Nimejiwekea msimamo; Sipandi bodaboda za hivi mimi, mara mia nitembee

Nimejiwekea msimamo; Sipandi bodaboda za hivi mimi, mara mia nitembee

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
11,793
Reaction score
22,552
Ni misimamo yangu kwamba;
  1. Sipandi bodaboda isiyo kuwa na kioo (side mirror), maana mambo ya kugeuziwa shingo kila muda ujinga huo sitaki, Mara ageuke nyuma akosee tuelekee mtaroni spendi kabisa!
  2. Sipandi bodaboda ya bonge au mtu mwenye kitambi; Haiwezekani mi nilipe buku halafu siti yote akalie yeye bure mimi nikae kwenye chuma (value for money)
  3. Sipandi bodaboda ya mtu mfupi Mimi, ujasiri huo sina, Mambo ya kuwekana roho juujuu kwenye mchanga au utelezi siyataki, maana miguu yake haifiki chini hadi nimsaidie mimi kukanyaga chini.
  4. Sipandi boda boda yenye na dreva aliyevaa singirendi yenye kuonyesha makwapa!
  5. Sipandi bodaboda anaesalimia kila mtu njiani mimi siyo mgombea sina ukarimu huo
  6. Sipandi bodaboda ya yule kiduku anaekalia tako upande upande mawenge sitaki!
  7. Mwisho ingawa siyo kwa umuhimu, Bodaboda mwenye kujidai ana haraka kuliko mimi abiria huwa naomba anishushe ili nimuache awahi anakoenda!
 
Mie sipandi boda boda kuna mtu humu alitaka kunipandisha boda boda nikamwambia ukitaka tugombane nipandishe boda boda akacheka sana
😂😂😂😂😂😂 Akaniambia BAK basi utakuwa umbali mdogo nikakaza mimi sipandi boda boda.
🤣🤣🤣🤣
 
Namba moja uko sahihi na ndiyo kwa asilimia nyingi husababisha ajali, anaendesha pikipiki hata ukiangalia pembeni tu wakati pikipiki inaenda ujue hutokwepa ajali
 
Hakikisha hupandi bodaboda ambae hajavaa viatu vya kufunika. Bodaboda akiwa amevaa sendo usithubutu kupanda hiyo pikipiki.

Mjini bodaboda anaesalimia kila mtu unamtoa wapi?
 
Hakikisha hupandi bodaboda ambae hajavaa viatu vya kufunika. Bodaboda akiwa amevaa sendo usithubutu kupanda hiyo pikipiki.

Mjini bodaboda anaesalimia kila mtu unamtoa wapi?
 
Back
Top Bottom