Nimeibiwa ATRIUMS hotel Sinza.

Nimeibiwa ATRIUMS hotel Sinza.

Chacha wa Mwita

Senior Member
Joined
May 17, 2008
Posts
167
Reaction score
34
Nilikuwa Dar Es Salaam kwa muda wa week moja, nilikaa Atriums Hotel na nikaibiwa night ya nne, niliibiwa chumbani usiku wa saa 3 wakati nikiwa restaurant nakula hapo hapo hotelini... Niliibiwa digital camera 2, na simu aina ya HTC, na pesa taslim usd 2300.., mbaya zaidi mmiliki wa hotel anaitwa Erik Shingongo alifika hapo hotelin baada ya kupigiwa sim na meneja wake ndugu Sunday nilieripoti wizi huo muda huo huo. Shigongo aliniambia kuwa anawajua wezi nimpe muda wa saa 3 atarudisha vitu vyangu, baada ya masaa 3 kupita alikuja tena akiwa na maaskari 3 toka kituo cha polis kijitonyama na wakanitaka kutoa maelezo., na wakati huo, ikiwa saa 7 usiku shigongo aliniambia kuwa tayari kesha washika wezi wanne ambao ni wafanyakazi wa hotelini hapo HIVYO nitulie nitapata mali zangu.Nimesubiri bila mafanikio, nikapewa maelekezo ya kumwona RCO wa osterbay, kamanda Wambura ambae alitoa maagizo ya kuwepo mkutano kati yangu na shigongo na meneja wake bwana sunday, mkutano ufanyike ofisin kwa rco ili tuweze kukubaliana namna ya kurudisha vitu nilivyoibiwa. Shigongo hakutokea, meneja wake alifika na akiwa amepewa na maagizo na Shigongo kuwa msimamo wa hotel ni kutolipa au kutoa fidia ya aina yeyote, kuwa wao kama hotel wanaona ilikuwa ni kosa langu kwenda hotelin ATRIUMS. na pia alisema hakuna wa kumfanya lolote Tanzania hii hata nikiripoti kwa RPC, RCO akaridhia na akaniambia hana la kufanya na sheria haimpi nafasi ya kumbana shigongo.
hiyo ndo ilikuwa final na kesi ikafungwa, Tanzania ya watanzania raia hana haki, hadi polis wanaubariki wizi na kuutetea, pale ATRIUMS ni kichaka cha kufuga wezi, mwizi namba moja akiwa Erik Shigongo. namba 2 meneja wake na namba 3 team yake ya wafanyakazi, Kuweni makini msiumie kama mimi.
 
Pole bana, ndo yule jamaa anaejinadi kufundisha watu ujasiria mali?!!.. pole ndugu yetu siku nyingine nenda hotel zenye kutambulika na zenye ulinzi imara.
 
duh pole,hivi hotelini sio kama guesthouse kuwa unatakiwa uache vitu reception kama unatoka??????kama ndio hivyo usiwalaumu....kama sivyo,then kata rufaa mkuu they should be made accountable for the loss.......
 
pole sana kamanda ila si ustaarabu kuacha pesa kiasi hicho hotelini, naamini kilichowatamaanisha hao ni pesa tu na hivyo vingine ilikuwa kama nyongeza tu.
 
ukiwa hotelini valuables zako beba, sasa unaachaje pesa chumbani?

Tena usd mbona zinafit vyema kwenye wallet?

Halafu ukiona mtu anauza magazeti yamejaa ngono, kufumaniwa uchawi nk sio wa kumuamini,hata hoteli zake zikimbie....
 
shigongo huyu mwenye magazeti ya udaku..halafu jamaa kila anachoongea lazima amtaje mungu. hii ngumu kuamini.
 
Pole sana lakini jofunze kuweka fedha bank mambo ya kutembea hotel na dola 2300 ni uzembe.
 
Mkuu, pole sana ila chumba cha hoteli hasa za kwetu (tz) si salama hivyo kiasi cha kuacha vitu kwa muda wa zaidi ya robo saa. Ni wazi wafanyakazi wa hapo wamekufanyia huo unyama kwa kujua sheria ya kuacha valuables reception itawalinda. Shigongo ni opportunist, ili mradi anapata faida basi wanaoumia kwa "ujasiriamali" wake si lolote.
 
uliweka pesa kwenye safety box nasema zile zinazo funguliwa kwa vinamba unayoseti mwenyewe?

bila hivyo ni tabu sana, ni njama ya watu wote wa hapo hotelin labda huyo Eric anawatuma mwenyewe wawaibie wateja

ni no go area hiyo hoteli wadau.

pole
 
Wakuu angalieni sana hoteli zingine wanafunga camera maalumu ambazo hata mteja huwezi kuziona. Hiyo yote ni kutengeneza mazingira ya kutokea vitu kama hivyo. Waswahili wanasema "asifuye mvua.....!!
 
Ilikuwa Nashera ya Morogoro, sasa Atriums ya Dar, sasa hotel gani yenye usalama? Hili ni doa kwa hiyo hotel.
 
Pole sana,hiyo hotel ni ya kuchinjia vya pori(hotel ya wazinzi),hivyo uhuni na umafia wa kila aina lazima uwepo!Next time nenda hotel zenye security na pia angalia visitors register,ukiona wageni wengi wanatoka Dar kwenda Dar ogopa!Next time nenda Landmark,Blue Pearl na zingine za hadhi hiyo.Na chukua ushauri wa wadau kuwa:bank your money,handover your valuables at reception & trust nobody but yourself!
 
Jamani ndugu zangu, hebu acheni kuwa watu wakusukumwa na kila mtu akiwemo huyu mkunga, kama uliibiwa nenda kaweke mwanasheria acha ubahili persue hiyo kesi hata miaka 100 people are getting away with murder, yaani unaweka na kupokea hela za wateja halafu unasema huwajibiki na wao kuibiwa hotelini kwako? hata mgeni anayetutembelea majumbani kwetu tunawajibika juu ya upotevu wa mali zao na usalama wao wakiwa ndani kwetu, kwa hiyo ukiwa hapo hotelini ukaingiliwa na kuumizwa ama kuuawa bado hutaki kuwa responsible?, hivi kweli kwa nini tuna simplify maisha yetu hivi? mnataka kuniambia kuna authority inayotoa kibali shigongo afungue hoteli lakini asiwe responsible for mali na maisha ya wateja wake? sasa hii ni hoteli ama machinjio? Nakataa kabisa hakuna mahali penye sheria kama hizi, ni sisi watanzania na upumbavu wetu kama tunaoufanya hapa tunaohalalisha ushenzi wa watu wenye vijisenti kama hivi, hebu weka wanasheria waulize, kwa hiyo hao askari hapo wanafanyanini? ama wanamlinda yeye mwenyewe na vitu vyake? tusijibweteke hela ulizoibiwa na mali ni kubwa sana weka nusu ya hizo mpeleke mahakamani hata kama anamamilioni ashughulikiwe hii haikubaliki
 
duh pole,hivi hotelini sio kama guesthouse kuwa unatakiwa uache vitu reception kama unatoka??????kama ndio hivyo usiwalaumu....kama sivyo,then kata rufaa mkuu they should be made accountable for the loss.......
We inaelekea huwa hulali hotelini so hujui haya mambo. Chumba kinatakiwa kiwe na sehemu maalum ya kutunzia vitu vya thamani, yaani kasafe fulani hivi. Kukabidhi mapokezi ni hotel za uswahilini, pale Atriums ni buku 70 halafu ni jirani sana na kona bar kama jamaa aliingia na MDUDU wanaweza kuwa wamem ADAM MALIMA. Shigogo my brother, its too LOW to pretend you are above the Law while you belong in group of very corrupt individuals in the country. Kumbuka ulikotoka Erick, umewadhalilisha sana akina dada katika magazeti yako ili uuze na umetajirika, nchi za watu ungefilisiwa. Watendee haki washkaji zako kina Ridhiwani wasilazimike kupindisha sheria kattika vitu vidogo kama hii ishu.
 
Mkuu bila kutafuna maneno wewe ni mzembe! Sijapenda ulivyoibiwa ila inamaana wewe ni mara ya kwanza kulala hotel? Mbona sheria za hotel zipo wazi dunia nzima kwamba valuables tembea nazo or kabidhi reception! Wewe uliachaje chumbani ukaenda kula? Bt more so walijuaje wewe ni pedejee lazima ulionesha mazingira ya kujifanya uko njema wakakutime. Kwa hilo Shigongo humuwezi coz sheria zipo waziiii!
Nilikuwa Dar Es Salaam kwa muda wa week moja, nilikaa Atriums Hotel na nikaibiwa night ya nne, niliibiwa chumbani usiku wa saa 3 wakati nikiwa restaurant nakula hapo hapo hotelini... Niliibiwa digital camera 2, na simu aina ya HTC, na pesa taslim usd 2300.., mbaya zaidi mmiliki wa hotel anaitwa Erik Shingongo alifika hapo hotelin baada ya kupigiwa sim na meneja wake ndugu Sunday nilieripoti wizi huo muda huo huo. Shigongo aliniambia kuwa anawajua wezi nimpe muda wa saa 3 atarudisha vitu vyangu, baada ya masaa 3 kupita alikuja tena akiwa na maaskari 3 toka kituo cha polis kijitonyama na wakanitaka kutoa maelezo., na wakati huo, ikiwa saa 7 usiku shigongo aliniambia kuwa tayari kesha washika wezi wanne ambao ni wafanyakazi wa hotelini hapo HIVYO nitulie nitapata mali zangu.Nimesubiri bila mafanikio, nikapewa maelekezo ya kumwona RCO wa osterbay, kamanda Wambura ambae alitoa maagizo ya kuwepo mkutano kati yangu na shigongo na meneja wake bwana sunday, mkutano ufanyike ofisin kwa rco ili tuweze kukubaliana namna ya kurudisha vitu nilivyoibiwa. Shigongo hakutokea, meneja wake alifika na akiwa amepewa na maagizo na Shigongo kuwa msimamo wa hotel ni kutolipa au kutoa fidia ya aina yeyote, kuwa wao kama hotel wanaona ilikuwa ni kosa langu kwenda hotelin ATRIUMS. na pia alisema hakuna wa kumfanya lolote Tanzania hii hata nikiripoti kwa RPC, RCO akaridhia na akaniambia hana la kufanya na sheria haimpi nafasi ya kumbana shigongo.
hiyo ndo ilikuwa final na kesi ikafungwa, Tanzania ya watanzania raia hana haki, hadi polis wanaubariki wizi na kuutetea, pale ATRIUMS ni kichaka cha kufuga wezi, mwizi namba moja akiwa Erik Shigongo. namba 2 meneja wake na namba 3 team yake ya wafanyakazi, Kuweni makini msiumie kama mimi.
 
Nilikuwa Dar Es Salaam kwa muda wa week moja, nilikaa Atriums Hotel na nikaibiwa night ya nne, niliibiwa chumbani usiku wa saa 3 wakati nikiwa restaurant nakula hapo hapo hotelini... Niliibiwa digital camera 2, na simu aina ya HTC, na pesa taslim usd 2300.., mbaya zaidi mmiliki wa hotel anaitwa Erik Shingongo alifika hapo hotelin baada ya kupigiwa sim na meneja wake ndugu Sunday nilieripoti wizi huo muda huo huo. Shigongo aliniambia kuwa anawajua wezi nimpe muda wa saa 3 atarudisha vitu vyangu, baada ya masaa 3 kupita alikuja tena akiwa na maaskari 3 toka kituo cha polis kijitonyama na wakanitaka kutoa maelezo., na wakati huo, ikiwa saa 7 usiku shigongo aliniambia kuwa tayari kesha washika wezi wanne ambao ni wafanyakazi wa hotelini hapo HIVYO nitulie nitapata mali zangu.Nimesubiri bila mafanikio, nikapewa maelekezo ya kumwona RCO wa osterbay, kamanda Wambura ambae alitoa maagizo ya kuwepo mkutano kati yangu na shigongo na meneja wake bwana sunday, mkutano ufanyike ofisin kwa rco ili tuweze kukubaliana namna ya kurudisha vitu nilivyoibiwa. Shigongo hakutokea, meneja wake alifika na akiwa amepewa na maagizo na Shigongo kuwa msimamo wa hotel ni kutolipa au kutoa fidia ya aina yeyote, kuwa wao kama hotel wanaona ilikuwa ni kosa langu kwenda hotelin ATRIUMS. na pia alisema hakuna wa kumfanya lolote Tanzania hii hata nikiripoti kwa RPC, RCO akaridhia na akaniambia hana la kufanya na sheria haimpi nafasi ya kumbana shigongo.
hiyo ndo ilikuwa final na kesi ikafungwa, Tanzania ya watanzania raia hana haki, hadi polis wanaubariki wizi na kuutetea, pale ATRIUMS ni kichaka cha kufuga wezi, mwizi namba moja akiwa Erik Shigongo. namba 2 meneja wake na namba 3 team yake ya wafanyakazi, Kuweni makini msiumie kama mimi.

We hujamalizia vyote uliibiwa pia na laptop 3 za 5m,blackberry 3 za 5.5 m pete mbili za shaba za 2.5m,tsh 1.5m,na mabegi ya nguo matatu hawawezi kukulipa kwakuwa ulipoingia ulipewa masharti yao kuwa vitu vya thamani uviache reception hukuacha,na pili wameandika kabisa kulala at ur own risk na pia kamera zimekurekodi ukiingia na dada mweupe mrefu usiku ambaye hoteli haimtambui kwakuwa uliingia kama single na si double!!
 
Back
Top Bottom