Nimegundua Bashe hajui maana ya Food Security

Nimegundua Bashe hajui maana ya Food Security

Mkuli.ma hawezi kutolewa kafala ili wengine wzpate chakula kwa bei nafuu. Wakati mkulima huyo huyo akiuziwa mbolea bei juu hakukuwa na makelele ya kumtetea.

Mvua ilipokata wakati kisha ingia gharama za kulima, kupanda na kupalilia watu wzlikaa kimya, basi endeleeni kukaa kimya wakati mkulima anarudisha gharama zake.
Mkulima harudishi gharama zake kwa mahindi debe kufika 25000. Mnashindwa kutofautisha Kati ya soko lilivyo na inflation.

Hakuna mkulima analima kila aina ya mazao. Mahindi yakifika 25000 kwa debe hiyo sio dalili nzuri kwa maana mkulima huyo huyo atalazimia na yeye kununua maharage au mafuta au bidhaa nyingine kwa bei kubwa. Usije ukafikiri mahindi debe likiwa 25000 basi mkulima kazi yake yeye ni kukupata faida tu, kumbuka ana mahitaji mengine nayo yanapanda.

Kikubwa serikali kudhibiti mfumuko wa bei(inflation), haina maana kabisa mkulima anauza mahindi gunia 150000, aalafu yote hiyo anaitumia kununua bidhaa nyingine zilizopanda bei.

Ni bora mkulima auze gunia 70000, alafu mbolea anunue 40000, kuliko kuuza gunia 150000 alafu mbolea ainunue kwa 170000. Bado hajaenda kweye mahitaji ya kawaida ya nyumbani, mwisho kauza kwa pesa nyingi alafu yote anaimalizia kwenye mahitaji na haitoshi.

Usikariri bei kubwa ni muuzaji kunufaika bila kufikiria pia muuzaji atahitaji mahitaji mengine kwa bei kubwa.
 
Sina nia ya kumtetea Bashe lakini ngoja Kwa ufupi nikuwekee hapa mchanganuo wa gharama za kuzalisha mahindi japo sio rasmi lakini japo ikupe picha.

Kukodi shamba heka shs 50000
Kulima shamba heka shs 60000
Mbolea ya kupandia shs 170000,×2
Mbolea ya kukuzia shs 150000×3
Palizi ya 1&2. Shs 100000
Kuvuna & kupaki shs 70000

Huu ni mchanganuo usio rasmi wa mkulima wa kitanzania na hapo ujumlishe na muda wa miezi sita baada ya gharama hizo wakulima wetu walio wengi hupata kati ya gunia 12 - 15 kwa heka.

Kwa huo mlinganyo niliouweka hapo maana yake kama atauza Kwa bei ya sasa ambapo anauza gunia shs 50000 atapata shs kati ya 600000 hadi 750000.

Ukichukua kiasi Cha pale juu ukatoa Kwa mauzo utaona hakuna serikali iliyo serious na watu wake itawazuia kuuza mazao Kwa bei nzuri.

Na hapo sijakuwekea risk factors za ukame mafuriko wadudu waharibifu udhaifu wa ardhi nk
Ikiwa bado Kuna inflation bado mkulima hata aruhusiwe kuuza nje bado hatafaidika. kikubwa serikali ni kucontrol inflation. Unauza mahindi gunia 100k, alafu litre ya mafuta unainunua kwa 8k. Bado hujafanya kitu.
 
Kama kuna kenge ni pamoja na watu kama hii kenge hapa.

Wanaosafirisha mazao nje ni wa wachuuzi na si wakulima.Wakulima wanauza kwa bei ya kunyonywa sana.Ila kwa vile ni kenge haitanielewa
Wachuuzi ni wanyonyaji hili lipo wazi, lakini kwann usinunue moja kwa moja kwa wakulima? Huwezi sababu unasubiri wachuuzi wakutafutie, wakufungashie, wakusafirishie ww uje ununue. Kama kuna ugumu kuwafikia wakulima basi kubali kulipia gharama za anayekufanyia hiyo kazi. Kama gharama za vitu ni juu, na wewe pandisha huduma zako kuwa juu huwezi teseka unless huduma zako hazihitajiki au hazipo.
 
Kasemaje ?!!!

For future records ni bora ukaweka alichosema Ad Verbatim na wewe ukaweka hoja yako..., sisi wapita njia tuone kama yaliyomo yamo....
 
Naamini anajua kiiengeleza sasa namuwekea hapa maana yake.

Food security is the measure of the availability of food and individuals' ability to access it. According to the United Nations' Committee on World Food Security, food security is defined as meaning that all people, at all times, have physical, social, and economic access to sufficient, safe, and nutritious food that meets their food preferences and dietary needs for an active and healthy life.

Akishamaliza kusoma hapo, namwagiza (mimi ninae lipa kodi ili alipwe) apitie upya hari ya upatikanani wa chakula nchini, ili ikiwezekana aagize baadhi ya mazao yasiuzwe nje.

Vyakula vimepeta bei sana huku mtaani, ila kwa vile yeye waziri analishwa hawezi ona hii shida.

Tusipo rekebisha hii hari, hadi December tutaanza kununua unga na mchele kutoka kenya, tena kwa bei ya juu zaid.

Tozo zinateketeza biashara ndogongodo (chechemshi).
ndio maana kwa kiasi fulani JPM alikuwa na maono.alisema kipindi cha corona wakati wengine wako lockdown sisi tuendelee kuchapa kazi ili majirani wetu wakikosa chakula tuwauzie kwa bei ya juu.kinachofanyika kwa sasa wakulima wetu wanadanganywa na wenzetu wa nchi jirani kwa kuwapa bei kiasi fulani na wao wakiamini ni bei ya juu.wakiishakinunua kwa sasa wanakihodhi na baada ya muda mfupi hali tunayoiona sasa itakuwa maradufu ndipo watakileta tena hapa kwetu kwa bei ya kuruka.
 
wakulima wanaponunua mbolea shilingi 170,000 kwa mfuko wa kg 50 mbona hukujitokeza kulisemea. Acha wakulima wafaidi jasho lao kwa kuuza mazao yao mahali popote kwa bei wanayoitaka.
Nami naweka msisitizo hapo hapo ndugu yangu!
 
Kama kuna kenge ni pamoja na watu kama hii kenge hapa.

Wanaosafirisha mazao nje ni wa wachuuzi na si wakulima.Wakulima wanauza kwa bei ya kunyonywa sana.Ila kwa vile ni kenge haitanielewa
Hawa watu wahawa ufahamu wowote, ni wakulima wangapi ambao hadi wana mazao yao!!wengi walipovuna tu wakayauza na kutimiza mahitaji yao, wanaofaidika sasa ni wafanya biashara walioyanunua kwa bei ndogo, na kuyahifadhi.
 
Sina nia ya kumtetea Bashe lakini ngoja Kwa ufupi nikuwekee hapa mchanganuo wa gharama za kuzalisha mahindi japo sio rasmi lakini japo ikupe picha.

Kukodi shamba heka shs 50000
Kulima shamba heka shs 60000
Mbolea ya kupandia shs 170000,×2
Mbolea ya kukuzia shs 150000×3
Palizi ya 1&2. Shs 100000
Kuvuna & kupaki shs 70000

Huu ni mchanganuo usio rasmi wa mkulima wa kitanzania na hapo ujumlishe na muda wa miezi sita baada ya gharama hizo wakulima wetu walio wengi hupata kati ya gunia 12 - 15 kwa heka.

Kwa huo mlinganyo niliouweka hapo maana yake kama atauza Kwa bei ya sasa ambapo anauza gunia shs 50000 atapata shs kati ya 600000 hadi 750000.

Ukichukua kiasi Cha pale juu ukatoa Kwa mauzo utaona hakuna serikali iliyo serious na watu wake itawazuia kuuza mazao Kwa bei nzuri.

Na hapo sijakuwekea risk factors za ukame mafuriko wadudu waharibifu udhaifu wa ardhi nk
mbona hujatuambia kutoa mazao shamba ya kuyaleta nyumbani,magunia,madawa ya kuhifadhia na nk
 
Mkuli.ma hawezi kutolewa kafala ili wengine wzpate chakula kwa bei nafuu. Wakati mkulima huyo huyo akiuziwa mbolea bei juu hakukuwa na makelele ya kumtetea.

Mvua ilipokata wakati kisha ingia gharama za kulima, kupanda na kupalilia watu wzlikaa kimya, basi endeleeni kukaa kimya wakati mkulima anarudisha gharama zake.
Katika mwaka tuliopiga hela wakulima basi ni huu wa 2021/2022. Nimeuza mchele kwa shilingi 2,500 kwa kilo na viazi shilingi 90,000 kwa gunia huko huko shambani. Wachuuzi watawaletea kwa bei wanayoijua wao! Sisi tumeshamalizana nao.
 
  • Thanks
Reactions: RMC
Wachuuzi ni wanyonyaji hili lipo wazi, lakini kwann usinunue moja kwa moja kwa wakulima? Huwezi sababu unasubiri wachuuzi wakutafutie, wakufungashie, wakusafirishie ww uje ununue. Kama kuna ugumu kuwafikia wakulima basi kubali kulipia gharama za anayekufanyia hiyo kazi. Kama gharama za vitu ni juu, na wewe pandisha huduma zako kuwa juu huwezi teseka unless huduma zako hazihitajiki au hazipo.
Umezungumza kama layman, kila mtu akioandisha gharama kutakua na mfumuko wa bei na athari zake unazijua. Kuuza kwa bei kubwa kila mtu sio ndio kupesa. Ingekua bidhaa kuwa na bei kubwa ni kupata pesa basi Zimbabwe na Sudan wananchi wake wangekua mabilione.

Mkulima mahindi gunia anauza milion 1, alafu akienda kununua mkate naye anauziwa laki 1. Akienda kununua sabuni anauziwa laki 2. Sasa kutakua na uchumi tena hapo. Unakua na pesa nyingi mfukoni alafu haina thamani
 
Umezungumza kama layman, kila mtu akioandisha gharama kutakua na mfumuko wa bei na athari zake unazijua. Kuuza kwa bei kubwa kila mtu sio ndio kupesa. Ingekua bidhaa kuwa na bei kubwa ni kupata pesa basi Zimbabwe na Sudan wananchi wake wangekua mabilione.

Mkulima mahindi gunia anauza milion 1, alafu akienda kununua mkate naye anauziwa laki 1. Akienda kununua sabuni anauziwa laki 2. Sasa kutakua na uchumi tena hapo. Unakua na pesa nyingi mfukoni alafu haina thamani
Sasa kama nchi yako inamfumuko wa bei, na mm ni layman ww huduma zako shusha bei. Mnapambana na uzalendo mnasahau kuwa uzalendo wa nchi unaanzia kwenye tumbo la watoto wako na familia yako. Nimekwambia huwezi kuwafikia wakulima, na wachuuzi wameongeza gharama, basi na ww pandisha gharama za huduma zako ili watoto wako wasife na usikae unalalamika tu. Hakuna atakaye kuonea huruma kabla hajajihurumia kwanza. Kwani huko Zimbabwe walionacho wamekufa baada ya uchumi kuanguka? Still asiye nacho ndo anateseka hata tukiamia kwenye dola.
 
Katika mwaka tuliopiga hela wakulima basi ni huu wa 2021/2022. Nimeuza mchele kwa shilingi 2,500 kwa kilo na viazi shilingi 90,000 kwa gunia huko huko shambani. Wachuuzi watawaletea kwa bei wanayoijua wao! Sisi tumeshamalizana nao.
Hii dhana ya kupiga pesa katikati ya mfumuko huwa siielewi. Huna mahitaji mengine? Unauza mchele kilo 2500, sawa. Mahitaji mengine nayo umeyanunua kwa bei ile ile ya siku zote?

Wengi somo la uchumi limewapita kushoto hamfahamu thamani ya pesa haitokani na idadi ya pesa uliyonayo. Wewe unaonyesha nchi Kama Zimbabwe ungekuwa unaishi kwa amani maan huko kilo ya mchele ni zaidi ya sh 4000. Lakini haimaanishi wakulima wa huko ni matajiri kwa kuwa mahitaji mengine bei ipo juu Sana.
 
Sasa kama nchi yako inamfumuko wa bei, na mm ni layman ww huduma zako shusha bei. Mnapambana na uzalendo mnasahau kuwa uzalendo wa nchi unaanzia kwenye tumbo la watoto wako na familia yako. Nimekwambia huwezi kuwafikia wakulima, na wachuuzi wameongeza gharama, basi na ww pandisha gharama za huduma zako ili watoto wako wasife na usikae unalalamika tu. Hakuna atakaye kuonea huruma kabla hajajihurumia kwanza. Kwani huko Zimbabwe walionacho wamekufa baada ya uchumi kuanguka? Still asiye nacho ndo anateseka hata tukiamia kwenye dola.
Hakuna napolalamika Bali nakuweka sawa. Bidhaa kupanda bei hakuamriwi na mtu. Huwezi kuamka na kusema kuanzia Leo dukani kwangu nauza mkate elfu 10. Bei za bidhaa kupanda ni masuala ya kiuchumi.

Hata hii bei ya sasa ya mazao wala sio wakulima waliopandisha. Nilichokuwa nakueleza ni kuwa bidhaa Kuuzwa bei kubwa sio ndio watu kupata pesa, ndio maana unaona serikali zote duniani huangaika kucontrol hali hiyo.

Na hata hapa serikali inahangaika usiku na mchana kucontrol bei za bidhaa ili kulinda thamani ya pesa.

Kuhusu kusema kwani Zimbabwe wamekufa, hili mbona lipo wazi uchumi wa nchi ukianguka watu watakufa. Hata Zimbabwe watu wamekufa. Hakuna serikali inayokubali uchumi wa nchi uanguke ndio maana Kuna serikali.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Back
Top Bottom