Mkuu kama ccbrt wameshindwa hapo muhimbili wataweza kweli?
Tengeneza juisi ya Karoti uwe uankunywa kila siku macho yako yatarudi nuru yake na hutoweza tena kutumia miwani. tumia kisha uje unipe Feedback Health serviceHabari wa jukwaa letu la lfdoctor?
Jamani nimekata tamaa ya kupona macho, nimetembea kwenye hospital nyingi tu naambiwa hawaoni tatizo wananipa tu ushauri wa kula vyakula na matunda na pia kutumia miwani ili kurekebisha uono hafifu, hii ina maana kuwa hospital hakuna tiba ya macho zaidi ya kupewa miwani tu.
Mimi binafsi sipendi kutumia miwani bali ni kupona kabisa tatizo la macho, niliwahi kuambiwa nimechezewa lakini hata tiba za jadi hazijanisaidia zaidi ya kufuja pesa. naombeni ushauri wadau nifanyeje?
tumia mafuta ya mawese kuna jamaa yangu alikua na tatizo kana lako now havai miwani!
No. Nakunywa supu ya macho ya mifugo. Supu ya pweza haioni ndani hapo.
Na nikijiangalia siwezi kula macho ya samaki! Khaaa!
Mkuu kama unaona matumizi ya miwani hayafai, jifunze kupapasa na hudhuria shule ili uelewe kusoma maandishi ya vinundu!
Mi ushauri wangu ndio huo vinginevyo endelea kuliwa hela.
kwa umri wako huo 50+ huwezi kurudia tena hali yako ya kwanza