Nimefika Katavi na kujionea jinsi watu wanavyotajirika kupitia Kilimo

Nimefika Katavi na kujionea jinsi watu wanavyotajirika kupitia Kilimo

Jifunafu

Senior Member
Joined
May 25, 2020
Posts
182
Reaction score
693
Wanajamvi Aslam,
Hama baada ya salamu ndugu zangu Ile safari yangu ya kwenda mji wa Mpanda kuona fursa za kilimo imetimia.
Nilipata nafasi ya kutembelea baadhi ya vijiji tofauti tofauti Kwaajili ya kuangalia maeneo, ni kweli natoa ushuhuda kwamba kilimo kimetajilisha watu wengi hususani Mji wa Mpanda na wengi wao wakiwa ndugu zetu wasukuma na wageni kutoka mikoa mbali mbali wanakuja kuwekeza.

Nilibahatika kupitia vijiji vya wilaya ya Mlele na kutembelea na kisha kwenda hadi wilaya ya Tanganyika inayopakana na mkoa wa Kigoma, vijiji kama Mwese na kuona jinsi mapori yalivyojazana huko na mashamba mazuri na mabonde.

Kweli Tanzania ni kubwa na kuwa masikini ni kujitakia wenyewe, wasukuma wanaivisha huko magunia na magunia ya mahindi. Ardhi unapewa hata bure unaweka watu wanafyeka mianzi unalima bure tu, mahindi yanatoka baraa.

Kijijini kilichonivutia zaidi na kuamua kukodi na mashamba ni Kijiji cha Kapanga, ni center iliyochangamka na magari yanasomba mahindi Kila kukicha na wafanyabiashara wamejaa kutafuta mahindi.Kiujumla mpanda ni mji unakuwa Kwa kasi na mabosi wengi ni wakulima.

Vijana tuamkie kilimo na kilimo kinalipa, mambo ya kuzunguka na bahasha za kaki haina maana, mashamba tele hayajawai kulimwa tangu kuwepo kwa dunia.

View attachment 2339026
 
Asante sana kwa taarifa..vijana waache kujazana mjini waende maeneo kama hayo wakapambane..

Vipi debe la mahindi bei gani huko?

#MaendeleoHayanaChama

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
kwenye jumuiya ya east Africa tuungane ardhi wa Kenya,Uganda,Rwanda n,k wapewe nafasi ya kulima,kufuga kama raia wa tz alafu tuone mziki.akuna mkenya au Mganda atakuja kupanga chupi barabarani afanye umachinga wakati utajiri upo huko katavi,Singida,Manyara n,k
 
kwenye jumuiya ya east Africa tuungane ardhi wa Kenya,Uganda,Rwanda n,k wapewe nafasi ya kulima,kufuga kama raia wa tz alafu tuone mziki.akuna mkenya au Mganda atakuja kupanga chupi barabarani afanye umachinga wakati utajiri upo huko katavi,Singida,Manyara n,k
Inatafakarisha sana adse

Vijana tuamke

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu weka weka na picha kadhaa basi...
 
Wanajamvi Aslam,
Hama baada ya salami ndugu zangu Ile safari yangu ya kwenda mji wa mpanda kuona furusa za kilimo imetimia.
Nilipata nafasi ya kutembelea baadhi ya vijiji tofauti tofauti Kwaajiri ya kuangalia maeneo,ni kweli natoa ushuhuda kwamba kilimo kimetajilisha watu wengi hususani mji wa mpanda na wengi wao wakiwa ndugu zetu wasukuma na wageni kutoka mikoa mbali mbali wanakuja kuwekeza.

Nilibahatika kupitia vijiji vya wilaya ya mlele na kutembelea na Kisha kwenda Hadi wilaya ya Tanganyika inayopakana na mkoa wa kigoma, vijiji Kama mwese na kuona jinsi mapori yalivyojazana huko na mashamba mazuri na mabonde,kweli Tanzania ni kubwa na kuwa masikini ni kujitakia wenyewe, wasukuma wanaivisha huko magunia na magunia ya mahindi.
Aridhi unapewa hata bure unaweka watu wanafyeka mianzi unalima bure tu,mahindi yanatoka baraa.

Kijijini kilichonivutia zaidi na kuamua kukodi na mashamba ni Kijiji Cha kapanga,ni center iliyochangamka na magari yanasomba mahindi Kila kukicha na wafanyabiashara wamejaa kutafuta mahindi.Kiujumla mpanda ni mji unakuwa Kwa kasi na mabosi wengi ni wakulima.
Vijana tuamkie kilimo na kilimo kinalipa,Mambo ya kuzunguka na bahasha za kaki Haina maana,mashamba tele hayajawai kulimwa tangu kuwepo Kwa Dunia.
View attachment 2339026
Njoo Tanganyika tufuge!
 
Back
Top Bottom