Nimegundua kuna member humu anatembea na mke wangu, nitakachomfanya tusilaumiane

Mleta amani

Member
Joined
Dec 6, 2019
Posts
25
Reaction score
124
Nimegundua kuna member humu ndani anatembea na mke wangu kutokana na uzi aliouandika humu.
Uzi wenyewe ni huu Nimejikuta nina mahusiano na mke wa mtu ila kuna kitu nimejifunza na wengine itawafunza

Member alieandika huu uzi anatembea na mke wangu, na mke wangu amemdanganya vitu vingi sana kuhusu mimi na kumjaza maneno ya uongo, ikiwemo ya kwamba nilimkuta bikra.

Pamoja na hayo, huyu jamaa ni wale wanaume marioo wanaopenda kulelewa kwani amekua akipewa pesa na mke wangu, pesa ambazo mimi nazitafuta kwa jasho na damu, yeye anazila kirahisi tu. Nilishashtukia kuwa kuna mtu ananilia vyangu kutokana na mabadiliko ya tabia kwa mke wangu, pamoja na kuwa na matumizi makubwa ya pesa ninayompa bila maelezo ya kujitosheleza.

Leo nimehakikisha na kumjua mbaya wangu. Sitaki kuzungumzia mapungufu ya huyo mwanamke hapa, ila tu nawataarifu kuwa kwa nitakachomfanyia huyu jamaa tusije tukalaumiana kabisa.

Nitamuonyesha kuwa mali ya mwanaume hailiwi bure. Kinachokwenda kumpata atahadithia hadi wajukuu zake.

Nimemaliza.

Unaweza pia kusoma >> Kuweka kumbukumbu sawa kuhusu kutokumjali mke wangu na kumsababishia kuchepuka
 
Familia nzima mko Jf🙌🙌
 
Mkuu elewa kuwa tatizo si la huyo jamaa anayemchakata mkeo.
Tatizo ni la mkeo na wewe mwenyewe maana hata ukimfanyizia huyo jamaa , mkeo si atatafuta mwingine kum do?
Sasa utawafanyizia wangapi?
 
Wewe achana na huyo mke malaya usijiingize kwenye jinai
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…