Nimeamua nisiwe nakula mchana, je kuna madhara yoyote kiafya?

mkata-mkaa

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2016
Posts
296
Reaction score
181
Kutokana na ugumu wa maisha ...nimeamua nisiwe nakula mchana ..yaan nakula asubuhi na usiku tu....je kuna madhara yoyote kiafya?
Nb: kwa upande wa jf naingia mara moja kwa mwezi na bado lile la sh. 500... mb 600
 
Iwapo kazi yako sio ya kutumia nguvu nyingi naamini hakuna madhara, ilimradi unazingatia kupata "balanced diet" katika milo hiyo miwili iliyobaki.
 
Ongera watu wanalilia hata mlo mmoja nasikia mmepigwa marufuku kukata mkaa mkuu kaza shida hazikupandwa kwako ipo siku utapifa ata mitano
 
Madhara yapo, kwani mtu anaekula milo miwili ni tofauti na anaekula milo yote mitatu
 
Hio inaitwa pasi ndefu.sio mbaya
 
Badili Ratiba ili uwe unakula Asbh na Mchana ili Usiku usiwe una kula
 
Reactions: MTK
HahahaaMaisha magumu(yanachanganya),unakuta mtu anaumwa kichwa anaweka bando alalamike mtandaon anaumwa.
Huyu jamaa yupo sahihi kujinyima mlo mmoja wa mchanamchana ili aweke bando ajue madhara ya kutokula kwasababu pesa ya bando ya siku moja haiwezi kumfanya ale mchana kwa siku zinazofuata. Hata mimi nakula milo miwili tu kwa siku, asubuhi nakandamiza breakfast kubwa ikifika saa tisa nagonga Chakula cha mchana, usiku napiga Dash, ni mwaka wa pili huu sijambo kabisa
 
Reactions: MTK
Inategemea na kifungua kinywa chako kikoje. Kama nacho ni njiwa basi unaweza kuathiri afya yako.

Kutokana na ugumu wa maisha ...nimeamua nisiwe nakula mchana ..yaan nakula asubuhi na usiku tu....je kuna madhara yoyote kiafya?
 
Vipi anaeumwa ananunua bando alalamike mtandaon badala ya kununua dawa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…