Nimejikusanya na kupata 350,000; TRA wananikadiria kodi kubwa, nifanyeje?

Si kweli kwamba wanajipigia tu wanavyotaka.. Kuna guide book yao ambayo wanaifata kwa aina za biashara ambazo hazina vitabu vya mahesabu
Kuna Supermarket hapo Ilala inalipa 84,000 annually sas hebu nitajie guide book gan walitumia hawa.?
 
Ulichokosea ni hyo biashara ya tgo pesa,mpesa na Airtel money kuwaambia T.R.A ilitakiwa uombe kulipia kodi ya genge kwa hyo wangekupa tin no.ya genge ambayo n kima cha chini 150,000 per year.....
 
Naona unawashwa wewe, matusi ya nini sasa!?? C uelezee taratibu, halafu ye c kaenda sema ukweli, alitakiwa aulize iko vp kwa wazoefu, unakuwa kama unapumuliwa bhana [emoji84]
 
Jirani yangu ana genge la samaki na mboga mboga kwa zaidi ya miaka 10 na hajui hata TIN number ni nini. Mtaji wake siyo chini ya milioni moja na kwa harakaharaka mauzo yake ni kama laki mbili kwa siku. Wewe mleta mada ulikurupuka kwenda kuomba TIN number ya genge. Labda ungeenda kwaaajili ya hiyo biashara ya MPESA tuu
 
Kwani kupata TIN si inakuwa bure then unakwenda Manispaa kwa ajili ya Leseni au
Huwezi kupata leseni bila kuwa na TAX CLEARANCE ambayo unaipata TRA, ukishapewa TIN aunaenda tra wanakuuliza maswali ya mtaji ulionao na aina ya biashara unayotaka kufanya, wanakadiria mapato yako kwa siku, halafu wanakadiria kodi, unaenda kulipa benk, ukirudi na slip ya malipo ndipo unakwenda kuomba leseni ukiwa umeambatanisha copy ya TIN na hiyo TX clearance., bila hiyo HAKUNA KUPATA LESENI.
 
Kuna Supermarket hapo Ilala inalipa 84,000 annually sas hebu nitajie guide book gan walitumia hawa.?
Amelipa mwaka gani?? Kwasababu kima cha chini kabisa cha kodi ni 150,000/- sasa wewe hiyo 84,000 unayosema ni either fix unapiga hapa au imelipwa kwa kipindi cha miezi 6...

Ukienda kwa afisa yeyote wa TRA kuchukua TIN ya biashara hapo kwenye kupigiwa hesabu lazima kuna maswali anakuuliza ili aweze kuestimate ni kipato gani unapata ndio ukupigie hesabu za tax. Na hapa wengi ndio hujichanganya maana wakiulizwa wanataja pesa nyingi ili waonekane matajiri lakini mwisho wa siku ndio hiyo unapigwa kodi kubwa.. Lakini hata ukitaja ndogo sana na ndio unaanza biashara basi afisa atakupa hiyo 150,000 ukailipe..
 
Kwanza ulichokiandika hapa sidhani kama kina ukweli..

Lakini kwa upande mwingine ndio uzuri wa vitabu vya mahesabu.. Ukiwa na vitabu vya mahesabu vilivyokaguliwa na Auditors basi kuna uwezekano wa kuwa unafanya biashara za mamillion lakini kodi ikalipa ya kawaida sababu kwenye vitabu kuna faida na hasara.. Biashara zote za bima lazima ziwe na vitabu vya mahesabu, sasa kwa mwaka huo aliolipa 134,500 unayosema japo siihafiki yawezekana kampuni ilionyesha imepata faida kidogo kwahiyo TRA wakikata percent ya kodi hapo ndio kikaja hicho kiasi kidogo cha kulipa.. Ila kama huna vitabu ndio hapo wataishia kukukadiria mapato na kodi inakokotolewa kutoka kwenye annual turnover waliyoikokotoa na si faida..
 
Naona unawashwa wewe, matusi ya nini sasa!?? C uelezee taratibu, halafu ye c kaenda sema ukweli, alitakiwa aulize iko vp kwa wazoefu, unakuwa kama unapumuliwa bhana [emoji84]
Haaa wew tena unasema me Napumuliw halaf unanionya kuhus matusi.? Wew si ndo mwalimu wa wanaopumuliwa.? Wanafunzi wako waliohitimu si ndo yule mmoja alihojiwa Clouds Tv [emoji23] [emoji23] [emoji23]
#ChekaKwaDharaaau
 
Sidhani kama una spirit ya biashara boss, Yan unajipeleka Tra wkt hata biashara haija changanyia
 
Ili upate line ya uwakala wa tigopesa, mpesa etc (Till) lazima uwe na TIN pamoja na leseni ya biashara. Hapo ndipo unapolazimika kulipia kiwango cha chini cha Tsh 150,000 tra na leseni ya biashara ni kama Tsh 70,000 kwa mwaka kama sijakosea kwa manispaa hata kama hujaanzisha biashara bado.
 

Attachments

  • INDIVIDUAL TAX.PNG
    15.9 KB · Views: 71
Kinachofanywa na TRA ni kukupatia TIN na kufanya makadirio estimate ya kodi unayotakiwa kulipa baada ya hapo wanakupatia clearance form ambayo utaenda nayo manispaa kupewa lesseni ya biashara yako na leseni inalipiwa kwa viwango tofauti tofauti kulingana na aina ya biashara yako...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…