Nimejikagua na kujipima upya kuhusu mwenendo wa uchumi, nimekosa raha

Nimejikagua na kujipima upya kuhusu mwenendo wa uchumi, nimekosa raha

mwanyaluke

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2015
Posts
704
Reaction score
2,435
Kujikagua na kujipima ni jambo la muhimu sana , hebu tafakari miaka mitano yako nyuma na sasa, huko ulimiliki nini na sasa unamilki nini , shughuli zako za kiuchumi je zimetanuka na atleast zinatosheleza mahitaji yako au bado mechi Ngumu sana upande wako ukichukua muda wako ukajitenga na kukaa chini na kujiuliza kwa umakini sana nini umefanya kwa miaka iliyopita na unajiona wapi miaka mitano ijayo inatisha sana ule mtazamo uliokuwa nao wakati wa ujana kuhusu maisha bado unao ule ule, zarau ulizokuwa nazo enzi hizo kuhusu watu wazima unapowaona wanaishi maisha magumu bado unazo, unaipa elimu ya darasani asilimia ngapi kwenye mchango wa kipato chako , vipi ajira yako inatosheleza kipato chako ? vitu vingi ukijiuliza vinatia hasira sana

Mimi binafsi nimejitafakafari nimejikuta kwenye huzuni tu ,ndio napiga hatua , ndio yapo mabadiliko fulani lakini bado sana , zipo transactions ambazo nilikuwa siwezi kufanya sasa nafanya bado mechi ni ngumu sana upande wangu , kipato nilichonacho hakinipi nguvu ya kusimama mbele za watu kama mtu ninayejiamini, nauchukia sana umaskini lakini bado hautaki kunitoka , nahisi kuna umuhimu wa kubadili mbinu za utafutaji ila tu zisihusu uchawi, uporaji na utapeli , nahisi kuongeza muda wa kufanya kazi na kuongeza muda wa kuomba MUNGU
 
MI NAJISHANGAA SANA,,,,

SMART PHNE NIMEUZA
TV NIMEUZA
KTANDA NSHAUZA
GODORO BADO SIJAPATA MTEJA,,
TOROROO NSHAUZA
BAADHI YA NGUO ZANGU ZA GHARAMA NIMEUZA
KIWANJA CHANGU NSHAUZA

UKWELI NILIUZA VITU NA BADO MIKOPO MIKUBWA.NIKIPIGA HESABU NI KAMA NIMERUDI HATUA MIA NYUMA NA KAZ BADO NAFANYA!

MAPAMBANO KWANGU NDO YAMEKUWA MAGUMU SANA KAMA SIFANYI KAZ VILE!
KWASASA NAPOKEA USHAURI KUTOKA HATA KWA WADOGO ZANGU WAKATI HAPO NYUMA HATA BABU HASINGEWEZA NIAMBIA KITU!
 
Dah aisee mimi nilifikiri kupata kazi serikalini ndo kutoboa ila baada ya kupata ajira sasa siifurahii ajira juat imagine nishaangukia kwenye mamikopo umiza na jana walikuja wale wazungu wakupitisha vyombo vya mkopo maofisini wameniingiza cha kike subwoofer yao nimechukua kwa mkopo 120000 kila mwezi kwa miezi minne wakati kwa cash zinauzwa sijui laki mbili zile sa speaker tano..inshort naona kazi miyeyusho borea hata zamani nilivokuwa nauza duka..ila wakati mwingine me sipendi kazi za site naonaga naenda kutembea tu yaani posho yote inaishia hukohuko site
 
Mimi kwa vitabu na kupitiapitia jeiefu labda nimeongeza maarifa ila kiuchumi. Mmmh kiuchumi tunajikongoja.

Ofcoz kiuchumi kuna ongezeko (mfano kupata 'baiskeli' ya kutembelea yenye injini😃)lakini zaidi ni kama nipo mulemule tu. Nahisi na inflation nayo inachangia mazee.
 
Back
Top Bottom