Cantalisia
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 5,221
- 2,930
Ulinzi shirikishi,polisi jamii tupo kazini,safiri salama mama ngina
mie nitamuuguza baba ngina ondoa hofu loh....
Wakati naumwa nilipewa likizo ya naniliu ya miezi mitatu ili nipone, sasa likizo imeisha na yeye anataka kusafiri, hivi kweli katika mazingira kama hayo, unaweza kweli kufurahi...............! Kusema kweli nilikuwa nahitaji uangalizi wake wa karibu sana tena sana maana miezi mitatu sio mchezo.
Eheee, umenikumbusha halafu Bishanga aliahidi kutembea na mke wa mtu mwaka huu, hayo yalikuw ani miongoni mwa yale aliyoyakusudia mwaka huu...............Ngoja nifanye utafiti, maana mama Ngina aliisoma ile posti akacheka sana.................LOLyaani hii post nilikuwa naipitapita maana nilikuwa nashangaa ni mpuuzi anamuacha mke wake ila nilivyoifungua ilibidi nicheke. Vipi utampa bodyguard wakumsindikiza maana asije akawa anapitia kwa akina Bishanga
Hana haja ya kuweka ulinzi shirikishi, mwanangu Ngina anatosha, wala hahitaji usaidizi wa Cantalisa na King'asti. Huyu Ngina ni balaa ni mkuda hafai.....................mie roho haijadunda sana mana nilivyoona heading nikaanza na paragraph ya mwisho kwenda juu. mama ngano safiri salama ila rudi kabla wa wiki uliyopewa afu usitoe taarifa ya ujio wako. fanya suprise mtambuzi atafurahi sana na hyo suprise
imeaandikwa mwanamume atawaacha wazazi wake naye ataambatana na mkewe watakuwa mwili mmoja.....
sasa hapa kuna vitu vya kuvikubali kwanza (hii kwa uelewa wangu) inamaana mwanamke yeye haachi wazazi wake hivyo lazima aende maandiko hayajamfunga lakini la pili ni kwamba sielewe vizuri mkiwaacha wazazi ukiambatana na mkeo inamaana unaenda kwao hivyo nenda naye ka vipi kwa sababu maandiko hayakutoa mnaaenda wapi
lakin katka hali ya kawaida ni vizuri akaenda likizo ni siku nyingi akirudi atakuwa na akili mpya na mawazo mapya kuliko ukin'gangania akae hapo (japo kwa shida na raha) vumilia m2 wangu
Eheee, umenikumbusha halafu Bishanga aliahidi kutembea na mke wa mtu mwaka huu, hayo yalikuw ani miongoni mwa yale aliyoyakusudia mwaka huu...............Ngoja nifanye utafiti, maana mama Ngina aliisoma ile posti akacheka sana.................LOL
hapa itabidi nimulike mwizi
Halafu kuna wale aliokuwa akicheza nao ule mchezo wa kibaba na mama, na Kidali Po, sio kwamba watakumbushana...........Aaaaaagh! Kumbeeee, Hii safari inanifanya machale yanicheze, Jamani yaani naibiwa hivi hivi, ngoja niongee na yule dada yangu wa Chabo kama anaweza kunipa likizo ya wiki moja tuambatane. Nimeshtuka
Khaaa..............yaani we Babu umesababisha mshale wa kumoyo ugande ghafla ndo nini kuanza na heading ya ukanjanja. Nilishaanza kulia nani atanipikia uji. Namtakia Mama Ngano safari njema.
Hana haja ya kuweka ulinzi shirikishi, mwanangu Ngina anatosha, wala hahitaji usaidizi wa Cantalisa na King'asti. Huyu Ngina ni balaa ni mkuda hafai.....................
Sijajivua gamba bana, usipotoshe habari
Heshima yako baba,
Dah hiyo heading imenistua nikampigia mama kabla sijasoma akawa hapokei na uzi ukawa umeshafunguka lol!
Sijui ingekuwaje kwa nilichokuwa nimepanga kumuuliza,
Poa tunamtakia mama safari njema,na mungu ampeleke salama na amrudishe salama.
Kichwa cha habari kama gazeti la udaku vile. . . Lolz
Nwy mtakie safari njema, awarudie na zawadi toka kijijini.
Mtambuzi katika siku uliyoniudhi ni leo.......................................
Kichwa cha habari kama gazeti la Uwazi??? Umeanza lini kuandika "UDAKU"
Hovyo kabisa wewe yaani nimekuja mbio kujiandaa kutoa ushauri kumbe ndani ni hivi
Muone kwanza sura mbayaaa kaa nani hii...........................