Nimechoka kupokea wageni

Nimechoka kupokea wageni

Hellow Africa

Dah ninaishi na wife huu mwaka wa nne sasa ila kero kubwa wageni hawakauki hapa nyumbani ndugu zake wanaingia na kutoka kiasi kwamba mtu huwezi kuweka akiba yako.

Juzi kaja mgonjwa wa vidonda vya tumbo Jumapili huwa tuna kawaida ya kupika pilau yeye tukampikia ndizi lakini wapi eti kaenda kugombania ukoko wa pilau na mwanangu wa mwisho mpaka kaja kuniambia chumbani.
Acha uchoyo..... Yaani Baba wa familia unawaza Mambo ya ukoko wa pilau... Shame on You.
 
Kumbe kakaangu ww ni msukumaa, hapo nimeelewa ila punguzeni kidogo daah! Mnaumiza makabila mengine undugulization unazidi jamani...mtuhurumiee
Asili yetu sio hivo na hatuwez acha Sisi tunakaa na mtu yeyote kikubwa awe mwaminifu TU na utalelewa vizr ni tofaut na wachagga uchoyo na gubu la kijinga

Sasa kama mwanaume mweny akili timamu unalaumu dungu kala ukoko seriously na mwanamke unajifeel umeolewa kabisa
 
Kama ndg. wa mkeo bado ni tegemezi (Wanafunzi) wavumilie tu, familia zetu hizi akibahatika mmoja wa familia akawa na mwanga kidogo mzigo wote unamwangukia.

Ila kama ni watu wazima na si wanafunzi na una miradi ambayo unaweza kuwaweka wakusaidie fanya hivyo. Wasibweteke tu nyumbani, wazalishe.

Kama hakuna miradi midogo midogo ya wao kukusaidia, kaa na mkeo mpe nyeusi na nyeupe, warudi kwao.

Wewe ndo unayeujua uhalisia wa maisha ya kwao. Pia kama unaweza kuwasaidia kwa kuwatafutia sehemu ya kujishikiza unaweza kufanya hivyo.
 
Back
Top Bottom