Nimekata mtaji, nakodisha akili na nguvu; niokoeni wanajamii.

Nimekata mtaji, nakodisha akili na nguvu; niokoeni wanajamii.

Rene Jr.

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2014
Posts
3,714
Reaction score
2,376
Salaam wakuu,
Kama kichwa cha habari kinavyosomeka, mwenzenu nimekwama hivyo naangalia upande wa pili. Nilikuwa na kazi zangu za kijasiriamali kwa miaka kadhaa, mambo si mambo yakatukia ya kutukia nikaanguka, I just dont have the luxury to give up, najaribu kuinuka na kujikung'uta vumbi niangalie usawa mwingine wa kusonga mbele.

Nimejaribu kuangalia options kibao, lakini kila iliyopo kichwani inahitaji pesa ambazo sina!! Baada ya kuwaza ndugu jamaa na marafiki nikawaza JF, najua kuna watu wengi humu wanaweza kunisaidia na mimi nikawasaidia nguvu na akili katika kazi zao. Mimi niko flexible sana wakuu nafanya kazi yoyote popote, Kama una shamba sehemu unahitaji mtu wa kusimamia mi ntavaa buti na kuhamia huko, kama una ofisi sehem unahitaji mtu mwenye knowledge ya IT nitavaa tai na nitashinda na kukesha nyuma ya computer, lengo nikufurahishe katika kazi yako uone tofauti katika utendaji na uzalishaji ili mwisho wa mwezi na mimi unifurahishe nijikusanyie kijimtaji cha kulianzisha tena, maana mwenzenu nina familia ya mke na watoto wawili, posho ya mama haitoshi kitu.

Mara zote huwa najitahidi kuangalia mambo upande chanya, nina imani hapa kuna watu wanaoweza kunisaidia, KAZI YOYOTE WAKUU MI NAFANYA, alimradi tuelewane maslahi na majukumu tu.

Nakaribisha majadiliano PM, pia kama kuna mambo unapenda kufahamu.

Natanguliza shukrani.
 
Pole lakini hongera kwa kuwa muwazi na jasiri kukubali hali yako wengine tungeficha kichwa kama mbuni jangwani. Ushauri wako pamoja na kuomba kazi ingekuwa vizuri zaidi ukauza skills zako au uzoefu wako ktk biashara gani, si unajua tena pamoja na kuwa willing but watu watataka kumweka mtu angalau mwenye ujuzi wa kitu husika, labda tuanzie tu mfano na hiyo IT utaje utawasaidia vitu gani? kusimamia biashara uzoefu hasa kwenye nini inaongezea mvuto kwenye ombi lako. Ushauri mwingine sio lazima uajiriwe bali waweza kuingia partnership na mtu kw abiashara ulizokuwa na uzoefu nazo na kwenye equity sharing wewe utakuwa huna ila utalipwa kulingana na mapato huku ukinunua shares hadi usimame vizuri, huku ukilipwa kama manager wa mradi. Nakutakia heri na Baraka.
 
Pole sana mkuu, kama ulikuwa umejiajiri na sasa unataka kuajiriwa naona kama utapotea zaidi, mimi nakushauri fanya analysis uone wapi ulikosea then uanze taratibu kwa mtaji mdogo, punguza matumizi, tafuta nyumba ya bei nafuu kama wewe ni mpangaji. Kuwa na imani kwa biashara utakayoanzisha, ukiwa jasiri utasimama, lakini ukiwa muoga na kutaka hata kwenda kufanya kibarua kwenye shamba la mtu utapotea kabisa. Kama kweli ulikuwa mjasiriamali naamini una skills kukufanya uinuke, keep up, keep the faith, keep believing
 
Nashukuru sana Mama Joe , mimi huwa naamini katika uwazi, nikificha maradhi haitanisaidia sana upande wangu. Nikifungua kwenye computer nitaongeza details kwenye post yangu.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nkobe ukisoma vizuri kwenye post yangu nimeonesha nahitaji kufanya kazi na mtu ili kutoka kwake nipate mtaji wa kusimama tena, its the only option I think I currently have, nimejaribu altenative ya kukopa lakini its just not working, (labda mnipe mawazo zaidi wakuu, ndiyo maana nimeleta mada hapa). Costs nyingi nilishazi-cut kitambo tu baada ya kuona mambo hayaendi kwa jinsi yalivyokuwa yanatakiwa yaende.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu, Crocodiletooth nilikuwa nauza vifaa vya ICT, pia nlikuwa nafanya ict solutions. Kilichotokea nilituma pesa sehem ikapotea zikiwamo pesa zisizo zangu hivyo nikalazimika kuchukua kila kilicho changu kucover the loss, ni habari ndefu mkuu. Lengo hasa ni kurejea kwenye kazi, maana mipango nilikuwa nayo mingi ya kunieletea pesa nzuri, tatizo mtaji ndiyo haupo tena ndiyo najaribu kuangalia upande wa pili nijikusanye tena, maana hata mtaji wa mwanzo nilifanya kazi nikapata mkuu hivyo naamini nikifanyakazi naweza kupata tena. Tupeane mawazo mkuu wangu, nikiwaangalia hawa watoto naona nina majukumu makubwa mno natakiwa kuwa na kipato cha kueleweka maana kila kunapokucha mahitaji yao yanaongezeka.
 
Last edited by a moderator:
ushauri wa nkobe ni muhimu pamoja na kuwa muwazi vya kutosha mtu anaweza kukuajiri lakini kutokana na maelezo yako temporary/contract job ndo inakufaa.
 
Huo ndio uanaume haswaa..kisichokuua kinakukomaza, naamini umekomaa sasa sababu uko hai. All the Best mkuu
 
Mwenyezezi Mungu na akusimamie na hakika kwa myo huo utasimama tena!
 
wasiliana na msocrates ana huruma sana mimi namfahamu anaweza akakupa kazi hata ya ulinzi kwenye migodi yake.
 
Pole ndgu,! nikiangalia maelezo yako inaonekana uko Taiti sn kwa waTZ tuliowengi huwa 2napenda kumtumia m2 7bu ya matatzo yake so unaweza kupewa kiBARUA bt Incom,haitoshi hata kwa matumizi ya Familia manake utapotea kabisa! Ushauri wangu km itawezekana jaribu kuweka gharama za Prject yako atakaekuwa tayari labda muuziane hisa au kugawana Faida pia ikijulikana kiasi cha mtaji hataukipata kidg unaweza kuipeleka kwenye SACCOS unakopa mara MBILI ya unachoweka huenda ukacmama tena ndg yangu!
 
Nilipoona hii post imenibidi niitafite hii post ya 4hrs ago katika ukurasa wa fcbk! Ebu fuatilia masna mpk sasa hakuna hata aloapply, huenda itakuwa yako..mtafute huyu bwana ni marketing officer ImageUploadedByJamiiForums1395319328.833363.jpg

Cc: Rene Jr


Sent from Mchina
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom