Nimeingiwa na hofu kufuatia wizi wa madirisha site


Ukishaanza kuweka bati na ukaweka grill weka mtu akae hapo saiti mana bora huyo dirisha wengine wanabebewa wireling ya nyumba nzima ukitaka kujua utamu wake nenda dukani kanunue vifaa vya umeme uone kiboksi unachobeba afu hela unayoachaaaa sas
 
Tulisha weka mlinzi, siku mmoja tukakuta mlinzi hayupo na vifaa including machuma ya dirishani havipo. Mlinzi hakupatikana tena
 
Mie nimejenga sehemu nyingi hapa jijini DSM. Nyumba ikishafikia level za grill na milango tafuta mtu akae. Mwekee wavu wa mbu na choo temporary.

Pia ni vizuri ukaweka mtu mwenye mke ili iwe ngumu kutoroka


Watu wengi mjini hawana kodi za kulipa hata chumba kimoja. Ukiwapa makazi na hela kidogo ya ulinzi utaokoa mali zako dhidi ya wizi
 
Pole sana kwa hofu. Mm kwa ushauri wangu siku unaweka firisha piga na plasta koplo ili isionekane ni wapi walitindua ili kufitisha.
 
Wengine nasikia ukifanya hivyo wanakupuliza nyumba inakua haimaliziki, yani pesa unapata Ila wazo lakuimalizia haliji! miaka inasogea wao wanaishi bure tu.

Kuna story ya mtu kusahau nyumba yake ilipo kisa kamweka mmakonde amlindie!!
 
Wengine nasikia ukifanya hivyo wanakupuliza nyumba inakua haimaliziki, yani pesa unapata Ila wazo lakuimalizia haliji! miaka inasogea wao wanaishi bure tu.

Kuna story ya mtu kusahau nyumba yake ilipo kisa kamweka mmakonde amlindie!!
Hizo story tu. Utasahau vipi nyumba ambayo umeweka fundi mkuu anakushauri. Ndugu jamaa na marafiki pamoja na familia yako wote hao hawajui kuhusu site? Mtu kafulia anasingizia wamakonde. Ukiwa na mawazo hayo hutoboi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…