji, nimepata mchumba nikiwa hapohapo Kwa Shemeji yangu. Usishangae Kwa nini natafuta mchumba wakati naishi Kwa shemeji na sina kipato cha uhakika, umri unaruhusu kufanya hivyo. Ninamiaka 31 ningefanyaje, kuniona sina akili ni kuonyesha wewe ni mbumbumbu!
Mchumba wangu naye anaishi Kwa Shemeji yake. Wote twaishi Kwa mashemeji.
Kila nikutana na Mchumba wangu tunahadithiana changamoto zinazotusibu kwenye nyumba za mashemeji.
Zangu zinavumilika lakini zake sio kitoto, huyo Shemeji yake mshenzi sana, anataka Kumla Mchumba wangu. Hii kidogo inanipasua kichwa.

Jana Shemeji yangu ananijia na habari ambayo nilidhani ni taarifa ya habari ya uchumi aliyoisikiliza ITV. Akaniambia; Taikon hivi unajua kilo moja ya Unga ni Tsh 1,800 wakati kilo ya mchele ni Tsh 2,300/=,
Nikamjibu Mimi sikusomea uchumi.
Tumekwazana, ati anasema majibu yangu ni yadhihaka, anafikiria namna ya kunifukuza hapa nyumbani.

Mimi nimemuambia siondoki mpaka atimize ahadi yake ya kunitafutia kazi.
Nimemuambia Mchumba wangu ni mwanasheria, nitaenda Mahakamani kumfungulia Shauri Kwa kosa la kunidanganya na kunipotezea miaka mitano nyumbani kwake. Huku nikifanya kazi bila malipo yoyote.

Mchumba wangu kaniambia atanisapoti na tayari tumeanza kusoma makarabrasha ya uendeshaji wa kesi.

Ushahidi wa Meseji alizonitumia nikiwa kijijini Makanya kutaka nije mjini kuna kazi ninao, ushahidi wa kumfukuza Housegirl ninao, na Mimi kuchukua nafasi ya housegirl pasipo malipo yoyote.

Mwanasheria wangu(mchumba wangu) ameniambia hata akisema Kwa mwezi alikuwa anamlipa mfanyakazi Tsh 50,000/= Kwa mwezi.
Basi hizo pesa Kwa miaka mitano ni 3,000,000/= na usumbufu basi tutapata milioni Saba hivi.

Milioni Saba hiyo tumeiwekea bajeti ya matumizi Yafuatayo;
1. Milioni 1. Mahari
2. Milioni 1.5. Vitu vya ndani.
3. Milioni 1. Kodi ya Miezi sita Kwa chumba cha laki na nusu.
4. Milioni 3. Mtaji wa Biashara ya Dagaa.
5. Laki tano. Matumizi.

Tuombeane uzima Taikon ndio natoka hivyo.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Arusha.
 
Baada ya kutoka tu matatizoni..japo nilikuwa nina afya njema..dada yangu alieolewa dodoma aliniita niende nikamtembelee lakini pia kutokana na kwamba nilikuwa nimetoka matatizoni alipende niende kwake nikarifresh mind.....basi bhana pale kwa shemeji nilikaa wiki moja na siku kama tano hivi lakini maneno na vita iliyokuwa inapigwa kutoka kwa ndugu wa shemeji ilinifanya nisitamani kurudi pale mpaka leo...huwa napita tu kusalimia lakini nikiambiwa walau nilale siwezi kukubali......
 
Baada ya kutoka tu matatizoni..japo nilikuwa nina afya njema..dada yangu alieolewa dodoma aliniita niende nikamtembelee lakini pia kutokana na kwamba nilikuwa nimetoka matatizoni alipende niende kwake nikarifresh mind.....basi bhana pale kwa shemeji nilikaa wiki moja na siku kama tano hivi lakini maneno na vita iliyokuwa inapigwa kutoka kwa ndugu wa shemeji ilinifanya nisitamani kurudi pale mpaka leo...huwa napita tu kusalimia lakini nikiambiwa walau nilale siwezi kukubali......


😀😀😀

Hayo mambo ya kukaa Kwa mashemeji Yana wenyewe, na wenyewe ndio Sisi wenye mikanda mekundu
 
Kwenye mti mmoja mjenzi anaona mbao mganga anaona dawa mpishi anaona kuni ndege anaona makazi mwingine anaona kivuli kila mtu nafasi yake ataamua aone nini na kwanini ndio maana mtu mzuri kwako mbaya kwa wengine
 
Umesema kweli Mkuu
Nimewakopia tu kisha nikawatupia just imagine mtu umlishe umtunze na gharama za kumtunza mtu mmoja kwa siku pamoja na accomodation haipungui 6000 kwa siku.
achilia mbali unamwondoa House girl ili asije kuwa na mke ambaye sio chaguo lake kisha anakuja kwenye jukwaa lakini akiwa amejazwa ujinga na eti mchumba wake ambaye kiukweli kama huyu ndo mke mhn! haya anayetegemea kuanzisha maisha kwa kunyonga! anadhamilia kukushitaki kweli!
 
Nilimaliza form four mkoani kigoma advance nikasoma bwiru boy's (likizo zote nilikuwa nakaa kwa shemeji)

Nikaenda chuo (field zote akawa ananitafutia na field zote nimefanyia taasisi za walamba asali na matumizi shemeji yangu akawa ananisapoti)

Nikamaliza chuo nikarudi home kigoma nikakaa miezi miwili shemeji akanita kwake mwanza nikakaa miezi 4 nikizunguka nae sehemu mbali mbali za TZ (shemeji yangu ni idara nyeti anadili zaidi na kodi)

Then nikarudi kigoma nikafanya kazi kwenye kampuni yake ya usafirishaji kwa miezi 5 then akanita Dar for emergency Akanitumia ticket ya ndege

Nikafika Dar saa 9 na nusu (mwaka Huo ambao siutaji) saa kumi na mbili jioni nikiwa nimeongozana na shemeji yangu Nikapewa barua ya utambulisho wa kazi TPA plus mkataba (yote haya yalifanyika nyumbani kwa kigogo mmoja wa TPA ambae kwa sasa ni marehemu)

Kesho yake asubuhi nikaelekea mwanza kwa ndege pia business class kwa gharama za shemeji yangu pia

Like the last born kwa mama akawa anataka niwe nae karibu so nilivyomambia tu shemeji baada ya wiki mbili nikahamishiwa kigoma Ambapo ndio home kabisa pamoja na yote bado naishi kwetu na mama


KUSAIDIWA NA MASHEMEJI SIO VIBAYA NGUGU ZANGU KIKUBWA NI KUJIELEWA TU ISIWE MZIGO USIOBEBEKA sijawai kufanya kosa lolote kazini na wala sijawai kuingia kwenye ugomvi na mgogoro wowote ule

UKISAIDIWA KUMBUKA WEMA SOMETIME huwa nampiga TAFU shemeji yangu kwa kuwalipia ADA Watoto wake

Mashemeji wenye ROHO za KINABII WAPO
MUNGU AKUBARIKI SAANA SHEMEJI YANGU UMEFANYA NISIJUE MSOTO WA KUZUNGUSHA CV [emoji847][emoji847]

Sent from my SM-G570F using JamiiForums mobile app
 
Nilimaliza form four mkoani kigoma advance nikasoma bwiru boy's (likizo zote nilikuwa nakaa kwa shemeji)

Nikaenda chuo (field zote akawa ananitafutia na field zote nimefanyia taasisi za walamba asali na matumizi shemeji yangu akawa ananisapoti)

Nikamaliza chuo nikarudi home kigoma nikakaa miezi miwili shemeji akanita kwake mwanza nikakaa miezi 4 nikizunguka nae sehemu mbali mbali za TZ (shemeji yangu ni idara nyeti anadili zaidi na kodi)

Then nikarudi kigoma nikafanya kazi kwenye kampuni yake ya usafirishaji kwa miezi 5 then akanita Dar for emergency Akanitumia ticket ya ndege

Nikafika Dar saa 9 na nusu (mwaka Huo ambao siutaji) saa kumi na mbili jioni nikiwa nimeongozana na shemeji yangu Nikapewa barua ya utambulisho wa kazi TPA plus mkataba (yote haya yalifanyika nyumbani kwa kigogo mmoja wa TPA ambae kwa sasa ni marehemu)

Kesho yake asubuhi nikaelekea mwanza kwa ndege pia business class kwa gharama za shemeji yangu pia

Like the last born kwa mama akawa anataka niwe nae karibu so nilivyomambia tu shemeji baada ya wiki mbili nikahamishiwa kigoma Ambapo ndio home kabisa pamoja na yote bado naishi kwetu na mama


KUSAIDIWA NA MASHEMEJI SIO VIBAYA NGUGU ZANGU KIKUBWA NI KUJIELEWA TU ISIWE MZIGO USIOBEBEKA sijawai kufanya kosa lolote kazini na wala sijawai kuingia kwenye ugomvi na mgogoro wowote ule

UKISAIDIWA KUMBUKA WEMA SOMETIME huwa nampiga TAFU shemeji yangu kwa kuwalipia ADA Watoto wake

Mashemeji wenye ROHO za KINABII WAPO
MUNGU AKUBARIKI SAANA SHEMEJI YANGU UMEFANYA NISIJUE MSOTO WA KUZUNGUSHA CV [emoji847][emoji847]

Sent from my SM-G570F using JamiiForums mobile app
Naongezea hapa kipindi nakaa kwa shemeji Nilimsaidia kusimamia ujenzi wa nyumba zake 3

.Hizo nyumba zote skimming,Rangi nilifanya mwenyewe peke yangu yeye alikuwa ananunua vifaa tu (Wajomba zangu ni mafundi nilijifunzia kwao) blundering na gypsum nilifanya mimi (hapa nilisaidiana na mafundi mimi ndio nikawa fundi mkuu

.mifumo ya umeme na maji niliweka mwenyewe peke yangu (hapa shemeji alinipa zawadi ya hii simu ambayo naitumia hapa japo ninayo nyingine)

.Security system kama camera na waya za umeme (hizi aliweka fundi ambae ni rafiki yangu na alipewa Elfu 90 tu)


.kuosha vyombo
Kupiga deki
Kuogesha watoto
Kupika
Kufua nguo za watoto
NIMEFANYA SAAANA HIZO KAZI SO KAA KWA SHEMEJI BUT MAKE SURE UNA FAIDA

Note
USIENDEE KUKAA TU FOR NOTHING kama shemeji yako ni kajiajiri jumuika nae kazini kwake ukamsaidie chochote kile usinywe pote wala usitumie kilevi chochote JISHUSHE usipendee kukaa sebuleni muda mwingi

Sent from my SM-G570F using JamiiForums mobile app
 
Naongezea hapa kipindi nakaa kwa shemeji Nilimsaidia kusimamia ujenzi wa nyumba zake 3

.Hizo nyumba zote skimming,Rangi nilifanya mwenyewe peke yangu yeye alikuwa ananunua vifaa tu (Wajomba zangu ni mafundi nilijifunzia kwao) blundering na gypsum nilifanya mimi (hapa nilisaidiana na mafundi mimi ndio nikawa fundi mkuu

.mifumo ya umeme na maji niliweka mwenyewe peke yangu (hapa shemeji alinipa zawadi ya hii simu ambayo naitumia hapa japo ninayo nyingine)

.Security system kama camera na waya za umeme (hizi aliweka fundi ambae ni rafiki yangu na alipewa Elfu 90 tu)

😀😀😀

Huyu ningemburuza Mahakamani.


.kuosha vyombo
Kupiga deki
Kuogesha watoto
Kupika
Kufua nguo za watoto
NIMEFANYA SAAANA HIZO KAZI SO KAA KWA SHEMEJI BUT MAKE SURE UNA FAIDA

Note
USIENDEE KUKAA TU FOR NOTHING kama shemeji yako ni kajiajiri jumuika nae kazini kwake ukamsaidie chochote kile usinywe pote wala usitumie kilevi chochote JISHUSHE usipendee kukaa sebuleni muda mwingi

Sent from my SM-G570F using JamiiForums mobile app
 
Nilimaliza form four mkoani kigoma advance nikasoma bwiru boy's (likizo zote nilikuwa nakaa kwa shemeji)

Nikaenda chuo (field zote akawa ananitafutia na field zote nimefanyia taasisi za walamba asali na matumizi shemeji yangu akawa ananisapoti)

Nikamaliza chuo nikarudi home kigoma nikakaa miezi miwili shemeji akanita kwake mwanza nikakaa miezi 4 nikizunguka nae sehemu mbali mbali za TZ (shemeji yangu ni idara nyeti anadili zaidi na kodi)

Then nikarudi kigoma nikafanya kazi kwenye kampuni yake ya usafirishaji kwa miezi 5 then akanita Dar for emergency Akanitumia ticket ya ndege

Nikafika Dar saa 9 na nusu (mwaka Huo ambao siutaji) saa kumi na mbili jioni nikiwa nimeongozana na shemeji yangu Nikapewa barua ya utambulisho wa kazi TPA plus mkataba (yote haya yalifanyika nyumbani kwa kigogo mmoja wa TPA ambae kwa sasa ni marehemu)

Kesho yake asubuhi nikaelekea mwanza kwa ndege pia business class kwa gharama za shemeji yangu pia

Like the last born kwa mama akawa anataka niwe nae karibu so nilivyomambia tu shemeji baada ya wiki mbili nikahamishiwa kigoma Ambapo ndio home kabisa pamoja na yote bado naishi kwetu na mama


KUSAIDIWA NA MASHEMEJI SIO VIBAYA NGUGU ZANGU KIKUBWA NI KUJIELEWA TU ISIWE MZIGO USIOBEBEKA sijawai kufanya kosa lolote kazini na wala sijawai kuingia kwenye ugomvi na mgogoro wowote ule

UKISAIDIWA KUMBUKA WEMA SOMETIME huwa nampiga TAFU shemeji yangu kwa kuwalipia ADA Watoto wake

Mashemeji wenye ROHO za KINABII WAPO
MUNGU AKUBARIKI SAANA SHEMEJI YANGU UMEFANYA NISIJUE MSOTO WA KUZUNGUSHA CV [emoji847][emoji847]

Sent from my SM-G570F using JamiiForums mobile app
Kuna watu mna bahati sana dunia hii
 
Back
Top Bottom