Ndugu wanajamvi naombeni msaada wenu,
Mimi ni mlinzi katika eneo letu la kazi, inasadikika kulitendeka wizi jambo la kushangaza lindo hilo lina zaidi ya walinzi 13.
Baada ya mpelelezi wa kituo cha polisi Kilwa Road kufika eneo la tukio aliuomba uongozi wa walinzi kupeleka jumla ya walinzi wanne kituoni. Katika shifti hiyo ya jumla ya walinzi 13 sijui niseme ni bahati mbaya au kusudi kiongozi huyo alinichukua mimi badala ya mwenzangu aliyehitajika kituoni kati ya watu wale wanne.
Nilipofika kituoni nilimfafanulia mpelelezi huyo kwa jina anaitwa Subira Tossi kuwa mimi sio kati ya watu wale wanne aliowahitaji, alichokijibu ni kuwa kama umeleta huyu basi shifti nzima ya watu 13 iletwe kituoni.
Kiongozi yule hakufanya hivyo mpaka kesi inapelekwa mahakamani tulichukuliwa watu watano yaani wale wanne na mimi niliyepelekwa kimakosa.
Tafadhali msaada wenu ili niweze kujua haki ya msingi ipo wapi au hapa kuna mazingira ya rushwa?
Mimi ni mlinzi katika eneo letu la kazi, inasadikika kulitendeka wizi jambo la kushangaza lindo hilo lina zaidi ya walinzi 13.
Baada ya mpelelezi wa kituo cha polisi Kilwa Road kufika eneo la tukio aliuomba uongozi wa walinzi kupeleka jumla ya walinzi wanne kituoni. Katika shifti hiyo ya jumla ya walinzi 13 sijui niseme ni bahati mbaya au kusudi kiongozi huyo alinichukua mimi badala ya mwenzangu aliyehitajika kituoni kati ya watu wale wanne.
Nilipofika kituoni nilimfafanulia mpelelezi huyo kwa jina anaitwa Subira Tossi kuwa mimi sio kati ya watu wale wanne aliowahitaji, alichokijibu ni kuwa kama umeleta huyu basi shifti nzima ya watu 13 iletwe kituoni.
Kiongozi yule hakufanya hivyo mpaka kesi inapelekwa mahakamani tulichukuliwa watu watano yaani wale wanne na mimi niliyepelekwa kimakosa.
Tafadhali msaada wenu ili niweze kujua haki ya msingi ipo wapi au hapa kuna mazingira ya rushwa?