Nimegundua biashara ya ng'ombe ni nzuri sana

Nimegundua biashara ya ng'ombe ni nzuri sana

JOH CARLOS

JF-Expert Member
Joined
May 13, 2016
Posts
579
Reaction score
269
Habari.

Biashara ya ng'ombe nimekuja kugundua ni nzuri sana baada ya kutembelea mikoa ya kagera kuelekea hadi mpakani mwa uganda na tanzania.

Imekua ni biashara iliowapa vijana wadogo ambao hawakuweza kupata elimu na ambao hawakuweza kuendelea na elimu ajira nzuri na kuweza kuwalipa vzuri sana ...

Ipo ivi vijana wananunua ng'ombe toka kwa wafungaji(endapo ataitaji kuuza mfugo wake) na kwenda kumuuza mnadani na kupata faida ya sio chini ya 50 elfu kwa ng'ombe nguvu kazi yake yeye na kuswaga ng'ombe kutoka aliponunua mpaka mnadani.

Kijana anaweza anza kwa mtaji wa ng'ombe moja lakin kwa mwezi akaweza nunua mwingine...na wasio na mtaji kabisa huanza kuswaga ng'ombe za watu na hivyo kulipwa kwa safari moja sh laki moja hivyo kujitengenezea mtaji.

Nilikua naomba kwa wanaojua biashara hii ya ng'ombe ipo kweli mikoa ya arusha na kilimanjaro nijaribu kuwekeza uko.
 
Ooooh naona ata mi niliwai kuwaza ni kitu kuzuri kufanya ngoja wajuzi waje
 
Hawa huwezi kuwaweka kwenye kundi la biashara ya ng'ombe Ilitakiwa useme wachuuzi wa ng'ombe
Biashara ya ng'ombe ni wafugaji wanapambana na upupu na msiba ili ng'ombe wale na baadae wapate mbolea, maziwa, nyama au ng'ombe wenyewe Kiukweli hiyo ni bonge la biashara
 
Back
Top Bottom