Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]Tatizo si TFF,bali tatizo ninaloliona na mindset zetu.Katika kila kitu hatufanyi vizuri ila kwa vile vitu vingine havina kipimo kujilinganisha na mataifa mengine,tunadhani tuko vizuri.
Kuanzia elimu,biashara,michezo,na hata siasa.
Tuna tabia ya uongo unaofikia hata kujidanganya sie wenyewe.Tunajidanganya tuko vizuri kielimu lakini angalia wasomi wetu!Wamejaa kiburi na majivuno lakini kichwani hawana lolote zaidi ya vyeti tu.Mf Rais aliwahi kushangaa idadi ya PhD pale BOT na huku akizidi kuona hawamsaidii kwenye upande wa masula ya fedha ipasavyo.
Ona aina ya biashara tunazofanya.Nyingi ni biashara za kichuuzi tu.Mtu ana mabilioni anakwenda China kufuata bidhaa ambazo hata sisi tuna uwezo wa kuzizalisha hapa!Tatizo ni nini?-Hakuna nia ya kweli ya serikali kuhimiza wazawa kufungua viwanda kwa kuwawekea mazingira mazuri.Utaona mtu akianza tu,TRA hawa na wanakuja kama vile unataka kuanzisha kiwanda cha kusindika bange!Bila huruma utaambiwa kodi ambayo hata serikali haijawahi kuipata.
Katika michezo tunadhani tunajua lakini kuna mambo mengi tunahitaji kijifunza.Hatupendi kujifunza kwa vile tunajua!
Tatizo liko kwenye akili na sio laana kama ambavyo unaweza kufikiri.
Hata hicho unachotaka kukiweka madarakani CHADEMA kinalaana zaidi ,kinameza matapishi na kujinadi nayo sikuhizi [HASHTAG]#LOWASSA[/HASHTAG],[HASHTAG]#NYARAMBAA[/HASHTAG]Kuna vyama vina laana, mkiviondoa mtapeta sana
Believe me, yakianzishwa mashindano ya kuongea tutashika mkia.Kipaji chetu ni kuongea
Siku akili zikiwakaa sawa mbona haya yote yanawezekana kabisa.View attachment 633302
Jamani Tanzania na Watanzania milioni 52 sasa tuna dhambi kubwa kiasi gani, toka tuliposhiriki mara ya mwisho mwaka 1980 nchini Nigeria mpaka leo mwaka 2017 hata dalili za kunusa kushiriki sizioni.
Shida kubwa hasa ni nini?
Hakuna mahusiano yoyote na mada husikaSiku akili zikiwakaa sawa mbona haya yote yanawezekana kabisa.
Yaani siku akili zikiwarejea ambapo mtaacha kutumia nguvu nyingi kwenye kudhoofisha upinzani na kutambua kwamba kuliko kuwahonga wapinzani kumbe mnaweza kuwekeza fedha hizo kwenye kuendeleza sekta muhimu ya michezo na baadae tukaingia rasmi kwenye ulimwengu wa ushindani wa kimichezo na kujizolea sifa kubwa kama hao unawaona kwenye hiyo picha
Lakini kwa sasa hivi hilo unalolitaka haliwezekani kabisa kwa sababu bado mnaamini wapinzani wa kisiasa ndio mchawi wa kila kitu katika taifa na wao ndio kipaumbele namba moja.
Waziri wa michezo yuko bize kukimbizana na magazeti yanayoandika habari zisizo mpendeza boss wake, wakati huo hajui hata idadi ya timu zinazoshiriki ligi kuu halafu eti ndio anaeratibu mipango yote ya kimichezo.
Hebu acheni tuendelee kuwa watazamaji mpaka siku fahamu zikiwarejea na kuwa serious kwenye vitu vya msingi.
sisi tuna dili vyama vya siasa vivuke boda kwa siasa si mpira kwa nchii nduguView attachment 633302
Jamani Tanzania na Watanzania milioni 52 sasa tuna dhambi kubwa kiasi gani, toka tuliposhiriki mara ya mwisho mwaka 1980 nchini Nigeria mpaka leo mwaka 2017 hata dalili za kunusa kushiriki sizioni.
Shida kubwa hasa ni nini?