Nimeanza kufuga kwa mara ya kwanza

hongera sana - huyo mgonjwa mshike mlishe pilipili nzima - kutwa mara tatu - atapona - kama huna pilipili - tafuta ugoro mchanganyie kwenye maji. Otherwise kama ulivyoshauriwa na wengi wape kuku wote chanjo - unalitakiwa chanjo iwe kitu cha kwanza kabisa ...............hata hivo hujachelewa - jitahidi kuwapa chanjo - wakimaliza maji yao weka majani ya olevera - wakinywa - watapona.
Hakikisha banda ni safi halina utitiri au viroboto - NAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA UFUGAJI :A S thumbs_up::A S thumbs_up:
 
Ugonjwa wa kideri hauna dawa. Wapatie chanjo ya kuzuia kideri. Kila siku wasikose vitamin.
nashukuru mkuu! nimewapa dawa inaitwa vetoxy-20 kwa siku mbili na naendelea kuwapa kwa wiki hii nzima nimeambiwa inatibu kideri na magonjwa mengine yanayo wasumbua kuku sasa nawasikilizia lakini kuna mmoja naona anasinzia sinzia
 
Kwakweli unajitaidi ila jitaidi kufuga kuku chotara wenye maumbo makubwa hata ukimpeleka sokoni utamuuza bei ghali hicho kijogoo kinakuaibisha angekua chotara ungefrahia
 

Ukitaka KUCHI wa uhakika nenda pale kijiji cha Mbiti au Ngulyati utapata kuchi wa uhakika, wenyeji wanauza jogoo kwa 18,000 hadi 20,000... Au kama una network nenda Sengerema kijiji kinaitwa Nyampande ndio kuna PURE kuchi, jogoo linakuwa na Kg 4 ukilisha vizuri.

Kila la heri mkuu, hata mbuyu ulianza kama mchicha....
 
Hongera sana kwa kuthubutu, jitahidi kufuata ushauri bora unaopewa na wataalamu wa hapa JF na kwingineko, huenda ikawa mwakani kipindi kama hiki unahesabu kuku maelfu.
Safari ni hatua.
 
ndugu zangu baada ya kujaribu kufuga kuku kwa mara mbili na kuambulia vifo nimeamua kubadili ufugaji na sasa nimehamia kwenye ufugaji wa noah, maendeleo ni mazuri nina miezi mitatu tangia nianze na nimefanikiwa kuzalisha nguruwe wawili mpaka sasa na wengine sita wapo kwenye joto muda wowote nawapandisha
 
Dawa ya kideli kama una maanisha coccidiosis sawa ipo (any anticoccidial) lakini wengine kideri humaanisha Newcastle disease hiyo kaka haina ugonjwa...just palliative treatment (water+vitamin+antibiotics). Mwanzo mzuri na mimi napenda watu wanaoanza kufuga mifugo ya kienyeji kuliko kuanza na wa kigeni (exotic) wanasumbua sana kama huna uzoefu.
 
Hongera sana araway, mi nakutia moyo umeanza vizuri, usikate tamaa we fata ushauri mzuri unaotolewa hapa na bla bla nyingine zipotezee utafanikiwa
 

Mkuu hawa jamaa wanalipa saana
Nakushauri uwe kama SIMBA anayewinda................hakikisha unaweka akilizako.....muda...na resourse kwa hao jamaa.................naamini muda mfupi tu lazima wakutoe.............chamsingi.......jifunze namna ya kuwalisha...chakula.....magonjwa......soko......kama una internet kila kitu kipo mkuu............na kwa kupunguza garama ....................unaweza jitahidi wakawa wengi...ukawa unauza kama vitoto pesa utakuwa unapata iwe unaitumia kuwatunza...........namaanisha mradi uwe unajiendesha wenyewe.............na rafiki yangu Mkenya anafuga,.......anawatoa kila baada ya miezi sita na kila moja unakuta anakilo 80 mpaka 100.......ukitaka ushauri usisite kuwasiliana kwani utapata ufumbuzi mapema saana........................


Kila la kheri
 
mkuu nashukuru kwa ushauri! nitahitaji menu ya chakula anayotumia huyo jamaa yako mkenya ili nione kama na mimi naweza kuwalisha ndani ya miezi sita awe na kilo angalau 60. maana hao unaowaona wamezaliwa january na sasa wanamiezi nane na sizani kama wanaeza fikisha kilo 40. nitaku pm namba yangu mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…