Mshua's
JF-Expert Member
- May 22, 2013
- 804
- 553
Takribani miaka 8 nimekuwa nikikabiliwa na tatizo la kuongezeka uzito wa Kg 2.125 kwa mwaka. Uzito wangu wa kawaida ulikuwa ni Kg 75, hadi kufikia April,2013 nilikuwa na Kg 92 ambazo ni ongezeko la Kg 17. Urefu ni Sm 178 na umri wangu ni miaka 31.
Nimekuwa nikitumia asali mbichi kwa kuitia kwenye maji ya moto yaliyochanganywa na Tangawizi iliyo pondwa pondwa asubuhi kwenye kifungua kinywa na jioni kabla ya mlo wa jioni. Nilipunguza kiasi cha chakula nilichokuwa nakula na asubuhi nilikuwa natembea Km 4, 2 wakati wa kwenda na 2 wakati wa kurudi. Tangu April -August, 2013 nimepunguza Kg 8 na sasa nina uzito wa Kg 84 tu na bado naendelea kupunguza.
Ingawa kitambi bado kipo, naamini kitakwisha kabisa. Suruali zote zimepwaya na sasa nanunua nguo zingine.
Natoa shukrani zangu kwa Mzizi mkavu na wadau wengine wote , haya ni matunda ya michango yenu hapa JF Doctor!
Nimekuwa nikitumia asali mbichi kwa kuitia kwenye maji ya moto yaliyochanganywa na Tangawizi iliyo pondwa pondwa asubuhi kwenye kifungua kinywa na jioni kabla ya mlo wa jioni. Nilipunguza kiasi cha chakula nilichokuwa nakula na asubuhi nilikuwa natembea Km 4, 2 wakati wa kwenda na 2 wakati wa kurudi. Tangu April -August, 2013 nimepunguza Kg 8 na sasa nina uzito wa Kg 84 tu na bado naendelea kupunguza.
Ingawa kitambi bado kipo, naamini kitakwisha kabisa. Suruali zote zimepwaya na sasa nanunua nguo zingine.
Natoa shukrani zangu kwa Mzizi mkavu na wadau wengine wote , haya ni matunda ya michango yenu hapa JF Doctor!