Nimegundua kumbe mimi na tajiri sana toka zamani

Nimegundua kumbe mimi na tajiri sana toka zamani

msumeno

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2009
Posts
2,826
Reaction score
1,734
Waungwana mimi kaka yenu nimezaliwa kijijini kwetu hukoooo Tabora,, mimi ni mtoto pekee kwa wazazi wangu... wazazi wangu kwa kweli hali yao ni kama ya wengi wetu hapa Tanzania hasa sisi wa Bush... ila faraja ni kwamba baba ana mashamba makubwa na mengi saaana kule kijijini... yaani kifupi yoooote yangu. sasa mikakati niliyo nayo ni kuyaendeleza kwa kufanya yafuatayo

  • Kufuga..... kianzio kipo
  • kilimo cha cha mazao ya kudumu kama michikichi .. korosho... na mengine ... mtaji naweza upata Insha Allah
  • Kuyasajiri yoote ili nisije nikavamiwa na wajanja kwa kigezo cha uwekezaji
Kwa mipango hii kweli mimi ni masikini tena??manake nimeona nikikalia politik za thithiemu na chandumu na kafu a.k.a UKAWA ntakuwa mshangiliaje wa maendeleo ya wengine..... wao wakipiga domo kule mjengoni wanavuta mshiko wa nguvu sisi je??? politik. wengi wenu mko kama mimi sema hatulijui hili...

TURUDI VIJIJINI TUKAVUNE UTAJIRI WALIOTUACHIA WAZAZI WETU... KILIMO NA UFUGAJI NDO MPANGO MZIMA
 
Hujachelewa mkuu, jipange sawasawa! kwenye sekta ya kilimo kukata mtaji ni suala la kawaida sana japo hili lipo ktk kila biashara.
Mhimu, fanya upembuzi yakinifu kabla hujaanzisha mladi wa aina yoyote. Lima kisasa pia uhakika wa maji ni mhimu sana ili kilimo kiwe motivational.
Pia soko la mazao yako ndo karata ya mwisho kucheza nayo.
 
Wazo njema kaka umeshajaribu kulima au ndyo unanza?je wajua changamoto za kilimo?kilimo kinakutoa umaskini endapo utazingatia kanuni zake
 
hujachelewa mkuu, jipange sawasawa! Kwenye sekta ya kilimo kukata mtaji ni suala la kawaida sana japo hili lipo ktk kila biashara.
Mhimu, fanya upembuzi yakinifu kabla hujaanzisha mladi wa aina yoyote. Lima kisasa pia uhakika wa maji ni mhimu sana ili kilimo kiwe motivational.
Pia soko la mazao yako ndo karata ya mwisho kucheza nayo.

c lazima eneo liwe na maji wapo wanaolima nch kavu hadi ekari 3000 nawapo wazuri kiuchumi
 
avatar19754_4.gif
 
c lazima eneo liwe na maji wapo wanaolima nch kavu hadi ekari 3000 nawapo wazuri kiuchumi

Mkuu unamaanisha nini kusema "Nchi kavu"
Suala mhimu ni kujihusisha na kilimoja cha kisasa kwa maana ya kucontrol hitaji la maji kwenye mmea.
Mazao kama ufuta, alizeti na tumbaku hayahitaji mvua nyingi. So mwaka ukiwa na mvua nyingi ujue hutapata kitu.
 
Kuna rafik yangu,tunasoma naye.
Alitumia milion moja na nusu kulima mahindi MBUGANI
bahat mbaya mvua imekuwa kubwa mazao yamezidiwa uwezo.
Na maji
amevuna gunia 6.sita tu
amerud hana kitu
 
c lazima eneo liwe na maji wapo wanaolima nch kavu hadi ekari 3000 nawapo wazuri kiuchumi

ulishawahi kulima hata tuta la mchicha lakini?!! amekwambia uhakika wa maji, kama kutakuwa na mvua za kueleweka, kama chini yatakuwepo maji ya kutosha yasiyo na chumvi, kama kuna ziwa karibu, kama kuna mto, kama kuna bwawa, huo ndiyo uhakika wa maji! Misri asilimia kubwa ni jangwa lakini wanalima mpaka cha kusaza kwa sababu wana chanzo cha uhakika cha maji mto nile!utalima nchi kavu bila maji hiyo mimea utainywesha vumbi?!!!
 
Kweli mkuu mwana Tabora mwenzangu, rudi piga kazi ngoja sisi huku mjini tufatilie kidogo mambo ya CCM na UKAWA tukiona wazidi kuzingua tutarudi tabora tushike jembe tu.
 
Back
Top Bottom